ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,904
- 6,904
Hbr wana Jamvi.
Nitangaze kukipenda CDM. Nilipata kadi ya CDM mwaka 2007 wakati Dr. Slaa, Prof. Baregu na wengine wengi walipofanya mdahalo ukumbi mmoja pembeni ya mliman city, eneo la survey ilikuwa 2007, Kipindi hicho nilikuwa 2nd year. Niliamua kuchukua kadi yao kwa kuwa niliamini CDM kimebeba matumaini ya watanzania. Na kwa kazi waliyoifanya kipindi kile CDM walistahili pongezi na ndo iliwafanya wafike hapo walipo leo.
Siku zote maisha ni kupanda na kushuka. Katika medani za siasa,
(i) NCCR Mageuzi ilipanda chat sana, lakini baada ya muda ikashuka 1995-2000
(ii) Kushuka kwa NCCR, kukatoa mwanya wa CUF kupanda ambapo wameshika hatamu kwa vipindi viwili mfululizo hasa kwa kuwa na idadi ya wabunge wengi. 2000-2010. Kuingia kwao kwenye makubaliano na CCM,ndo ukawa mwisho wao wa kushika hatamu kwa vyama vya upinzani Tanzania.
(iii) CHADEMA, wakatumia mwanya huo, mpaka wameshika hatamu ambayo itawafikisha 2015, lakini naamini watafika 2015 wakiwa hoi kama hawatafanya mabadiliko ya kiutendaji ndani na nje ya CHAMA. Kinachowaua ni kile kilichowaua CUF, KUINGIA MIKATABA YA KILAGHAI na CCM
Swali langu ni je, iwapo CDM ambacho kimekuwa kikitumainiwa na wananchi waliowengi, na kilikuwa mbioni kuaminiwa kupewa nchi, kama hawatabadilika na kupotosha matamko yaliyotolewa na Mnyika baada ya wao kuingia makubaliano maalum na CCM, ya kutoshiriki kwa namna yoyote ile mchakato wa kupatikana katiba mpya, na kusitisha MAANDAMANO yaliyowafikisha hapo walipo. NANI ATASHIKA HATAMU? WATANZANIA WATAMWAMINI NANIU TENA? TLP? UDP? UPDP au SAU?
Naona akilini mwangu nashuhudiwa kuwa Tanzania hakuna upinzani, bali wote wamekuwa ni vibaraka wa CCM. Mrema alianza vizuri, mwisho karudi nyumbani=CCM, Maalim Seif alipanda chat, lakini karudi CCM, CDM, wamepanda chat mwisho wake wamerudi CCM, hii ni kwa makubaliano waliyoyafanya na kisha kumtuma MNYIKA kuwa msemaji wa CHAMA.
Dr. Slaa na Zitto vipenzi wa wengi nchini na wenye ushawishi, wako wapi?
Tujadili kwa manufaa ya kukuza demokrasia nchini
Nitangaze kukipenda CDM. Nilipata kadi ya CDM mwaka 2007 wakati Dr. Slaa, Prof. Baregu na wengine wengi walipofanya mdahalo ukumbi mmoja pembeni ya mliman city, eneo la survey ilikuwa 2007, Kipindi hicho nilikuwa 2nd year. Niliamua kuchukua kadi yao kwa kuwa niliamini CDM kimebeba matumaini ya watanzania. Na kwa kazi waliyoifanya kipindi kile CDM walistahili pongezi na ndo iliwafanya wafike hapo walipo leo.
Siku zote maisha ni kupanda na kushuka. Katika medani za siasa,
(i) NCCR Mageuzi ilipanda chat sana, lakini baada ya muda ikashuka 1995-2000
(ii) Kushuka kwa NCCR, kukatoa mwanya wa CUF kupanda ambapo wameshika hatamu kwa vipindi viwili mfululizo hasa kwa kuwa na idadi ya wabunge wengi. 2000-2010. Kuingia kwao kwenye makubaliano na CCM,ndo ukawa mwisho wao wa kushika hatamu kwa vyama vya upinzani Tanzania.
(iii) CHADEMA, wakatumia mwanya huo, mpaka wameshika hatamu ambayo itawafikisha 2015, lakini naamini watafika 2015 wakiwa hoi kama hawatafanya mabadiliko ya kiutendaji ndani na nje ya CHAMA. Kinachowaua ni kile kilichowaua CUF, KUINGIA MIKATABA YA KILAGHAI na CCM
Swali langu ni je, iwapo CDM ambacho kimekuwa kikitumainiwa na wananchi waliowengi, na kilikuwa mbioni kuaminiwa kupewa nchi, kama hawatabadilika na kupotosha matamko yaliyotolewa na Mnyika baada ya wao kuingia makubaliano maalum na CCM, ya kutoshiriki kwa namna yoyote ile mchakato wa kupatikana katiba mpya, na kusitisha MAANDAMANO yaliyowafikisha hapo walipo. NANI ATASHIKA HATAMU? WATANZANIA WATAMWAMINI NANIU TENA? TLP? UDP? UPDP au SAU?
Naona akilini mwangu nashuhudiwa kuwa Tanzania hakuna upinzani, bali wote wamekuwa ni vibaraka wa CCM. Mrema alianza vizuri, mwisho karudi nyumbani=CCM, Maalim Seif alipanda chat, lakini karudi CCM, CDM, wamepanda chat mwisho wake wamerudi CCM, hii ni kwa makubaliano waliyoyafanya na kisha kumtuma MNYIKA kuwa msemaji wa CHAMA.
Dr. Slaa na Zitto vipenzi wa wengi nchini na wenye ushawishi, wako wapi?
Tujadili kwa manufaa ya kukuza demokrasia nchini