Siasa kiini cha matatizo lakini si suluisho la hata 15% ya matatizo yetu

Mtazamaji

JF-Expert Member
Feb 29, 2008
5,937
1,437
Wanachadema poleni na hongereni. Wana Cuf poleni. CCM mhh ili chama kijijenge mlitakiwa mpoteze Kiti hicho.

Baada ya uchaguzi wa igunga sasa natoa mwito kwa wansasa na wenye nafasi za kiasa na kimaamuzi wote ( Wabunge, madiwani, Mawaziri etc ) bila kujai itikadi ya chama.

Asimilia kubwa ya matatizo yaliyopo Tanzania yanatokana na siasa. Iwe ni mgao wa umeme , Iwe ni UFISADI, iwe ni ajali za barabarani, iwe ni kiwango cha elimu Elimu duni , Iwe ni Uchumi yanachangikiwa wa kiasi ikubwa na siasa.

  • Je wanasiasa wa Tanzania wamefanya vya kutosha kujua suluisho la matatizo mballi mbali au bado wanaendelea na kasumba ya kudhani ukiwa mbunge, Diwani utajua nini suluisho sahihi la kila kitu?
  • Mbona watu wanaandika na kupendekeza baadhi suluisho matatzio lakini wanasiasa wawe wa upiznai na wa utawala Hwaonekani kujali a kutilia maanani ?
  • Je wanasiasa wanajua kuna mambo hawayajui au hawana taarifa zake na kama wangembiwa na kuyajua basi tungekuwa hatua moja mbele

CDM, CUF , NCCR zaidi ya siasa kuna mambo yanaweza ufanyika na kuvijenga zaidi vyama vyenu kisiasa . CDM wana nafasi nzuri sababu wanaongoza baadhi ya Halmashauri.


Nawasilisha
 
Sijawai kusikia wabunge wanaojiita vijana kama kina ziito, Makamba . H mdee na wnegine Wakiomba free time eg dar city center hata pale chuo cha IFM kwa dk japo 30 ili kupokea maoni na ushauri wa watu wa fani mbali mbali kotoa ofisi mbali mbali juu ya mambo kama
  • ICT
  • Uhandisi
  • walimu na elimu
  • Madereva
Nje ya kamati zao za bunge wabunge wanapata wapi taarifa na ushauri mbali mbali za kitaalam ambazo zinawza kusaidia kuhoji kama si kusuluisha matatizo mbali mbali?
 
Sijawai kusikia wabunge wanaojiita vijana kama kina ziito, Makamba . H mdee na wnegine kama kina Wakiomba free time kwnye dars maja hata pale chua cha IFM kwa dk japo 30 ili kupokea maoni na ushauri wa watu wa fani mbali mbali juu ya mambo kama
  • ICT
  • Uhandisi
  • walimu na elimu
  • Madereva
Nje ya kamati zao za bunge wabunge wanapata wapi taarifa na ushauri mbali mbali za kitaalam ambazo zinawza kusaidia kuhoji kama si kusuluisha matatizo mbali mbali?

Nadhani huwa wanategemea JF kama chombo chao cha kukusanyia maoni. Ila mtu kama Mbowe hata sijawahi kumuona humu, angalau Slaa na Zitto huwa wanachungulia mara moja moja.
 
Am with NN on this. Afrika bila Wachina, Wajapan au Wazungu ndani ya Serikali - bado tutakuwa na safari ndefu, tena sana tu katika kupata maendeleo tuyatamaniyo!! Sijasema Waarab, maana tunaowengi Serikalini. Sijasema Wahindi, maana nao tunaowengi tu.

Somewhat, naamini katika mchanganyiko wa watu wa asili mbalimbali kama chachu ya maendeleo; haswa ndani ya jamii yenye watu waliowengi zaidi wenye silka na hulka kama zetu (Waafrika, Wabantu). Uchu na ubinafsi dhidi ya jamii na wanajamii wenzetu ndo' maisha. Hivyo uwepo wa wanajamii wengine miongoni mwetu kwaweza [naamini itakuwa] kabisa kuwa chachu ya maendeleo. South Africa na Zimbambwe ni mifano tosha katika hili. Tunaona walipoweza na pale waliposhindwa.

