Siasa za CCM na muungano wa Zanzibar

nanchi

Member
Jan 29, 2012
66
7
Ndugu wanajamvi naomba kufahamu kutoka kwenu kuhusu muungano wa tanganyika na zanziba.1;nini sababu iliyopelekea kuwa na muungano.2;watanganyika na wazanzibar waliafiki?3;viongozi hawa walitumia njia gani kupata maoni ili kuidhinisha huo muungano?inanishangaza pale ninaposia suala la muungano kwenye katiba mpya halijadiliwi.
 
Msome Joseph Mihangwa kwenye magazeti ya Raia Mwema matoleo ya nyuma. Majibu ya maswali yako yote utayapata.
 
lengo la mwalimu lilikuwa kuiunganisha afrika iwe moja na akaanza na kuunga zanzibar baadaye kenya na uganda. kura ya maoni haikuitishwa. bahati mbaya kenya na uganda wakakataa. sasa sababu ya kuwa nchi mbili badala ya tatu au moja ni uwiano tofauti kati ya zanzibar na tanganyika
 
Siamini mpaka leo unaulizia majibu ya maswali amabayo yako wazi miaka nenda miaka rudi
 
Siamini mpaka leo unaulizia majibu ya maswali amabayo yako wazi miaka nenda miaka rudi

Haukulazimishwa kuchangia mm nilitaka kujua na wenye busara wamefanya hivyo,usishobokee usicho kiweza.
 
Johmbaaa tulia hapa hapa, naingia Maktaba yangu naenda kukuchukulia nondo za kujibu maswali yako!
 
Hujaridi bado mpemba mbishi ..? Nasubiri nondo hizo yakhe ...

Katika
kuuangalia muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwanza ni
vyema zijulikane sababu hasa
zailizopelekea Tanganyika na Zanzibar
kufikia uamuzi wa kuungana. Kwa
mujibu wa mafundisho ya mashuleni
na vyuoni sababu kubwa za kuungana baina ya Tanganyika na
Zanzibar ni hizi zifuatazo. Kwanza ni
udugu wa damu na wenye mizizi
mirefu uliyopo baina ya wanganyika
na wazanzibari. Kwa kuirejea historia
ya mafungamano baina visiwa vya Zanzibar na bara la Afrika itagundulika
kwamba mafungamano hayo
yameanzia kwa karne nyingi sana
nyuma kiasi cha karne ya 15 au 16
wakati muungano wa Tanganyika na
Zanzibar uliibuka katikaki ya karne ya 20 ambapo asili za kibantu kwa
wazanzibari tayari zimeshapotea kwa
kiasi kikubwa kutokana na
kuchanganya damu na watu wa asili
za mbali mbali za kiasia ambao ndio
wengi zaidi. Hata hivyo asili za wazanzibari ni vyanzo vingi vikiwemo
Afrika, Pashia, India na Arabia.
Ijapokuwa Afrika ni miongoni mwa
vyanzo vya asili za wazanzibari lakini
ifahamike kuwa ni kutokea sehemu
mbali mbali za Afrika zikiwemo Tanganyika, Msumbiji, Malawi, Kenya,
Uganda, Rwanda, Comoro nk. Sababu nyengine inayohusishwa na
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ni historia ya ushirikiano kati
ya chama cha TANU na ASP, ambavyo
vyote ni vyama vya kupigania
ukombozi wa watu weusi kupitia harakati za kudai uhuru zilozozuka
miaka ya 1950 na 60 katika bara la
Afrika. Hapa ikumbukwe kuwa sio
chama cha ASP peke yake
kilichoshiriki mapambano ya
kumng’oa mkoloni Zanzibar. Bila shaka kilichomvutia Nyerere na
kuamua kukiunga mkono chama cha
ASP peke yake na kufanya
mashiriukiano nacho katika harakati
za kudai uhuru wa Zanzibar ni ile ile
itikadi ya mapambano dhidi ya watu wasio na ngozi nyeusi mambo
ambayo yalikuwa yamepamba siasa
za Karume. Vyama vyengine vya
kizalendo vya wazanzibari havikuwa
na mvuto wowote kwa Nyerere.
Wakati chama cha TANU kinaongozwa na sera ya “uafrika” katika kupigania
uhuru na hivyo kuwaunganisha
watanganyika wote, ASP kwa upande
wake iliifumania sera ya “ugozi
mweusi” ikidhania kuwa ndio uafrika
wenyewe na hivyo kuwatenga wazanzibari wengine. Vyama vya
TANU na ASP vilisahau kwamba
asilimia kubwa ya wazanzibari tofauti
na watanganyika wakiwemo hao
wenye ngozi nyeusi wana asili zao
kutoka nje ya bara la Afrika. Muungano ni matokeo ya hofu mbili
Hizi zilizotangulia kutajwa labda
zinaweza kuwa sababu ndogo ndogo
za muungano huu. Sababu muhimu
hasa zilizopelekea muungano wa
Tanganyika na Zanzibar ni hofu mbili zifuatazo. Hofu ya ya kwanza ilitokana
na uwezo mdogo sana wa kijeshi na
kiulinzi iliokuwanao serikali ya
mwanzo ya mapinduzi. Nguvu za
kijeshi na kiulinzi zikitegemea sana
mizinga ya kichina na kisovieti ya kutungulia ndege pamoja na silaha
ndogo ndogo (Armit 1986). Uwezo
huo mdogo wa kujihami
unawezakuwa ulijenga hofu kwa
Karume na Nyerere juu ya uwezekano
wa Sultani na Moh’d Shamte kujipanga na kurudi ili kufanya mapinduzi
mapya (counter revolution) dhidi ya
serikali ya Karume. Kutokana na hofu
hiyo basi Nyrere alimshauri Karume
kuziunganisha nchi zao ili kupata
nguvu kubwa ya kiulinzi ya kuihami Zanzibar dhidi ya mapinduzi mapya. Hii
inaweza kuwa ndio sababu kubwa ya
Karume kushishitiza kwamba
muungano huu utakuwa ni wa kipindi
cha miaka kumi tu ambapo itabidi
utathminiwe upya kama unahitajika au laa. Karume alifahamu wazi
kwamba ndani ya kipindi hicho cha
miaka kumi tayari serukali yake
imeshajiimarisha vya kutosha kwa
nguvu za kijeshi. Hofu ya pili ni ile iliyozifanya dola za
magharibi kuiona serikali mpya ya
mapinduzi ya Zanzibar kuwa
ingeweza kuwa angamizo la ubepari
katika ulimwengu na bara la Afrika.
Ushiriki wa Babu na wakomyunisti katika mapinduzi ya 1964 iliiifanya
serikali mpya ya mapinduzi kuwa ni
tishio kwa Marekani na dola za
magharibi. Hofu hii ya nchi za
magharibi inathibitishwa na simu ya
balozi wa marekani nchini Tanganyika wakati huo bwana William Leonhart
alioituma kwa wizara ya mambo ya nje
ya serikali ya marekani siku ya tarehe
27 Aprili 1964 : “Sina wasiwasi kwamba
watanganyika wanategemea kuwa
wakomyunisti waliomo katika serikali
ya Zanzibar watazimwa kwa
kufunikwa na kutofungamana
upande wowote kwa Tanganyika, lakini kutokana na kasi na nguvu za
mwendo wa wakomyunisti
wanaokwenda mbio nchini Zanzibar
na sio kuitishia ka kuitumilia hali
katika njia ambazo serikali ya
Tanganyika haitoweza kuzifikiria. Ninaamin kwamba ni muhimu Nyerere
apewe msaada wa kimya kimya wa
kiasi kikubwa iwezekanavyo na nchi
za magharibi tokea mwanzo” (Armit
1986). Ingawa wengi wa makomred
wakiongozwa na Babu waliukataa
kwa nguvu zote muungano huo lakini
Bwana Ali Sultan Bin Issa anasema
katika kitabu cha Burgess cha The
race, revolution and sruggle for human rights in Zanzibar: “Mimi binafsi sikuona tatizo kuukubali
muungano. Japo kuwa lengo la
Nyerere ilikuwa ni kuwameza
wazanzibari, mimi niliona ni ukombozi
na jukwaa kubwa zaidi la siasa zetu
(za kikomyunisti). Pia ni fursa pekee ya kueneza ukomyunisti Tanzania
bara” (Burgess 2009). Mkataba wa muungano
Siku ya tarehe 22 Aprili 1964 Nyerere
na Karume walitia sahihi mkataba wa
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar. Kumbukumbu za kihistoria
zinasonyesha kuwa Karume alidhani alitia sahihi mkataba wa kuzitambua
nchi mbili huru zenye mamlaka kamili.
