Lowassa alipokuwa waziri wa ardhi alikuwa anatumia madaraka hayo kuwanyang'anya viwanja wahindi huku akitangaza RTD kuwa kafanya hivyo kwa fiada ya umma lakini baadaye akawa anapokea hela nyingi sana kutoka kwa hao hao aliotanganza kuwanyang'anya viwanja, na baadaye akawarudishia viwanja hivyo kimya kimya. Hicho ndicho kilichokuwa chanzo cha utajiri wa Lowassa. Alipokuwa Waziri Mkuu, alitumia madaraka hayo kulazimisha RichMondulian kupewa tenda ya umeme wa dharura bila kufuata taratibu, jambo ambalo limeiingiza Tanzania katika matatizo makubwa sana ya kisheria kimataifa. Alifanya yote hayo akiwa ni waziri anayewajibika kwa rais. Je mtu huyu akiwa ndiye rais mwenyewe mwenye uamuzi wa mwisho ataacha kufanya lipi kwa manufaa yake binafsi na kulisahau taifa hili? Kikwete mwenyewe ambaye ni nafuu kidogo bado kaliangamiza taifa hile je Lowassa atatuachia nini?
Uongozi wa mwisho unahitaji sana hekima maadili, ambayo nadhani Lowassa hana kabisa. Ni mtaalamu wa kufukuzia mali na kuwashinda wengine kwenye madili ya fedha; akiwa na madaraka atafukuzia sana na kuwazuia watanzania wengine wote wanaoingia katika njia yake ya mali. Inanitisha sana Tanzania tunakoenda!
huu uchapa kazi wa lowassa kama upo kweli bila maadili ya uongozi ni kazi bure kwa taifa..uchapa kazi bila maadili unaweza kufanywa pale kwenye taasisi ndogo ndogo zisizoathiri maisha ya mamilioni ya watu lakini siyo kiti cha Urais. Hata kama atakua mkali kiasi gani na mfuatiliaji na mfokaji huu mfumo uliomnufaisha na atakaoacha imara zaidi utakuja leta vita tanzania ya watoto wetu.