Siku Za Utawala Wa SMZ Na CCM Yake Zanzibar Zinahesabika...

Junius

JF-Expert Member
Mar 11, 2009
3,181
139
Na Jabir Idrissa
NAFURAHI kuona Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma ameramba matapishi yake mwenyewe. Amegeuka.
Hamza ameivua Marekani na tuhuma alizoitupia pale aliposema hadharani kuwa nchi hiyo imehusika katika matukio ya milipuko ya mabomu iliyokuwa yameshamiri kisiwani Pemba.
Japo amefanya hivyo kwa kuzidisha udanganyifu – akidai kwamba yeye hajawahi kusema wamehusika – bado ukweli unabaki palepale kwamba “amejirudi kwenye uhalisia wa mambo.”
Hamza alitamka hadharani na kukaririwa na vyombo vya habari ikiwemo Televisheni ya Serikali ya Mapinduzi, TVZ, akiituhumu serikali ya Marekani kufahamu kinachoendelea Pemba wakati wa uandikishaji wapiga kura, baada ya nchi hiyo kutoa taarifa kwa raia zake wasifike Pemba kwa kuwa yanayotokea yanaashiria ukosefu wa amani.
Taarifa ya ilani ya Marekani iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje (State Department) mjini Washington na nakala ya taarifa hiyo kupatikana mjini Zanzibar, ilisema wazi kuwa ilitokana na utafiti walioufanya.
Lakini hata pale msemaji wa wizara hiyo alipotoa taarifa ya pili akirejelea matamshi ya ovyo ya Hamza, alisisitiza kuwa Marekani imechukua hatua hiyo kwa maslahi ya raia zake wala haikuhitaji kumuuliza kiongozi yeyote wa Tanzania.
Bila ya shaka matamshi ya ovyo ya Hamza yaliikasirisha Marekani, na hatua hii mpya ya waziri huyo kujirudi ndani ya Baraza la Wawakilishi inaonekana haikuwa hivihivi, bali ni kwa kuzingatia maafikiano ya kidiplomasia kati ya Marekani na Tanzania.
Tatizo la Hamza kuwa hataki kuwa muungwana katika kujirudi. Anajizonga kwa kuanzisha uhasama na vyombo vya habari; eti vilimsingizia. Hivi Hamza asingiziwe ili iwe nini? Anajulikana mkate wake umeongezeka siagi miaka hii kutoka ule wa kutegemea ushoni aliokuwa akitegemea Mikunguni.
Ninaisema kwa makusudi hii ili akae vizuri na mtindo anaouanzisha wa kurudisha lawama kwa wasiohusika kwa kosa alilojitia mwenyewe, tena kwa hiari yake na raha zake.
Lakini hii haikuwa mada yangu, ila nimelazimika kugusia hapo kwa kuwa nilipata kumsihi Hamza kuwa “hayawezi madhambi ya SMZ.”
Leo nikitaka hasa kueleza hofu yangu kwamba kwa kuwa mwenendo wa dola haujabadilika; kwamba haijafuata ukweli kuwa inanyonga haki za wananchi; basi sitarajii mabadiliko yoyote uandikishaji wapiga kura utakapoingia Mkoa wa Mjini Magharibi.
Ni dhahiri kwamba misimamo ya viongozi wa vyama vya upinzani itabaki ileile ya kukataa kushiriki katika mduara wa ushetani wa kuhalalisha maovu yanayotendeka dhidi ya mfumo wa demokrasia.
Ninamaanisha kuwa hawatahamasisha wananchi wanaowatii kujitokeza kwenye vituo vya uandikishaji ili kuandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) la Zanzibar.
Na siyo tu kwamba hawatawahamasisha watu kujitokeza vituoni, bali pia watawaelekeza kujipanga vizuri ili kuzuia wale waliopatiwa kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi wasiandikishwe.
Naiona hali hiyo kwa sababu bado tatizo liliopo – ambalo limekwamisha uandikishaji wenye ufanisi kiasi cha kusikitisha wakuu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kama inavyodhihirika katika taarifa zake kwa umma – halijatatuliwa.
