The Worshiper
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 302
- 89
Ni miaka mingi sasa imepita tangu kuanzishwa kwa mamlaka ya ustawishaji makao makuu Dodoma – CDA (Capital Development Authority) huku ikipewa majukumu ya kupanga, kuratibu, kuustawisha na kuuendeleza mkoa kufikia na kubeba hadhi ya makao makuu.
Kama ilivyo kawaida mambo mengi ya mustakbari wa nchi huamuliwa na siasa ndivyo vivyo hivyo inavyoendeshwa mamlaka hii (kisiasa) miaka nenda rudi. Ndiyo maana haishangazi kuona kwa miaka yote hiyo toka kuanzishwa kwake ikiwa hakuna lolote la maana likiwa limefanyika kufikia lengo na wala haieleweki uanzishwaji na utekelezaji wa mipango yake ilikuwa ni wa muda gani.
Kazi nyingi inazozifanya kwa sasa ni zile ambazo zingekuwa zinafanywa na Manispaa ya Dodoma hivyo inashindwa kueleweka tofauti kati ya kazi za Mamlaka na Manispaa.
Cha kujiuliza hapa ni kwamba; Je, kazi ya CDA ni moja tu kupima na kugawa viwanja? Kama ni hivyo uwepo wa Manispaa ya Dodoma ni nini? Kwasasa ukipita pale utakutana na magari ya kifahari kwa ajili ya maafisa wao lakini ukiingia ndani utakutana na mifumo duni na ya kizamani ya utendaji kazi huku urasimu ukiwa umeshika hatamu na ubadilishwaji wa wawakurugenzi usiyo na tija.
Uwepo wa mamlaka hii hauonekani kuwa na tija sana kwa mji kwakuwa hata robo ya malengo yake hayajafikiwa na inaonekana kuwa ucheleweshwaji wa maamuzi ya serikali kuhamia Dodoma (unaofanywa makusudi na serikali ya CCM) una manufaa kwa watu na pengine kama hilo lingekuwa limefanyika ingekuwa inamaanisha kukata mirija ya viongozi hawa serikalini iliyochomekwa kwenye mamlaka hii. Hii inamaanisha kuzidi kuzama gizani kwa mkoa wa Dodoma kimaendeleo ndiyo kuneemeka kwa kwa baadhi ya viongozi.
Siasa ndiyo inayoamua CDA ifanye nini, itende nini na iache kipi na ni ngumu kwa mkurugenzi kuja na kuendeleza mawazo mapya tofauti na yale aliyoyakuta ambayo inaonekana ni ngumu kutekelezeka kwakuwa yeye ni kama kivuli cha wakubwa serikalini.
Naomba kuwasilisha
Kama ilivyo kawaida mambo mengi ya mustakbari wa nchi huamuliwa na siasa ndivyo vivyo hivyo inavyoendeshwa mamlaka hii (kisiasa) miaka nenda rudi. Ndiyo maana haishangazi kuona kwa miaka yote hiyo toka kuanzishwa kwake ikiwa hakuna lolote la maana likiwa limefanyika kufikia lengo na wala haieleweki uanzishwaji na utekelezaji wa mipango yake ilikuwa ni wa muda gani.
Kazi nyingi inazozifanya kwa sasa ni zile ambazo zingekuwa zinafanywa na Manispaa ya Dodoma hivyo inashindwa kueleweka tofauti kati ya kazi za Mamlaka na Manispaa.
Cha kujiuliza hapa ni kwamba; Je, kazi ya CDA ni moja tu kupima na kugawa viwanja? Kama ni hivyo uwepo wa Manispaa ya Dodoma ni nini? Kwasasa ukipita pale utakutana na magari ya kifahari kwa ajili ya maafisa wao lakini ukiingia ndani utakutana na mifumo duni na ya kizamani ya utendaji kazi huku urasimu ukiwa umeshika hatamu na ubadilishwaji wa wawakurugenzi usiyo na tija.
Uwepo wa mamlaka hii hauonekani kuwa na tija sana kwa mji kwakuwa hata robo ya malengo yake hayajafikiwa na inaonekana kuwa ucheleweshwaji wa maamuzi ya serikali kuhamia Dodoma (unaofanywa makusudi na serikali ya CCM) una manufaa kwa watu na pengine kama hilo lingekuwa limefanyika ingekuwa inamaanisha kukata mirija ya viongozi hawa serikalini iliyochomekwa kwenye mamlaka hii. Hii inamaanisha kuzidi kuzama gizani kwa mkoa wa Dodoma kimaendeleo ndiyo kuneemeka kwa kwa baadhi ya viongozi.
Siasa ndiyo inayoamua CDA ifanye nini, itende nini na iache kipi na ni ngumu kwa mkurugenzi kuja na kuendeleza mawazo mapya tofauti na yale aliyoyakuta ambayo inaonekana ni ngumu kutekelezeka kwakuwa yeye ni kama kivuli cha wakubwa serikalini.
Naomba kuwasilisha