Shule za watoto wenye vipaji bado zimefutwa?

mtatifikolo

Member
Feb 9, 2008
43
7
Je, utaratibu wa shule maalum kwa wanafunzi wenye vipaji kielimu upo mpaka sasa?
Ninakumbuka miaka 5 iliyopita ndugu Mungai alitoa proposal ya kufuta utaratibu wa Ilboru, Mzumbe, Kibaha kuwa shule za vipaji.
Je, bado zimefutwa?

My take:
1. Tunahitaji shule za vipaji nchini ili kuwepo na 'centers of excellence'?
2. Kama mitihani ya NECTA inayofanywa na wote ni mirahisi kwa wanafunzi wa shule za vipaji, inabidi ianzishwe mitihani maalum ambayo ni migumu zaidi kwa ajili yao pekee.
3. Kuwa na shule kama hizo zinaweza wasaidia wanafunzi wake kupata admission katika vyuo mahiri duniani kutokana na publicity. Alliance High School na Starehe Boys Centre kule Kenya wanautaratibu mzuri. Hizi nazo ni shule za vipaji, na kila mwaka wanafunzi wake kadhaa wanachaguliwa kwenda kusoma nje kwenye vyuo 10 bora.


Shule za watoto wenye vipaji kufutwa

2004-01-03 22:35:31
Na Mawazo Malembeka, PST, Njombe
Wizara ya Elimu na Utamaduni inatarajia kufuta utaratibu wa sasa wa kuwepo na shule za sekondari za wanafunzi wenye vipaji maalum kiakili.

Waziri wa wizara hiyo, Bw Joseph Mungai amesema mjini hapa kwamba, uamuzi huo unatokana na changamoto iliyotolewa na wataalamu wa elimu katika mkutano mkuu wa elimu wa hivi karibuni ambapo wataalamu hao walisema kuwa utaratibu huo una mapungufu.

"Wataalamu hao waligawanyanyika mno na kuhoji kuwa ni vipi mwanafunzi mwenye kipaji maalum au cha pekee apimwe kwa mtihani ambao hata wanafunzi wengine wanaufanya," alisema.

Bw Mungai alisema kuwa wataalamu hao walisema kama kweli wapo watoto wenye vipaji maalumu, hakuna sababu ya basi ya kuwekwa tena katika shule moja badala ya kuwachanganya na wanafunzi wengine ili kuwepo na dhana ya kuwasaidia wanafunzi wadhaifu kiakili.

Alisema kuwa wataalamu hao pia walihoji uwezo au ubora wa shule zinazoitwa za wenye vipaji maalum au vya pekee na kwamba kama shule hizo ni bora au nazo ni za kipekee, na kwamba zinawafundisha nini hasa wanafunzi hao wenye vipaji vya kipekee.

Bw. Mungai alisema wataalamu hao walisema labda kungekuwepo na shule za wanafunzi waliofaulu vizuri mtihani ingawa pia walisema hata kama kungekuwa na
shule za namna hiyo haikupaswa wanafunzi waliofaulu vizuri warundikwe pamoja.

Bw. Mungai alisema wanauangalia upya utaratibu huo na kwamba baada ya kukamilika utaratibu mpya unaoandaliwa, utaratibu wa shule hizo utaondolewa mara moja.

Mpaka sasa kuna jumla ya shule sita za namna hiyo ambazo kwa wasichana ni Msalato, Kilakala, Tabora wakati kwa wavulana ni Mzumbe, Ilboru na Kibaha.
 
Criteria gani zilikuwa zinatumika kuwapeleka wanafunzi kwenye shule hizo za vipaji? Matokeo ya mtihani ya mwisho tu hayatoshi zaidi kwa sababu tunajua mbinu za kupata division 1 ni nyingi Tanzania. Mfumo wetu wa elimu siku hizi umeporomoka mpaka unasikitisha. Halafu wakaunganisha Chemistry na Physics, sijui ndio ikaitwaje hiyo, uuwii!
 
Mtatifikolo,

Ahsante!

1. Yaani kwa creteria hizi Moshi International School and International School of Tanganyika are in the list of best 100 schools in Africa.

Shule nyingine za Tz nzuri did not qualify? Majority of WaTz who are good today did not use International schools kama za Moshi!

2. Is this the kind of Edn our country we desire? Maana naona majority ya hizi ni Za dini na private and majority are from South Africa and Kenya!

Hizo za International School Moshi na Watz wangapi watoto wa maskini vipanga wataweza kwenda huko?
 
hizi shule ziliondolewa na kuitwa za kawaida, mimi nimesoma enzi hizo za vipaji na shule niliyochaguliwa kwenda ilikuwa na waalimu wazuri saana. Hivi ninavyoandika aslimia 95 wote tulijiunga na vyu vikuu mbali mbali hapa nchini,kwa sasa shule hizi waliziharibu na matokeo yake wanafunzi wanapata hadi division zero, waalimu wazuri hamna tena.Kipindi kile baraza la mitihani lilikuwa serious.wanafunzi waliokuwa wengi ktk shule hizo walitokea mikoa yote ya tanzania hivyo wizi haukuwepo wa mitihani.
 
Je, utaratibu wa shule maalum kwa wanafunzi wenye vipaji kielimu upo mpaka sasa?
Ninakumbuka miaka 5 iliyopita ndugu Mungai alitoa proposal ya kufuta utaratibu wa Ilboru, Mzumbe, Kibaha kuwa shule za vipaji.
Je, bado zimefutwa?

My take:
1. Tunahitaji shule za vipaji nchini ili kuwepo na 'centers of excellence'?
2. Kama mitihani ya NECTA inayofanywa na wote ni mirahisi kwa wanafunzi wa shule za vipaji, inabidi ianzishwe mitihani maalum ambayo ni migumu zaidi kwa ajili yao pekee.
3. Kuwa na shule kama hizo zinaweza wasaidia wanafunzi wake kupata admission katika vyuo mahiri duniani kutokana na publicity. Alliance High School na Starehe Boys Centre kule Kenya wanautaratibu mzuri. Hizi nazo ni shule za vipaji, na kila mwaka wanafunzi wake kadhaa wanachaguliwa kwenda kusoma nje kwenye vyuo 10 bora.


[B

Mtatifikolo, heshima yako mkuu. Lakini umeon=mb ridhaa kwa mhusika kutumia jina hilo?? natambua mhusika ni professor pale UDSM au ni mwanafunzi wake nini?. Anyway tuache hayo, mkuu hoja yako ni mhimu kuliko maelezo. Nadhani hata mungai alikuwa sahihi kufuta utaratibu wa shule za vipaji kulingana na namna ambavyo shule hizi zinaoperate. hata hivyo shule hizi ni muhimu ila utaratibu ndio sio mzuri. Hakuna sababu ya kuita shule za vipaji wakati mitihani ni ile ile. au mazingira hayafanani. Vipaji ni muhimu lakini shule zote zinatakiwa kuwa na mazingira yakufanana kutoka idadi ya walimu na miundombinu theni wali vipanga watajulikana otherwise ni ubaguzi katika elimu.

Vile vile kama wadau walivyochangia kubase kwenye final exams peke yake na kumuita mtu fulani anakipaji si sahihi na hili lilisha dhihirishwa katika vyuo vikuu. Nadhani tunahitaji shule za watu wenyevipaji but utaratibu uboreshwe
 
It was nice na hata miongoni mwa ma-mentors hapa wengi wanatoka special schools hizo za wakati huo n autaona hoja zao zina chembechembe za unabii vile, Ilboru, Mzumbe and the list goes on to Tabora School
 
Back
Top Bottom