Shule ya msingi Muhimbili

Rosweeter

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
1,171
4,432
Nimekuwa nikiguswa sana na hali ya mazingira ya Shule ya msingi Muhimbili. Imekuwa ni kawaida kwa maji machafu kufurika na kumiminika katika mazingira ya shule hiyo. Hali inakuwa tata zaidi inyeshapo mvua. Nina miaka saba katika maeneo haya na siku zote hali imekuwa ikijirudia mara kwa mara.

Mazingira haya ni hatarishi sana hasa kwa watoto wadogo wanaosoma shule hapo. Ninaamini afya za watoto hawa zinalindwa kwa kudra za mwenyezii Mungu tu kwani wako katika mazingira hatarishi sana hasa yatokeapo magonjwa ya milipuko. Ninachoshangaa ni jinsi ambavyo wahusika wamelifumbia macho suala hili na kuonekana kuridhika kwa kukaa bila kuboresha miundo mbinu katika shule hiyo na mazingira yanayoizunguka. Uongozi wa shule na kamati ya shule hawalioni jambo hili? Wazazi mnaosomesha wenye watoto katika shule hii mmeridhika na hali hii? Watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, ni wajibu wenu kuhakikisha miundo mbinu inaboreshwa.

Wito wangu naomba Halmashauri husika ilifanyie kazi suala hili siyo kusubiri mpaka maafa yatokee ndiyo ionekane kuna tatizo kama ambavyo tumeshazoea.

Nawasilisha.
 
Yapo upande gani maji hayo? Mwanangu anasoma hapo...
Ni huku upande wa makaburinii au...?
 
Yapo upande gani maji hayo? Mwanangu anasoma hapo...
Ni huku upande wa makaburinii au...?

Yakianza kutitirika siyo ya kutafuta mpaka getini na barabara kubwa ya United Nations, kiasi kwamba hata kuvuka barabara huwa ni shida.
 
Labda sereakli yenu iko kwenye MCHAKATO wa kulishughulikia vuteni subira kidogo.
 
Yakianza kutitirika siyo ya kutafuta mpaka getini na barabara kubwa ya United Nations, kiasi kwamba hata kuvuka barabara huwa ni shida.

mi siishi Dar.. Kwa kipindi hiki hali si shwari kutokana na uhaba wa mvua au..?
 
mmmh!!! subiri serikali iunde kamati ya kuchunguza miundombinu ya maji taka shuleni hapo and then watalipana posho kibao trust me!!!
 
hizi shule zilizopo mijini ni ambazo wajanja wanasubiri watanganyika wanaofahamu ni mali ya umma wafe wote ili wajimilikishe viwanja. Mojawapo ni shule ya msingi bunge. Watanzania mtakaobaki na kuuliza mtaambiwa hivi vilikuwa viwanja vye tuliviacha tu,sasa tumeamua kuvitumia,mtaoneshwa na hati kabisa. Miaka kumi ijayo pale takutana na minara ya nyumba mingi,bila serikali ya magamba kutoka madarakani we are dead!
 
Back
Top Bottom