kajukeg
Member
- Jul 22, 2010
- 39
- 0
Wapendwa wana jamvi jana ilikuwa ni siku ya mashujaa wa tanzania,kila mtanzania mwenye damu ya kitanzania alikuwa na fursa ya kukumbuka watu muhimu waliolipigania taifa letu kiasi cha hata kupoteza maisha yao.
nilikuwa nasikiliza hotuba ya mkuu wa inchi wa wakati ule hayati baba wa taifa mwl nyerere alioitowa wakati akilihutubia taifa kwenye uwanja wa taifa dar ktk siku ya mashujaa mwaka 1979.
moja kati nukuu zake muhimu ambazo zimepelekea mimi kuguswa na kuandika ujumbe huu ni hii; nanukuu,
"Katika vita hii kuna wengine wamerudi wengine hawakurudi,wengine wamerudi na majerha makubwa ambayo wengi wao wametibiwa na wamepona na wamerudi majumbani mwao lakini wengine wamepata vilema vya maisha hawatapona kabisa,hivyo jukumu la maisha yao ya baadaye ni jukumu letu.na wale ambao hawakurudi kabisa mwenyezi mungu azilaze roho za marehemu mahali pema,tunatoa pole kwa ndugu wa marehemu mana huzuni yao ni yetu pia na msiba wao ni wetu pia na jukumu la maisha yao ya baadae ni jukumu letu" mwisho wa kunukuu.
swali langu linakuja hapo ni kweli kwamba waathirika hawa waliopata vilema vya maisha pamoja na ndugu wa waliopoteza maisha ktk vita hivyo bado wanahudumiwa ipasavyo mpaka leo na serikali yetu,ama kauli ile ya mwl iliishia siku ilelile pale uwanja wa taifa? ama wahusika wote hawapo tena duniani,ama ndo ukweli wa usemi usemao ' waache wafu wawazike wafu wenzao ndo unaendelea'
Tujadili ndugu zangu.
nilikuwa nasikiliza hotuba ya mkuu wa inchi wa wakati ule hayati baba wa taifa mwl nyerere alioitowa wakati akilihutubia taifa kwenye uwanja wa taifa dar ktk siku ya mashujaa mwaka 1979.
moja kati nukuu zake muhimu ambazo zimepelekea mimi kuguswa na kuandika ujumbe huu ni hii; nanukuu,
"Katika vita hii kuna wengine wamerudi wengine hawakurudi,wengine wamerudi na majerha makubwa ambayo wengi wao wametibiwa na wamepona na wamerudi majumbani mwao lakini wengine wamepata vilema vya maisha hawatapona kabisa,hivyo jukumu la maisha yao ya baadaye ni jukumu letu.na wale ambao hawakurudi kabisa mwenyezi mungu azilaze roho za marehemu mahali pema,tunatoa pole kwa ndugu wa marehemu mana huzuni yao ni yetu pia na msiba wao ni wetu pia na jukumu la maisha yao ya baadae ni jukumu letu" mwisho wa kunukuu.
swali langu linakuja hapo ni kweli kwamba waathirika hawa waliopata vilema vya maisha pamoja na ndugu wa waliopoteza maisha ktk vita hivyo bado wanahudumiwa ipasavyo mpaka leo na serikali yetu,ama kauli ile ya mwl iliishia siku ilelile pale uwanja wa taifa? ama wahusika wote hawapo tena duniani,ama ndo ukweli wa usemi usemao ' waache wafu wawazike wafu wenzao ndo unaendelea'
Tujadili ndugu zangu.