Siasa za CHADEMA kama za CCM

Kwanza nashukuru ndugu yangu kwamba tumetoka kubishana hadi sasa kujadiliana, hayo ndiyo mabadiliko ya kweli na Uhuru wa Kweli ambao CHADEMA inaupigania.

Igunga hoja kubwa ilikuwa kama Igunga ni maskini au si maskini na kama ni maskini ni nani kausababisha huo umaskini. Kwa hoja hii CDM walishinda kwani wananchi wenyewe wa Igunga wanajua umaskini wao. Pia Igunga walikuwa hawawachagui hao niliowaorodhesha bali walikuwa wanataka kuchagua Kashindye mwana Igunga mwenzao na mwalimu maarufu anayefahamika na wengi.

CUF hawakuchaguliwa kwa sababu wenyewe waliwekeza kidogo kwenye upelekaji wa ujumbe wao kwa wananchi hadi wakashindwa kujitofautisha wao na CCM ambao wananchi wa Igunga walishaamini ndiyo wezi wa rasirimali zao na ndiyo waliosababisha wao wawe maskini.


Hakuna anayejua kwenye suala la kura ni za nani zilikwenda CDM. Kwa nini usifikiri kwamba za CUF zilikwenda CCM na CDM wao walichota za CCM?
Kura za CUF zilipungua kwa sababu walikuwa hawana hoja mahsusis inayokubalika kwa wananchi. Halafu kumbuka ndoa ya CCM na CUF ni mzigo unaowatesa CUF huku Tanzania Bara.



Hivi vyama vyote ulivyovitaja uwekezaje wake wa kifedha na rasirimali watu huwezi kuufananisha na CCM na CDM. CDM walikuwa na Helkopta moja wenzao wa CCM walikuwa nazo mbili. Igunga kuna kata 26 hivi vyama vingine hata magari walifanya kukodisha au walikuw nayo chakavu. kwa mantiki hiyo utaona ni kwa nini mvutano ulikuwa ni kwa CCM na CDM na CUF kwa Mbaaali.

Wabunge wa CCM na CDM walikuwa wanapishana mbugani na magari yao huku wengine wa vyama hivi hata kuzindua kampeni zao walikuwa na Horn speakers tu. heri yule wa UPDP alituburudisha kwa Mayenu.

umenijibu vema!
 
TAFAKARI CHUKUA HATUA. Ujumbe umefika maana hakuna ata mtu anayepinga kwa ushahidi kama ulivyofanya wewe.

A/c ilifungulia mwaka gani?na rasta alikuwa na nafac gani chadema.Mbowe alioa mwaka gani kwa Mzee Mtei?na chadema ilianzishwa lini?cdm ndio inaanza kujulikana nchi nzima,hivyo ilikuwa ni lazima ipate viongozi ambayo wameshailewa.
 
hata wakiwa wote pilipili usiyoila yakuwasha nini? Buku 2 ya lunch imekutoa leo.

Unashangaza. Yaani suala la chama cha siasa ambacho ni taasisi ya umma kupachikana madarakani kwa upendeleo unaita pilipili usiyoila! Kweli wewe umepauka kichwani.
 
Unashangaza. Yaani suala la chama cha siasa ambacho ni taasisi ya umma kupachikana madarakani kwa upendeleo unaita pilipili usiyoila! Kweli wewe umepauka kichwani.

wewe mchumia tumbo utashauri nini? Kelele zako ni sawa na za mfa maji.Nakushauri maliza kwanza uasi na makundi kwenye chama chako Magamba
 
hata wakiwa wote pilipili usiyoila yakuwasha nini? Buku 2 ya lunch imekutoa leo.

Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.

Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.

Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.

Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni
 
migwanda bwana sasa nape anahisika nn hapo au kawashika sana.. mbona hamkanushi kama ni uongo huo ulioandikwa...

Huyu jamaa kila post yake lazima amtaje nape, sijui kwa nini lakini uwezi kujua asifie mvua imemnyea...Ha! Ha! Ha! Ha!
 
