Awali kabla ya uchaguzi mkuu wa 2010 nilikuwa nikiipenda sana TBC1 lakini tangu wafanye madudu yale katika utangazaji wa matokeo, sina hamu nayo, M. Hassan alipokuwa akitaja jina la mbuge wa cdm aliyeshinda katika jimbo mojawapo, aliwahi kutamka jimbo hilo limekwenda kwa cdm na akasema sijui huyu mbunge anaitwa nani, anaposema hayo alikuwa na jina mkononi la yule Mbunge na akalisoma kwa kujichanganya changanya,
Leo kilichonudhi zaidi katika kipindi chao cha asubuhi wakati wa kupokea ujumbe mbalimbali kutoka kwa wasikilizaji
Aliyekuwepo studio amekatisha kusoma ujumbe wa mtu, kwa kipande alichokisoma kilisomwa hivi "Serikali ni kweli imefilisika kwa maana hata wazabuni wana...." yule msomaji akakatisha kusoma ujumbe ule.
Nimeumia sana ,uhuru wa mtu kutoa maoni uko wapi? nikawaza kuwa pengine huyu mtu aliyekatishiwa ujumbe wake ni Mzabuni na anauchungu wa kutokulipwa deni lake au alikuwa na hoja na mfano wa wazabuni wanayo idai serikali lakini ndo hivyo ujumbe wake ukakatishwa kusomwa
Leo kilichonudhi zaidi katika kipindi chao cha asubuhi wakati wa kupokea ujumbe mbalimbali kutoka kwa wasikilizaji
Aliyekuwepo studio amekatisha kusoma ujumbe wa mtu, kwa kipande alichokisoma kilisomwa hivi "Serikali ni kweli imefilisika kwa maana hata wazabuni wana...." yule msomaji akakatisha kusoma ujumbe ule.
Nimeumia sana ,uhuru wa mtu kutoa maoni uko wapi? nikawaza kuwa pengine huyu mtu aliyekatishiwa ujumbe wake ni Mzabuni na anauchungu wa kutokulipwa deni lake au alikuwa na hoja na mfano wa wazabuni wanayo idai serikali lakini ndo hivyo ujumbe wake ukakatishwa kusomwa