Siasa za Zanzibar na status quo

Geza Ulole

JF-Expert Member
Oct 31, 2009
59,185
79,368
Naomba wana great thinker tujiulize ni kipi kimejiri kuhusu ile ajali ya boat MV Islander? Je kuna mtu amechukuliwa hatua kwenye serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) au ndo mambo ya interest za kisiasa ku-overrule taking responsibilities? Kwa wale wenzangu wanaofuatilia hii issue naskia waziri husika wa Usafirishaji na mwenye boat chinjachinja wote wametokea CUF na ndo mana hii issue ilibidi ife kimya kimya yaani wahusika CUF hawakutaka hata chembe hilo swala kizungumziwa wakihofia kupoteza wizara na pia kiti cha Ubunge maana mwenye boat ni Mbunge wa CUF.

Sasa tujiulize kwa mwenendo huu hatari inayotukabilli kwa siye tunaodhani CUF ni chama Mbadala kwa CCM! Siasa zao tumeziona, walidiriki hata ku-divert attention via radicalizing watu kipindi ajali ilipotokea kuanza kuelekeza shutma kwa Vodacom as if Vodacom ndio waliokuwa wanaendesha hiyo boat na kwavile Wazanzibari ni watu wa siasa za visa kuliko ukweli wakauzika kilaini huku asilimia 2 ya Wapemba wameangamia na kesi iliyoanza naskia imezimwa! hata huyo kapteni wa meli ataachiwa huru!

Naomba Jussa aje anijibu huku kwa nini niwapigie kura yangu CUF kama utendaji wao uko namna hiyo? Tukiachia mbali ndoa ya CUF na CCM ilivyomfunika Maalim seif!

Mh Ismail Jussa njo ujibu hapa hatua gani mmechukua? au ndo mkuki kwa nguruwe kwa binadam Mchungu sio? Tuwaamini vp mpo tofauti na CCM? maana katika zile siasa za jicho na kidole (chokochoko) upo wa kwanza kuongea tukiachilia mbali vile vipeperushi ila kwenye mambo ya mustakabali wa usalama na ustawi wa Wazanzibari mpo kimya...! Naomba jibu hapa kwa nini nisiende CHADEMA!
 
Back
Top Bottom