Twaweza kuelimika kwa elimu kubwa sana na kuwa wachapa kazi wazuri tu, lakini linapokuja swala la maadili ya uongozi, haswa kwenye mambo yanayoshikamana moja kwa moja na siasa; kuna utomvu mkubwa wa maadili. Ubinafsi na tamaa hushika hatamu. Don't know specifically what it is... but it's like an inborn inability to run effectual and successful governments based on transparency and accountability.
 
Hivi
  • wabunge wagapi wajua some practical appplication of ICT Kwenye ELIMU zinavyoweza kubadilisha ubora wa elimu
  • Wabunge wetu wanajua nini nahawajui nini Kuhusu ICT?
  • kama wanajua ni wangapi wamehoji kwa nini serikali haijatekeleza?
  • Kama hawajui mbona watu wanaandika humu JF na wengine ingawa tuna knowldge ndogo mpaka tumewa PM but

Nimeteolea mifano ya ICT lakini naamin kuna vijana na watu weye fani mbali mbali wana some Ideas nzuri sema hazijajulikana kwa wenye sauti na wenye sauti hawajapenda kuzisikia au kuzitafuta.
 
............
Twaweza kuelimika kwa elimu kubwa sana na kuwa wachapa kazi wazuri tu, lakini linapokuja swala la maadili ya uongozi, haswa kwenye mambo yanayoshikamana moja kwa moja na siasa; kuna utomvu mkubwa wa maadili. Ubinafsi na tamaa hushika hatamu. Don't know specifically what it is... but it's like an inborn inability to run effectual and successful governments based on transparency and accountability.

But for politician na wabunge wa vyama vyote kuna tendecy wao kudhani wanajua kila kitu. Mpaka mambo yaende ombo ndio wanajaibu kuwa wasikivu.

Ndio matoeo yake rais wetu anaongea kauli za kisiasa kama kila mwaafuzi atapata laptop. Wakati hakuna hata mpango wa kila shule ya sekondary kuwa VISUAL/VIDEO labaratory

Mi Nikiona documenatry ya BBC za elimu kama jiography, na masomo mengine nasema ningeziona hizi enzi zangu basi ningefsalimika na DIV IV teh teh teh . Sasa kwa wanafuzi sasa nini kinashindiana . Wanasiasa watakumbia Mkonga ukikamilika hayo yote yatafuta..........

Ni wakati wanasiasa wapate muda kuwasikiliza wataalam
 
Hivi kuna mbunge anajua mshahara wa
  • Afisa elimu wa mkoa na wila ni kiasi gani ngapi
  • Afisa mifugo wa wilaya au moa ni shilingi ngapi
  • Afisa nyuki (kama wapo au wnaoneana hawana umuhimu)
  • Mhandisi wa mkoa au wilaya
  • Afisa Maji, Mkoa au wilaya (kama wapo)
  • RPC wa Mkoa

Kwa nini hatuoni Proffessor wa SUA anaacha kazi chuo kwenda kuwa AFISA mifugo wa ARUSHA au AFISA Kilimo RUKWA badala yake wanakimbilia kwenye SIASA tu?

Wabunge wanapimaje uzito na umuhimu na ukubwa wa kazi za nafasi hizo na kazi zao za KISIASA? Ni majukumu yapi ni muhimu kwa taifa hili? Wamefanya nini ili zaidi ya maendeleo ya Kisiasa yaje maendeleo mengine?

Nawaomba kina Zitto, Myika, Kingwala, Mdee, Lema Regia mtema , etc Ebu tafuteni njia za kukusanya maoni ya wataalam mbali mbali nje ya siasa Siku moja mmpuase kama wasikilizaji.
 
Back
Top Bottom