Siku 30 Nzito za Maisha Yangu. ooh, Glory to God!!!

Ms Judith

JF-Expert Member
Dec 24, 2010
2,563
918
wapendwa,

niko chumani kwangu saa hizi na nahisi pumzi zinataka kukauka. nina mchanganyiko wa wasiwasi na matumaini, japo najiamini kwa hili ninalotarajia kulifanya, lakini tashwishi na mchecheto vinanizinga, nimeona niwashirikishe huenda nikapata tafu japo kidogo!!

ni kwamba baada ya siku 30 zijazo yaani jumatano ya tarehe 1 june 2011, nitamuarifu rasmi kijana mmoja kuwa nimemteua kuwa mchumba wangu!!!

ni uamuzi mgumu na mzito sana kwangu mimi binafsi. kijana huyu nimemfahamu tangu mwaka 2006 alipoanza kunitaka mapenzi, tumezunguka naye sana katika mitaa ya mapenzi huku nikihakikisha kuwa anaupata moyo wangu kikamilifu japo mwili wangu sikumruhusu kuufunua. kwa kweli tumehangaika naye sana na tumewahi "kukosana" naye mara kadhaa kisha tunarudiana. natumaini mnanielewa vyema ninaongea nini hasa ninaposema "kukosana"

baada ya misukosuko yote, hatimaye alinielewa vyema nami nikamuelewa, sasa kila kilichokuwa kinazuia sisi kuwa mwili mmoja kimeondoshwa kwa neema za Mungu. nimeamua kuwa June mosi nitamthibitishia kuwa ndiye mume wa ndoto zangu. naam, mume wa ujana wangu! kama hatakuwa na objection, siku ya jumamosi ya tarehe 4 June, nitamtambulisha nyumbani kwetu na kumtaka naye apange siku ya kunipeleka na kunitambulisha kwao. kama mambo yataenda kama ninavyoomba, ndoa itafungwa mwezi october au novemba 2011!!

sasa nadhani mnaweza kuuhisi wakati niliomo ni wa aina gani.

naomba maombi yenu wote tuweze kuvuka salama. mimi naanza maombi mazito mfululizo kumkabidhi Mungu siku hizi zote 30 (and beyond) aziratibu mwenyewe kwa kadiri ya wingi wa rehema na fadhili zake

Mungu awabariki sana

mpenzi wenu Miss Judith (Mrs mtarajiwa)

Glory to God!
 
wapendwa,

niko chumani kwangu saa hizi na nahisi pumzi zinataka kukauka. nina mchanganyiko wa wasiwasi na matumaini, japo najiamini kwa hili ninalotarajia kulifanya, lakini tashwishi na mchecheto vinanizinga, nimeona niwashirikishe huenda nikapata tafu japo kidogo!!

ni kwamba baada ya siku 30 zijazo yaani jumatano ya tarehe 1 june 2011, nitamuarifu rasmi kijana mmoja kuwa nimemteua kuwa mchumba wangu!!!

ni uamuzi mgumu na mzito sana kwangu mimi binafsi. kijana huyu nimemfahamu tangu mwaka 2006 alipoanza kunitaka mapenzi, tumezunguka naye sana katika mitaa ya mapenzi huku nikihakikisha kuwa anaupata moyo wangu kikamilifu japo mwili wangu sikumruhusu kuufunua. kwa kweli tumehangaika naye sana na tumewahi "kukosana" naye mara kadhaa kisha tunarudiana. natumaini mnanielewa vyema ninaongea nini hasa ninaposema "kukosana"

baada ya misukosuko yote, hatimaye alinielewa vyema nami nikamuelewa, sasa kila kilichokuwa kinazuia sisi kuwa mwili mmoja kimeondoshwa kwa neema za Mungu. nimeamua kuwa June mosi nitamthibitishia kuwa ndiye mume wa ndoto zangu. naam, mume wa ujana wangu! kama hatakuwa na objection, siku ya jumamosi ya tarehe 4 June, nitamtambulisha nyumbani kwetu na kumtaka naye apange siku ya kunipeleka na kunitambulisha kwao. kama mambo yataenda kama ninavyoomba, ndoa itafungwa mwezi october au novemba 2011!!

