Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Naamini kuwa siku ya kuikomboa Tanzania sio siku ile CCM itakapong'olewa madarakani, au siku ile CHADEMA watakaposhika dola bali siku ya kuikomboa Tanzania ni siku ile watanzania tutakapoanza kuwaza na kufikiri zaidi ya hawa viongozi wetu wa kisiasa, siku ile ambayo wanachadema watawaza na kutafakari zaidi ya Mbowe, Dr Slaa, Lissu, Lema, Zitto n.k na pale wana ccm watakapowaza zaidi ya Dr Kikwete,Lowasa, Nape, Mukama n.k.
siku ambayo wote tutawaza kama binadamu na sio kama watu, siku tutakayowaza kama watanzania wenye uwezo wa kuwaza wenyewe bila msaada wa mtu yeyote.
siku ambayo tutakubali kuyakubali mawazo yote mazuri bila kuangalia yametolewa na nani! SIKU HIYO IKIFIKA NDIYO ITAKUWA SIKU YA KUIKOMBOA TANZANIA, NA SIO HAYA MAIGIZO YASIYO NA FAIDA YA UKOMBOZI YA CCM, CHADEMA, CUF N.K TUNAYOYAONA KILA SIKU.
siku ambayo wote tutawaza kama binadamu na sio kama watu, siku tutakayowaza kama watanzania wenye uwezo wa kuwaza wenyewe bila msaada wa mtu yeyote.
siku ambayo tutakubali kuyakubali mawazo yote mazuri bila kuangalia yametolewa na nani! SIKU HIYO IKIFIKA NDIYO ITAKUWA SIKU YA KUIKOMBOA TANZANIA, NA SIO HAYA MAIGIZO YASIYO NA FAIDA YA UKOMBOZI YA CCM, CHADEMA, CUF N.K TUNAYOYAONA KILA SIKU.