Na hivi ndivyo ilivyokuwa katika
mkataba huu wa mwanzo wa
muungano. Yaani kwa mujibu wa
mkataba huo mahusiano ya Tanganyika na Zanzibar kisiasa ni
kama yalivyokuwa mahusiano baina
ya Ireland ya Kaskazini na Uingereza.
Mkataba huu wa mwanzo wa
muungano uliiachia Zanzibar kiasi
Fulani cha madaraka yake ya ndani kama vile polisi, mahakama, kilimo nk
wakati madaraka muhimu kama vile
mambo ya nje, ulinzi, biashara,
shughuli za muungano, udhibiti wa
fedha za kigeni na kuchagua maafisa
(watendaji) wajuu kabisa wa Jamhuri ya muungano yalikuwa chini ya
mamlaka yaserikali kuu ya
muungano. Siku ya tarehe 25 Aprili
1964 Bunge la Jamhuri ya Tanganyika
ililiridhia sheria ya muungano kama
ilivyoridhiwa na baraza la mapinduzi la serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.
Sheria ya muungano wa Tanganyika
na Zanzibar ilielekeza mambo kumi na
moja (11) yaliotokana moja kwa moja
na “mkataba wa muungano”. Mkataba
wa muungano uliutaka muungano huo hapo mwanzoni udumu kwa
muda wa miaka kumi (10) tu, yaani
kutoka 1964 hadi 1974. Hata hivyo
mkataba hu wa asili ulio na saini za
waasisi wawili wa muungano huo
Karume na Nyerere haujulikani uliktokomea hadi leo hii. Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ulifanywa kukidhi matakwa
ya kisiasa ya watu wawili, Nyerere na
Karume. Hakuna kura ya maoni wala
mazingira yeyote ya kidemokrasia
yalioandaliwa na kufanywa ili kuwasikiliza wananchi wa pande mbili
za muungano kama wangependelea
kuunganishwa kwa nchi zao au laa.
Kifungu cha 6 (1) cha mkataba wa
muungano kinasema kwamba “Rais
wa kwanza wa Jamhuri ya muungano atakuwa Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere”. Kifungu cha 6 (2) kinasema
“Makamo wa kwanza wa rais kwa
mjibu wa mabadiliko yanayopatikana
kwenye aya ya (c) kifungu kidogo (1)
ya sehemu ya 5 atakuwa sheikh Abeid Karume”. Kuwepo kwa kifungu hichi
cha 6 kwenye sheria ilioanzisha
muungano (sheria namba 22, ya 1964
kwa upande wa Tanganyika ni ishara
ya wazi wazi kuwa muungano huu
uliundwa kukidhi matashi ya watu wawili na sio dola mbili. Waasisi hawa
wa muungano waligawana madaraka
vile walivyoona wao wenyewe inafaa. Hapa ndipo safari ya Zanzibar
kumezwa na Tanganyika ilipoanzia.
Sheria ya muungano namba 22 ya
1964 ilkuwa na dhamira nzuri pale
jina la Jamhuri mpya ya muungano
lilipoainishwa kuwa ni Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar. Kubadilishwa
kwa jina hilo na kuitwa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania ni kiini macho
muhimu katika hatua za awali za
Nyerere za kuimeza Zanzibar. Hakuna
mwanasiasa au mwanasheria anayeweza kuonyesha ni sheria ipi
iliyoruhusu kutumika jina la Tanzania
kwa Jamhuri ya muungano. Lengo
hapa ilikuwa ni kulipoteza kabisa
kabisa jina Tanganyika na ndio maana
hata kulitaja baada ya muungano huo na hadi hivi sasa ni kero kubwa kwa
viongozi wakuu wan chi wa upande
wa Tanganyika. Mwanzoni kulitaja jina
Tanganyika kulifananishwa na nia ya
kutaka kuvunja muungano. Hadidu za
makubaliano ya muungano zilibakisha baadhi ya mamlaka ya
Zanzibar kwa raisi mtendaji wa
Zanzibar ambaye alikuwa ni makamo
raisi wa kwanza wa Jahmhuri ya
muungano ili kulinda masilahi ya
Zanzibar katika muungano. Hadidu hizo za muungano pia zilibakisha
baadhi ya mamlaka ya Tanganyika
kwa raisi mtendaji wa Tanganyika
ambae alikuwa ni raisi wa kwanza wa
Jamhuri ya muungano ili kulinda
masilahi ya Tanganyika katika muungano. Hata hivyo Nyerere
kimkakati na kwa makusudi aliamua
kuitupilia mbali haki ya kuwa na raisi
mtendaji wa Tanganyika ili yeye
(Nyerere) abakie kuwa ndie mwenye
nguvu zote na mamlaka ya juu kiutendaji kwa Tanganyika na
Zanzibar. Hatua nyengine inaonesha
mtego mkubwa ambao Karume
alitegwa bila ya kuunasua ni vile
kukubali kuendelea kutumika kwa
muda katiba ya Tanganyika kama katiba ya Jamhuri ya muungano
katika kipindi cha mpito hadi
itakapotungwa katiba mpya ya
Jamhuri ya muungano. Jambo hili
lilimpa nafasi Nyerere kuendesha
mambo ya muungano vile anavyoona yeye inafaa kama alivyokuwa
akiiendesha serikali ya Tanganyika
kwa kipindi cha miaka 13 kuanzia
mwaka 1964 mpaka mwaka 1977
ambapo katika ya Jamhuri ya
muungano ilipatikana. Baada ya kuona mamlaka aliyonayo
katika Jamhuri ya muungano
hayamtoshi, Nyerere aliamua
kuviunganyisha vyama vya TANU na
ASP baada ya kifo cha Karume. Tarehe
5 mwezi Februari 1977 wakati Zanzibar ikiwa ndani ya utawala wa
Maalim Aboud Jumbe vyama vya TANU
na ASP viliunganishwa na kufanya
chama kipya chama cha mapinduzi
(CCM) kilichohodhiwa kimamlaka na
Nyerere. Huu ulikuwa ni mkakati wa kuusukuma mbele muungano na
kuyatanua madaraka ya muungano
huo ndani ya mikono ya Nyerere. CCM
ilimfanya Nyerere kushika hatamu na
kutoa maamuzi yasiopingika kama
vile kulazimishwa kujiuzulu Maalim Aboud Jumbe. Halkadhalika kundi la
wabunge 55 (G55) lilipozua suala la
kuanzishwa kwa serikali ya
Tanganyika mwaka 1992 lilikumbana
na mkono mrefu wa madaraka ya
Nyerere na kuzimwa mara moja. Ili kufanikisha malengo ya kuimaliza
Zanzibar kwa kisingizio cha
muungano ilimbidi Nyerere
kuyashikiia madaraka ya Jamhuri ya
muungano kwa muda wa miaka 20
na uwenyekiti wa CCM kwa muda wa miaka 10. Hata hivyo baada ya kustaafu Nyerere
bado aliionekana kuongoza nyuma ya
pazia. Wengi hawakulitegemea jina la
“chama cha mapinduzi” kuwa ndio
jina la chama kipya baada ya
kuunganishwa ASP na TANU mwaka 1977. Vyama vilivyoungana ni viwili
kimoja ni TANU kilichoongoza uhuru
wa Tanganyika na chengine ni ASP
kilichoshiki mapinduzi ya Zanzibar.