sasa nadhani mnaweza kuuhisi wakati niliomo ni wa aina gani.

naomba maombi yenu wote tuweze kuvuka salama. mimi naanza maombi mazito mfululizo kumkabidhi Mungu siku hizi zote 30 (and beyond) aziratibu mwenyewe kwa kadiri ya wingi wa rehema na fadhili zake

Mungu awabariki sana

mpenzi wenu Miss Judith (Mrs mtarajiwa)

Glory to God!

Samahani judith,
kuna mahali sijakuelewa,
ina maana wewe ndiyo unaanza kumwambia kuwa umemteua kuwa awe mumeo?,
tarehe mwezi wa ndoa umeupanga mwenyewe hata kabla yeye hajathibitisha kama naye amekuteua kuwa mke wake?,hapo kwenye blue pameonesha hivyo.
kwa kusoma maelezo hayo naona kama kila kitu umekipanga wewe,


SIjakuelewa kabisa, nahis ksb ya utu uzima,
akili inachukua muda mrefu kuelewa mambo,
naomba nidadavulie kidogo mdogo wangu....lol
 
Samahani judith,
kuna mahali sijakuelewa,
ina maana wewe ndiyo unaanza kumwambia kuwa umemteua kuwa awe mumeo?,
tarehe mwezi wa ndoa umeupanga mwenyewe hata kabla yeye hajathibitisha kama naye amekuteua kuwa mke wake?,hapo kwenye blue pameonesha hivyo.
kwa kusoma maelezo hayo naona kama kila kitu umekipanga wewe,


SIjakuelewa kabisa, nahis ksb ya utu uzima,
akili inachukua muda mrefu kuelewa mambo,
naomba nidadavulie kidogo mdogo wangu....lol

Hehehehhe zoea bwana maana siku hizi hata wasichana wanaomba uchumba!!
Nadhani bibie amepanga hayo yote akiwa anaamini kwamba yote waliyopitia pamoja yalikua yanawaelekeza kwa hicho kinachowezekana wote wanakitaka!!Kupanga tarehe japo ni too much kwa mapema hii nadhani inaonyesha tu ni jinsi gani yuko tayari kua na huyo kijana!!
 
hongera mamaa km utamwambia yote uliyopanga nae akaitikia ndio mzee nitakuita mwanamke mwenye bahati........swali la kizushi....umesema hujawahi kumpa hata sikumoja je nawewe hujawahi kutoa huko nyuma yeye ndio atakuwa wa kwanza?........tafadhali miss judy nijibu hapo...!
 
Hehehehhe zoea bwana maana siku hizi hata wasichana wanaomba uchumba!!
Nadhani bibie amepanga hayo yote akiwa anaamini kwamba yote waliyopitia pamoja yalikua yanawaelekeza kwa hicho kinachowezekana wote wanakitaka!!Kupanga tarehe japo ni too much kwa mapema hii nadhani inaonyesha tu ni jinsi gani yuko tayari kua na huyo kijana!!

Mmmh! haya LIZZY nimekuelewa,
itabidi nianze kuelewa manake ndiyo mambo ya kisasa haya,
siye wazee wa zamani tulikuwa tunasubiri kutamkiwa kila kitu,
na mwanaume, lakin sasa inaonesha wanaume wa sasa hivi wanachukua muda sana,
kuwatamkia wanetu au wadogo zetu wa kike mnaamua kujitoa KIMASOMASO.

