Siasa na dini

Kuhusu kumpigia kura mtu fulani kwa misingi ya dini ni 'speculations' tu. Hakuna kwenye data. Kwamba baadhi ya viongozi wa dini waliwahubiria waumini wao wapige kura kiaina inaweza kuwa kweli ingawa baadhi ya viongozi wa dini walisingiziwa pia. Mimi ninataka tukiongea vitu tuongee vile ambavyo tunaweza kuvithibitisha na kama hatuwezi na bado tunaviongelea tunakuwa tunajidhalilisha. Namna hii ya kufikiri mimi naiita 'intellectual masturbation'.

Ndio maana hata mimi sisemi kwamba viongozi wote wa dini walihubiri hivyo. Nimesema inaweza kuwa wachache sana kati yao. Nakubali pia wapo waliosingiziwa. Na hilo la kuwepo watu au vyombo vya habari kuwasingizia viongozi wa dini kuhubiri udini ni tatizo la hisia za udini ambayo halipaswi kuachwa bila dawa.

Naheshimu mtizamo wako juu ya kuongea tunavyoweza kuthibitisha japo natofautiana nawe kimtizamo. Kama unasema mtu fulani specifically amefanya kosa fulani huna haki ya kuongea bila ushahidi. Ila kama kuna tuhuma za ujumla kuwepo kwa tatizo fulani una haki ya kulijadili kulingana na vyanzo vya tuhuma hiyo hata kama huna uhakika wa ukweli wa tuhuma hizo. Ni katika kujadili tuhuma hizo ndipo pia mnaweza kubaini ukweli au uongo wa tuhuma hizo. Kukaa kimya inaweza kuwa tatizo kama tuhuma hizo zikiwa za kweli. Mimi kwa msimamo wangu kila kinachosemwa kina chanzo. Ima aliekisema alikisikia na kukielewa vibaya au amekipotosha kwa makusudi. Tutaelewaje ukweli juu ya hili kama tutakaa kimya na kuogopa kusema kwa kuwa hatuna takwimu? Mara nyingine hata kujadiliana juu ya mambo haya ni aina moja wapo ya utafiti . Ndio maana toka mwanzo sijawa tayari kumnyoshea mkono mtu yoyote.
 
Kitu ambacho nimegundua pia ni kwamba baadhi ya vyombo vya habari vinafanya 'propaganda' (kutoa ushawishi kwa wasomaji na kwa umma wakati kitu kinachozungumziwa hakipo ila kinafanywa kama kipo). Vyombo hivi haziripoti matukio au habari bali vinatoa maoni kulingana na 'perception' yao. Wakifanya hivyo, wana'form an opinion' juu ya kitu fulani. Mind you an opinion is not a fact! Halafu sisi tunatoa maoni juu ya maoni ya mtu fulani juu ya kitu fulani. Hapa ndipo tunapokosea. Tungekuwa tunatoa maoni juu ya tukio fulani na siyo maoni ya mtu juu ya tukio fulani. Mwisho wa siku, unakuta kwamba maini yatu mara nyingi yamejenwa juu ya maoni ya watu wengine na siyo kile kilichotokea. Mfano, The SundayCitizen ya Aprili au Mei 2010 waliandika habari fulani juu ya Ilani ya Christian Professionals of Tanzania (CCT) kuhusu Uchaguzi Mkuu 2010. Kichwa cha habari kilikuwa kinasema (nitaandika kwa kiswahili maan text yake kwa Kiingereza sina kwa sasa na sitaki nikosee) Kanisa Katoliki linawaandaa waumini wake kumchagua kiongozi Mkristo. Lakini article nzima haikuwa na sehemu iliyosema vile. Baada ya watu kusoma hicho kichwa cha habari na hata bila ya kutafuta hiyo Ilani walianza kuchangia na kulaani vikali na hapo ndipo kauli za udini ziliianza kuibuka. Unaona kitu ninachojaribu kukionesha kuhusu kutoa maoni juu ya maoni ya mtu mwingine na siyo tukio au habari yenyewe?

Tatizo hilo katika vyombo vyetu vya habari ni kubwa mno. Habari nyingi kuhusu matukio fulani zinakuwa simejengwa katika maoni binafsi na tafsiri binafsi ya muandishi kuhusiana na tukio husika, maoni ambayo yanaweza kuwa si sahihi. Lakini wasomaji wengi wa kawaida wakisoma maoni kama hayo wanayachukulia yenyewe kama yenyewe kuwa ndio ukweli wa mambo na wanabaki na fikra hizo hizo na wanapandikiza fikra kama hizo kwa watu wengi. Kwa maoni yangu tunapaswa kuyajadili maoni hayo kama maoni na kuyatofautisha ama kuyaowanisha na tukio linalojadiliwa. Hii itawasaidia wananchi wa kawaida kupata picha kamili. Ndio maana hata mimi katika maoni yangu sikujikita katika kumtafuta mchawi. Nimelijadili kama lisemwalo ili kama lipoi maoni yangu yahusike na kama litakuwa hypothetical tu lifae kwa mafundisho.
 
