kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Baba mmoja nchini Misri amempa mtoto wake mchanga jina la Facebook kama shukurani yake kwa tovuti ya Facebook kwa kusaidia kuwaunganisha Wamisri katika kumung'oa dikteta rais Hosni Mubarak aliyeitawala Misri kwa miaka 30.
Katika kusherehekea mapinduzi ya kumng'oa rais Hosni Mubarak, baba mmoja nchini Misri ameamua kumpa jina Facebook mtoto wake mchanga.
Jamal Ibrahim alikuwa miongoni mwa vijana nchini Misri walioshiriki kikamilifu katika kumshinikiza Mubarak aachie ngazi katika mapinduzi makubwa yaliyoanzia januari 25.
Kwa mujibu wa gazeti la Al-Ahram la nchini Misri, Jamal katika kuishukuru tovuti ya Facebook kwa kuwa chanzo cha kuwaunganisha waandamanaji, aliamua kumwita binti yake Facebook.
Jina kamili la mtoto wake litakuwa Facebook Jamal Ibrahim na tayari ndugu na jamaa wameanza kukusanyika nyumbani kwa Ibrahim ili kumuona mtoto Facebook.
Nchini Misri kuna watumiaji wa Facebook milioni tano, idadi ambayo ni kubwa kuliko nchi zote za mashariki ya kati.
Jumla ya makundi 32,000 yalianzishwa na Wamisri kwenye Facebook wakati wa kipindi cha mapinduzi ya kuuondoa utawala wa rais Mubarak.
Katika kusherehekea mapinduzi ya kumng'oa rais Hosni Mubarak, baba mmoja nchini Misri ameamua kumpa jina Facebook mtoto wake mchanga.
Jamal Ibrahim alikuwa miongoni mwa vijana nchini Misri walioshiriki kikamilifu katika kumshinikiza Mubarak aachie ngazi katika mapinduzi makubwa yaliyoanzia januari 25.
Kwa mujibu wa gazeti la Al-Ahram la nchini Misri, Jamal katika kuishukuru tovuti ya Facebook kwa kuwa chanzo cha kuwaunganisha waandamanaji, aliamua kumwita binti yake Facebook.
Jina kamili la mtoto wake litakuwa Facebook Jamal Ibrahim na tayari ndugu na jamaa wameanza kukusanyika nyumbani kwa Ibrahim ili kumuona mtoto Facebook.
Nchini Misri kuna watumiaji wa Facebook milioni tano, idadi ambayo ni kubwa kuliko nchi zote za mashariki ya kati.
Jumla ya makundi 32,000 yalianzishwa na Wamisri kwenye Facebook wakati wa kipindi cha mapinduzi ya kuuondoa utawala wa rais Mubarak.