Hivyo basi wengi walitaraji jina la
chama kipya litabeba dhima zote mbele yaani ile ya uhuru na ile ya
kimapinduzi. Kinyume chake dhima ya
kimapinduzi tu ndio iliyofanya jengo la
chama kipya. Kwa wale wadau wa
muungano kwa upande wa Zanzibar,
wahafidhina wa kimapinduzi waliona kutumika jina “mapinduzi” kwenye
chama hicho kipya ni fahari ya
Zanzibar na hatua nyengine ya
kuyalinda mapinduzi na serikali ya
mapinduzi kwani kwao kudumu kwa
mapinduzi ya 1964 ndio masilahi makuu yaliyokuwa yakiwatosha
katika muungano. Watanzania
wanaelekea nusu karne tokea
kuasisiwa muungano wao huku nchi
mbili zikiwa katika mitafaruku chungu
mzima iliyozalikana na muungano huo uliokosa muundo wa usawa,
mitafaruku ambayo hupewa jina la
kupunguzwa makali yake kwa kuitwa
“kero za muungano” Changamoto za Muungano
Hapo awali suala la kuzungumzia
kasoro za muungano liilichukuliwa na
watawala kama uhaini. Aliyejaribu
kufanya hivyo alinyamazishwa kimya
au alikutana na mkono wa chuma wa serikali. Kufuatia ujio wa mfumo wa
vyama vingi vya siasa Tanzania, fursa
ya kuujadili mungano wa Tanzania
ilipatikana. Hivi sasa mjadala kuhusu
muungano wa Tanzania na kasoro
zake sio kitu cha ajabu tena nchini Tanzania. Mambo ambayo mara nyingi
huonekana kugonga vichwa vya
mijadala ya muungano au maeneo
yanayoonekana kuwa na kasoro ni
haya yafuatayo.
• Muundo wa muungano • Faida za muungano kwa pande zote
mbii za muungano Changamoto kubwa ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar ni muundo
wa mungano huo. Muundo wa serikali
mbili ulisimikwa na waasisi wawili wa
muungano, Nyerere na Karume.
Baadhi ya wanasiasa, wachambuzi na wananchi wanashauri mabadiliko
kutoka serikali mbili kuelekea serikali
moja ili kuifanya Tanzania kuwa nchi
moja kamilifu, au kuelekea serikali
tatu na kuifanya Tanzania kuwa
shirikisho kamili. Utafiti uliofanyika katika mwaka wa 1994 na 2006
unatoa tofauti ya maoni kati ya
wananchi wa Tanzania bara, Unguja
na Pemba kuhusiana na muundo wa
muungano huo. Hii bila shaka ni
ushawishi wa misimamo ya vyama vya siasa ambavyo wananchi hao
wanaviunga mkono katika maeneo
yao hayo pamoja na masilahi ya
kisiasa ya sehemu hiyo ndani ya
muungano. Takwimu zilizokusanywa
na kamati ya Jaji Nyalali zinaonyesha kwamba muundo wa serikali mbili
unaungwa mkono kwa kiwango cha
juu Unguja (63.2%) na kiwango cha
chini zaidi Pemba (34.6%). Muundo
wa serikali moja unaonekana kuwa
na wapenzi wengi Tanzania bara (27.5%) na wapenzi kidogo zaidi
Pemba (4.1%). Kwa upande wa
serikali tatu, muundo huu una
ushabiki mkubwa katika kisiwa cha
Pemba (32.4%) na ushabiki mdogo
zaidi Unguja (9.4%). Wakati Zanzibar ilipounganishwa na
Tanganyika, Karume na Nyerere
walikuwa na maana tofauti kuhusu
muungano huo. Wakati Nyerere
alikuwa na maana ya Zanzibar
kugeuka kipande kidogo cha ardhi ya Jamhuri mpya, Karume yeye
hakuelewa hivyo bali alifahamu
kwamba muungano ulikusudia kutoa
uhusiano katika mambo Fulani,
uhusiano ambao hautaleta hasara
kwa pande zote mbili. Changamoto kubwa ya muungano wa Tanganyika
na Zanzibar ni muundo wake. Wakati
duniani kuna mifumo miwili mikuu ya
muungano, mfumo wa serikali moja
(unitary) na mfumo wa serikali za
majimbo (federal), mfumo wa muungano wa Tanzania hauonekani
kuwa na sifa yoyote kati ya mifumo
hiyo miwili mikuu iliyopo duniani.
Mfano wa unitary ni kama vile taifa la
Marekani (United States of America)
ambapo madola mengi yameungana na kuunda dola moja kubwa. Mfano
wa federal ni kama vile taifa la
Uengereza (United Kingdoms)
ambapo madola mengi yameungana
na kufanya dola moja ya Uengereza.
Pamoja na kuwepo kwa dola moja kubwa ya Uengereza, nchi
zilizoungana zimewachiwa mamlaka
yake ya ndani. Nchi zote ndogo
ndogo zina utiifu kwa serikali kuu ya
Uengereza. Tanzania kwa upande
wake ina mfumo wa kipekee katika muundo wa serikali mbili, serikali ya
Jamhuri ya Muungano ambayo ni
serikali iliyopotea ya Tanganyika ya
awali ambayo imeongezewa mamlaka
zaidi hadi visiwa vya Unguja na Pemba
na serikali ya Zanzibar ambayo iko chini ya serikali ya Jamhuri ya
Muungano. Hivyo basi matokeo ya
muungano huo ni kuifanya serikali ya
Tanganyika kutumia mamlaka zaidi
nyuma ya pazia juu Zanzibar kwa jina
la Jamhuri ya muungano. Kwa kuwa muundo huo uliotokana
na mawazo na usomi wa Nyerere
peke yake na hauko duniani kote
ndio sababu umeshindwa kuzaa
mfumo mzuri wa kiserikali na kutoa
uhusiano wa kisiasa na kiutawala unaozikinaisha pande zote mbili
zilizoungana. Muundo huo
umesababisha kuzaliwa kwa ukaka
baina ya pande mbili zilizoungana
ambazo kabla ya kuungana zilikuwa
na uhuru na mamlaka sawa sawa. Wako wasomi na wanasiasa
wanaoutoa kasoro muundo huu wa
serikali mbili na badala yake
kupendekeza muundo wa serikali
moja. Wengi wanaotoa mawazo haya
ni wanasiasa na wasomi wa Tanzania bara. Ukweli ni kwamba muundo wa
serikali moja ni kuzidisha matatizo ya
muungano na kuuvuruga zaidi
uhusiano mwema wa pande mbili
uliopo. Mtu anaweza kujiuliza ni kwa
nini iwe hivyo na ilhali itakapokuwepo serikali moja wazanzibari watakuwa
na uwezo wa kuzifaidi na kuzitumia
fursa na rasili mali zote za Tanzania
bara kama vile wanyama pori, madini
nk ijapokuwa fursa na rasilimali hizo
zinakosekana kabisa Zanzibar. Halkadhalika pato la Tanzania bara
sasa litaweza kutumika kwa ajili ya
kuchangia maedeleo ya Zanzibar. Muundo wa serikali moja una athari
nyingi kwa Zanzibar zikiwemo za
kijamii na kiuchumi. Hapa
zitazungumzwa chache muhimu.