Ndio maana hata mimi sisemi kwamba viongozi wote wa dini walihubiri hivyo. Nimesema inaweza kuwa wachache sana kati yao. Nakubali pia wapo waliosingiziwa. Na hilo la kuwepo watu au vyombo vya habari kuwasingizia viongozi wa dini kuhubiri udini ni tatizo la hisia za udini ambayo halipaswi kuachwa bila dawa.

Naheshimu mtizamo wako juu ya kuongea tunavyoweza kuthibitisha japo natofautiana nawe kimtizamo. Kama unasema mtu fulani specifically amefanya kosa fulani huna haki ya kuongea bila ushahidi. Ila kama kuna tuhuma za ujumla kuwepo kwa tatizo fulani una haki ya kulijadili kulingana na vyanzo vya tuhuma hiyo hata kama huna uhakika wa ukweli wa tuhuma hizo. Ni katika kujadili tuhuma hizo ndipo pia mnaweza kubaini ukweli au uongo wa tuhuma hizo. Kukaa kimya inaweza kuwa tatizo kama tuhuma hizo zikiwa za kweli. Mimi kwa msimamo wangu kila kinachosemwa kina chanzo. Ima aliekisema alikisikia na kukielewa vibaya au amekipotosha kwa makusudi. Tutaelewaje ukweli juu ya hili kama tutakaa kimya na kuogopa kusema kwa kuwa hatuna takwimu? Mara nyingine hata kujadiliana juu ya mambo haya ni aina moja wapo ya utafiti . Ndio maana toka mwanzo sijawa tayari kumnyoshea mkono mtu yoyote.

George, kama huna uhakika wa kilichotokea unapata wapi hoja za kujadili kitu au kuchangia kuhusu mwendelezo wake? Kuna principle moja inayoniongoza mimi: 'If you doubt about something suspend judgement!' Mfano, kama sina uhakika kama nimeona au kumskia A, siwezi kusema kwa uhakika kuwa nimemwona au kumsikia A. Why? Kwa sababu sina grounds za kufanya hivyo. Na kama nitafanya, nitakuwa nina 'speculate' (to form opinions about something without having the necessary information or facts - to make guesses). Intelligent people don't entertain this type of reasoning or arguing!

Binafsi, kama sina uhakika wa tukio fulani kutokea nafunga mdomo wangu au nadadisi ili nijue issue hasa ni nini kablya ya kuchangia. In fact, ni vizuri kuuliza ili kujua what's the issue kuliko kujadili kitu out of ignorance or speculation. Na hili ndilo tatizo letu la msingi. Unakuta tunajadili kitu ambacho hatujui kipo au hakipo!

Padre mmoja (Mkatoliki) Mholanzi alikuwa Uganda na kulikuwa miongoni mwa waumini wake cases nyingi zinazohusu uchawi na ambazo zilikuwa zinazua hofu kubwa na kuzuia shughuli za maendeleo katika jamii ile. Yeye akaanza kufanya utafiti. Ili afanye hivyo, alihitaji msaada wa watu waliokwisha waona wachawi wakifanya mambo yao.

Watu kadhaa wakamuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha na baadhi yao wakajitolea kutoa ushahidi. Alipoanza kuwatembelea ili waleleze walichoona, A alidai aliambiwa na B. Padre akasema waende kwa B na B akasema hakuona ila alisikia kutoka kwa C. Padre hakukata tamaa, akawaomba waende kumwona C na yeye alidai alipata habari kutoka kwa D na D naye akasema aliambiwa na E na iliendelea hivyo hata mwisho akagundua kuwa hakuna aliyekwisha kumwona mchawi (hakuna aliweza kutoa ushahidi) bali ilikuwa hisia tu za kushtumiana zinazotokana na misuguano, fitina au chuki katika maisha ya kawaida ya wanajamii.

Na hata mabadiliko tunayodai tunataka yafanyike katika nchi yetu hatuwezi kuyaleta kwa 'speculation' au maoni yasiyojengwa juu ya uhalisia wa kitu. We have to engage in intelligent inquiry or search of the truth... and if we give opinions, thye should base on facts/things that can be verified otherwise we'll be wasting time!
 
Back
Top Bottom