Siasa za Mbeya 2005-2010

Hujuma dhidi ya Mwakyembe zafichuka

na Christopher Nyenyembe

NJAMA nzito za kutaka kudhibiti mapokezi ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, yaliyoandaliwa na wananchi yasifanikiwe, zikiwa zimeongozwa na mkuu wa wilaya hiyo hatimaye zimefichuka.

Kufichuka kwa njama hizo kunatokana na barua za siri zilizoandikwa zikilielekeza Jeshi la Polisi wilayani humo kudhibiti nyendo za waandaaji wa mapokezi hayo na jinsi michango inavyochangwa, ili kufanikisha shughuli hiyo.

Mkuu wa wilaya hiyo (DC), Mashimba Mashimba, katika kile kinachodaiwa kuwa yumo kwenye mpango madhubuti wa kuhujumu mapokezi hayo amediriki kumtumia nakala ya barua hiyo, John Mwakipesile kama barua binafsi na si ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umegundua kuwapo barua aliyoiandika Februari 21 mwaka huu kwenda kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kyela, ikiwa inamtahadharisha juu ya mapokezi hayo na nakala yake kutumiwa Mwakipesile ikiwa haijaonyesha wadhifa wa mkuu wa mkoa kama ilivyo kawaida kwa barua za serikali.

Barua hiyo inamwelekeza Mkuu wa Polisi wa wilaya hiyo kufuatilia kwa karibu mchakato mzima wa maandalizi hayo kwa madai ya kuzingatia usalama wa raia na mali zao na taratibu za michango nchini.

“Taarifa yako imejaa aina fulani ya utetezi kana kwamba jambo hilo ni la kawaida na halina madhara ya aina yoyote ya kiusalama ndani ya wilaya,” alisema DC huyo ikiwa ni sehemu ya barua yake inayoonyesha msisitizo na hofu aliyonayo kuhusu mapokezi hayo.

Msimamo wa mkuu wa wilaya hiyo unakinzana na taarifa iliyomo kwenye barua ya mkuu wa polisi (OCD) kuhusu nia yake ya kutokuwa na mashaka na mapokezi hayo hasa ikizingatiwa usalama mkubwa uliopo sambamba na kazi ya Jeshi la Polisi kulinda usalama wa raia na mali zao.

Katika barua ya Mkuu wa Polisi wa wilaya hiyo ambayo Tanzania Daima imefanikiwa kuipata, imemtaka mkuu wa wilaya hiyo kutokuwa na wasiwasi wowote juu ya mapokezi hayo wakiamini kuwa ulinzi wa kutosha upo kwa ajili ya kudhibiti vurugu zozote zinazoweza kutokea.

Ujasiri ulioonyeshwa na OCD wa Kyela kwa kiasi kikubwa unaonyesha kumkera mkuu wa wilaya hiyo na watendaji wengine wa serikali kiasi cha kuandika barua yenye maelekezo hayo yakiipinga barua ya polisi ya Februari 19 inayoelezea kuruhusu mapokezi hayo.

Kufumuka kwa matukio hayo, ni njama za kudhoofisha mapokezi ya Dk. Mwakyembe ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati teule ya Bunge iliyokuwa ikichunguza mkataba wa Kampuni ya uzalishaji wa umeme wa dharura ya Richmond.

Mlolongo mzima wa njama hizo pia umesababisha watendaji wote wa serikali wilayani humo kuandaa safari za dharura ili siku ya mapokezi hayo wasiwepo kwenye wilaya hiyo na nafasi zao zimeachiwa wasaidizi wao.

Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Martin Mulwafu, alipohojiwa alikana kuiona barua yoyote inayotoa maelekezo ya kufuatilia nyendo za mapokezi hayo kutoka kwa mkuu wa wilaya hiyo na kwamba hajaachiwa msimamo wowote na DC huyo kuhusu kupokewa kwa Dk. Mwakyembe.


Source: Tanzania Daima
 
Mkuu wa polisi kafanya la maana sana kukataa amri hiyo isiyo halali ya mkuu wa wilaya.

Yeye Mwakipesile alivyoteuliwa kuwa mkuu wa mkoa na wakati alipotoka kuapishwa, aliandaliwa na kupokelewa kwa mapokezi makubwa sana.

Nyumba ya Mwakipesile iko barabarani kabisa unapoingia Kyela, sitashangaa
ikipigwa mawe. Wamelikuza hili jambo bila sababu muhimu na sasa inaonekana ni vita tena.