Athari ya kubwa zaidi ni kumalizika
kwa heshima ya utamaduni wa Zanzibar inayoongozwa na misingi ya
dini ya kiislamu. Utamaduni wa
Zanzibar wa wazanzibari unatokana
na dini ya kiislamu ambao una misingi
ya heshima, upole, ukarimu, utulivu,
kuaminiana na kushirikiana. Tabia za ulevi, kutovaa nguo za stara, kutokula
hadharani mwezi mtukufiu wa
Ramadhani, uhalifu, ujambazi nk ni
mambo ambayo hayaonekani
kupewa nafasi hata kidogo na misingi
ya utamaduni wa wazanzibari. Mambo hayo ambayo ni ya kawaida sana
huko Tanzania bara bila shaka
yanategemewa kuwa ya kawaida na
Zanzibar pale itakapokuwa sheria
zinazotawala Tanzania bara ndizo
zitakazotawala Zanzibar wakati huo Zanzibar itakapokuwa mkoa wa
Tanzania. Athari nyengine ipo katika
ardhi ya Zanzibar ambayo ni mali ya
wazanzibari. Itakapokuwa Zanzibar ni
mkoa mmoja wa Tanzania sheria ya
ardhi nayo itakuwa ni moja kwa Tanzania yote. Kwa sasa sheria ya
ardhi ya Zanzibar haimruhusu mtu
yeyote ambaye si mzanzibari kumiliki
ardhi Zanzibar. Sheria ya ardhi
itakaporuhusu kila matanzania
kumiliki ardhi Zanziba matokeo yake ni ardhi hiyo ambayo ni ndogo
kuvamiwa na mamilioni ya watanzania
bara na hivyo kupelekea wazanzibari
kusambaratika kwa kukosa maeneo
ya kuishi wao pamoja na kizazi chao
cha baadae. Matatizo ya muungano uliopo wa
Tanganyika na Zanziba ni mengi.
Athari kubwa zaidi imepatikana
upande wa mahusiano ya kiuchumi
kati ya Tanganyika na Zanzibar. Hapa
itazungumziwa kero moja ya kiuchumi ambayo itatosha kuitathmini athari
mbaya ya kero nyingi nyengine kwa
wazanzibari. Kero hii ni ile ya
kuingizwa kwa suala la mafuta na gesi
asilia katika orodha ya mambo ya
muungano. Kwa kuwa mafuta na gesi asilia ni miongoni mwa rasilimali za
machimbo ya chini ya ardhi ni jambo la
kushangaza kuona machimbo
mengine kama vile madini ya
dhahabu, chuma, Uranium na
Tanzanite hayakuingizwa katika kifungu hicho cha orodha ya mambo
ya muungano. Hili liko wazi kabisa
kwani mafuta na gesi asilia tafiti
zinathibisha kuwa yako kwa wingi
mno katika ardhi na bahari ya visiwa
vya Unguja na Pemba wakati machimbo mengine yako Tanganyika
pekee. Sababu ya kufanyika hivyo ni
kuipa uwezo Tanganyika kufaidi utajri
mkubwa utokanao na mafuta ambao
ni muhimili muhimu sana wa kiuchumi
ulimwenguni. Kampuni ya utafutaji wa mafuta ya
Canada iliingia Zanzibar kwa lengo la
kufanya utafiti juu ya upatikanaji wa
mafuta na gesi asilia kwa leseni ya
Tanzania Petroleum Development
Coorporatin (TPDC) bila hata ya ridhaa na ushauri achilia mbali ruhusa ya
Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar
katika mwaka wa 1997. Kiini cha
tatizo hili bila shaka ni vile kutolewa
kibali na TPDC kwa ajili kufanyika
utafiti katika maeneo ambayo kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar si eneo
la muungano. Mkataba rasmi
ukafungwa baina ya kampuni hiyo,
serikali ya Jamhuri ya muungano wa
Tanzania na TPDC kuanzisha shughuli
za utafiti. TPDC ni chombo cha wizara ya nishati na madini ya Jamhuri ya
muungano wa Tanzania, wizara
ambayo hufanya shughuli zake zote
kwa upande wa Tanganyika pekee. Wizara ya nishati na madini na TPDC
ndio vyombo vitakavyohusika na
ukusanyaji wa mapato ya leseni
ambazo makampuni ya uchimbaji
yatakuwa yakikata leseni hizo.
Hlkadhalika vyombo hivyo ndio vitakavyohusika na ukusanyaji wa
mapato ya uhuishaji wa leseni kila
mwaka. Kwa utaratibu huo basi
Zanzibar isengeambulia chochote.
Hapa Dr Salmin akahoji itakuwaje
chombo hicho bila shaka cha Tanzania bara kitakuwa na mamlaka ndani ya
mipaka ya eneo la Zanzibar kwa
kisingizio kwamba mafuta na gesi
asilia ni suala la muungano. Serikali ya
mapinduzi ya Zanzibar haikuweza
kulistahmilia hata kidogo suala hilo na hivyo kuamua kutokuiruhusu
kampuni hiyo kufanya shughuli zake.
Hapo ndipo wazanzibari walipoanza
kuwa kitu kimoja katika kudai suala la
mafuta na gesi asilia liondoshwe
katika orodha ya mambo ya muungano. Kamati ya waziri mkuu na
waziri kiongozi ya kujadili kero za
muungano iliyoanzishwa na Raisi
Kikwete katika kikao chake cha
mwanzo ilianza rasmi kulijadili suala
hili. Kampuni kubwa za kibiashara
ambazo zina makao yake upande wa
Zanzibar zinanyimwa ruhusa ya
kupanua biashara zao upande wa
Tanzania bara. Kampuni hizo
zinalazimishwa kuhamisha makazi yake kutokea Zanzibar na kuyapeleka
Tanzania bara na kulipa kodi kwa
serikali ya Jamhuri ya muungano
ndipo masharti ya kufanya kazi zao
Tanzania bara yatakapokamilika.
Halkadhalika kutokana na vikwazo mbali mbali, mazingira ya kibiashara
ya ndani ya Zanzibar hayawavutii
wafanyabiashara wakubwa wa
kizanzibari kuwekeza nchini mwao.
Wote wameamua kuhamishia mitaji
yao na kuiweka Dar es Salaam. Ofisi za taasisi za muungano ambazo zipo
Zanzibar zinaonekana kujazwa na
wafanyakazi kutokea Tanzania bara
zaidi kuliko Zanzibar na hivyo kutoa
sura kuwa taasisi hizo ni za
Tanganyika. Zanzibar kama nchi pia hainufaiki inavyostahili misaada
inayotolewa na marafaki zake.
Misaada yote huingia katika mkono
wa Tanganyika kwa kivuli cha
Jamhuri ya Muungano huku Zanzibar
ikiambulia patupu. Mustakbali wa Muungano
Maoni ya wananchi yaliwahi
kukusanywa kuhusu kuendelea au
kuvunjika kwa muungano kupitia
tume ya Jaji Nyalali. Kwa kuwa hakuna
chama hata kimoja cha siasa kilicho na msimamo wa kutaka kukoma kwa
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar basi inaweza kusemwa
kwamba maoni hayo yaliyokusanywa
ni ya wananchi wenyewe. Kiwango
cha juu zaidi cha maoni yaliopendekeza kuvunjika kwa
muungano kwa mujibu wa utafiti
uiofanywa na kamati hiyo ya Jaji
Nyalali mwaka wa 1994 ni kutoka
Pemba (15.6%) na kiwngo cha chini
kabisa ni kutoka Unguja (1.6%). Hii bila shaka ni kwa kuwa wapemba
wanauthamini sana sana uzalendo
wao na wanajivunia sana heshima na
hadhi ya nchi yao. Ndio maana asilimia
kubwa ya maoni kuhusu kuvunjika
kwa muungano usio na usawa na wenye kupendelea upande mmoja wa
muungano huo yakatokea Pemba.
