Si Magazeti Yote Ynafaa Kwa Kusoma, Si Magazeti Yote Yanaandika Habari.

Radio Producer

JF-Expert Member
Feb 4, 2011
724
295
Wadau,

Napenda kutoa hisia zangu juu ya mada hapo juu. Katika Tanzania hii ya leo SI KILA GAZETI LINAFAA KWA KUSOMA, NA SI KILA GAZETI LINAANDIKA HABARI. Nina chomaanisha hapa ni kuwa vyombo vya habari vya wananchi vinavyoweza kuwapa habari za kweli vimepoteza mtazamo na kujikuta vikitangaza, au kuandika habari kwa mapenzi au masilahi binafsi.

Kwa hapa Tanzania magazeti mengi kwa sasa, vyombo vya habari vingi ni kichefuchefu tu, vinatangaza matakwa ya mabosi wao na si habari. Na jinsi ilivyo kuwa vyombo vingi vya habari vinamilikiwa na wanasiasa hii itakuwa changamoto kubwa sana.

Kampuni yetu inaandaa mpango mahususi wa kuzisaidia radio za jamii ambazo ndizo pekee zinazoweza kutuletea ukombozi kwasasa hasa kama zikianzishwa na watu wasiojihusisha na masuala ya kisiasa. Tunaandaa mkakati na utaratibu utakao muwezesha kila anayetaka kuanzisha radio ya jamii kwa gharama za chini sana.

Tuijenge Tanzania yetu.
 
Back
Top Bottom