Hivi tunashangaa kwanini hatuendelei? Tunapoteza muda kubishana na kushughulikia mambo ambayo hayana maana kabisa badala ya kukimbizana na mambo ya maendeleo.
 
Mtanzania,

Maelezo yako hayo yanatosha kabisa, sasa naijua Mbeya vizuri. Hoja na dataz za watu kama wewe ndio zinatufanya wengine tuwe addicted na JF, ubarikiwe sana! Umenisaidia pia ku-confirm yale niliyokuwa nayajua kuhusu Dk wetu Mwakyembe. Haya mimi yalinikuta wakati tunamfanyia kampeni za ubunge za EAC, wewe acha kabisa, huyu jamaa ni kiboko. Huwezi kumjua Mwakyembe kwa kumsoma kwenye magazeti hadi ukae naye ana kwa ana kwa muda.

Tena hupaswi kabisa kumchukulia Mwakyembe on a face value. Yeye huwa anakubali kutumiwa na kutumia akili zake kufanikisha matakwa ya kisiasa ya watu wengine. Unakumbuka Mkapa alivyomtumia kuhalalisha yale mauaji ya polisi kule Zanzibar, alijenga hoja kidogo watu wakubali, kilichosaidia kusambaratisha hoja zake ni hoja maridadi za prof Haroub Othman. Hivyo basi hata kwenye hii report ambayo tunamsifu sana huyu mheshimiwa, mimi ninajua kuna wajanja wachache waliamua kutumia akili zake ili kufanikisha ajenda zao kisiasa. Uzuri wa haya mambo ni kwamba ukweli siku zote hujitenga na uongo, sio muda mrefu tutajua zaidi kuhusu dhamira ya ndani kabisa ya ile report!

In the meantime, ukweli ni kwamba hii report imeinyanyua nyota ya kisiasa ya Dk Mwakyembe ambayo ilikuwa inazidi kufifia; sasa swali ni je, itadumu hadi lini? Time will tell.
 
Mtanzania,

Maelezo yako hayo yanatosha kabisa, sasa naijua Mbeya vizuri. Hoja na dataz za watu kama wewe ndio zinatufanya wengine tuwe addicted na JF, ubarikiwe sana! Umenisaidia pia ku-confirm yale niliyokuwa nayajua kuhusu Dk wetu Mwakyembe. Haya mimi yalinikuta wakati tunamfanyia kampeni za ubunge za EAC, wewe acha kabisa, huyu jamaa ni kiboko. Huwezi kumjua Mwakyembe kwa kumsoma kwenye magazeti hadi ukae naye ana kwa ana kwa muda.

Tena hupaswi kabisa kumchukulia Mwakyembe on a face value. Yeye huwa anakubali kutumiwa na kutumia akili zake kufanikisha matakwa ya kisiasa ya watu wengine. Unakumbuka Mkapa alivyomtumia kuhalalisha yale mauaji ya polisi kule Zanzibar, alijenga hoja kidogo watu wakubali, kilichosaidia kusambaratisha hoja zake ni hoja maridadi za prof Haroub Othman. Hivyo basi hata kwenye hii report ambayo tunamsifu sana huyu mheshimiwa, mimi ninajua kuna wajanja wachache waliamua kutumia akili zake ili kufanikisha ajenda zao kisiasa. Uzuri wa haya mambo ni kwamba ukweli siku zote hujitenga na uongo, sio muda mrefu tutajua zaidi kuhusu dhamira ya ndani kabisa ya ile report!

In the meantime, ukweli ni kwamba hii report imeinyanyua nyota ya kisiasa ya Dk Mwakyembe ambayo ilikuwa inazidi kufifia; sasa swali ni je, itadumu hadi lini? Time will tell.


NJAMA nzito za kutaka kudhibiti mapokezi ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, yaliyoandaliwa na wananchi yasifanikiwe, zikiwa zimeongozwa na mkuu wa wilaya hiyo hatimaye zimefichuka.

Kufichuka kwa njama hizo kunatokana na barua za siri zilizoandikwa zikilielekeza Jeshi la Polisi wilayani humo kudhibiti nyendo za waandaaji wa mapokezi hayo na jinsi michango inavyochangwa, ili kufanikisha shughuli hiyo.

Mkuu wa wilaya hiyo (DC), Mashimba Mashimba, katika kile kinachodaiwa kuwa yumo kwenye mpango madhubuti wa kuhujumu mapokezi hayo amediriki kumtumia nakala ya barua hiyo, John Mwakipesile kama barua binafsi na si ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umegundua kuwapo barua aliyoiandika Februari 21 mwaka huu kwenda kwa Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kyela, ikiwa inamtahadharisha juu ya mapokezi hayo na nakala yake kutumiwa Mwakipesile ikiwa haijaonyesha wadhifa wa mkuu wa mkoa kama ilivyo kawaida kwa barua za serikali.

Barua hiyo inamwelekeza Mkuu wa Polisi wa wilaya hiyo kufuatilia kwa karibu mchakato mzima wa maandalizi hayo kwa madai ya kuzingatia usalama wa raia na mali zao na taratibu za michango nchini.
“Taarifa yako imejaa aina fulani ya utetezi kana kwamba jambo hilo ni la kawaida na halina madhara ya aina yoyote ya kiusalama ndani ya wilaya,” alisema DC huyo ikiwa ni sehemu ya barua yake inayoonyesha msisitizo na hofu aliyonayo kuhusu mapokezi hayo.

Msimamo wa mkuu wa wilaya hiyo unakinzana na taarifa iliyomo kwenye barua ya mkuu wa polisi (OCD) kuhusu nia yake ya kutokuwa na mashaka na mapokezi hayo hasa ikizingatiwa usalama mkubwa uliopo sambamba na kazi ya Jeshi la Polisi kulinda usalama wa raia na mali zao.

Katika barua ya Mkuu wa Polisi wa wilaya hiyo ambayo Tanzania Daima imefanikiwa kuipata, imemtaka mkuu wa wilaya hiyo kutokuwa na wasiwasi wowote juu ya mapokezi hayo wakiamini kuwa ulinzi wa kutosha upo kwa ajili ya kudhibiti vurugu zozote zinazoweza kutokea.

Ujasiri ulioonyeshwa na OCD wa Kyela kwa kiasi kikubwa unaonyesha kumkera mkuu wa wilaya hiyo na watendaji wengine wa serikali kiasi cha kuandika barua yenye maelekezo hayo yakiipinga barua ya polisi ya Februari 19 inayoelezea kuruhusu mapokezi hayo.

Kufumuka kwa matukio hayo, ni njama za kudhoofisha mapokezi ya Dk. Mwakyembe ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati teule ya Bunge iliyokuwa ikichunguza mkataba wa Kampuni ya uzalishaji wa umeme wa dharura ya Richmond.

Mlolongo mzima wa njama hizo pia umesababisha watendaji wote wa serikali wilayani humo kuandaa safari za dharura ili siku ya mapokezi hayo wasiwepo kwenye wilaya hiyo na nafasi zao zimeachiwa wasaidizi wao.
Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Martin Mulwafu, alipohojiwa alikana kuiona barua yoyote inayotoa maelekezo ya kufuatilia nyendo za mapokezi hayo kutoka kwa mkuu wa wilaya hiyo na kwamba hajaachiwa msimamo wowote na DC huyo kuhusu kupokewa kwa Dk. Mwakyembe.


Source: Tanzania Daima
 
Leo Kyela wamempokea mbunge wao kwa mbwembwe zote. Gari karibu 30 zilishiriki kwenye hayo mapokezi kutokea mpakani na Rungwe mpaka Kyela mjini.

Mkuu wa wilaya alikuwepo tofauti walivyosema Tanzania Daima. Aliwaambia wananchi kwamba kuna watu wamefanya mradi kuwachonganisha viongozi wa Kyela.

Sasa wameenda kujichana mpunga wa Kyela na kufaidi beer wakifurahia kifo cha Mmasai. Sijui akizinduka huko atakuja na upinde gani?

Maoni yangu: Laiti tu tungeliwahamasisha wananchi wetu kwa mambo ya maendeleo, huenda leo hii tusingelihitaji kumpamba Bush ili atupatie vyandarua, dawa za ukimwi na malaria.
 
Richmond yamfuata Mwakyembe Mbeya

na Christopher Nyenyembe, Kyela

KILA kukicha sakata la Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond linazidi kuibua mambo kama ilivyotokea jana wilayani Kyela wakati wa mapokezi ya aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati teule ya Bunge iliyochunguza mkataba wa kampuni hiyo, Dk. Harrison Mwakyembe, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kyela.

Katika mapokezi hayo, kile kilichokuwa kikizungmzwa kama tetesi kilipata uhakika baada ya Dk. Mwakyembe mwenyewe kuuthibitishia umma kuwa mapokezi hayo yalikuwa yanapingwa na ‘viongozi wa juu.’

Ingawa ‘viongozi hao wa juu’ hawakutajwa kwa majina, lakini katika hotuba yake, Dk. Mwakyembe aliwaambia waliohudhuria kuwa hata yeye alikwisha kupigiwa simu ya kuonywa, akitakiwa kusitisha mapokezi hayo mara moja.

Pamoja na kutoboa siri hiyo, Dk. Mwakyembe, ambaye ni mwanasheria kitaaluma, alikwenda mbali zaidi na kumtaja mtu ambaye alimpigia simu akimuonya kuachana na mapokezi hayo.

“Ndugu zangu nimefarijika sana na mapokezi makubwa kiasi hiki, ni juzi tu nimepigiwa simu na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mbeya, Nawab Mullar, akinitaka nisishiriki mapokezi yoyote kwa kuwa amepata maagizo kutoka juu,” alisema Dk. Mwakyembe.

Hata hivyo, Dk. Mwakyembe hakujali onyo hilo na kupokewa kama mfalme alipoingia katika wilaya hiyo jana na msafara wa magari zaidi ya 45 na kupata fursa ya kuwahutubia wananchi katika Uwanja wa Mwakangale.

Aliwaambia watu waliokuwa wanamsikiliza kuwa licha ya kupata vitisho hivyo kutoka kwa kiongozi mkuu wa CCM mkoani Mbeya, hakuvijali, kwa sababu anaamini kuwa hakuna kiongozi ambaye anaweza kupingana na nguvu za umma.

Alikuwa akimaanisha uamuzi wa wananchi kuandaa mapokezi hayo na kueleza kuwa hakuna mtu ambaye angeweza kuwapinga wananahci kuandaa mapokezi hayo kwa sababu walikuwa wamejipangia wenyewe bila kulazimishwa na mtu yeyote.

Hatua ya Dk. Mwakyembe kulitaja hadharani jina la Mullar, na kubainisha kuwa ni miongoni mwa watu waliokuwa wakishauri kutokuwepo kwa mapokezi hayo, inaweza kuzusha mtafaruku mkubwa wa kisiasa mkoani humu.

Aidha, hali si nzuri kisiasa pia kwa Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Mashimba Hussein Mashimba, ambaye alitumia muda mrefu kueleza sababu zilizowafanya watendaji wa serikali katika wilaya hiyo kuwa mbali na maandalizi ya mapokezi hayo.

Mashimba, aliyeonekana kuhitaji utetezi wa kina, ambaye inadaiwa kuwa alirejea ghafla kwenye kituo chake cha kazi, aliwalaumu baadhi ya watendaji wilayani mwake, aliodai kuwa kutokuwepo kwao katika shughuli hiyo kulikuwa kunasababisha hali ya utengano na kukuza makundi.

“Siasa za Mbeya bila kumtaja Dk. Mwakyembe na (John) Mwakipesile (Mkuu wa Mkoa wa Mbeya) hazinogi, na napenda kuwaambia, mimi sifanyi kazi kwa presha ya mkuu wa mkoa, nimeapishwa na nimekula kiapo mbele ya rais, siwezi kuongozwa na mtu, sifanyi kazi kwa presha, naomba mnielewe,” alisema Mashimba.

Wananchi wa Kyela, kupitia kamati yao ya mapokezi iliyoongozwa na Oscar Korosso na Emmanuel Kiketelo Mwamulinge, walisoma risala nzito, waliutaka umma wa Watanzania kutambua kuwa suala la Richmond si suala la Dk. Mwakyembe peke yake, bali ni kazi nzuri iliyofanywa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akisoma risala hiyo, Korosso alisema kwa kutambua mchango mkubwa wa Bunge, wananchi sasa wamejijengea imani na chombo hicho, hivyo kuyaepuka makundi yaliyoanza kueneza dhana ya ukabila katika sakata hilo.

Dk. Mwakyembe alisema kuwa kazi kubwa iliyofanywa na Kamati Teule ya Bunge imefungua mlango wa kuwashughulikia, hasa viongozi, waliokuwa na tabia ya kulindana, kuteteana na kufichiana makosa ambayo kwa kiasi kikubwa yamewaingiza wananchi kwenye lindi la umaskini, huku wakibanwa kuchangia michango mbalimbali ya maendeleo kwa nguvu.

Kwa kiasi kikubwa, mapokezi ya mbunge huyo yalionyesha jinsi wananchi wa wilaya hiyo walivyoguswa na hoja nzito za ufisadi kwani wazee kwa vijana, wanawake kwa watoto, walitanda barabarani huku wakiwa wameshika matawi mikononi, wengi wakionekana kumuombea dua Dk. Mwakyembe, ili aendelee kuwa jasiri kwa kazi zote atakazopewa.

Kwa kuonyesha shukrani zao, wananchi wa Kyela walimzawadia mbunge huyo ng’ombe dume kama ishara ya kuutambua mchango wake katika ujenzi wa taifa.

Maandalizi ya mapokezi ya Dk. Mwakyembe yaliibua joto la kisiasa mkoani humu na kusababisha msuguano, huku baadhi ya viongozi wakitajwa kula njama za kuhujumu mapokezi hayo.

Ilifikia wakati hata watumishi wa serikali wilayani Kyela, kwa kutaka kutoonekana kujihusisha na upande wowote katika sakata hilo, waliamua ‘kuzikimbia’ ofisi zao kwa muda wakati wa mapokezi hayo, kwa kujipangia safari za dharura.

Ni siri iliyo wazi kuwa kuna msuguano wa kisiasa baina ya Dk. Mwakyembe na Mwakipesile, chanzo kikiwa ni ubunge wa Kyela. Kabla Dk. Mwakyembe hajateuliwa na CCM kuwania nafasi hiyo, ilikuwa inashikiliwa na Mwakipesile, ambaye baada ya kuangushwa na CCM, aliteuliwa na Rais Kikwete kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya mara baada ya Uchaguzi Mkuu uliopita.

Source: Tanzania Daima
 
Pundit,

Mwakyembe sio mtu wa JK. Ila JK huwa hasemi tu na wala haonyeshi kirahisi kama anamchukia mtu au la.

Mwakyembe alifanya kosa kama la Msekwa. Alienda kuwambia JK kwamba anataka kuacha bunge la EA ili akagombee Kyela. JK akasema sawa, Mwakyembe akachukulia kama ni green light wakati JK alikuwa na yake.

Ilipofika uwaziri, Mwakyembe akaachwa nje.

Mwakyembe ndiye alikuwa mpiga debe namba moja wa prof. Mwandosya
kwahiyo
hakukuwa na uwezekano wa kuwa kitu kimoja na JK.

JK na Lowassa mtu wao kule Mbeya ni Mwakipesile. Pia Mwakipesile ndiye anaungwa mkono na vigogo wengi kutoka mkoa wa Mbeya. Mwakyembe anaungwa mkono na Prof. mwandosya.

Wakati mwingine inashangaza hapa jf. huu ni upuuzi, mwakyembe kwenda kumuomba jk agombee kyela!!!!?????

Then alipokubaliwa, baadaye anakuja msapoti mwandosya!! si maajabu haya!!

Takriban wabunge wote hugombea wakitaraji kuwa mawaziri, sio mwakyembe tu, na hii si kosa wala kitu cha ajabu, suala ni kuwatumikia watanzania.

Wakati mwingine tuache upotoshaji na kujifanya tunajua, kumbe wala mambo hayakuwa hivyo!!
 
Wakati mwingine inashangaza hapa jf. huu ni upuuzi, mwakyembe kwenda kumuomba jk agombee kyela!!!!?????

Then alipokubaliwa, baadaye anakuja msapoti mwandosya!! si maajabu haya!!

Takriban wabunge wote hugombea wakitaraji kuwa mawaziri, sio mwakyembe tu, na hii si kosa wala kitu cha ajabu, suala ni kuwatumikia watanzania.

Wakati mwingine tuache upotoshaji na kujifanya tunajua, kumbe wala mambo hayakuwa hivyo!!

Truevoter,

Kabla ya kukosoa wengine angalia facts zako.

Mwakyembe alimuunga mkono prof. Mwandosya kwenye mchakato wa urais kwa CCM ambao ulimalizika mwezi may 2005. Kikwete aliibuka mshindi wa uchaguzi huo.

Dr. Mwakyembe aliamua kugombea ubunge mwezi wa sita/saba na ndio wakati alipomwona JK. Wakati huo JK alikuwa tayari ni mgombea wa CCM na makundi yote yaliungana kumuunga mkono.

Kama ni upuzi sio lazima umeze au usome, wanaotaka kujua watasikia na kujifunza. Nilichoandika hapo juu nina uhakika nacho kwa asilimia 100.

Kama una facts tofauti andika hapa na wananchi watajua nani anasema ukweli na nani anakuja kusagia bila facts, hiyo ndiyo sifa ya JF mkuu.
 
Truevoter,

Kabla ya kukosoa wengine angalia facts zako.

Mwakyembe alimuunga mkono prof. Mwandosya kwenye mchakato wa urais kwa CCM ambao ulimalizika mwezi may 2005. Kikwete aliibuka mshindi wa uchaguzi huo.

Dr. Mwakyembe aliamua kugombea ubunge mwezi wa sita/saba na ndio wakati alipomwona JK. Wakati huo JK alikuwa tayari ni mgombea wa CCM na makundi yote yaliungana kumuunga mkono.

Kama ni upuzi sio lazima umeze au usome, wanaotaka kujua watasikia na kujifunza. Nilichoandika hapo juu nina uhakika nacho kwa asilimia 100.

Kama una facts tofauti andika hapa na wananchi watajua nani anasema ukweli na nani anakuja kusagia bila facts, hiyo ndiyo sifa ya JF mkuu.

Mtanzania.
You can connect political events in any form u want to make it bring the interpretation u need!

Lkn mwakyembe amekuwa mbunge a.mashariki, je huko alitaka awe nani??

Mambo haya ya kusema ukweli hadharani mabaya yanapotokea mwakyembe hajaanza sasa!! he dd the same alipokuwa boardmember wa NBC BANK hadi pale alipojiuzuru mwenyewe!!

Kwa maana hy ccm achilia mbali kikwete wanaufahamu msimamo wake vzr!! hata michango yake mingi bungen inajulikana!!

Si kweli kabisa kw mwakyembe alimuomba jk akagombee kyela!!! statement za namna hiyo zinaonyesha dharau kwa wananchi wa kyela ambao ndio wenye vote ya kuchagua mbunge wamtakae.

Hakuna mtu anaomba kibali kwa mtu kwenda kugombea ubunge!! hz ni fikra potofu!!! na kupotosha ukweli wala haziwasaidii watu.

Mwakyembe hajamwuliza au kuomba kibali mtu yeyote kwenda kugombea ubunge kyela!! ni maamuzi yake binafsi.

Usitake watu waamini kwamba nchi hii kugombea nafasi ya uanasiasa hadi upewe idhin na watu fulani, si kweli, ni competence yako tu!!
 
Mtanzania.
You can connect political events in any form u want to make it bring the interpretation u need!

Lkn mwakyembe amekuwa mbunge a.mashariki, je huko alitaka awe nani??

Mambo haya ya kusema ukweli hadharani mabaya yanapotokea mwakyembe hajaanza sasa!! he dd the same alipokuwa boardmember wa NBC BANK hadi pale alipojiuzuru mwenyewe!!

Kwa maana hy ccm achilia mbali kikwete wanaufahamu msimamo wake vzr!! hata michango yake mingi bungen inajulikana!!

Si kweli kabisa kw mwakyembe alimuomba jk akagombee kyela!!! statement za namna hiyo zinaonyesha dharau kwa wananchi wa kyela ambao ndio wenye vote ya kuchagua mbunge wamtakae.

Hakuna mtu anaomba kibali kwa mtu kwenda kugombea ubunge!! hz ni fikra potofu!!! na kupotosha ukweli wala haziwasaidii watu.

Mwakyembe hajamwuliza au kuomba kibali mtu yeyote kwenda kugombea ubunge kyela!! ni maamuzi yake binafsi.

Usitake watu waamini kwamba nchi hii kugombea nafasi ya uanasiasa hadi upewe idhin na watu fulani, si kweli, ni competence yako tu!!

Mkuu,

Sawa endelea kuamini unavyoamini na wengine tunavyoamini. Hizi ni siasa,
history ndio mwamuzi wa nani anasema ukweli hapa.

Kwenye siasa wala si kitu kipya kwa wanasiasa kwenda kuongea na baadhi ya viongozi kabla ya kuamua kugombea. Dr. Mwakyembe alikuwa ni mbunge wa EA na alitaka kuacha hiyo nafasi ili kwenda kugombea ubunge. Kwa mawazo yangu kwenda kumwambia JK ilikuwa ni makosa maana mtu hahitaji ruhusu ya mtu yeyote ili kugombea ubunge. Hata Msekwa alienda kumwambia JK kwamba anataka kuendelea kuwa spika, je ilikuwa lazima? Wala JK asingeliweza kusema hapana, maana hiyo ni uamuzi wa mtu binafsi.

Lengo la JF ni kuweka facts hapa kama huziamini sawa lakini pia lete facts zako kuonyesha tofauti.

Fuatilia maandiko yangu yote kuhusu politics za Mbeya, ninajua ninasema nini.
 
Inakera,inaudhi na inshangaza kwa hao wanaoleta vikwazo kwa wanaharakati wa kitanzania.Huyo mkuu wa mkoa ni fisadi na mkumbuke kwamba wakuu wa mikoa wako chini ya waziri mkuu,huyu RC lazima alikua connected na baba wa ufisadi TZ kwahiyo baada ya kuona bosi wake ametemeshwa unga yeye ameumia na anajua Ppinda atamuondoa tu.Hizo ni chuki zisizokua na msingi kwa muelewa.Kama kuna mtu anabackground ya shule yake hebu itumeni ili tujue tunamchambua nani.Ppinda tuondolee fisadi huyu wa Mbeya.
 
Siyo siri huyo bwana mkubwa wa Mby alipewa zawadi huko Mby na aliwekwa kwa kazi maalum kumumliza prof.Mwakyembe mbaya wake na mshabiki wa prof.Uliza watu wa Mby hakuna cha maana alichofanya mkoani so far.
 
Siasa za Mbeya kulikoni Mwandosya na Mwakipesile.soma Mtanzania Jumapili tarehe 7/9/2008.

attachment.php


attachment.php
 

Attachments

  • Scan10013.jpg
    Scan10013.jpg
    46.7 KB · Views: 312
  • Scan10014.jpg
    Scan10014.jpg
    287.1 KB · Views: 314
Nafikiri ni propoganda tu, huyo kijana anaitwa steven Mwakajumilo yuko bot mbeya nathibitisha sio tishio kwa Prof. haya ni mambo yanayokuzwa kwa makusudi na wanamtandao.Kijana huyo hana ujasiri huo unaozungumziwa hapa na ajaribu avune aibu aliyovuna mwenzake Thom Mwang'onda.
 
Nafikiri ni propoganda tu, huyo kijana anaitwa steven Mwakajumilo yuko bot mbeya nathibitisha sio tishio kwa Prof. haya ni mambo yanayokuzwa kwa makusudi na wanamtandao.Kijana huyo hana ujasiri huo unaozungumziwa hapa na ajaribu avune aibu aliyovuna mwenzake Thom Mwang'onda.

Taratibu mzee katika uringo wa demokrasia hakuna kutishana tumpe moyo kijana mwenzetu
 
Siasa za mbeya ndo zilivyo, ukabila ndo msingi mkuu, hata hivyo mmesahau kuwa mtanzania ni gazeti la fisadi rostam, mnategemema liandike lolote zuri kuhusu mwandosya?
 
Siasa za mbeya ndo zilivyo, ukabila ndo msingi mkuu, hata hivyo mmesahau kuwa mtanzania ni gazeti la fisadi rostam, mnategemema liandike lolote zuri kuhusu mwandosya?

Huo ukabila ni wajabu wanyakyusa wanachukiana wenyewe!!!!
 
Hii habari haina ukweli kabisa. Hakuna anayeweza kumwondoa Prof. Mwandosya kule Rungwe na hii ni kwasababu yeye ka deliver labda kuliko mbunge yeyote wa mkoa wa Mbeya.

Huyo kijana aende tu na ndio demokrasia, Prof. Mwandosya sio mungu, kama kuna mtu anataka kumpinga ni sawa tu ila sioni nafasi ya prof. Mwandosya kushindwa ubunge Rungwe.

Tutasikia mengi mpaka kufikia hapo 2010.

Hapa hakuna suala la ukabila, wala mambo ya prof. Mwandosya kule Mbeya sio ukabila bali ni siasa za migawanyiko ndani ya CCM.
 
Back
Top Bottom