Mnyonge Namba1
JF-Expert Member
- Jan 27, 2012
- 402
- 81
WanaJF, Kutokana na muungano wa Znz na Tanganyika kutokuwa na maslahi ya kijamii kwa pande zote mbili,binafsi na kwa hiari yangu mwenyewe nimeamua kutopumzika 26Aprili miaka yote kuanzia 2012.Nitakuwa nashinda shambani kulima kwa nguvu huku nikiiwaza Tanganyika iliyozikwa kwenye kivuli cha muungano wenye maslahi ya sisiem na sio ya jamii ya Wafugaji,Wakulima Wavuvi,Wachimbaji nk wanaozidi kuwa maskini kila uchao.Sababu kuu ni 1.Znz ipo na Tanganyika haipo 2.Watu wa Znz hawamuheshimu Baba wa Taifa"huwa wanatuambia'BABA YENU NYERERE' na sio Mwl Nyerere au Baba wa taifa"Dharau kubwa sana hii 3.Kuanzia sasa wanaleta ubaguzi kwenye ajira huko visiwani wakati wao huku bara wapo kwenye taasisi nyingi tu mfano airport,TMA,Mawizarani nk.Kwa ufupi tunanyonywa lakini sie tunaelekea kukatiwa mrija kule zenj. HUU NI MSIMAMO WANGU KAMA MTANGANYIKA ALIYEPORWA NCHI YAKE MWAKA 1964. Naomba Wazalendo Tuungane katika kuupinga Muungano huu feki. NAWASILISHA KWENU