siasa zetu zimefika hapa?

gfsonwin

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
18,274
20,673
mwan jf leo nilifuatilia bunge kwa umakini sana na kuyapata haya;
wabunge wote walikuwa na umoja sana hilikuwa ni ngumu kumtambua yupi mccm wala yupi mpinzani lakin kuna kitu mimi kimenikuna nacho ni;

Mhe Lissu alianza kwa sentensi yenye maana kwa aliposema hapa ndani naona wote wanapiga makofi na kushangilia lakin sidhani kama ninyi wa ccm kama mnamaanisha. tena hakuishia hapo akawaambia kwakua wao wako wengi kuliko upinzani basi waonyeshe nia yao ya dhati ya kutokuwa na imani na serikali.

Zitto aliomba mwongozo wa spika akitaka iletwe hansadi ili maneno ya Mhe.Mwanri aliyoyasema yarudiwe upya manake aliyoyasema Mwanri leo, ndiyo aliyoyasema last year. alisema kwa jazba sana tena akiwa na sura ya kazi. lakin kama haya aliyasema mwaka jana napata hisia kuwa hawa ccm wanatudanganya na wanatoa haya ilihali wanajua kuwa mbele ya serikali yao mikono yao inatakiwa iwe safi. Maneno haya ni ya msingi kwao na kama kweli magamba wako serious basi wajipange vizuri.

lLakini zuri zaid ni ushauri alioutoa mhe. Lissu kuwa wakati kamati zinafanya majumuisho basi waje na idea kwamba hawana imani ya serikali hivyo wapige kura ya kutokuwa na imani na serikali.

Hivi kwa hapa Tanzania kweli inawezekana kusaini petisheni????????????

sijui kama siasa zetu zimekomaa kwa kiasi hicho.

kwa wanaojua siasa vizuri je wazo hili likipita nini itakayo kuwa hatima ya serikali?

na je inamaana uchaguzi wote utarudiwa?
Nawasilisha kiongozi.
 
Ngoja nichat na Fredric Werema atujuze katika vifungu vya Katiba..
Ila mim nadhani uchaguzi wote unarudiwa..
 
Magamba hawatakubali ukizingatia upepo unavyo wavumia vibaya
 
Back
Top Bottom