Sikizeni enyi masheikh na maaskofu!

Yote mnayosema ni ubatili mtupu! Sisi huku mitaani tunapeta tu, wakristo kwa waislamu tunajichanganya bila shida yoyote. Hao Maaskofu na Mashehe ni njaa zao tu zinawasumbua!
 
Yote mnayosema ni ubatili mtupu! Sisi huku mitaani tunapeta tu, wakristo kwa waislamu tunajichanganya bila shida yoyote. Hao Maaskofu na Mashehe ni njaa zao tu zinawasumbua!


umesema jambo moja la kweli sana; yaani kinachofanywa sana siku hizi ni kujaribu kupigania roho za maskini kwa kutumia udini. Lakini, kinachonisumbua mimi zaidi ni ukimya wa watu fulani.
 
[/COLOR]

Wengine wetu hatukufurahishwa na tabia ya maaskofu ya kumtagza mtu kuwa ni chaguo la Mungu.Lakini wao walijua ni kwanini waliamua kufanya hivyo.Kwani nini sasa wamemgeuka? Jibu ni rahisi,walidhani ataendeleza yaleyale ya Nyerere aliyowaahidi wakrsitu kuwa atalipa kanisa fursa maalum(soma kitabu cha Padri John Sivalon cha Siasa za Tz na Kanisa Katoliki). Alipoingia madarakani yeye akajenga nchi ya wote badala ya kujenga kanisa,akaboresha maslahi ya madaktari na manesi hivyo baadhi yao wakaanza kuhama hospitali za kanisa kwenda serikalini,akaanzisha shule za kata zikaonekana ni tishio kwa shule za seminari,akataka kuondoa misamaha ya kodi kwa taasisi za kidni kwani wanazitumia vibaya.Hapo ndo walianza kumchukia lakini wakajificha kwenye kisingizio cha mahakama ya kadhi huku wakijua kuwa hata wakati wanamtangaza chaguo la Mungu kwenye ilani ya uchaguzi kilikuwepo.
Kwa mtazamo wako finyu unadhani kuwa maaskofu wamesoma kuliko mashekh,ni elimu gani unayozungumzia? Muislam hawi sheikh hadi awe amehitimu kiwango fulani cha elimu ya dini ya kiislamu.Kama walivyo maaskofu wengi wenye degree za theolojia pia wako mashekh wengi wenye degree za elimu ya kiislamu,wapo hadi maprofesa na madokta wa elimu ya kiislamu.
Suala sio jk kuwa ikulu kama muislamu suala ni kuona anapigwa vita na maaskofu hadi wameambukiza chuki hata kwa waumini wao kama wewe.Hili waislamu wote wanaliona waliosoma na wasiosoma alike

Kumshika mkono fisadi na kumnadi kuwa panga la zamani makali yale yale

kumtetea Mkapa kwamba tumuache mzee wetu apumzike wakati wakristo kina Mpendazoe Kimaro walisimama kidete Mkapa awajibishwe

kujiuzuru Lowasa ni ajali ya kisiasa

Epa richmond tangold dowans iptl

Na madhaifu mengi yaliyo dhahiri
YOTE HAYO NI KWELI ANAPIGWA VITA NA MAASKOFU? au anajipiga vita mwenyewe hadi waumini wanaona madhaifu hayo labda wewe mpaka uambiwe na shehe hili zuri hili baya huna akili ya kupembua!

MBONA MNATUCHANGANYA?
 
......... wewe hiyo hamna ! .......... mbingu na ardhi hutetemeka kwa kumwita "mtu" ni MUNGU !!!

Dogo maalim Kombo mbona mbingu na nchi haija tetemeka na watu toka zama za mtume mpaka mtume kafa bado watu wana itikadi hivyo? na Allaah haja warudi au kwa sababu wanasema NI MTU KWELI NA MUNGU KWELI?

Achana na hizo tuungane tujadili hatma yetu na vizazi vijavyo!
 