Tatizo ni kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, ambacho kuanzia mwaka 2006, kimeingizwa katika sheria ya uchaguzi kama shurti kwa kila Mzanzibari kukimiliki ndipo atambuliwe na kuandikishwa kama mpiga kura, kingali kinatolewa kibaguzi kwa kuzingatia nani kura yake ataitia kwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Kwa yule ambaye machoni mwa wenye kulea mfumo wa kidhalimu, ataonekana si miongoni mwa wakereketwa au makada wa CCM, itabaki tu kuwa shida kwake kuruhusiwa kupata kitambulisho na hivyo kujikuta hapenyi kwenye wigo wa watu wema.
Kwa mfumo wa utawala uliopo hadi sasa, watu wema ni wale tu ambao hata kama si hadharani, lakini wana sura ya kupigia kura mgombea wa CCM tu na si vinginevyo.
Asiyekuwa na chapa ya CCM kwenye paji lake la uso, ajue kura ya 2010 ataisikia tu. Ataisikia kwa sababu kwa kuwa hana kitambulisho, hatapata kuandikishwa. Asipopata kuandikishwa, hatapata kupiga kura.
Kitambulisho cha Mzanzibari kimekuwa dili. Baada ya kuanza kama maskhara, ingawa kilipingwa kwa nguvu nyingi kwa kuhofiwa kitatumika vibaya, tulipo kishathibitika kuwa kililetwa kwa dhamira mbaya hasa. Ukweli unaonekana.
Kimeshasababisha maelfu ya watu kunyimwa haki yao ya msingi ya kuingia katika daftari la wapiga kura. Hawa wamekalia kuti kavu kwani nafasi kwao kuingia ni sawa na mbuni kupita kwenye tundu la sindano. Labda ipite kudra ya Mwenyezi Mungu kabla ya Oktoba mwakani.
Ikija kudra hiyo basi ndipo ukweli utapodhihiri na uongo utapojitenga. Hapo ndipo mbivu itapoliwa na mbichi itaposubiriwa iwive ili nayo iliwe kwa wakati muafaka. Ni wakati huu nyuso za wakubwa zitakaposinyaa kwa aibu.
Watatahayari maana yale waliyoyapanga kutokea ili kujinufaisha nafsi zao, yatakuwa yametenguka. Ushetani waliolenga kuufanikisha utakuwa umekomeshwa. Wamenyamazishwa. Na hii si wao tu, bali hata mawakala wao wanaojitahidi kutetea wanachokifanya.
Uandikishaji utakapoingia majimbo ya wajanja na “wasemaji ovyo isivyomithilika” watunza takwimu za kupika wanaoishi kwa kujisuta, wataumbuka na kubaki kushangaa. Labda watatamani ardhi ipasuke wajifiche. Labda wataamua kuhama nchi. Sijui.
Tushaona uandikishaji ulivyoleta aibu kwa wakubwa katika majimbo ya Kaskazini Unguja. Tushajionea namna mikakati ya kuvuruga uchaguzi inavyoandaliwa. Tushafahamu kumbe bado wakubwa hawajaamini kuwa siku hazigandi.
Ukweli ni kwamba umma umeelewa dhamira hasa za viongozi wa CCM katika kuitisha uchaguzi. Kumbe ni kiinimacho na jambo la kudanganya ulimwengu. Masikini roho zao hawajui kwamba uchaguzi huru na wa haki si matamshi bali matendo.
Masikini roho zao hawajui kuwa hawana wafichacho. Kila kitu kipo kweupeni zama hizi. Hawajui kuwa ndani ya ofisi za umma wanazotumia kufanikisha udanganyifu wamo watu wema kwa Wazanzibari wenzao na nchi yao waipendayo kama mboni za macho yao.
Masikini roho zao viongozi hawa wahafidhina hawajui kwamba kwa sasa wanapuruziwa tu kamba kwani iko siku kila kitu kitabadilika na mambo yatageuka nyuma mbele, na wao watasaga mawe kama alivyofanya firauni na wenzake.
Hata kama si kesho na keshokutwa, hakuna chenye mwanzo kikakosa mwisho. Nasema hakuna kinachodumu milele iwapo binadamu mwenyewe ataukata na kurudi alikotoka. Basi mambo yatabadilika tu Inshaallah

SOURCE:MWANAHALISI
 
Wamebakiza siku kidoooogo tu...karibuni tu Wazanzibar watatoka katika utawala wa kidhalimu wa CCM...Itabaki historia tu, karibuni waungwana...bendera ya utu wenu karibu itapepea...chem chem za muruwa wenu zimeanza kutiririka...hofu zenu zimeanza kupata tiba na utulivu wa nafsi unachukuwa nafasi...waungwana wamekupokeeni, karibuni Zanzibar...karibuni nchi yenu mliyoijenga kwa kucha na meno, mkatolewa kwa dhulma na shinde...rejeeni mkiwa mashujaa na watoto walee wanakusubirini kukupokeeni...karibuni sana tu.
 