Hata hivyo takwimu hizi zinaweza
kuwa tofauti na hali ya sasa baada ya
miaka 15 ya kukuwa kwa siasa za
vyama vingi hapa nchini jambo lililosababishwa na kulegezwa makali
kwa baadhi ya kero za muungano. Ni ukweli usiopingika kwamba
maendeleo ya Zanzibar yamefifia sana
ndani ya muungano huo
ukilinganisha na upande wa pili wa
muungano na hakuna dalili zozote
zinazoashiria faraja. Kinachoonekana ni kama kwamba viongozi
wanawalazimisha wananchi
kuukubali muungano wa nchi zao
wakati wananch wenyewe hususan
wazanzibari wanaonekana wazi
kwamba hwaoni umuhimu mkubwa wa muungano huo. Bila shaka hata
mke mkifunga ndoa, na hata kama
mumejaaliwa kizazi katika ndoa hiyo,
ikiwa hamukubaliani katika maisha ya
ndoa kwea kutawaliwa na kero zisizo
kwisha, basi wazee wenye hekima huwashaurini watoto wao waachane
kwa salama kama vile walivyooana
kwa salama hapo mwanzo. Katika
mazingira hayo basi sio jambo la
kushangaza kuwaona Wazanzibari
wanauchukia Muungano, kwani wanaamini ndio kiini cha matatizo
mengi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa
kwa Zanzibar
 
Katika
kuuangalia muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwanza ni
vyema zijulikane sababu hasa
zailizopelekea Tanganyika na Zanzibar
kufikia uamuzi wa kuungana. Kwa
mujibu wa mafundisho ya mashuleni
na vyuoni sababu kubwa za kuungana baina ya Tanganyika na
Zanzibar ni hizi zifuatazo. Kwanza ni
udugu wa damu na wenye mizizi
mirefu uliyopo baina ya wanganyika
na wazanzibari. Kwa kuirejea historia
ya mafungamano baina visiwa vya Zanzibar na bara la Afrika itagundulika
kwamba mafungamano hayo
yameanzia kwa karne nyingi sana
nyuma kiasi cha karne ya 15 au 16
wakati muungano wa Tanganyika na
Zanzibar uliibuka katikaki ya karne ya 20 ambapo asili za kibantu kwa
wazanzibari tayari zimeshapotea kwa
kiasi kikubwa kutokana na
kuchanganya damu na watu wa asili
za mbali mbali za kiasia ambao ndio
wengi zaidi. Hata hivyo asili za wazanzibari ni vyanzo vingi vikiwemo
Afrika, Pashia, India na Arabia.
Ijapokuwa Afrika ni miongoni mwa
vyanzo vya asili za wazanzibari lakini
ifahamike kuwa ni kutokea sehemu
mbali mbali za Afrika zikiwemo Tanganyika, Msumbiji, Malawi, Kenya,
Uganda, Rwanda, Comoro nk. Sababu nyengine inayohusishwa na
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ni historia ya ushirikiano kati
ya chama cha TANU na ASP, ambavyo
vyote ni vyama vya kupigania
ukombozi wa watu weusi kupitia harakati za kudai uhuru zilozozuka
miaka ya 1950 na 60 katika bara la
Afrika. Hapa ikumbukwe kuwa sio
chama cha ASP peke yake
kilichoshiriki mapambano ya
kumng’oa mkoloni Zanzibar. Bila shaka kilichomvutia Nyerere na
kuamua kukiunga mkono chama cha
ASP peke yake na kufanya
mashiriukiano nacho katika harakati
za kudai uhuru wa Zanzibar ni ile ile
itikadi ya mapambano dhidi ya watu wasio na ngozi nyeusi mambo
ambayo yalikuwa yamepamba siasa
za Karume. Vyama vyengine vya
kizalendo vya wazanzibari havikuwa
na mvuto wowote kwa Nyerere.
Wakati chama cha TANU kinaongozwa na sera ya “uafrika” katika kupigania
uhuru na hivyo kuwaunganisha
watanganyika wote, ASP kwa upande
wake iliifumania sera ya “ugozi
mweusi” ikidhania kuwa ndio uafrika
wenyewe na hivyo kuwatenga wazanzibari wengine. Vyama vya
TANU na ASP vilisahau kwamba
asilimia kubwa ya wazanzibari tofauti
na watanganyika wakiwemo hao
wenye ngozi nyeusi wana asili zao
kutoka nje ya bara la Afrika. Muungano ni matokeo ya hofu mbili
Hizi zilizotangulia kutajwa labda
zinaweza kuwa sababu ndogo ndogo
za muungano huu. Sababu muhimu
hasa zilizopelekea muungano wa
Tanganyika na Zanzibar ni hofu mbili zifuatazo. Hofu ya ya kwanza ilitokana
na uwezo mdogo sana wa kijeshi na
kiulinzi iliokuwanao serikali ya
mwanzo ya mapinduzi. Nguvu za
kijeshi na kiulinzi zikitegemea sana
mizinga ya kichina na kisovieti ya kutungulia ndege pamoja na silaha
ndogo ndogo (Armit 1986). Uwezo
huo mdogo wa kujihami
unawezakuwa ulijenga hofu kwa
Karume na Nyerere juu ya uwezekano
wa Sultani na Moh’d Shamte kujipanga na kurudi ili kufanya mapinduzi
mapya (counter revolution) dhidi ya
serikali ya Karume. Kutokana na hofu
hiyo basi Nyrere alimshauri Karume
kuziunganisha nchi zao ili kupata
nguvu kubwa ya kiulinzi ya kuihami Zanzibar dhidi ya mapinduzi mapya. Hii
inaweza kuwa ndio sababu kubwa ya
Karume kushishitiza kwamba
muungano huu utakuwa ni wa kipindi
cha miaka kumi tu ambapo itabidi
utathminiwe upya kama unahitajika au laa. Karume alifahamu wazi
kwamba ndani ya kipindi hicho cha
miaka kumi tayari serukali yake
imeshajiimarisha vya kutosha kwa
nguvu za kijeshi. Hofu ya pili ni ile iliyozifanya dola za
magharibi kuiona serikali mpya ya
mapinduzi ya Zanzibar kuwa
ingeweza kuwa angamizo la ubepari
katika ulimwengu na bara la Afrika.
Ushiriki wa Babu na wakomyunisti katika mapinduzi ya 1964 iliiifanya
serikali mpya ya mapinduzi kuwa ni
tishio kwa Marekani na dola za
magharibi. Hofu hii ya nchi za
magharibi inathibitishwa na simu ya
balozi wa marekani nchini Tanganyika wakati huo bwana William Leonhart
alioituma kwa wizara ya mambo ya nje
ya serikali ya marekani siku ya tarehe
27 Aprili 1964 : “Sina wasiwasi kwamba
watanganyika wanategemea kuwa
wakomyunisti waliomo katika serikali
ya Zanzibar watazimwa kwa
kufunikwa na kutofungamana
upande wowote kwa Tanganyika, lakini kutokana na kasi na nguvu za
mwendo wa wakomyunisti
wanaokwenda mbio nchini Zanzibar
na sio kuitishia ka kuitumilia hali
katika njia ambazo serikali ya
Tanganyika haitoweza kuzifikiria. Ninaamin kwamba ni muhimu Nyerere
apewe msaada wa kimya kimya wa
kiasi kikubwa iwezekanavyo na nchi
za magharibi tokea mwanzo” (Armit
1986). Ingawa wengi wa makomred
wakiongozwa na Babu waliukataa
kwa nguvu zote muungano huo lakini
Bwana Ali Sultan Bin Issa anasema
katika kitabu cha Burgess cha The
race, revolution and sruggle for human rights in Zanzibar: “Mimi binafsi sikuona tatizo kuukubali
muungano. Japo kuwa lengo la
Nyerere ilikuwa ni kuwameza
wazanzibari, mimi niliona ni ukombozi
na jukwaa kubwa zaidi la siasa zetu
(za kikomyunisti). Pia ni fursa pekee ya kueneza ukomyunisti Tanzania
bara” (Burgess 2009). Mkataba wa muungano
Siku ya tarehe 22 Aprili 1964 Nyerere
na Karume walitia sahihi mkataba wa
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar. Kumbukumbu za kihistoria
zinasonyesha kuwa Karume alidhani alitia sahihi mkataba wa kuzitambua
nchi mbili huru zenye mamlaka kamili.
Na hivi ndivyo ilivyokuwa katika
mkataba huu wa mwanzo wa
muungano. Yaani kwa mujibu wa
mkataba huo mahusiano ya Tanganyika na Zanzibar kisiasa ni
kama yalivyokuwa mahusiano baina
ya Ireland ya Kaskazini na Uingereza.
