nyumba kubwa
JF-Expert Member
- Oct 8, 2010
- 10,309
- 8,369
Amejichanganya kweli kweli; mara sihitaji kuolewa; mara nilokuwa nao walikuwa si waoaji; mara kuolewa ni bahati wako wanaojichanganya na hawajaolewa; mara huwezi subiri hizi ndoa uchwara za siku hizi; mara nimeshamwambia boyfriend wangu kama anataka kuoa aoe; mara nimemwambia boyfriend wangu nataka mtoto amekubali; mara hapo nilipo mtoto anacheza tumboni. Sijuhi lipi ni lipi sasa. Kwani huyo current boyfriend wako alikwambia anataka kuoa au kukuoa wewe? Isije kuwa huyu alokupa mimba na kukataa kukuoa ndio amekupelekea kuandika huu uzi unaoonyesha umepoteza matumaini.
Ukichukua maneno ya mwanzo ya post hii ulinganishe na post zako nyingine ktk uzi huu, utagundua kuwa unajichanganya sana! Pole sana dadaangu.