Na Jabir Idrissa
NAFURAHI kuona Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma ameramba matapishi yake mwenyewe. Amegeuka.
Hamza ameivua Marekani na tuhuma alizoitupia pale aliposema hadharani kuwa nchi hiyo imehusika katika matukio ya milipuko ya mabomu iliyokuwa yameshamiri kisiwani Pemba.
Japo amefanya hivyo kwa kuzidisha udanganyifu – akidai kwamba yeye hajawahi kusema wamehusika – bado ukweli unabaki palepale kwamba “amejirudi kwenye uhalisia wa mambo.”
Hamza alitamka hadharani na kukaririwa na vyombo vya habari ikiwemo Televisheni ya Serikali ya Mapinduzi, TVZ, akiituhumu serikali ya Marekani kufahamu kinachoendelea Pemba wakati wa uandikishaji wapiga kura, baada ya nchi hiyo kutoa taarifa kwa raia zake wasifike Pemba kwa kuwa yanayotokea yanaashiria ukosefu wa amani.
Taarifa ya ilani ya Marekani iliyotolewa na Wizara ya Mambo ya Nje (State Department) mjini Washington na nakala ya taarifa hiyo kupatikana mjini Zanzibar, ilisema wazi kuwa ilitokana na utafiti walioufanya.
Lakini hata pale msemaji wa wizara hiyo alipotoa taarifa ya pili akirejelea matamshi ya ovyo ya Hamza, alisisitiza kuwa Marekani imechukua hatua hiyo kwa maslahi ya raia zake wala haikuhitaji kumuuliza kiongozi yeyote wa Tanzania.
Bila ya shaka matamshi ya ovyo ya Hamza yaliikasirisha Marekani, na hatua hii mpya ya waziri huyo kujirudi ndani ya Baraza la Wawakilishi inaonekana haikuwa hivihivi, bali ni kwa kuzingatia maafikiano ya kidiplomasia kati ya Marekani na Tanzania.
Tatizo la Hamza kuwa hataki kuwa muungwana katika kujirudi. Anajizonga kwa kuanzisha uhasama na vyombo vya habari; eti vilimsingizia. Hivi Hamza asingiziwe ili iwe nini? Anajulikana mkate wake umeongezeka siagi miaka hii kutoka ule wa kutegemea ushoni aliokuwa akitegemea Mikunguni.
Ninaisema kwa makusudi hii ili akae vizuri na mtindo anaouanzisha wa kurudisha lawama kwa wasiohusika kwa kosa alilojitia mwenyewe, tena kwa hiari yake na raha zake.
Lakini hii haikuwa mada yangu, ila nimelazimika kugusia hapo kwa kuwa nilipata kumsihi Hamza kuwa “hayawezi madhambi ya SMZ.”
Leo nikitaka hasa kueleza hofu yangu kwamba kwa kuwa mwenendo wa dola haujabadilika; kwamba haijafuata ukweli kuwa inanyonga haki za wananchi; basi sitarajii mabadiliko yoyote uandikishaji wapiga kura utakapoingia Mkoa wa Mjini Magharibi.
Ni dhahiri kwamba misimamo ya viongozi wa vyama vya upinzani itabaki ileile ya kukataa kushiriki katika mduara wa ushetani wa kuhalalisha maovu yanayotendeka dhidi ya mfumo wa demokrasia.
Ninamaanisha kuwa hawatahamasisha wananchi wanaowatii kujitokeza kwenye vituo vya uandikishaji ili kuandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) la Zanzibar.
Na siyo tu kwamba hawatawahamasisha watu kujitokeza vituoni, bali pia watawaelekeza kujipanga vizuri ili kuzuia wale waliopatiwa kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi wasiandikishwe.
Naiona hali hiyo kwa sababu bado tatizo liliopo – ambalo limekwamisha uandikishaji wenye ufanisi kiasi cha kusikitisha wakuu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kama inavyodhihirika katika taarifa zake kwa umma – halijatatuliwa.