Mkataba huu wa mwanzo wa
muungano uliiachia Zanzibar kiasi
Fulani cha madaraka yake ya ndani kama vile polisi, mahakama, kilimo nk
wakati madaraka muhimu kama vile
mambo ya nje, ulinzi, biashara,
shughuli za muungano, udhibiti wa
fedha za kigeni na kuchagua maafisa
(watendaji) wajuu kabisa wa Jamhuri ya muungano yalikuwa chini ya
mamlaka yaserikali kuu ya
muungano. Siku ya tarehe 25 Aprili
1964 Bunge la Jamhuri ya Tanganyika
ililiridhia sheria ya muungano kama
ilivyoridhiwa na baraza la mapinduzi la serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.
Sheria ya muungano wa Tanganyika
na Zanzibar ilielekeza mambo kumi na
moja (11) yaliotokana moja kwa moja
na “mkataba wa muungano”. Mkataba
wa muungano uliutaka muungano huo hapo mwanzoni udumu kwa
muda wa miaka kumi (10) tu, yaani
kutoka 1964 hadi 1974. Hata hivyo
mkataba hu wa asili ulio na saini za
waasisi wawili wa muungano huo
Karume na Nyerere haujulikani uliktokomea hadi leo hii. Muungano wa Tanganyika na
Zanzibar ulifanywa kukidhi matakwa
ya kisiasa ya watu wawili, Nyerere na
Karume. Hakuna kura ya maoni wala
mazingira yeyote ya kidemokrasia
yalioandaliwa na kufanywa ili kuwasikiliza wananchi wa pande mbili
za muungano kama wangependelea
kuunganishwa kwa nchi zao au laa.
Kifungu cha 6 (1) cha mkataba wa
muungano kinasema kwamba “Rais
wa kwanza wa Jamhuri ya muungano atakuwa Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere”. Kifungu cha 6 (2) kinasema
“Makamo wa kwanza wa rais kwa
mjibu wa mabadiliko yanayopatikana
kwenye aya ya (c) kifungu kidogo (1)
ya sehemu ya 5 atakuwa sheikh Abeid Karume”. Kuwepo kwa kifungu hichi
cha 6 kwenye sheria ilioanzisha
muungano (sheria namba 22, ya 1964
kwa upande wa Tanganyika ni ishara
ya wazi wazi kuwa muungano huu
uliundwa kukidhi matashi ya watu wawili na sio dola mbili. Waasisi hawa
wa muungano waligawana madaraka
vile walivyoona wao wenyewe inafaa. Hapa ndipo safari ya Zanzibar
kumezwa na Tanganyika ilipoanzia.
Sheria ya muungano namba 22 ya
1964 ilkuwa na dhamira nzuri pale
jina la Jamhuri mpya ya muungano
lilipoainishwa kuwa ni Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar. Kubadilishwa
kwa jina hilo na kuitwa Jamhuri ya
muungano wa Tanzania ni kiini macho
muhimu katika hatua za awali za
Nyerere za kuimeza Zanzibar. Hakuna
mwanasiasa au mwanasheria anayeweza kuonyesha ni sheria ipi
iliyoruhusu kutumika jina la Tanzania
kwa Jamhuri ya muungano. Lengo
hapa ilikuwa ni kulipoteza kabisa
kabisa jina Tanganyika na ndio maana
hata kulitaja baada ya muungano huo na hadi hivi sasa ni kero kubwa kwa
viongozi wakuu wan chi wa upande
wa Tanganyika. Mwanzoni kulitaja jina
Tanganyika kulifananishwa na nia ya
kutaka kuvunja muungano. Hadidu za
makubaliano ya muungano zilibakisha baadhi ya mamlaka ya
Zanzibar kwa raisi mtendaji wa
Zanzibar ambaye alikuwa ni makamo
raisi wa kwanza wa Jahmhuri ya
muungano ili kulinda masilahi ya
Zanzibar katika muungano. Hadidu hizo za muungano pia zilibakisha
baadhi ya mamlaka ya Tanganyika
kwa raisi mtendaji wa Tanganyika
ambae alikuwa ni raisi wa kwanza wa
Jamhuri ya muungano ili kulinda
masilahi ya Tanganyika katika muungano. Hata hivyo Nyerere
kimkakati na kwa makusudi aliamua
kuitupilia mbali haki ya kuwa na raisi
mtendaji wa Tanganyika ili yeye
(Nyerere) abakie kuwa ndie mwenye
nguvu zote na mamlaka ya juu kiutendaji kwa Tanganyika na
Zanzibar. Hatua nyengine inaonesha
mtego mkubwa ambao Karume
alitegwa bila ya kuunasua ni vile
kukubali kuendelea kutumika kwa
muda katiba ya Tanganyika kama katiba ya Jamhuri ya muungano
katika kipindi cha mpito hadi
itakapotungwa katiba mpya ya
Jamhuri ya muungano. Jambo hili
lilimpa nafasi Nyerere kuendesha
mambo ya muungano vile anavyoona yeye inafaa kama alivyokuwa
akiiendesha serikali ya Tanganyika
kwa kipindi cha miaka 13 kuanzia
mwaka 1964 mpaka mwaka 1977
ambapo katika ya Jamhuri ya
muungano ilipatikana. Baada ya kuona mamlaka aliyonayo
katika Jamhuri ya muungano
hayamtoshi, Nyerere aliamua
kuviunganyisha vyama vya TANU na
ASP baada ya kifo cha Karume. Tarehe
5 mwezi Februari 1977 wakati Zanzibar ikiwa ndani ya utawala wa
Maalim Aboud Jumbe vyama vya TANU
na ASP viliunganishwa na kufanya
chama kipya chama cha mapinduzi
(CCM) kilichohodhiwa kimamlaka na
Nyerere. Huu ulikuwa ni mkakati wa kuusukuma mbele muungano na
kuyatanua madaraka ya muungano
huo ndani ya mikono ya Nyerere. CCM
ilimfanya Nyerere kushika hatamu na
kutoa maamuzi yasiopingika kama
vile kulazimishwa kujiuzulu Maalim Aboud Jumbe. Halkadhalika kundi la
wabunge 55 (G55) lilipozua suala la
kuanzishwa kwa serikali ya
Tanganyika mwaka 1992 lilikumbana
na mkono mrefu wa madaraka ya
Nyerere na kuzimwa mara moja. Ili kufanikisha malengo ya kuimaliza
Zanzibar kwa kisingizio cha
muungano ilimbidi Nyerere
kuyashikiia madaraka ya Jamhuri ya
muungano kwa muda wa miaka 20
na uwenyekiti wa CCM kwa muda wa miaka 10. Hata hivyo baada ya kustaafu Nyerere
bado aliionekana kuongoza nyuma ya
pazia. Wengi hawakulitegemea jina la
“chama cha mapinduzi” kuwa ndio
jina la chama kipya baada ya
kuunganishwa ASP na TANU mwaka 1977. Vyama vilivyoungana ni viwili
kimoja ni TANU kilichoongoza uhuru
wa Tanganyika na chengine ni ASP
kilichoshiki mapinduzi ya Zanzibar.