2025 January Makamba na Zitto kabwe wananchukua nchi kupitia CCM au mseto wa magamba na magwanda. Its funny how democracy fools walalahoi na wafanyakazi wa kawaida wakati its an elite game. cha kufanya msibishane sana ingieni CDM gombeeni nafasi za uongozi hamjachelewa sana, CCM kumejaa 2025 itawakuta bado hata udiwani hamjapata.
kumbuka nchi maskini uongozi ni nafasi ya kujiweka sawa kifamilia zaidi na kidogo kusaidia wananchi wasife njaa kwa sababu ukiwasaidia sana watataka kushirika na wenyewe kuongoza na democracy is elitist yaani kitu cha wachache
 
Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.

Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.

Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.

Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni

naona una hasira leo lunch kakunyima nini? Ukiwa na post chache unashindia chips dume
 
Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.

Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.

Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.

Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni

Kweli wewe hamnazo sasa hivyo navyo ni vitu vya kutangaza kwa watu,mbona ni vya kawaida sana kila mtu anavyo,anyway inawezekana wewe ni mshamba sana.
 
CHADEMA na wafuasi wake wanapeana vyeo hii inaitwa nepotism itakuaje hawa akina mama mzazi Zitto, mke wa Slaa, binti ya ndesamburo, dada wa lissu, hawa akina Komu etc wana vigezo gani kushinda au kuchanguliwa hivyo viti na CHADEMA kama itakuja kushika dola inabidi ituonyeshe kwanza yenyewe haichagui watu katika vikao informal vya watu wachache kama wafanyavyo CCM. lazima kuwe na demokrasia kutoka ndani ya chama. Kuna wagombea nawajua walikua na sifa za kutosha kupata hivyo viti na hawakupata viti hivyo maalum.
 
CHADEMA na wafuasi wake wanapeana vyeo hii inaitwa nepotism itakuaje hawa akina mama mzazi Zitto, mke wa Slaa, binti ya ndesamburo, dada wa lissu, hawa akina Komu etc wana vigezo gani kushinda au kuchanguliwa hivyo viti na CHADEMA kama itakuja kushika dola inabidi ituonyeshe kwanza yenyewe haichagui watu katika vikao informal vya watu wachache kama wafanyavyo CCM. lazima kuwe na demokrasia kutoka ndani ya chama. Kuna wagombea nawajua  walikua na sifa za kutosha kupata hivyo viti na hawakupata viti hivyo maalum. 
 
Aliyekuwa diwani wa kata ya kaloleni kupitia CHADEMA inasemekana anatafutwa na Polisi kwa tuhumu za kumtapeli mwekezaji mwenza kwenye biashara yao ya utalii. Charles David Mpanda (Rasta) anadaiwa kumtapeli Margaret Lema kiasi cha Dola 16,400 kutoka kwenye akaunti yao ya pamoja.

Hili jambo limenifanya nifikirie upya siasa za bongo. Margaret ni Mdogo wake God bless Lema Mbunge wa Arusha Mjini kwa maana nyingine yale yanayotokea CCM kwa watu wa ukoo mmoja kumiliki chama yanatokea na CHADEMA pia. Mbowe kaoa mtoto wa Edwin Mtei Muasisi wa CHADEMA, Lucy Owenya mbunge wa viti maalum ni mtoto wa Philimon Ndesamburo Mbunge wa Moshi Mjini.

Ukikutana na Rose Kamili Mbunge wa viti maalum ujue ni mzazi mwenzie Dr. Wilbroad Slaa pia ujue kwamba ukikutana na Christina LIssu ni Mdogo wake na Tundu Lissu, na Moulida au Anna Komu Mbunge Viti maalum ni Mke wa mkuu wa Idara ya fedha Makao Makuu CHADEMA, Anthony Komu. Hawa ni wale wanaohusiana kimapenzi na kiukoo hatujui wale wanaohusiana kimaslahi kama vile kibiashara wako wangapi na kwenye ngazi zipi. Lakini jambo hili kwa sababu limetokea CDM basi litatetewa weeee hadi mijasho itukauke.

Aliyekuwa mkuu wa upelelezi Kanda Maalum ya Dar es salaam Abdalah Zombe alidai kwamba Godbless Lema alikuwa ni mwizi wa magari. Sijaona mcharuko mkubwa angalau wa kumshinikiza Zombe aseme anavyojua wizi wa magari wa Lema wala wa kumshinikiza Lema kueleza historia yake ya nyuma kabla hajawa Mbunge inahusiana vipi na wizi wa magari. Wote tuko kimyaa kwa sababu ni mtoto wa nyumbani. Rage kuonyesha Bastola ilikuwa nongwa lakini la Lema ni "Uzushi' wa magamba.