Tatizo ni kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, ambacho kuanzia mwaka 2006, kimeingizwa katika sheria ya uchaguzi kama shurti kwa kila Mzanzibari kukimiliki ndipo atambuliwe na kuandikishwa kama mpiga kura, kingali kinatolewa kibaguzi kwa kuzingatia nani kura yake ataitia kwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Kwa yule ambaye machoni mwa wenye kulea mfumo wa kidhalimu, ataonekana si miongoni mwa wakereketwa au makada wa CCM, itabaki tu kuwa shida kwake kuruhusiwa kupata kitambulisho na hivyo kujikuta hapenyi kwenye wigo wa watu wema.
Kwa mfumo wa utawala uliopo hadi sasa, watu wema ni wale tu ambao hata kama si hadharani, lakini wana sura ya kupigia kura mgombea wa CCM tu na si vinginevyo.
Asiyekuwa na chapa ya CCM kwenye paji lake la uso, ajue kura ya 2010 ataisikia tu. Ataisikia kwa sababu kwa kuwa hana kitambulisho, hatapata kuandikishwa. Asipopata kuandikishwa, hatapata kupiga kura.
Kitambulisho cha Mzanzibari kimekuwa dili. Baada ya kuanza kama maskhara, ingawa kilipingwa kwa nguvu nyingi kwa kuhofiwa kitatumika vibaya, tulipo kishathibitika kuwa kililetwa kwa dhamira mbaya hasa. Ukweli unaonekana.
Kimeshasababisha maelfu ya watu kunyimwa haki yao ya msingi ya kuingia katika daftari la wapiga kura. Hawa wamekalia kuti kavu kwani nafasi kwao kuingia ni sawa na mbuni kupita kwenye tundu la sindano. Labda ipite kudra ya Mwenyezi Mungu kabla ya Oktoba mwakani.
Ikija kudra hiyo basi ndipo ukweli utapodhihiri na uongo utapojitenga. Hapo ndipo mbivu itapoliwa na mbichi itaposubiriwa iwive ili nayo iliwe kwa wakati muafaka. Ni wakati huu nyuso za wakubwa zitakaposinyaa kwa aibu.
Watatahayari maana yale waliyoyapanga kutokea ili kujinufaisha nafsi zao, yatakuwa yametenguka. Ushetani waliolenga kuufanikisha utakuwa umekomeshwa. Wamenyamazishwa. Na hii si wao tu, bali hata mawakala wao wanaojitahidi kutetea wanachokifanya.
Uandikishaji utakapoingia majimbo ya wajanja na “wasemaji ovyo isivyomithilika” watunza takwimu za kupika wanaoishi kwa kujisuta, wataumbuka na kubaki kushangaa. Labda watatamani ardhi ipasuke wajifiche. Labda wataamua kuhama nchi. Sijui.
Tushaona uandikishaji ulivyoleta aibu kwa wakubwa katika majimbo ya Kaskazini Unguja. Tushajionea namna mikakati ya kuvuruga uchaguzi inavyoandaliwa. Tushafahamu kumbe bado wakubwa hawajaamini kuwa siku hazigandi.
Ukweli ni kwamba umma umeelewa dhamira hasa za viongozi wa CCM katika kuitisha uchaguzi. Kumbe ni kiinimacho na jambo la kudanganya ulimwengu. Masikini roho zao hawajui kwamba uchaguzi huru na wa haki si matamshi bali matendo.
Masikini roho zao hawajui kuwa hawana wafichacho. Kila kitu kipo kweupeni zama hizi. Hawajui kuwa ndani ya ofisi za umma wanazotumia kufanikisha udanganyifu wamo watu wema kwa Wazanzibari wenzao na nchi yao waipendayo kama mboni za macho yao.
Masikini roho zao viongozi hawa wahafidhina hawajui kwamba kwa sasa wanapuruziwa tu kamba kwani iko siku kila kitu kitabadilika na mambo yatageuka nyuma mbele, na wao watasaga mawe kama alivyofanya firauni na wenzake.
Hata kama si kesho na keshokutwa, hakuna chenye mwanzo kikakosa mwisho. Nasema hakuna kinachodumu milele iwapo binadamu mwenyewe ataukata na kurudi alikotoka. Basi mambo yatabadilika tu Inshaallah

