Shujaa Tundu Lissu apata ajali, ni mzima

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Yule shujaa na mpambanaji wa haki, Mwanasheria wa Mahakama Kuu, Tundu Lissu, amepata ajali akiwa njiani kuelekea Singida na Manyoni.

Kwa mujibu wa Saed Kubenea aliyezungumza na Lissu, gari yake Lissu limeharibika vibaya lakini yeye hakuumia, mbali ya maumivu madogo. Hata hivyo upo uwezekano wa kuwa amepata maumivu ya ndani. Tutaendelea kuwahabarisha na yeyote mwenye taarifa zaidi aziweke humu
 
Pole Lissu, wishing you a quick recovery tunakuhitaji sana kwenye vita tulivyo navyo!
 
Pole sana Tundu Lissu, wishing you a speedy recovery uendelee kupambana na mafisadi!
 
Pole Mkuu Tundu

Natumai mambo yatakuwa poa na mapambano yataendelea kama kawa. Mungu hawezi kuwa mpuuzi kukuchukua wakati mechi haijafika hata dakika 45 za mwanzo. Tuko na wewe Mzee shujaa Lissu.
 
pole Tundu Lissu, mungu akupe afya njema ili tuendeleze mapambano ya kuikoa nchi yetu katika dimbwi la uchafu wa kila aina. Amen
 
Pole sana, Lissu -- Mungu anapenda uwe nasi katika mapambano haya magumu kwa wakati huu.
 
Mkuu Lissu, Get well soon! Unahitajika sana kny mpambano mkali tulionao sasa Tanzania!
 
Pole sana Tundu Lisu unakubalika mno mno...endeleza libeneka Mungu atakupa nafuu haraka urudi kwenye mpambano...
 
Pole sana Lissu,Watanzania wengi masikini wanakuhitaji,Mungu aendelee kukulinda uwe salama na afya njema.
 
Pole mpiganaji Lissu, we pray for your soonest recovery. mapambano ndo kwanza yanaanza
 
Pole Kiongozi,we wish you fast recovery to come back and take the charge of the war started already.
 
Back
Top Bottom