VIKWAZO
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 1,899
- 580
MAMLAKA za vijiji, kata na wilaya zimeagizwa kuhakikisha vijana wanajiunga katika vikundi vya uzalishaji mali kwa kuwawezesha ili waondokane na umasikini unaowakabili na wengi wao kutokuwa na ajira.
Kauli hiyo imetolewa mjini hapa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira wakati alipokuwa akihutubia mikutano ya hadhara katika vijiji vya Tairo na Nyamatoke wilayani humo.
Wassira ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Bunda amesema kuwa ni wajibu wa serikali za vijiji na wilaya kote nchini kuweka mikakati kabambe ya kuhakikisha kuwa vijana ambao ni nguvu kazi tegemezi ya taifa kuwezeshwa kwa kadri inavyowezekana ili waweze kujiajiri badala ya
kuwaacha wazurure mitaani.
"Vijana wetu hawa tunawasomesha sawa, lakini lazima tuwawekee misingi imara ya maisha yao ya kesho maana hawa ndio nguvukazi ya taifa hili.
Lazima serikali za vijiji, kata na wilaya muone namna ya kuwaokoa mara moja," alisema
Wassira.
Alisema serikali za vijiji na kata zinapaswa kuwahamasisha vijana hao kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali kama vile vya kilimo, uvuvi na ufugaji na kuvisaidia kupatiwa mikopo ya mitaji na nyenzo za kazi.
Alisema kutokana na vijana wengi kutokuwa na ajira za kuwaingizia mapato ndiyo sababu wanachotwa kirahisi na wanasiasa uchwara wanaowahamasisha kushiriki katika vurugu za kile kinachoitwa kudai haki.
"Wasipowezeshwa ndio maana wanasiasa uchwara wanawashawishi kirahisi kushiriki katika
maandamano ambayo wengi wao wanapoteza maisha yao na hivyo kupotea kwa nguvu kazi muhimu ya taifa hili," amesema Wassira
maoni yangu: hivi kwa hali ilivyo sasa kuna kijiji kinaweza kusaidia kuondoa tatizo la ajira kwa wasome wa nchi hii?
hizo wilaya anazosema ni lini zimeanza kupanga mipango ya taifa ili?
kama wameshindwa kuzalisha ajira walisosema waseme mapema ili tujua cha kufanya,
habari ya kuita watu wanasiasa uchwara yeye na sisi vijana nani anatumia akili?
mimi nadhani huyu ana petrol kichwa jua ikiwaka anakuwa kama analipuka, maana petrol inaweza kuwa hata kwa jua
Kauli hiyo imetolewa mjini hapa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira wakati alipokuwa akihutubia mikutano ya hadhara katika vijiji vya Tairo na Nyamatoke wilayani humo.
Wassira ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Bunda amesema kuwa ni wajibu wa serikali za vijiji na wilaya kote nchini kuweka mikakati kabambe ya kuhakikisha kuwa vijana ambao ni nguvu kazi tegemezi ya taifa kuwezeshwa kwa kadri inavyowezekana ili waweze kujiajiri badala ya
kuwaacha wazurure mitaani.
"Vijana wetu hawa tunawasomesha sawa, lakini lazima tuwawekee misingi imara ya maisha yao ya kesho maana hawa ndio nguvukazi ya taifa hili.
Lazima serikali za vijiji, kata na wilaya muone namna ya kuwaokoa mara moja," alisema
Wassira.
Alisema serikali za vijiji na kata zinapaswa kuwahamasisha vijana hao kujiunga katika vikundi vya uzalishaji mali kama vile vya kilimo, uvuvi na ufugaji na kuvisaidia kupatiwa mikopo ya mitaji na nyenzo za kazi.
Alisema kutokana na vijana wengi kutokuwa na ajira za kuwaingizia mapato ndiyo sababu wanachotwa kirahisi na wanasiasa uchwara wanaowahamasisha kushiriki katika vurugu za kile kinachoitwa kudai haki.
"Wasipowezeshwa ndio maana wanasiasa uchwara wanawashawishi kirahisi kushiriki katika
maandamano ambayo wengi wao wanapoteza maisha yao na hivyo kupotea kwa nguvu kazi muhimu ya taifa hili," amesema Wassira
maoni yangu: hivi kwa hali ilivyo sasa kuna kijiji kinaweza kusaidia kuondoa tatizo la ajira kwa wasome wa nchi hii?
hizo wilaya anazosema ni lini zimeanza kupanga mipango ya taifa ili?
kama wameshindwa kuzalisha ajira walisosema waseme mapema ili tujua cha kufanya,
habari ya kuita watu wanasiasa uchwara yeye na sisi vijana nani anatumia akili?
mimi nadhani huyu ana petrol kichwa jua ikiwaka anakuwa kama analipuka, maana petrol inaweza kuwa hata kwa jua