SOURCE:MWANAHALISI

Lisemwalo lipo na kama halipo laja .
 
mnamkumbuka mama mouldin kastiko?

alisema na hakupata kupingwa na viongozi wa SMZ, "sisi tumepindua hatuwezi kutoa nchi kwa vikaratasi".

shida ya zanzibar ni ubaguzi wa rangi, hii ccm na cuf ni uchochoro tu wakupitia. ccm enzi hizo ni asp wanahisi walibaguliwa na ushirika wa znp na zppp wakiongozwa na serikali ya shamte, wakapindua...cuf zanzibar si bara...wanahisi walipinduliwa na kuondolewa madarakani sivyo halali....kilichofuatia mapinduzi...mauaji na unyanyasaji uliofanywa na asp kimeacha makovu mpaka leo...kitu kimoja tu kinaweza kuinusuru zanzibar...south african model...ukweli na maridhiano...watu wakae waangalie historia yao nani alifanya nini na kwanini ijulikane...na kisha wasameheane au adhabu zitolewe..na kisha wakubaliane a way forward...lakini kwa kura katu...
 
Iam dying to see such beautiful changes in my age!
Mungu ibariki Zanzibar!...Tunangoja hiyo HESHIMA ya juu kwa hamu!
 
mnamkumbuka mama mouldin kastiko?

alisema na hakupata kupingwa na viongozi wa SMZ, "sisi tumepindua hatuwezi kutoa nchi kwa vikaratasi".

shida ya zanzibar ni ubaguzi wa rangi, hii ccm na cuf ni uchochoro tu wakupitia. ccm enzi hizo ni asp wanahisi walibaguliwa na ushirika wa znp na zppp wakiongozwa na serikali ya shamte, wakapindua...cuf zanzibar si bara...wanahisi walipinduliwa na kuondolewa madarakani sivyo halali....kilichofuatia mapinduzi...mauaji na unyanyasaji uliofanywa na asp kimeacha makovu mpaka leo...kitu kimoja tu kinaweza kuinusuru zanzibar...south african model...ukweli na maridhiano...watu wakae waangalie historia yao nani alifanya nini na kwanini ijulikane...na kisha wasameheane au adhabu zitolewe..na kisha wakubaliane a way forward...lakini kwa kura katu...
WW unaongea uwongo hapa...kwanza aliyesema maneno hayo si Moudline Castico bali ni Asha Bakari Makame ambaye sasa ni Mwenyikiti wa UWT(kama sijakosea), pili ni unafiki na upotofu kudai kuwa eti CUF ndio waliopinduliwa 1964...CUF haijawahi kushika madaraka...ila wamewahi kushinda uchaguzi mwaka 1995 n.k hawakupewa nchi...mawazo potofu kama yako ya kuhusisha mfumo wa vyama vingi wa sasa na historia za Mapinduzi,ujio wa CUF na uhuisano na ZNP&ZPPP na matatizo ya kisiasa ya sasa na historia hiyo ni unafiki ambao mtu wa mwanzo kuu-document...uzandiki huo ni Omar Ramadhani Mapuri...na ndiye mtu wa mwanzo aliyeleta siasa za kibaguzi za Uunguja na Upemba ambazo hazikuwa maarufu hata vipi katika kabla ya mfumo wa vyama vingi kurejeshwa mwaka 1991. Mapuri aliueneza na kuusambaza uongo wake kupitia kitabu chake cha historia ya Mapinduzi kiitacho "1964 Revolution and Its Achievements" humo mna mawazo kama hayo uliyoyaandika hapo juu na unafiki wa kugeuza akili za watu kuamini kuwa CUF wamekuja kulipa kisasi cha yaliyotokezea 1964, wakati hilo siyo lengo la kurejeshwa mfumo wa vyama vingi kwa mujibu wa katiba na CUF ni chama kiichosajiliwa kwa mujibu wa sheria za kuanzishwa mfumo huo kama vyama vyengine vyote, sasa nashangaa habari za "uhizbu" na "u-afroshirazi" zinakujaje tena!
Mimi nilifikiri kadiri wazanzibar wanavyoelewa madhumuni ya mfumo wa vyama vingi kwa kadiri siku zinavyokwenda wameelewa sasa kuwa kumbe habari zile za Omar Mapuri zilikuwa ni uongo uliokusudia kujenga chuki na uhasama kati ya watu wa Unguja na Pemba ambao wameishi miaka yote hiyo hata baada ya Mapinduzi kwa udugu wa kufa na kuzikana.
you will die without it!:D
Wewe tunakujuwa bana umenyweshwa maji ya rangi ya kijani..kwa hiyo bado una waza "chanikiwichi" ie photosynthes
 