Hivyo basi wengi walitaraji jina la
chama kipya litabeba dhima zote mbele yaani ile ya uhuru na ile ya
kimapinduzi. Kinyume chake dhima ya
kimapinduzi tu ndio iliyofanya jengo la
chama kipya. Kwa wale wadau wa
muungano kwa upande wa Zanzibar,
wahafidhina wa kimapinduzi waliona kutumika jina “mapinduzi” kwenye
chama hicho kipya ni fahari ya
Zanzibar na hatua nyengine ya
kuyalinda mapinduzi na serikali ya
mapinduzi kwani kwao kudumu kwa
mapinduzi ya 1964 ndio masilahi makuu yaliyokuwa yakiwatosha
katika muungano. Watanzania
wanaelekea nusu karne tokea
kuasisiwa muungano wao huku nchi
mbili zikiwa katika mitafaruku chungu
mzima iliyozalikana na muungano huo uliokosa muundo wa usawa,
mitafaruku ambayo hupewa jina la
kupunguzwa makali yake kwa kuitwa
“kero za muungano” Changamoto za Muungano
Hapo awali suala la kuzungumzia
kasoro za muungano liilichukuliwa na
watawala kama uhaini. Aliyejaribu
kufanya hivyo alinyamazishwa kimya
au alikutana na mkono wa chuma wa serikali. Kufuatia ujio wa mfumo wa
vyama vingi vya siasa Tanzania, fursa
ya kuujadili mungano wa Tanzania
ilipatikana. Hivi sasa mjadala kuhusu
muungano wa Tanzania na kasoro
zake sio kitu cha ajabu tena nchini Tanzania. Mambo ambayo mara nyingi
huonekana kugonga vichwa vya
mijadala ya muungano au maeneo
yanayoonekana kuwa na kasoro ni
haya yafuatayo.
• Muundo wa muungano • Faida za muungano kwa pande zote
mbii za muungano Changamoto kubwa ya muungano wa
Tanganyika na Zanzibar ni muundo
wa mungano huo. Muundo wa serikali
mbili ulisimikwa na waasisi wawili wa
muungano, Nyerere na Karume.
Baadhi ya wanasiasa, wachambuzi na wananchi wanashauri mabadiliko
kutoka serikali mbili kuelekea serikali
moja ili kuifanya Tanzania kuwa nchi
moja kamilifu, au kuelekea serikali
tatu na kuifanya Tanzania kuwa
shirikisho kamili. Utafiti uliofanyika katika mwaka wa 1994 na 2006
unatoa tofauti ya maoni kati ya
wananchi wa Tanzania bara, Unguja
na Pemba kuhusiana na muundo wa
muungano huo. Hii bila shaka ni
ushawishi wa misimamo ya vyama vya siasa ambavyo wananchi hao
wanaviunga mkono katika maeneo
yao hayo pamoja na masilahi ya
kisiasa ya sehemu hiyo ndani ya
muungano. Takwimu zilizokusanywa
na kamati ya Jaji Nyalali zinaonyesha kwamba muundo wa serikali mbili
unaungwa mkono kwa kiwango cha
juu Unguja (63.2%) na kiwango cha
chini zaidi Pemba (34.6%). Muundo
wa serikali moja unaonekana kuwa
na wapenzi wengi Tanzania bara (27.5%) na wapenzi kidogo zaidi
Pemba (4.1%). Kwa upande wa
serikali tatu, muundo huu una
ushabiki mkubwa katika kisiwa cha
Pemba (32.4%) na ushabiki mdogo
zaidi Unguja (9.4%). Wakati Zanzibar ilipounganishwa na
Tanganyika, Karume na Nyerere
walikuwa na maana tofauti kuhusu
muungano huo. Wakati Nyerere
alikuwa na maana ya Zanzibar
kugeuka kipande kidogo cha ardhi ya Jamhuri mpya, Karume yeye
hakuelewa hivyo bali alifahamu
kwamba muungano ulikusudia kutoa
uhusiano katika mambo Fulani,
uhusiano ambao hautaleta hasara
kwa pande zote mbili. Changamoto kubwa ya muungano wa Tanganyika
na Zanzibar ni muundo wake. Wakati
duniani kuna mifumo miwili mikuu ya
muungano, mfumo wa serikali moja
(unitary) na mfumo wa serikali za
majimbo (federal), mfumo wa muungano wa Tanzania hauonekani
kuwa na sifa yoyote kati ya mifumo
hiyo miwili mikuu iliyopo duniani.
Mfano wa unitary ni kama vile taifa la
Marekani (United States of America)
ambapo madola mengi yameungana na kuunda dola moja kubwa. Mfano
wa federal ni kama vile taifa la
Uengereza (United Kingdoms)
ambapo madola mengi yameungana
na kufanya dola moja ya Uengereza.
Pamoja na kuwepo kwa dola moja kubwa ya Uengereza, nchi
zilizoungana zimewachiwa mamlaka
yake ya ndani. Nchi zote ndogo
ndogo zina utiifu kwa serikali kuu ya
Uengereza. Tanzania kwa upande
wake ina mfumo wa kipekee katika muundo wa serikali mbili, serikali ya
Jamhuri ya Muungano ambayo ni
serikali iliyopotea ya Tanganyika ya
awali ambayo imeongezewa mamlaka
zaidi hadi visiwa vya Unguja na Pemba
na serikali ya Zanzibar ambayo iko chini ya serikali ya Jamhuri ya
Muungano. Hivyo basi matokeo ya
muungano huo ni kuifanya serikali ya
Tanganyika kutumia mamlaka zaidi
nyuma ya pazia juu Zanzibar kwa jina
la Jamhuri ya muungano. Kwa kuwa muundo huo uliotokana
na mawazo na usomi wa Nyerere
peke yake na hauko duniani kote
ndio sababu umeshindwa kuzaa
mfumo mzuri wa kiserikali na kutoa
uhusiano wa kisiasa na kiutawala unaozikinaisha pande zote mbili
zilizoungana. Muundo huo
umesababisha kuzaliwa kwa ukaka
baina ya pande mbili zilizoungana
ambazo kabla ya kuungana zilikuwa
na uhuru na mamlaka sawa sawa. Wako wasomi na wanasiasa
wanaoutoa kasoro muundo huu wa
serikali mbili na badala yake
kupendekeza muundo wa serikali
moja. Wengi wanaotoa mawazo haya
ni wanasiasa na wasomi wa Tanzania bara. Ukweli ni kwamba muundo wa
serikali moja ni kuzidisha matatizo ya
muungano na kuuvuruga zaidi
uhusiano mwema wa pande mbili
uliopo. Mtu anaweza kujiuliza ni kwa
nini iwe hivyo na ilhali itakapokuwepo serikali moja wazanzibari watakuwa
na uwezo wa kuzifaidi na kuzitumia
fursa na rasili mali zote za Tanzania
bara kama vile wanyama pori, madini
nk ijapokuwa fursa na rasilimali hizo
zinakosekana kabisa Zanzibar. Halkadhalika pato la Tanzania bara
sasa litaweza kutumika kwa ajili ya
kuchangia maedeleo ya Zanzibar. Muundo wa serikali moja una athari
nyingi kwa Zanzibar zikiwemo za
kijamii na kiuchumi. Hapa
zitazungumzwa chache muhimu.
Athari ya kubwa zaidi ni kumalizika
kwa heshima ya utamaduni wa Zanzibar inayoongozwa na misingi ya
dini ya kiislamu. Utamaduni wa
Zanzibar wa wazanzibari unatokana
na dini ya kiislamu ambao una misingi
ya heshima, upole, ukarimu, utulivu,
kuaminiana na kushirikiana. Tabia za ulevi, kutovaa nguo za stara, kutokula
hadharani mwezi mtukufiu wa
Ramadhani, uhalifu, ujambazi nk ni
mambo ambayo hayaonekani
kupewa nafasi hata kidogo na misingi
ya utamaduni wa wazanzibari. Mambo hayo ambayo ni ya kawaida sana
huko Tanzania bara bila shaka
yanategemewa kuwa ya kawaida na
Zanzibar pale itakapokuwa sheria
zinazotawala Tanzania bara ndizo
zitakazotawala Zanzibar wakati huo Zanzibar itakapokuwa mkoa wa
Tanzania. Athari nyengine ipo katika
ardhi ya Zanzibar ambayo ni mali ya
wazanzibari. Itakapokuwa Zanzibar ni
mkoa mmoja wa Tanzania sheria ya
ardhi nayo itakuwa ni moja kwa Tanzania yote. Kwa sasa sheria ya
ardhi ya Zanzibar haimruhusu mtu
yeyote ambaye si mzanzibari kumiliki
ardhi Zanzibar. Sheria ya ardhi
itakaporuhusu kila matanzania
kumiliki ardhi Zanziba matokeo yake ni ardhi hiyo ambayo ni ndogo
kuvamiwa na mamilioni ya watanzania
bara na hivyo kupelekea wazanzibari
kusambaratika kwa kukosa maeneo
ya kuishi wao pamoja na kizazi chao
cha baadae. Matatizo ya muungano uliopo wa
Tanganyika na Zanziba ni mengi.