Huu utapiamlo wa udini utaifikisha wapi Tanzania? Viongozi wa kweli wa kidini hawaweki maslahi binafsi mbele, kinachoongelewa hapa ni ubinafsi tu hakuna dini, viongozi wa kweli wa kidini hukemea maovu bila kujali nani anaongoza, uraisi wa Kikwete unamnufaisha vipi muislamu wa kawaida? Watanzania wengi wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha badala ya kuongelea masula ya kimsingi, tunakwepesha hoja na kuangelea mambo ambayo hayana maslahi kitaifa. Dini ina nafasi yake ndani ya jamii lakini ni hatari inapotumika kuendeleza maovu. Tuangalie mfano hai Tunisia waliomuondoa madarakani Beni Alli si waislamu bali watunisia waliopinga udhalimu wake. Dini na siasa haviendi pamoja, mashekhe na maaskofu/mapadri mnaotaka kujiingiza kwenye siasa vueni kanzu na majoho vinginevyo mtakuwa wanafiki.
 
Yote mnayosema ni ubatili mtupu! Sisi huku mitaani tunapeta tu, wakristo kwa waislamu tunajichanganya bila shida yoyote. Hao Maaskofu na Mashehe ni njaa zao tu zinawasumbua!

kweli kabisa..
 
Ni ukweli usiopingika kuwa watanzania wengi wamepata mwamko wa kutafuta na kuhoji mambo mbalimbali yanayoendelea katika serikali yao baada ya uongozi wa mkapa. Nadhani hii ni baada ya uhuru mkubwa wa vyombo vya habari katika uongozi wa kikwete. Katika uongozi wa Nyerere na Mwinyi hakuna anayezungumzia madudu yaliyokuwa yanafanywa na serikali zoa akiwemo mwanakijiji. Napenda kumkumbusha ndugu mwanakijiji kwamba, kabla maaskofu hawajasimama na kuomba radhi kwa kutozungumzia mauaji ya pemba na mwembechai, Wkristo na waislam wote waombe radhi kwa kutozungumza chochote katika uongozi wa Nyerere na Mwinyi, baadae ndio wakristo waombe radhi kwa kutowazungumzia wa mwembechai na pemba. Lakini, Ni kwanini waislam wanaangalia udini wa viongozi katika kukemea na wasiwakemee kama viongozi wa werikali bila kuangalia ni dini gani?? Kwanini tusiangaliane na kukemeana kama watanzania badala ya kuangalia dini zetu? Waislam ni moja ya jamii zilizoumizwa na uongozi fisadi wa mkapa, kwanini wasimkemee kama kiongozi wao wanasubiri wakristo wamkemee kama mkristo? Huu ni ujinga na udini usio na maana.
 
Kumshika mkono fisadi na kumnadi kuwa panga la zamani makali yale yale

kumtetea Mkapa kwamba tumuache mzee wetu apumzike wakati wakristo kina Mpendazoe Kimaro walisimama kidete Mkapa awajibishwe

kujiuzuru Lowasa ni ajali ya kisiasa

Epa richmond tangold dowans iptl

Na madhaifu mengi yaliyo dhahiri
YOTE HAYO NI KWELI ANAPIGWA VITA NA MAASKOFU? au anajipiga vita mwenyewe hadi waumini wanaona madhaifu hayo labda wewe mpaka uambiwe na shehe hili zuri hili baya huna akili ya kupembua!

MBONA MNATUCHANGANYA?
Kawni mwenzangu una kiwango gani cha elimu?
Tz tunatumia sheria za muingereza amabzo mtu yeyote hana hatia mpaka apatikani na kosa na mahakama (Every body is innocent until proved guilty). Ktk nchi inayofuata utawala wa sheria kama tz ni makosa kuwahukumu akina Mramba na wenzake kuwa ni mafisadi wakati mahakama haijathibitisha hilo.

Jk alichokifanya ni kuwapeleka mahakamani,tambua kuwa katika utawala wa sheria Rais hatakiwi kuingilia mahakama kwani ni mihimili tofauti.Kazi ya mahakama ni kuwahukumu. Lakini wengine wenu kwa ufinyu wa uelewa mnataka jk awaweke ndani tu kwa tuhuma,huo si utawala wa sheria.
Suala la maaskofu kumpiga vita jk hilo sio siri kwani hatuishi mbinguni tunaishi hapahapa tz tunapata habari yanayoongelewa makanisani,kumbuka tuna mchanganyiko wa familia moja kukuta waumini wa dini mbalimbali hivyo kuna mambo ambayo ni vigumu ndugu yako wa damu kukuficha hata kama mko dini tofauti.Mbona sijawahi sikia maaskofu wakisimama na kusema kuwa Mkapa ashitakiwe kwa makosa aliyofanya akiwa Rais?
 
