Siasa za Kisasa au Kupoteza Dira kwa Vyama vya Siasa Tanzania? CCM, CUF na CHADEMA!

CCM - Wanaiogopa CHADEMA na kutumia nguvu kupita kiasi kukidhibiti: Wamesahau/wameifunika itikadi yao imara ya 'Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea'

Je ni kwasababu wametekwa na woga wa kivuli chao kinacho sababishwa na mwanga wa CHADEMA? Au ni makusudi kwakuwa viongozi wake wamekiuka miiiko ya chama na wanahangaikia mapenzi yao binafsi? Je vingozi hawa wanaopotosha misingi imara ya Chama cha Mapinduzi wanahofia kuadhbiwa ndo maana wanapambana chama kubaki madarakani au wana nia ya kweli ya nchi hii? chama hiki kitapona na shutuma za undugu?

CHADEMA- Wanadai mabadiliko, yapi? Sikumbuki kuona orodha! Na wanaletaje mabadiliko hayo wanayodai? Wamefanikiwa kuwatisha viongozi wa CCM, kwakuwa wako gizani wamewamulika na tochi ya ghafla, Mwanga wa CHADEMA unatokana na kurunzi yenye tochi imara au za muda tu ambazo zinaweza kufifia kutokana na jazba badala ya sera? Chama hiki kitapona na shutuma za ukabila?

CUF- Walilewa mapenzi ya CCM huko Zanzibar, wanaibuka na kukumbuka wakati wa uchumba, mambo yalikuwa machungu, lakini wakakubali ndoa, sasa wanashtuka kuwa ndoa yenyewe inaweza kuwa chungu kama ile ya uchumbani? Je wameanzisha itikadi ileile ya misingi ya "Kufa baadhi ili wengine waishi milele"? Hawa waliozinduka ni watoto wa kambo wa bara? Wa Zanzibar wana hisia zile zile bado? Je wamegundua kuwa kuna Mke mpya anakutarajiwa kuolewa na CCM? Na wivu umewajaa wanaanzisha kampeni za kumchukia mume wao ili hata huyo mrembo mpya asiingie? Safari Hii CUF itapona na shutuma za udini?

Nia yao ya kugombania kushika madaraka ya nchi hii ni dhati na ya kweli? Au tutaona ya nchi jirani za Zambia na Malawi ambapo waliogombania madaraka kutoka upinzani walifanya madudu zaidi ya yale tuliyoyaona?

Nani kati ya hawa watatu ambao bila ubishi wanashikilia hatamu ya siasa za Tanzania, atatupeleka kwenye nchi yenye neema na amani kwa watu wote bila kujali itikadi, hali yao kiuchumi, kisasa, kidini au kiasili? unahitaji nini kati yao, moja wapo ya chama hiki au Kiongozi kati yao atakaebadilisha upepo na kutuepusha na mgao unaofanywa na vyama vyote hivi (kwa manufaa ya hao wanaoongoza vyama hivi kwa kuwa wanataka kuendelea kuwepo madarakani?) Huko madarakani kuna nini?

Nani atatuambia tutatokaje na siku moja itakayolengwa kwa sisi kuwa sehemu ya taifa Afrika, au Duniani imara kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kimaendelo kwa ujumla (sayansi, usalama wa chakula, nafasi sawa ya elimu kwa wote, huduma za afya wote, maji safi kwa wote, ziada ya fedha, dhahabu na mafuta ambavyo tunavyo na kila mtu akimvumilia mwenzake na kumheshimu).

Kama ungependa kunukuu makala hii kwenye gazeti, wasiliana nami kwa kuni PM.

CCM ni chama kilichojiimarisha vizuri kwa sera zake nzuri na mara zote kimekuwa kinajiweka karibu na wananchi kwa lengo la kupata ushirikiano wao,matumizi ya rasirimali za nchi zikiwemo watu,mali asili,ardhi na fedha za walipa kodi zimeisaidia CCM kuendelea kuonekana kama chama kinachopendwa zaidi,hii ni kwa sababu watu wamekuwa wakinufaika na utajiri huu mkubwa ulionao CCM katika nafasi mbalimbali na hasa katika uongoz wa chama na wasomi wachache wanaotumiwa na CCM kwa mda mrefu sasa!!!CCM kama vilivyo vyama vya siasa vingine lengo lake kubwa ni kuendelea kukaa madarakani kwa njia yoyote ile ndo maana wako tayari kutumia kiasi chochote kile cha gharama kuendelea kubaki madarakani hata kama ni kuwanyima wananchi haki zao za msingi zikiwemo za kuchagua wakipendacho na kuheshimiwa kwa maamzi yao!!!TATIZO KUBWA LA CCM ni kuwanyima uhuru wanachama wake na hasa viongozi wa ngazi za chini kuamus na kupendekeza kile wanachokitaka na badala yake mambo mengi wamekuwa wakiamriwa na wakubwa wao na kulazimishwa kufuata kwa kigezo cha kwamba ndo msimamo wa chama,kwa sababu hiyo wanapuuza yote yatakayosemwa na wote ambao wanapingana na msimamo wa chama hata kama si katika suala husika.....imani yangu ni kuwa viongozi wengi wa CCM wanapinga mengi ya upande wa pili kwa sababu tu yanatoka upande wa pili lakini wanajua wazi ni maoni yenye msingi na tija kubwa kwa taifa kutokana na hili viongozi/wanachama wengi wa CCM wamekuwa wakishirikiana na upande wa pili either kwa kutoa siri au kwa kusaidia harakati za kutendea haki wananchi....uelewa mdogo wa wananchi wa vijijini juu ya mageuzi na demokrasia ni silaha kubwa kwa CCM kuendelea kuaminika kwa wananchi hao!!!!!!!!!!SIASA ZA UDUGU kama ilivyo kwa nchi nyingi za kiafrika hii sasa inaonekana ni kawaida lakini ubaya siuoni kwa sababu asilimia kubwa wanauwezo na baadhi yao wamechaguliwa na wananchi wenyewe!!!CCM bado ina nafasi kubwa katika siasa za TZ cha msingi wajitahidi kuleta demokrasia ndani ya chama ambayo imekuwa haipo kwa mda mrefu ni lazima wasome alama za nyakati BILA hivyo itapata usaliti mkubwa na kuparanganyika,kitu cha pili wajitahidi kusoma na kuelewa mambo hii itawasaidia kujibu hoja bila jazba na lugha za kejeli,wao ni chama tawala lazima wawe mfano mzuri.