Athari kubwa zaidi imepatikana
upande wa mahusiano ya kiuchumi
kati ya Tanganyika na Zanzibar. Hapa
itazungumziwa kero moja ya kiuchumi ambayo itatosha kuitathmini athari
mbaya ya kero nyingi nyengine kwa
wazanzibari. Kero hii ni ile ya
kuingizwa kwa suala la mafuta na gesi
asilia katika orodha ya mambo ya
muungano. Kwa kuwa mafuta na gesi asilia ni miongoni mwa rasilimali za
machimbo ya chini ya ardhi ni jambo la
kushangaza kuona machimbo
mengine kama vile madini ya
dhahabu, chuma, Uranium na
Tanzanite hayakuingizwa katika kifungu hicho cha orodha ya mambo
ya muungano. Hili liko wazi kabisa
kwani mafuta na gesi asilia tafiti
zinathibisha kuwa yako kwa wingi
mno katika ardhi na bahari ya visiwa
vya Unguja na Pemba wakati machimbo mengine yako Tanganyika
pekee. Sababu ya kufanyika hivyo ni
kuipa uwezo Tanganyika kufaidi utajri
mkubwa utokanao na mafuta ambao
ni muhimili muhimu sana wa kiuchumi
ulimwenguni. Kampuni ya utafutaji wa mafuta ya
Canada iliingia Zanzibar kwa lengo la
kufanya utafiti juu ya upatikanaji wa
mafuta na gesi asilia kwa leseni ya
Tanzania Petroleum Development
Coorporatin (TPDC) bila hata ya ridhaa na ushauri achilia mbali ruhusa ya
Serikali ya mapinduzi ya Zanzibar
katika mwaka wa 1997. Kiini cha
tatizo hili bila shaka ni vile kutolewa
kibali na TPDC kwa ajili kufanyika
utafiti katika maeneo ambayo kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar si eneo
la muungano. Mkataba rasmi
ukafungwa baina ya kampuni hiyo,
serikali ya Jamhuri ya muungano wa
Tanzania na TPDC kuanzisha shughuli
za utafiti. TPDC ni chombo cha wizara ya nishati na madini ya Jamhuri ya
muungano wa Tanzania, wizara
ambayo hufanya shughuli zake zote
kwa upande wa Tanganyika pekee. Wizara ya nishati na madini na TPDC
ndio vyombo vitakavyohusika na
ukusanyaji wa mapato ya leseni
ambazo makampuni ya uchimbaji
yatakuwa yakikata leseni hizo.
Hlkadhalika vyombo hivyo ndio vitakavyohusika na ukusanyaji wa
mapato ya uhuishaji wa leseni kila
mwaka. Kwa utaratibu huo basi
Zanzibar isengeambulia chochote.
Hapa Dr Salmin akahoji itakuwaje
chombo hicho bila shaka cha Tanzania bara kitakuwa na mamlaka ndani ya
mipaka ya eneo la Zanzibar kwa
kisingizio kwamba mafuta na gesi
asilia ni suala la muungano. Serikali ya
mapinduzi ya Zanzibar haikuweza
kulistahmilia hata kidogo suala hilo na hivyo kuamua kutokuiruhusu
kampuni hiyo kufanya shughuli zake.
Hapo ndipo wazanzibari walipoanza
kuwa kitu kimoja katika kudai suala la
mafuta na gesi asilia liondoshwe
katika orodha ya mambo ya muungano. Kamati ya waziri mkuu na
waziri kiongozi ya kujadili kero za
muungano iliyoanzishwa na Raisi
Kikwete katika kikao chake cha
mwanzo ilianza rasmi kulijadili suala
hili. Kampuni kubwa za kibiashara
ambazo zina makao yake upande wa
Zanzibar zinanyimwa ruhusa ya
kupanua biashara zao upande wa
Tanzania bara. Kampuni hizo
zinalazimishwa kuhamisha makazi yake kutokea Zanzibar na kuyapeleka
Tanzania bara na kulipa kodi kwa
serikali ya Jamhuri ya muungano
ndipo masharti ya kufanya kazi zao
Tanzania bara yatakapokamilika.
Halkadhalika kutokana na vikwazo mbali mbali, mazingira ya kibiashara
ya ndani ya Zanzibar hayawavutii
wafanyabiashara wakubwa wa
kizanzibari kuwekeza nchini mwao.
Wote wameamua kuhamishia mitaji
yao na kuiweka Dar es Salaam. Ofisi za taasisi za muungano ambazo zipo
Zanzibar zinaonekana kujazwa na
wafanyakazi kutokea Tanzania bara
zaidi kuliko Zanzibar na hivyo kutoa
sura kuwa taasisi hizo ni za
Tanganyika. Zanzibar kama nchi pia hainufaiki inavyostahili misaada
inayotolewa na marafaki zake.
Misaada yote huingia katika mkono
wa Tanganyika kwa kivuli cha
Jamhuri ya Muungano huku Zanzibar
ikiambulia patupu. Mustakbali wa Muungano
Maoni ya wananchi yaliwahi
kukusanywa kuhusu kuendelea au
kuvunjika kwa muungano kupitia
tume ya Jaji Nyalali. Kwa kuwa hakuna
chama hata kimoja cha siasa kilicho na msimamo wa kutaka kukoma kwa
muungano wa Tanganyika na
Zanzibar basi inaweza kusemwa
kwamba maoni hayo yaliyokusanywa
ni ya wananchi wenyewe. Kiwango
cha juu zaidi cha maoni yaliopendekeza kuvunjika kwa
muungano kwa mujibu wa utafiti
uiofanywa na kamati hiyo ya Jaji
Nyalali mwaka wa 1994 ni kutoka
Pemba (15.6%) na kiwngo cha chini
kabisa ni kutoka Unguja (1.6%). Hii bila shaka ni kwa kuwa wapemba
wanauthamini sana sana uzalendo
wao na wanajivunia sana heshima na
hadhi ya nchi yao. Ndio maana asilimia
kubwa ya maoni kuhusu kuvunjika
kwa muungano usio na usawa na wenye kupendelea upande mmoja wa
muungano huo yakatokea Pemba.
Hata hivyo takwimu hizi zinaweza
kuwa tofauti na hali ya sasa baada ya
miaka 15 ya kukuwa kwa siasa za
vyama vingi hapa nchini jambo lililosababishwa na kulegezwa makali
kwa baadhi ya kero za muungano. Ni ukweli usiopingika kwamba
maendeleo ya Zanzibar yamefifia sana
ndani ya muungano huo
ukilinganisha na upande wa pili wa
muungano na hakuna dalili zozote
zinazoashiria faraja. Kinachoonekana ni kama kwamba viongozi
wanawalazimisha wananchi
kuukubali muungano wa nchi zao
wakati wananch wenyewe hususan
wazanzibari wanaonekana wazi
kwamba hwaoni umuhimu mkubwa wa muungano huo. Bila shaka hata
mke mkifunga ndoa, na hata kama
mumejaaliwa kizazi katika ndoa hiyo,
ikiwa hamukubaliani katika maisha ya
ndoa kwea kutawaliwa na kero zisizo
kwisha, basi wazee wenye hekima huwashaurini watoto wao waachane
kwa salama kama vile walivyooana
kwa salama hapo mwanzo. Katika
mazingira hayo basi sio jambo la
kushangaza kuwaona Wazanzibari
wanauchukia Muungano, kwani wanaamini ndio kiini cha matatizo
mengi ya kijamii, kiuchumi na kisiasa
kwa Zanzibar

Shukran nimekuelewa ambaye hataelewa hii akapewe pilau ale ..

Sent from my HTC Incredible S using Tapatalk
 
Back
Top Bottom