NAOMBA NISEME HONGERA JUDITH, ALL THE BEST,
Lizzy keshanitoa tongotongo la uelewa.....lol
 
Nakukubali pale ambapo unamshirikisha Mungu '30 days" i like it kama ni ni mpango wa Mungu no one to object it. Kila la kheri! May God enlighten your path!
 
wapendwa,

niko chumani kwangu saa hizi na nahisi pumzi zinataka kukauka. nina mchanganyiko wa wasiwasi na matumaini,
Aisee...hakikisha unakunywa maji ya kutosha na chumba kiwe na hewa kwa wingi...

ni uamuzi mgumu na mzito sana kwangu mimi binafsi. kijana huyu nimemfahamu tangu mwaka 2006 alipoanza kunitaka mapenzi
,

Huyo jamaa ana moyo sana, miaka 5...nadhani kwenye akili yake anajua wewe ni girlfriend wake, na sijui ana miaka mingapi?
tumezunguka naye sana katika mitaa ya mapenzi
Sidhani kama ni uamuzi mgumu ukiwa 'umezunguka' naye sana

jumamosi ya tarehe 4 June, nitamtambulisha nyumbani kwetu na kumtaka naye apange siku ya kunipeleka na kunitambulisha kwao.
Hapo umeamua jambo zuri sana, tena sana, hongera kwa kuweka mambo wazi
kama mambo yataenda kama ninavyoomba, ndoa itafungwa mwezi october au novemba 2011!!

Mbona una haraka hivyo?? wewe ndo unamlipia mahari..au mlishapanga kwamba muoane tarehe hiyo...mbona humpi nafasi huyo mume mtarajiwa hata ya kupumua..naona unaamua wewe tu..duh

naomba maombi yenu wote tuweze kuvuka salama. mimi naanza maombi mazito mfululizo kumkabidhi Mungu siku hizi zote 30 (and beyond) aziratibu mwenyewe kwa kadiri ya wingi wa rehema na fadhili zake
Mungu awabariki sana

mpenzi wenu Miss Judith (Mrs mtarajiwa)

Tutakuombea sana tu..tena sana..
 
Aisee...hakikisha unakunywa maji ya kutosha na chumba kiwe na hewa kwa wingi...


,

Huyo jamaa ana moyo sana, miaka 5...nadhani kwenye akili yake anajua wewe ni girlfriend wake, na sijui ana miaka mingapi?

Sidhani kama ni uamuzi mgumu ukiwa 'umezunguka' naye sana


Hapo umeamua jambo zuri sana, tena sana, hongera kwa kuweka mambo wazi


Mbona una haraka hivyo?? wewe ndo unamlipia mahari..au mlishapanga kwamba muoane tarehe hiyo...mbona humpi nafasi huyo mume mtarajiwa hata ya kupumua..naona unaamua wewe tu..duh



Tutakuombea sana tu..tena sana..

Nilijua ukija tu lazima umwage hekima zako . . . .
 
Hongera mwaya kwa kufikia uamuzi huo na kila la kheri katika kumfikishia mhusika habari hizo zinazoweza kua njema sana kwake!!
Nawaombea yote yaliyo mema!!!

asante sana dada mpenzi, tuendelee kuombeana

Samahani judith,
kuna mahali sijakuelewa,
ina maana wewe ndiyo unaanza kumwambia kuwa umemteua kuwa awe mumeo?,
tarehe mwezi wa ndoa umeupanga mwenyewe hata kabla yeye hajathibitisha kama naye amekuteua kuwa mke wake?,hapo kwenye blue pameonesha hivyo.
kwa kusoma maelezo hayo naona kama kila kitu umekipanga wewe,


SIjakuelewa kabisa, nahis ksb ya utu uzima,
akili inachukua muda mrefu kuelewa mambo,
naomba nidadavulie kidogo mdogo wangu....lol

ni kwamab kutokana na haiba yangu nina marafiki wengi sana wake kwa waume na siku zote niliamini kuwa mchumba wangu nitamteua (kwa kumkubali) kutoka miongoni mwa marafiki zangu. kama nilivyoeleza, huyu ninayekusudia kumteua alikuwa rafiki yangu toka 2006 na ni mmoja tu kati ya wengi kiasi waliotokea kunipenda kwa dhati maishani mwangu. sio kuwa mimi ndiye ninamuanza (japo kumuanza mie sioni tabu yoyote kama moyo wangu umeridhia) la hasha bali namkubalia ombi lake mwenyewe baada ya miaka kama mitano sasa tangi aliponiomba!! ubarikiwe sana mpendwa

Glory to God!!

