Shedafa
JF-Expert Member
- May 21, 2008
- 802
- 173
Wandugu napenda kuelezea hisia zangu kwa hili tangazo la TAMWA, linalomuonyesha binti wa shule akipambana na vikwazo na majaribu mbalimbali nimelipenda sana. Siku zote nilikuwa nikifikiri njia mbadala za uhamasishaji wa mabinti zetu badala ya kutupa lawama kwa akina FATAKI tu, zinaweza kuwa na impact kubwa zaidi. Tangazo hili linawajengea kujiamini fulani hivi mabinti zetu, na kama ilivyo kawaida ya nguvu ya matangazo inatia raha sasa kila ukipita unasikia kabinti kanasema SIDANGANYIKI!. BRAVO TAMWA!