Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Bara na Visiwani zinaweza kuwa nchi mbili majirani na zenye uhusiano wa karibu wa kihistoria. Zote zimewahi kuwa nchi mbili tofauti huko nyuma. Kweli zinahistoria ambayo imeiingilia kiasi kwamba haiwezekani kuandika historia ya upande mmoja bila kugusia historia ya upande mwingine.
Siamini katika serikali tatu kwa sababu tulizikataa mwanzo na sababu ya kuzikataa toka mwanzo hazijabadilika hadi hivi sasa. Ninaamini njia nzuri ni aidha twende kwenye serikali moja ya mifumo mbalimbali ya kiutawala kama ilivyo Uchina (ambapo Hong Kong inautawala na mfumo wake tofauti na Bara) au Canada ambako Quebec kama Jimbo wana uhuru wa aina fulani fulani. Ipo mifano mingine ya aina mbalimbali ya mahusiano ya kiutawala katika pande mbalimbali; Afrika ya Kusini kwa mfano mahusiano kati ya serikali kuu na majimbo yake na makabila yake.
Kwa upande mwingine hata hivyo ninaamini katika mazingira ambapo Muungano wa sasa hauna watetezi na wengi wanaanza kushabikia "serikali tatu" bila kujibu maswali ambayo Mwalimu aliyauliza kwenye "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" kuhusu uendeshaji na gharama ya serikali tatu na mambo mengine ya msingi sana.
NI katika kufikiria hayo nimejikuta ninaamini uchaguzi uliopo huko tunakokwenda kuelekea katiba mpya jambo kubwa kabisa ambalo ni lazima tuliamue ni uhusiano katika ya Zanzibar na Tanzania Bara. Siamini kabisa kuwa uhusiano wa serikali tatu ni muafaka ni aidha serikali moja yenye mifumo mbalimbali ya utawala au kutengana kwa Zanzibar kupiga kura ya maoni 2014 kama walivyofanya kwenye kura ya Katiba yao.
Kura hiyo ya maoni iwe huru kabisa ikiwa na uchaguzi wa aina mbili tu; Muungano wa serikali moja na mifumo mbalimbali ya utawala au Zanzibar kutoka kwenye Muungano na kuwa taifa kamili kama walivyofanya Sudan.
One Nation, One Country or Separation - Taifa Moja, Nchi Moja au Utengano!
Hili lipigiwe kura kabla hatujaamua juu ya Katiba Mpya kwani hatuwezi kuwa na Katiba Mpya bila kuamua suala la Muungano. Suala la Muungano ni zito na kubwa sana sawasawa kabisa na suala la Katiba Mpya. Muungano lazima ujadiliwe in light ya kuandikwa kwa Katiba Mpya.
Siamini katika serikali tatu kwa sababu tulizikataa mwanzo na sababu ya kuzikataa toka mwanzo hazijabadilika hadi hivi sasa. Ninaamini njia nzuri ni aidha twende kwenye serikali moja ya mifumo mbalimbali ya kiutawala kama ilivyo Uchina (ambapo Hong Kong inautawala na mfumo wake tofauti na Bara) au Canada ambako Quebec kama Jimbo wana uhuru wa aina fulani fulani. Ipo mifano mingine ya aina mbalimbali ya mahusiano ya kiutawala katika pande mbalimbali; Afrika ya Kusini kwa mfano mahusiano kati ya serikali kuu na majimbo yake na makabila yake.
Kwa upande mwingine hata hivyo ninaamini katika mazingira ambapo Muungano wa sasa hauna watetezi na wengi wanaanza kushabikia "serikali tatu" bila kujibu maswali ambayo Mwalimu aliyauliza kwenye "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" kuhusu uendeshaji na gharama ya serikali tatu na mambo mengine ya msingi sana.
NI katika kufikiria hayo nimejikuta ninaamini uchaguzi uliopo huko tunakokwenda kuelekea katiba mpya jambo kubwa kabisa ambalo ni lazima tuliamue ni uhusiano katika ya Zanzibar na Tanzania Bara. Siamini kabisa kuwa uhusiano wa serikali tatu ni muafaka ni aidha serikali moja yenye mifumo mbalimbali ya utawala au kutengana kwa Zanzibar kupiga kura ya maoni 2014 kama walivyofanya kwenye kura ya Katiba yao.
Kura hiyo ya maoni iwe huru kabisa ikiwa na uchaguzi wa aina mbili tu; Muungano wa serikali moja na mifumo mbalimbali ya utawala au Zanzibar kutoka kwenye Muungano na kuwa taifa kamili kama walivyofanya Sudan.
One Nation, One Country or Separation - Taifa Moja, Nchi Moja au Utengano!
Hili lipigiwe kura kabla hatujaamua juu ya Katiba Mpya kwani hatuwezi kuwa na Katiba Mpya bila kuamua suala la Muungano. Suala la Muungano ni zito na kubwa sana sawasawa kabisa na suala la Katiba Mpya. Muungano lazima ujadiliwe in light ya kuandikwa kwa Katiba Mpya.