Sijaoga siku mbili...

Kutokana na mishemishe za English Premier League wikiendi hii, pamoja na AFCON 2012 iliyoanza rasmi J'mosi, nikajikuta sijaoga tangu IJUMAA... Usiulize wapi, Dar hiyo! Tena hukuhuku katikati ya mji, na joto balaa.
Basi ile kuingia kwa bafu (lenye miksa choo humohumo), nikataka nighairi kuoga afta gogo heavy, lakini nikapiga moyo konde! Potelea mbali...
Nikaoga kiroho ngumu, kila nikipaka sabuni, kitu kinadunda, utadhani niko Tabata naogea maji ya chumvi. Mwisho wa siku ndoo ya maji ikakata kabla nitakate.
Ila nikamshukuru Mungu kwa kuwa zoezi lilikamilika, ila dah?
Nahisi nimepungua mwili...
Ulitaka kushindana na wazungu sio? Manaake wengi wao huoga mara moja au mbili kwa wiki!
 
Ulitaka kushindana na wazungu sio? Manaake wengi wao huoga mara moja au mbili kwa wiki!

wale nadhani wanafanya vile kwa sababu ya baridi. Hata mimi kuna kipindi nilienda Mbeya, huwezi amini, katika wiki mbili nilizokaa nilioga siku naondoka tu.
 
Ww ndo unadanganya! Katikati ya mji unaoga na maji ya ndoo? Unajua 'kujimasakisha'? Wasalimie tabata, waambie mbunge wao akifa wanichague mie niwapelekee maji manake ya visima hayafai yanamaliza sabuni japo ya mche!
jamani?
Kwa hiyo kusema ukweli imekuwa nongwa? Tatizo mshazoea kudanganywa...
 
Ww ndo unadanganya! Katikati ya mji unaoga na maji ya ndoo? Unajua 'kujimasakisha'? Wasalimie tabata, waambie mbunge wao akifa wanichague mie niwapelekee maji manake ya visima hayafai yanamaliza sabuni japo ya mche!

aku!
Nilivyosema katikati ya mji sikumanisha Post wala Kipata St. miksa Gerezani.
Mimi nakaa Mikocheni uswahilini, nyumbani hakuna bomba la mvua, ndoo ndo mpango mzima ingawa kitu cha DAWASCO kama kawaida.
Sabuni ya magadi siijui mie...
 
wale nadhani wanafanya vile kwa sababu ya baridi. Hata mimi kuna kipindi nilienda Mbeya, huwezi amini, katika wiki mbili nilizokaa nilioga siku naondoka tu.
Suala sio baridi bali wanaogopa kwamba kuoga kila siku kutaharibu ngozi. Maji ya moto kwao sio shida kama bongo ambako umeme unakatika kila saa!
 
ha ha haaaa! Pole sana mkuu...Ingekuwa ni enzi zile wakati mimi nasoma tungeenda kukuogesha na steel wire!!
 
Suala sio baridi bali wanaogopa kwamba kuoga kila siku kutaharibu ngozi. Maji ya moto kwao sio shida kama bongo ambako umeme unakatika kila saa!

kumbe kuoga kunaharibu ngozi eh?
Nitaongeza rate ya kutokuoga aisee... Nashukuru kwa kunifungua macho!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom