ELNIN0
JF-Expert Member
- Nov 26, 2009
- 4,161
- 1,460
Wakuu si ushabiki ila nasema ki ukweli kabisa for the first time katika uchaguzi huu tunaona CCM - Ikiweweseka, juzi na jana nilikuwa Arusha nimezunguka sana mjini, talk of the town ilikuwa CCM wapuuzi kumpandikizia kesi DR Slaa eti tumshushie imani yetu kwake hatudanganyiki na kibaya zaidi hii issue imechukuliwa 100% na wananchi wa arusha kuwa ni njama za CCM kutaka kumchafua - vijiwe vya taxi, bodaboda, bajaji, daladala na hata kwa kina mama lishe mazungumzo yalikuwa hayo tu.
Utamaduni wa mwafrika huwa hautilii sana maanani masuala haya na ndiyo maana wengi wao walisikika wakisema " Huyo mwanaume ni mwanaume kweli yaaani hadi unanyang'anywa mke unakuwa wapi ?, sasa eti anataka hela za mezani alipwe na mwanaume mwenzake aisee fanya kazi wewe acha kuomba pesa ya mezani babanguu ni ujinga huo" haya yalikika kwa baadhi ya maoni wananchi hapo Arusha.
Baada ya kushindwa hoja ya U - Padri na udini sasa hii hoja nayo imegonga mwamba, pamoja na magazeti hasa ya Rai, Mtanzania achilia mbali haya ya udaku kuandika jambo hili kiushabiki lakini wananchi bado wana imani kubwa sana na mgombea wa CHADEMA mheshimiwa DR. Slaa.
Kuhusu magazeti yaliyokuwa yanagawiwa bure Wananchi wamesema hawadanganyiki na pesa za CCM kujaribu kumharibia DR. Slaa na wakaenda mbali zaidi na kusema kwamba hawatamchagua mgombea wa CCM arusha mjini sababu ameolewa zanzibar - aende akaishi ya mumewe aiache Arusha yetu.
Mgombea huyo wa Ubunge Arusha Mjini kwa tiketi ya CCM ambaye pia ni waziri ktka serikali ya sasa alikwepa mdahalo uliondaliwa na NEC bila kutoa sababu za msingi.
Wakuu nilitaka niwahabarishe hayo yaliyojiri hapo arusha mjini katika pitapita zangu za juzi na jana kabla ya kurudi DAR.
Utamaduni wa mwafrika huwa hautilii sana maanani masuala haya na ndiyo maana wengi wao walisikika wakisema " Huyo mwanaume ni mwanaume kweli yaaani hadi unanyang'anywa mke unakuwa wapi ?, sasa eti anataka hela za mezani alipwe na mwanaume mwenzake aisee fanya kazi wewe acha kuomba pesa ya mezani babanguu ni ujinga huo" haya yalikika kwa baadhi ya maoni wananchi hapo Arusha.
Baada ya kushindwa hoja ya U - Padri na udini sasa hii hoja nayo imegonga mwamba, pamoja na magazeti hasa ya Rai, Mtanzania achilia mbali haya ya udaku kuandika jambo hili kiushabiki lakini wananchi bado wana imani kubwa sana na mgombea wa CHADEMA mheshimiwa DR. Slaa.
Kuhusu magazeti yaliyokuwa yanagawiwa bure Wananchi wamesema hawadanganyiki na pesa za CCM kujaribu kumharibia DR. Slaa na wakaenda mbali zaidi na kusema kwamba hawatamchagua mgombea wa CCM arusha mjini sababu ameolewa zanzibar - aende akaishi ya mumewe aiache Arusha yetu.
Mgombea huyo wa Ubunge Arusha Mjini kwa tiketi ya CCM ambaye pia ni waziri ktka serikali ya sasa alikwepa mdahalo uliondaliwa na NEC bila kutoa sababu za msingi.
Wakuu nilitaka niwahabarishe hayo yaliyojiri hapo arusha mjini katika pitapita zangu za juzi na jana kabla ya kurudi DAR.