Kwenye hili la maslahi ya kitaifa masheikh watoeni,kwenye maslahi ya waislamu pekee na dini yao..........count them in! Wao wanaamini shida walizonazo zinatokana na wao kuwa waislamu na kutokupewa haki sawa kwa kuwa wao ni waislamu na si kama watanzania as if shida zimegawanyika kutokana na dini au effect za ufisadi zinaenda kwa watu wa dini fulani tu.
Maaskofu tuko nao kwenye maslahi ya kitaifa na ya kujenga roho,sasa sioni wapi watakutana???wawe na sauti moja. kila mmoja ana priority na kufikia malengo yao kuna wanaotumia akili na busara na wapo wanaotumia hisia.:A S 39:

Kwa mtizamo wangu "Ni heri kinachoua MWILI ambao hata hivyo UTAKUFA kuliko kinachoua ROHO ambayo haifi". SUALA LA USHOGA AMBALO MAASKOFU WANALIFANYA HATA HAPA TANZANIA LINAUA ROHO KWA KIWANGO KIKUBWA HASA KATIKA MAZINGIRA AMBAYO WANAWAKE NI WENGI KULIKO WANAUME.
Pia suala la kuushabikia mzinzi na Mwasherati kama ilivyotokea kwa Dr. Slaa linawatoa kabisa kwenye kushulikia Roho na Ufalme wa Mbingu kwa Ujumla. Kwa hiyo kundi la MAASKOFU linabaki kuwa ni kundi MASLAHI TU. Ndiyo maana wanaanaglia sana opportunity ya nani yupo Madarakani.
Kwa upande wa MASHEIKH wao wako zaidi katika kutengeneza ROHO zaidi kuliko masalahi. Mfano ni pale walipofanikiwa kuwaandaa waumini kumpinga MWINYI katika suala la Kondomu hata ikifikia kumpiga. Suala la Hamisi Dibagula ni mfano mwingine na Mabucha ya Nguruwe. Na pia wameonyesha kutomshabikia Dr. Slaa hasa kutokana na Tabia yake ya Uasherati. Katika suala la maslahi nadhani masheikh yapo mambo muhimu yakitekelezwa hawana tatizo na utawala uliopo hata kama ni dhalimu. mfano ni OIC, Kadhi n.k. Kwao wao IMANI inatangulia halafu Usalama wa Nchi kisha Utawala. Kwa MAASKOFU wao Maslahi ya kanisa kwanza, Utawala, imani si suala lenye kipaumbele - kila mtu aende kivyake halafu mwisho ni usalama wa nchi.

Na hapo ndipo tofauti inapokuja kati ya MASHEIKH na MAASKOFU.

Maswali ya Msingi:
1.0 Nini jukumu jukumu la Masheikh na Maaskofu?
2.0 Ya Kaisari mpe Kaiasari na ya Mungu mpe Mungu inamuhusu nani??
 
Kwenye hili la maslahi ya kitaifa masheikh watoeni,kwenye maslahi ya waislamu pekee na dini yao..........count them in! Wao wanaamini shida walizonazo zinatokana na wao kuwa waislamu na kutokupewa haki sawa kwa kuwa wao ni waislamu na si kama watanzania as if shida zimegawanyika kutokana na dini au effect za ufisadi zinaenda kwa watu wa dini fulani tu.
Maaskofu tuko nao kwenye maslahi ya kitaifa na ya kujenga roho,sasa sioni wapi watakutana???wawe na sauti moja. kila mmoja ana priority na kufikia malengo yao kuna wanaotumia akili na busara na wapo wanaotumia hisia.:A S 39:
Mipishano ya mawazo at a manageable level huleta maendelea , hivyo JK awahi kuyaweka sawa haya makundi ya maaskofu na Mashehe/Imaam kabla mgogoro haujafika hatua ya pili (i.e unmanageable). Katika hatua hii ya awali naamini ataweza kupata suluhu ya kwanini kundi moja linawanyima haki zao wengine (kama ni kweli , maana kama ni hivyo hata JK anakosa hizo haki) etc
 
ndugu zangu,

nimeisoma hii thread lakini nadhani kuna kitu bado sijaelewa vizuri. tukisema maaskofu tunajua ni kiongozi wa taasisi fulani katika dini za kikriso na ama anachaguliwa kidemokrasia au anateuliwa kwa vigezo fulani.

hawa mashehe ni kina nani? wanaongoza taasisi gani? wanapatikanaje? wanasomeaje huo ushehe? kama wanaongoza taasisi fulani je zinatambulika na serikali na jamii? je, inawezekana muislamu yoyote akavaa kanzu na barakashehe akajiita shehe, na tukalazimika kuchukulia kauli yake kwa uzito sawa na ile ya Pengo au Laiza?
 
