Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,027
Hii nimeisikia leo Radio flani tanga:
Kuna njemba moja alioa msichana mmoja mzuri tu, huyu dada mama yake alikuwa RPC(Mkubwa wa Polisi), ndoa yao ilifana sana. Baada ya miezi michache matatizo yakaanza katika ile ndoa. Yule binti akawa analalamika kwa mme wake kwamba kabadilika na mara nyingi huwa anarudi usiku sana, matunzo sio mazuri, muda mwingine hata fedha haachi.
yule dada baadaya kuona hamna mabadiliko kwa mme wake akaamua kumshtaki yule jamaa kwa mama yake yule Polisi.(Mama Mkwe wa huyu jamaa). Kwa sababu mama mkwe anaheshima sana sehemu yoyote, basi busara ilitumika na yule jamaa akaitwa na Mama wa yule dada, jamaa akakalishwa chini na akaulizwa inakuaje siku hizi unarudi usiku sana na complain nyingine, jamaa akajitetea kwa kudai kazi tu nyingi kutafuta hela n.k, na akadai atajirekebisha, yakaisha.
Sasa siku moja kutokana na utaratibu wa jeshi la Polisi kugundua wazamiaji, wakaamua kufanya utaratibu wa kukagua gesti za mtaani usiku(huyu mama akiwa ndio mkubwa wa msako), sasa guest walipoenda wakaamuru mapokezi kuorodhesha wageni wao walikuwa vyumbani, na badae kwa utaratibu wa kawaida wakaamua kupitia chumba hadi chumba kuuliza uraia wa wageni mule hotelini/guest.
Sasa mlango wa kwanza kufungua jamaa uso kwa uso na mama mkwe, na alikuwa na kimwana ndani ya room, jamaa kutahamaki, mama mkwe...!!
Kama wewe ungefanyaje hapo ilhali siku chache za nyuma umekalishwa chini na huyu mama.??
Kuna njemba moja alioa msichana mmoja mzuri tu, huyu dada mama yake alikuwa RPC(Mkubwa wa Polisi), ndoa yao ilifana sana. Baada ya miezi michache matatizo yakaanza katika ile ndoa. Yule binti akawa analalamika kwa mme wake kwamba kabadilika na mara nyingi huwa anarudi usiku sana, matunzo sio mazuri, muda mwingine hata fedha haachi.
yule dada baadaya kuona hamna mabadiliko kwa mme wake akaamua kumshtaki yule jamaa kwa mama yake yule Polisi.(Mama Mkwe wa huyu jamaa). Kwa sababu mama mkwe anaheshima sana sehemu yoyote, basi busara ilitumika na yule jamaa akaitwa na Mama wa yule dada, jamaa akakalishwa chini na akaulizwa inakuaje siku hizi unarudi usiku sana na complain nyingine, jamaa akajitetea kwa kudai kazi tu nyingi kutafuta hela n.k, na akadai atajirekebisha, yakaisha.
Sasa siku moja kutokana na utaratibu wa jeshi la Polisi kugundua wazamiaji, wakaamua kufanya utaratibu wa kukagua gesti za mtaani usiku(huyu mama akiwa ndio mkubwa wa msako), sasa guest walipoenda wakaamuru mapokezi kuorodhesha wageni wao walikuwa vyumbani, na badae kwa utaratibu wa kawaida wakaamua kupitia chumba hadi chumba kuuliza uraia wa wageni mule hotelini/guest.
Sasa mlango wa kwanza kufungua jamaa uso kwa uso na mama mkwe, na alikuwa na kimwana ndani ya room, jamaa kutahamaki, mama mkwe...!!
Kama wewe ungefanyaje hapo ilhali siku chache za nyuma umekalishwa chini na huyu mama.??