CHADEMA ni chama kilichopata umaarufu TZ bara na hivyo kupata uungwaji mkono na watu wengi sana,ni chama kinachoisimamia serikali pasipokuogopa na viongozi wake wamejitoa kwa dhati kusimamia kile wanachokiita maslahi ya TAIFA,mara nyingi kimekuwa kikizua mambo ambayo mwanzoni huonakana kama uzushi lakini badae huonakana kuwa ni ukweli na hivyo wao huonekana ni watu makini na wenye vielelezo tosha na wenye kujishughulisha katika uchunguzi,utafiti,kujenga hoja na kuzisimamia,kina wabunge wachache lakini hutoa taswira nzima ya upande wa pili!!!CHADEMA ni chama chenye viongozi imara,thabiti na wasioogopa chochote katika kile wanachoamini wao kuwa ni haki ya wananchi,wameleta mapinduzi ya kweli katika siasa za TZ na kuleta msukumo mkubwa wa kimaendeleo katika nchi yetu,ni chama pekee TZ chenye sapoti kubwa toka vyama vingine ingawa sapoti hiyo inatoka kwa siri ili wasijekuadhibiwa...CHADEMA imejiimarisha sana mijini kutokana na uelewa mkubwa wa watu wa mjini,inayo kazi kubwa kuaminika vijijini kutokana na uelewa mdogo wa wananchi na uwekazaji mkubwa wa CCM.UKABIRA dhana hii imesikika kwa mda mrefu sana lakini kabla ya hii pia ilikuwepo dhana ya ukristu sasa inawia ugumu kuelewa kuwa baada ya kushtukiwa na ukristu sasa wameelekea kwenye ukabila???wasidharau kinachosemwa kama kweli wana nia ya dhati na taifa hili ingawa hoja hiyo haina nguvu yoyote kwa sababu hawajatoa masharti yoyote ya kikabila kwenye kujiunga na chama na hata kugombea uongozi!!!!!!CHADEMA bado kinaendelea kuwa chama bora cha upinzani TZ bara

CUF ni chama chenye umaarufu mkubwa ZNZB,ni chama thabiti chenye msimamo imara wa kusikiliza kile wananchi wanachokitaka na kukifanya,kimeendelea kuwa ni chama chenye mvuto ZNZB kuliko CCM na kinakuwa maarufu kadri siku zinapokwenda.CUF kilifanya maridhiano na CCM na kutengeneza serikali shirikishi hii ilikuwa ni baada ya vurugu baada ya uchaguzi,walishirikiana kwa lengo la kuepusha machafuko lakini si kwa mitazamo ya ki-sera na mitazamo,,CUF bado wameendelea kuwa misimamo yao na hivyo wakajikuta msimamo wao unaendana na msimamo wa CDM na NCCR hivyo ndoa yao kwa kiasi kikubwa imeegemea katka katiba mpya hasa muundo wa serikali....ingawa wanadai umoja huu ni endelevu lakini sizani kama utadumu muda mrefu...na kama utavunjika basi CHADEMA ndo watahasirika kwa kiasi kikubwa kwa sababu hoja zao karibu zote ni za kuitetea ZNZB/CUF kwa hiyo UKAWA ukivunjika CDM watapoteza nguvu za kutetea msimamo wao.CUF bado kina nguvu na ndo chama cha upinzani pekee chenye uwezo wa kushinda urais huko ZNZB.
 
Profesa: Hivi sasa hivi kuna CHADEMA au kuna UKAWA? Wewe unasikia jina la CHADEMA tena nchi hii? Sasa hivi ni UKAWA, utasikia majina ya CHADEMA, CUF na NCCR mwakani when it is too late!
 
Katika historia ya nchi hii ni chadema pekee ndo kimeweza kuwavuruga ccm kwa karibu miaka kumi sasa
 
Back
Top Bottom