Kwa mtizamo wangu "Ni heri kinachoua MWILI ambao hata hivyo UTAKUFA kuliko kinachoua ROHO ambayo haifi". SUALA LA USHOGA AMBALO MAASKOFU WANALIFANYA HATA HAPA TANZANIA LINAUA ROHO KWA KIWANGO KIKUBWA HASA KATIKA MAZINGIRA AMBAYO WANAWAKE NI WENGI KULIKO WANAUME.
Pia suala la kuushabikia mzinzi na Mwasherati kama ilivyotokea kwa Dr. Slaa linawatoa kabisa kwenye kushulikia Roho na Ufalme wa Mbingu kwa Ujumla. Kwa hiyo kundi la MAASKOFU linabaki kuwa ni kundi MASLAHI TU. Ndiyo maana wanaanaglia sana opportunity ya nani yupo Madarakani.
Kwa upande wa MASHEIKH wao wako zaidi katika kutengeneza ROHO zaidi kuliko masalahi. Mfano ni pale walipofanikiwa kuwaandaa waumini kumpinga MWINYI katika suala la Kondomu hata ikifikia kumpiga. Suala la Hamisi Dibagula ni mfano mwingine na Mabucha ya Nguruwe. Na pia wameonyesha kutomshabikia Dr. Slaa hasa kutokana na Tabia yake ya Uasherati. Katika suala la maslahi nadhani masheikh yapo mambo muhimu yakitekelezwa hawana tatizo na utawala uliopo hata kama ni dhalimu. mfano ni OIC, Kadhi n.k. Kwao wao IMANI inatangulia halafu Usalama wa Nchi kisha Utawala. Kwa MAASKOFU wao Maslahi ya kanisa kwanza, Utawala, imani si suala lenye kipaumbele - kila mtu aende kivyake halafu mwisho ni usalama wa nchi.

Na hapo ndipo tofauti inapokuja kati ya MASHEIKH na MAASKOFU.

Maswali ya Msingi:
1.0 Nini jukumu la Masheikh na Maaskofu?
2.0 Ya Kaisari mpe Kaisari na ya Mungu mpe Mungu inamuhusu nani??

3.0 Kilele cha USOMI (DR, Masters, PHD) ni mtu kuwa Shoga , Basha, au Mwasherati?
4.0 Je, Watanzania tunaona fahari ya kuwa na viongozi wa kiimani wa aina hii?
 
ndugu zangu,

nimeisoma hii thread lakini nadhani kuna kitu bado sijaelewa vizuri. tukisema maaskofu tunajua ni kiongozi wa taasisi fulani katika dini za kikriso na ama anachaguliwa kidemokrasia au anateuliwa kwa vigezo fulani.

hawa mashehe ni kina nani? wanaongoza taasisi gani? wanapatikanaje? wanasomeaje huo ushehe? kama wanaongoza taasisi fulani je zinatambulika na serikali na jamii? je, inawezekana muislamu yoyote akavaa kanzu na barakashehe akajiita shehe, na tukalazimika kuchukulia kauli yake kwa uzito sawa na ile ya Pengo au Laiza?

Mashiekh wanasoma elimu ya kiislamu hadi kuqulify kuwa sheikh,lakini haitoshi kusoma tu bado jopo la Masheikh linalotambuliwa na waislam linawapitisha kwa kufanya mtihani maalum wa usheikh.Ngojea nikupe kidogo taaluma za walioshiriki kuongoza tamko hilo.
1.Sheikh Profesa Juma Mikidadi (PHD)
2.Sheikh Kundecha.Degree ya Dini
3.Sheikh Aba Saleh.Degree ya Dini pia na Diploma ya ualimu wa sekula
4.Sheikh Al Hadi Musa.Degree ya Dini
5.Sheikh Dr.Hamduni Suleiman Degree ya Dini na( PHD) South Africa
6.Sheikh Dr.Tego.Degree ya Dini na (PHD) Muslim College London
7.Shiekh Juma Doga.Degree ya Dini Madina University
8.Sheikh Muhammad Idd.Degree ya Dini
NEED I SAY MORE?
 
DUUUUUU,

M.M.Mwanakijiji Kwa kweli nakuunga mkono 100 Kwa 100 Yote uliosema ni kweli hapa kuna mgongano wa mawazo baina ya Masheikh na Maaskofu.

Ili tuwaelewe na twende pamoja nao ni kweli wakae chini waelezane wapi kila mmoja alikosea na nini watanzania tunategemea kutoka kwao waelewe kuwa Dini ni imani lakini Amani bila Imani hakuna na ili tuwe na Imani thabiti ni vema wao wote wawe nalengo moja, sijafika Ulaya ila nasikia baadhi ya Majengo yaliyotumika kama nyumba zaibada yamegeuka kuwa Majumba ya starehe.

Hata hapa kwetu hilo siku moja litatokea pindi tu tukijua hawa jamaa wapo kwa maslahi yao na si Watanzania.

Tuungane kudai Maslahi ya Watanzania na si waislam wala wakristu.

Weweee, Acha ujuhaaa! Marehemu Fares Kabuye akiwa bungeni alikataza hii kitu!

Jokes!
 
Kadogoo,
Wito kwa maaskofu kuomba msamaha kama sharti la muungano kwa madai ambayo uhalali wake si thabiti ni kigingi kingine kufikia muungano huo. Viongozi wa dini kwa pamoja wakate shauri kuomba msamaha kwa kunyamazia uovu kisha waazimu kuanza safari ya pamoja ya matamko dhidi ya uovu. Kama viongozi wa dini wote kwa nyakati tofauti wanaamini kuna vitendo vya upendeleo ambavyo vilitendeka au vinatendeka kutokana na kiongozi wa nchi aliyekuwepo au aliyepo madarakani bila shaka udhaifu wa udhibiti wa mamlaka ya kiongozi mkuu unajipambanua kwa uwazi zaidi. Matamko ya pamoja yatazika hisia za hatuko pamoja na katiba mpya itadhibiti mwanya kwa watawala kupenyeza upendeleo.
 
M.M. Mwanakijiji​
Ili maaskofu wapate mahali pa kusimamia wanapoikosoa serikali ya Kikwete ni lazima kwanza waombe msamaha kwa ukimya wao wakati Watanzania wameuawa Pemba na Mwembechai; si kwa sababu Waislamu waliuawa bali kwa sababu wananchi wameuawa.

Uchambuzi wako mzuri Mwanakijiji lakini jiulize scandals za Kagonda, Richmond, Dowans, n.k. ziliwekwa hadaharani wakati wa utawala gani...maaskofu wangeota? Mauaji ya Pemba yalikuwa ya kisiasa kama ya Arusha, hayakuwa na sababu kwa maaskofu kuhusisha dini. Na isitoshe msingi wa kauli ya maaskofu haikutokana na sababu za waliouawa Arusha kuwa ni wakristo!!!!
 
Huu utapiamlo wa udini utaifikisha wapi Tanzania? Viongozi wa kweli wa kidini hawaweki maslahi binafsi mbele, kinachoongelewa hapa ni ubinafsi tu hakuna dini, viongozi wa kweli wa kidini hukemea maovu bila kujali nani anaongoza, uraisi wa Kikwete unamnufaisha vipi muislamu wa kawaida? Watanzania wengi wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha badala ya kuongelea masula ya kimsingi, tunakwepesha hoja na kuangelea mambo ambayo hayana maslahi kitaifa. Dini ina nafasi yake ndani ya jamii lakini ni hatari inapotumika kuendeleza maovu. Tuangalie mfano hai Tunisia waliomuondoa madarakani Beni Alli si waislamu bali watunisia waliopinga udhalimu wake. Dini na siasa haviendi pamoja, mashekhe na maaskofu/mapadri mnaotaka kujiingiza kwenye siasa vueni kanzu na majoho vinginevyo mtakuwa wanafiki.

umekuja vizuriii mwishoni umejchanganya

Huyu askofu au shehe katiba ya nchi inamruhusu kushiriki siasa
Pia ni kiungo kati ya binadamu na Mungu.

Utamkwepea wapi mtu wa dini
Hata siku moja Huwezi kumkwepa!
Mwizi unapo mkemea wewe ni mwizi acha Wizi sidhani kama atafurahi mwanangu.

Ukisikia kelele vueni majoho ujue hapo fisadi limebanwa kiukweli

siasa haina unifomu eti joho kanga au suti pia haina ubaguzi wa aina yeyote

Tumeanza kukua sasa mwanangu!
 
Back
Top Bottom