Nilizoea kusikia kauli za msichanganye dini na siasa kwa kasi kipindi chote kabla ya mwaka 2005, viongozi wa serikali , dini walisimama imara kuwakemea mashehe wakiwatuhumu moja kwa moja kuacha kujadili siasa misikitini. Kipindi hicho ufisadi uliokuwa ukifanywa na viongozi wa kisiasa haukuwa miongoni mwa mada za kujadiliwa, na watu waliojaribu kujadili walikemewa kutochanganya siasa na dini.
Nakumbuka mambo kadhaa ya kifisadi yalitendeka ambayo yamekuja kuwekwa bayana kipindi cha awamu ya 4 ya JK yakiwemo:
Hivi karibuni nimesoma tena Mwanachi, Maaskofu sasa wambana JK , ndani yake kuna masuala ya kisiasa ambayo bila shaka yaliyojadiliwa kanisani au viunga vyake.
Wapo wapi viongozi waliokuwa wanawakemea Mashehe wasijadili Siasa ?
Wapo wapi wazee wa Msichanganye dini na Siasa?
Nakumbuka mambo kadhaa ya kifisadi yalitendeka ambayo yamekuja kuwekwa bayana kipindi cha awamu ya 4 ya JK yakiwemo:
- Ununuzi tata wa Rada (watanzania acheni uvivu wa kufikiri)
- Ununuzi tata wa ndege ya rais(hata mkila majani ndege ya rais itanunuliwa)
- Meremeta
- Mikataba mibovu ya madini ,ambayo ilifanywa kuwa siri awamu iliyopita,
- Kuuzwa kwa bei ya kutupa NBC, na ubinafsishaji tata wa Shirika la Reli
- Mkapa kujimilikisha mradi wa kiwira.
- Kuuza Nyumba za serikali kwa bei ya kutupa
- EPA saga
- Ujambazi uliokithiri (umehusishwa na viongozi wa jeshi na watawala ref. hotuba ya Mkapa Hakuna nchi isiyokuwa na majambazi, Marekani, Uingereza ..
- N.k, N,k
Hivi karibuni nimesoma tena Mwanachi, Maaskofu sasa wambana JK , ndani yake kuna masuala ya kisiasa ambayo bila shaka yaliyojadiliwa kanisani au viunga vyake.
Wapo wapi viongozi waliokuwa wanawakemea Mashehe wasijadili Siasa ?
Wapo wapi wazee wa Msichanganye dini na Siasa?