Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ulitaka kushindana na wazungu sio? Manaake wengi wao huoga mara moja au mbili kwa wiki!Kutokana na mishemishe za English Premier League wikiendi hii, pamoja na AFCON 2012 iliyoanza rasmi J'mosi, nikajikuta sijaoga tangu IJUMAA... Usiulize wapi, Dar hiyo! Tena hukuhuku katikati ya mji, na joto balaa.
Basi ile kuingia kwa bafu (lenye miksa choo humohumo), nikataka nighairi kuoga afta gogo heavy, lakini nikapiga moyo konde! Potelea mbali...
Nikaoga kiroho ngumu, kila nikipaka sabuni, kitu kinadunda, utadhani niko Tabata naogea maji ya chumvi. Mwisho wa siku ndoo ya maji ikakata kabla nitakate.
Ila nikamshukuru Mungu kwa kuwa zoezi lilikamilika, ila dah?
Nahisi nimepungua mwili...
Ulitaka kushindana na wazungu sio? Manaake wengi wao huoga mara moja au mbili kwa wiki!
naona pele limepata mkunaji.
jamani?
Kwa hiyo kusema ukweli imekuwa nongwa? Tatizo mshazoea kudanganywa...
Kwa sasa umemweka kundi gani?Kumbe Amyner ulishamsoma huyu jamaa...
Kwenye ile thread yake kule nilikua sijamwelewa bado.
Ww ndo unadanganya! Katikati ya mji unaoga na maji ya ndoo? Unajua 'kujimasakisha'? Wasalimie tabata, waambie mbunge wao akifa wanichague mie niwapelekee maji manake ya visima hayafai yanamaliza sabuni japo ya mche!
Suala sio baridi bali wanaogopa kwamba kuoga kila siku kutaharibu ngozi. Maji ya moto kwao sio shida kama bongo ambako umeme unakatika kila saa!wale nadhani wanafanya vile kwa sababu ya baridi. Hata mimi kuna kipindi nilienda Mbeya, huwezi amini, katika wiki mbili nilizokaa nilioga siku naondoka tu.
Suala sio baridi bali wanaogopa kwamba kuoga kila siku kutaharibu ngozi. Maji ya moto kwao sio shida kama bongo ambako umeme unakatika kila saa!