you will die without it!:D

Hata mimi nna matumaini sitofariki Zanzibar itakuwa ishajitoa katika makucha ya Tanganyika....kama itatokezea struggle hii kutofanikiwa hadi nikifariki basi wanangu wataendeleza vita hii dhidi ya Tanganyika.

Tena bado wazanzibari hatujaanza na sera za Jihaad...tunavuta subra kidogo, lakini kujiripua mabomu hapo Manzese na Ilala ni halali kabisa!
 
Wamebakiza siku kidoooogo tu...karibuni tu Wazanzibar watatoka katika utawala wa kidhalimu wa CCM...Itabaki historia tu, karibuni waungwana...bendera ya utu wenu karibu itapepea...chem chem za muruwa wenu zimeanza kutiririka...hofu zenu zimeanza kupata tiba na utulivu wa nafsi unachukuwa nafasi...waungwana wamekupokeeni, karibuni Zanzibar...karibuni nchi yenu mliyoijenga kwa kucha na meno, mkatolewa kwa dhulma na shinde...rejeeni mkiwa mashujaa na watoto walee wanakusubirini kukupokeeni...karibuni sana tu.
Du!!!Waota ndoto za Nchana wewe.
 
Dodoma ndo mahala kwenu na huko ndo mustakabari wa Tz na Zanzibar unakopatikana,subirini muda tu CC ya CCM iwasaidie kupata rais
 
Hata mimi nna matumaini sitofariki Zanzibar itakuwa ishajitoa katika makucha ya Tanganyika....kama itatokezea struggle hii kutofanikiwa hadi nikifariki basi wanangu wataendeleza vita hii dhidi ya Tanganyika.

Tena bado wazanzibari hatujaanza na sera za Jihaad...tunavuta subra kidogo, lakini kujiripua mabomu hapo Manzese na Ilala ni halali kabisa!

Mh! Haya bwana.
 
Hivi wa zenji hamuwezi kujiamria mambo yanu mpaka mje Dodoma ndo mpangiwe flani awe rais?
 
Hata mimi nna matumaini sitofariki Zanzibar itakuwa ishajitoa katika makucha ya Tanganyika....kama itatokezea struggle hii kutofanikiwa hadi nikifariki basi wanangu wataendeleza vita hii dhidi ya Tanganyika.

Tena bado wazanzibari hatujaanza na sera za Jihaad...tunavuta subra kidogo, lakini kujiripua mabomu hapo Manzese na Ilala ni halali kabisa!
mbongo gani utamvalisha bomu??????? labda uanzishe chuo uanze kuwapiga sound hao wenzako kwanza
 
Dodoma ndo mahala kwenu na huko ndo mustakabari wa Tz na Zanzibar unakopatikana,subirini muda tu CC ya CCM iwasaidie kupata rais
Naomba unieleimishe yakhe. Hiyo CC ya CCM ni ipi na mchanganuo wa wajumbe wake uko vipi. Wewe unafahamu kuwa wamo wa kwetu humo katika CC. Na wakisema hawataki basi CC yako haiwezi kuamua dhidhi ya wasichokitaka? Historia ya za zama Nyerere ziweke kando ndugu yangu. CC yako haina ubavu kwa msimamo wa Zanzibar.. Hivi hujaelewa tu . Tafakari ya Dodoma na kadhia ya Muwafaka.
 
Back
Top Bottom