Hehehehhe zoea bwana maana siku hizi hata wasichana wanaomba uchumba!!
Nadhani bibie amepanga hayo yote akiwa anaamini kwamba yote waliyopitia pamoja yalikua yanawaelekeza kwa hicho kinachowezekana wote wanakitaka!!Kupanga tarehe japo ni too much kwa mapema hii nadhani inaonyesha tu ni jinsi gani yuko tayari kua na huyo kijana!!

asante sana dada kwa ufafanuzi huu.

ubarikiwe sana

hongera mamaa km utamwambia yote uliyopanga nae akaitikia ndio mzee nitakuita mwanamke mwenye bahati........swali la kizushi....umesema hujawahi kumpa hata sikumoja je nawewe hujawahi kutoa huko nyuma yeye ndio atakuwa wa kwanza?........tafadhali miss judy nijibu hapo...!

ndio maana naomba maombi yenu wote wapendwa wangu

hilo swali la kizushi, kama unatafakari sawasawa, utaona kuwa kama mtu ninayemuomba Mungu aniunganishe naye hakupata fursa ya "kunigusa", basi busara ya kawaida tu itakupa jibu unaloniuliza hapa.

asante na ubarikiwe sana

Mmmh! haya LIZZY nimekuelewa,
itabidi nianze kuelewa manake ndiyo mambo ya kisasa haya,
siye wazee wa zamani tulikuwa tunasubiri kutamkiwa kila kitu,
na mwanaume, lakin sasa inaonesha wanaume wa sasa hivi wanachukua muda sana,
kuwatamkia wanetu au wadogo zetu wa kike mnaamua kujitoa KIMASOMASO.

NAOMBA NISEME HONGERA JUDITH, ALL THE BEST,
Lizzy keshanitoa tongotongo la uelewa.....lol

asante mpendwa kwa maombi yako ya heri.

kama umesoma vizuri, si mimi ninayemtongoza, ila yeye alinitongoza tangu 2006 na mie ndiye niliyekuwa namkatalia hadi malengo fulani yatimie na sasa yametimia na sioni cha kutuzuia tena kuwa mwili mmoja

Glory to God!1

Kila heri, tunakuombea.

asante sana dada yangu.

Mungu akubariki sana
 
Kila la kheri Miss Judith.....Mungu akutimizie hitaji la moyo wako kama ni mapenzi yake. I admire your guts and strength!!
 
1. Ningependa uendelee kuishi katika maisha yakumtukuza Kristo, Mungu awabariki wewe na huyo mume mtarajiwa na kamwe alicho kiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe. Amen

Ningependa...
 
Aisee...hakikisha unakunywa maji ya kutosha na chumba kiwe na hewa kwa wingi...


,

Huyo jamaa ana moyo sana, miaka 5...nadhani kwenye akili yake anajua wewe ni girlfriend wake, na sijui ana miaka mingapi?

Sidhani kama ni uamuzi mgumu ukiwa 'umezunguka' naye sana


Hapo umeamua jambo zuri sana, tena sana, hongera kwa kuweka mambo wazi


Mbona una haraka hivyo?? wewe ndo unamlipia mahari..au mlishapanga kwamba muoane tarehe hiyo...mbona humpi nafasi huyo mume mtarajiwa hata ya kupumua..naona unaamua wewe tu..duh



Tutakuombea sana tu..tena sana..

ndugu mpendwa,

asante sana kwa kunitia nguvu. kuhusu hiyo unayoita haraka sio kuwa nimeisha ipanga tarehe ya harusi. kama umesoma vizuri umeona kuwa nimesema kuwa "kama mambo yataenda kama ninavyoomba, ndoa itafungwa mwezi october au novemba 2011!!' manake ni kwamaba hiyo october au november 2011 ni maombi yangu tu. tarehe halisi itategemeana na mambo memngine na ndio maana nawaalika tombeane.