Umemaliza mkuu? ukimaliza nijulishe ndio nichangie..............
 
Sasa wewe kila siku kelele tu kama una pesa kajenge Makao Makuu ya CDM pale Manyanya.

Makao Makuu utadhani ofisi ya Saccos ya Tandale.

Mimi kwa siku tu natumia all most $60 kwa ajili ya Internet tu, Laptop, Desktop, BlackBerry Touch.

Nakushauri fanya kazi acha kukaa kwenye vijiwe vya mbege na komoni

Wakuu huyu jamaa wa wapi? ha ha ha ha ha!!! Punguani sana wewe,yaani kweli unaleta uharo kama huu hapa JF? Na mods hivi mawazo majitaka kama haya tunafanyaje? Yaani wewe unafaa sana facebook,nenda kaweke picha yako pale na andika huu uharo pale,utapata marafiki mapunguani wenzako....
 
Mh..huyu kweli ni MPIGWANAJI..pointless kwa kwenda mbele.
So bwana mabunduki ana wife mwingine apart from jose?I DIDNT KNOW
 

Umemaliza mkuu? ukimaliza nijulishe ndio nichangie..............
Ukisubiri wamalize hoja itapotoshwa ,ni bora uchangie ingali moto. CHUMA KIKOLI MOTO. Nimewahi kuchangia kuhusu CDM kujipanga kufungua matawi mengi vijijini lakini nikatahadharisha kuwa vijana baadhi wa CDM hawana uwezo wa kujenga hoja kisayansi kuvutia hadhira hasa ya wenye umri wa miaka 50 hasa akina mama ambao ni mtaji mkubwa. Nimesoma michango hapa ni matusi, hoja hazishikiki, mtawapataje wanachama makini wanaotaka kushawishiwa taratibu? Watu wazima hawapokei mageuzi mara moja wanatafakari kwanza. Refer; CONSUMER BEHAVIOUR, hoja dhidi ya CDM hata zikiwa zinauma kiasi gani na ukweli ndani yake tusijibu kwa jazba as if CDM ni malaika,tunakosea.NGUVU YA NGUVU HAILETI TIJA EXCEPT HOJA YA NGUVU MAKES ALOT
 
.... lakini nikatahadharisha kuwa vijana baadhi wa CDM hawana uwezo wa kujenga hoja kisayansi kuvutia hadhira hasa ya wenye umri wa miaka 50 hasa akina mama ambao ni mtaji mkubwa
Hao vijana ndiyo balaa kwa kuporomosha "mistari" bila vina wakiulizwa kulikoni wanajitetea eti ni wapiganaji. Kwa taarifa yao wanamtandao waliomweka Kikwete madarakani mwaka 2005 ndiyo walikuwa wanajiita wapiganaji labda hili la "makamanda" ndiyo jipya.

Hasa akina mama ambao ni mtaji mkubwa. Nimesoma michango hapa ni matusi, hoja hazishikiki,mtawapataje wanachama makini wanaotaka kushawishiwa taratibu?
Ni kweli kwa sababu watu wenye umri mkubwa wanajua mengi wanakumbuka tangu enzi za AMNUT mpaka Mtikila alipotuletea misamiati ya "walalahoi" na "magabachori" huku akituchombeza na kauli mbiu "Saa ya ukombozi ni sasa. tumeona mengi.

Watu wazima hawapokei mageuzi mara moja wanatafakari kwanza. hoja dhidi ya CDM hata zikiwa zinauma kiasi gani na ukweli ndani yake tusijibu kwa jazba as if CDM ni malaika,tunakosea.

Hapo kwenye kuvumilia CDM kukosolewa ndipo udhaifu wa CDM ulipo. Zamani huko amerika ilikuwa ukitaka kumaliza mpinzani wako kisiasa unamwita Mkomunisti, basi Kwisha kazi. Hata kama jamaa alikuwa na hoja kiasi gani akishaitwa Mkomunisti inakuwa ndiyo mwisho wake kisiasa. Sasa hapa bongo tunaona watu wakiikosoa CDM basi inakuwa kama vile umeingiza mkono kwenye mzinga wa nyuki. Magamba huyo, fisadi, umetumwa, una njaa maneno mengine meengi yasiyo na maana.
 
Back
Top Bottom