ubarikiwe sana
 
asante sana dada mpenzi, tuendelee kuombeana



ni kwamab kutokana na haiba yangu nina marafiki wengi sana wake kwa waume na siku zote niliamini kuwa mchumba wangu nitamteua (kwa kumkubali) kutoka miongoni mwa marafiki zangu. kama nilivyoeleza, huyu ninayekusudia kumteua alikuwa rafiki yangu toka 2006 na ni mmoja tu kati ya wengi kiasi waliotokea kunipenda kwa dhati maishani mwangu. sio kuwa mimi ndiye ninamuanza (japo kumuanza mie sioni tabu yoyote kama moyo wangu umeridhia) la hasha bali namkubalia ombi lake mwenyewe baada ya miaka kama mitano sasa tangi aliponiomba!! ubarikiwe sana mpendwa

Glory to God!!



asante sana dada kwa ufafanuzi huu.

ubarikiwe sana



ndio maana naomba maombi yenu wote wapendwa wangu

hilo swali la kizushi, kama unatafakari sawasawa, utaona kuwa kama mtu ninayemuomba Mungu aniunganishe naye hakupata fursa ya "kunigusa", basi busara ya kawaida tu itakupa jibu unaloniuliza hapa.

asante na ubarikiwe sana



asante mpendwa kwa maombi yako ya heri.

kama umesoma vizuri, si mimi ninayemtongoza, ila yeye alinitongoza tangu 2006 na mie ndiye niliyekuwa namkatalia hadi malengo fulani yatimie na sasa yametimia na sioni cha kutuzuia tena kuwa mwili mmoja

Glory to God!1



asante sana dada yangu.

Mungu akubariki sana


Hongera judith, kwa hiyo forms tayari zimefungwa no more maombi, kura tayari na mgombea tayari kapatikana, mvua tano si mchezo ina mana wakati Mkulu yuko first term jamaa nae kaanza kampeni....ngoma nzito kweli...
 
1. Ningependa uendelee kuishi katika maisha yakumtukuza Kristo, Mungu awabariki wewe na huyo mume mtarajiwa na kamwe alicho kiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe. Amen

Ningependa...

mpendwa Chamoto,

ningependa kumshukuru Mungu kwa neema yake kuu juu yangu na katika maisha yangu kuniwezesha kufikia siku hii na uamuzi huu.

ningependa kukuhakikishia kuwa nitaendelea kuishi maisha yakumtukuza Kristo na kwa kweli sioni ni nini kitanitenga na upendo wa Kristo. hakuna njaa, magonjwa wala taabu zozote zitakazonitenga na upendo wake. nimeishajitoa sadaka kwake na kila ninalolifanya ni kwa utukufu wake.

mpendwa, Chamoto, ningependa mimi na wewe sote tumtukuza Mungu katika saa na wakati huu na kulihimidi jina lake takatifu kwa maana yeye katenda mambo makuu na ya ajabu. nikikumbuka kamba za majaribu zilivyonizinga na ujasiri alionijalia hata kuyashinda majaribu yote, nashindwa hata kueleza ukubwa wa neema hii ya ajabu!! naishia tu kusema kuwa nitalihimidi jina lake kila siku na kuliinua katikati ya mataifa kwa maana yeye ametenda mambo yaliyo makuu kupita ufahamu wa akili zetu

ubarikiwe sana mpendwa

ningependa........

kwa kweli, kwa kweli, kwa weli ningependa.............................. looh,

I am paused!!

Glory to God!!
 
Aisee! hii imekaa njema, nakutakia harakati njema na uweze kufikia malengo yako bila vipingamizi vyovyote vile.. Nitakuombea mpendwa..

Kumbe ndo maana PM huwa sijibiwi siku hizi, Lol......
 

Similar Discussions

24 Reactions
Reply
Back
Top Bottom