Should EU and US offer Political asylum to Tanzania' albino?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,462
39,928
I have written a "couple" of letters to some human rights group and a couple of foreign envoys suggesting to them that their respective countries should offer political asylum to Tanzanian Albinos who are living under constant fear of being mutilated and even being killed because some people believe that Albinos body part can be used in magic portion that would bring luck in businesses and other areas.

I have argued that, If these countries were to offer political asylum some of the Albinos who have no where else to go and who know that their government can not guarantee their security will take up the offer and move to another country where such threats are nonexistent.

The following were my major reasoning for such a suggestion:

a. The Chama cha Mapinduzi governmnet under President Kikwete's has miserably and demonstratively failed to stop the killings of Albinos since it got into power over three years ago. The killings have continued sporadically and with such impunity.

b. The security apparatus and law enforcement agencies of the country are not able to carry out a systematic, professional, and successful operation to collect intelligence, investigate, arrests and prosecute to the extent of the law all people who are accused of financing, carrying out, or profiteering from this abominable acts of violence.

c. The call by the Prime Minister Mizengo Pinda about fortnight ago for people to administer mob justice by carring out summary executions of people accused of killing albino is a clear indication and verifiable proof of government inability to curb the killings of Tanzanians with albinism a medical conditions that can be found in almost all species of the animal kingdom.

d. The western powers have already in the past and continue to do so, provided political asylum to minority groups which have been subjected to discrimination, torture or even killings. Such groups included racially minorities, transgender people, gay, religious minority, women fleeing FGM etc.

I believe that Albinos are a very tiny minority in the country and their conditions even more immutable and in a sense more recognizable than other conditions and hence deserve such protection which can not be guaranteed in their own country.

I hope the letters will be responded promptly by these government creating the conditions for prompt and scheduled movement of Albino to places where they will be safe from persecution.

M.M. Mwanakijiji

NB: I have not send these letters out yet, but depending on what happens tomorrow in the National Assembly nitaituma kesho. Nakubali masahihisho ya lugha, mawazo, na mpangilio wa fikra.
 
Last edited:
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu unayafanya haya kwa nia nzuri sana lakini sidhani kama utaratibu wa Asylum unakwenda hivyo, pamoja na kwamba barua yako ni nzito kichizi.....

Kwanza si wanatakiwa watoke nje, na wafike huko waendako wachukue hiyo asylum au unataka kunambia serikali ya Tanzania italazimishwa kuwapa visa na ticket hao Albino waondoke nchini baada ya kuwa granted asylum wakiwa ndani!.. Sijawahi kusikia wala kuona utaratibu kama huu!

Hata hivyo, mimi nadhani msaada mkubwa utapatikana ndani nchini yaani sisi wenyewe na vyombo hivyo vya kimataifa NGOs wanaweza kuwasaidia hawa jamaa zetu na suluhu ya maswala ya Albino yapo ndani chumbani mwetu.. Hawa sii kizazi kinachokwisha kesho kiasi kwamba tufikirie kuwatenga na sisi wananchi kukubali kuwa Tanzania sii mahala pao isipokuwa huko nje. Hawa ni raia, solution ni LAZIMA itoke ndani ikiwa sisi sote tunaamini kuwa serikali imeshindwa kuwalinda..

Na nikirudi ktk usemi huu wa serikali kushindwa kuwalinda, inaonyesha pia sisi wananchi tumeshindwa kuwalinda hivyo unapopingana na usemi wa waziri mkuu ni bora uje na suggestion ya kitu gani wananchi wanatakiwa kukifanya tofauti na waziri mkuu..Laa sivyo itaonyesha sisi sote tumejiunga kuwabagua hivyo wanapochukua asylum nje tutajumuishwa sote na serikali yetu kuwa tumewatenga...
Huo ndio ushauri wangu!..
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu unayafanya haya kwa nia nzuri sana lakini sidhani kama utaratibu wa Asylum unakwenda hivyo, pamoja na kwamba barua yako ni nzito kichizi.....

Kwanza si wanatakiwa watoke nje, na wafike huko waendako wachukue hiyo asylum au unataka kunambia serikali ya Tanzania italazimishwa kuwapa visa na ticket hao Albino waondoke nchini baada ya kuwa granted asylum wakiwa ndani!.. Sijawahi kusikia wala kuona utaratibu kama huu!

Hata hivyo, mimi nadhani msaada mkubwa utapatikana ndani nchini yaani sisi wenyewe na vyombo hivyo vya kimataifa NGOs wanaweza kuwasaidia hawa jamaa zetu na suluhu ya maswala ya Albino yapo ndani chumbani mwetu.. Hawa sii kizazi kinachokwisha kesho kiasi kwamba tufikirie kuwatenga na sisi wananchi kukubali kuwa Tanzania sii mahala pao isipokuwa huko nje. Hawa ni raia, solution ni LAZIMA itoke ndani ikiwa sisi sote tunaamini kuwa serikali imeshindwa kuwalinda..

Na nikirudi ktk usemi huu wa serikali kushindwa kuwalinda, inaonyesha pia sisi wananchi tumeshindwa kuwalinda hivyo unapopingana na usemi wa waziri mkuu ni bora uje na suggestion ya kitu gani wananchi wanatakiwa kukifanya tofauti na waziri mkuu..Laa sivyo itaonyesha sisi sote tumejiunga kuwabagua hivyo wanapochukua asylum nje tutajumuishwa sote na serikali yetu kuwa tumewatenga...
Huo ndio ushauri wangu!..

Hata mimi nilikuwa na mawazo kama yako....ila sina uhakika taratibu za asylum zikoje
 
Mwanakijiji nakwambia usishangae kukuta baadhi ya wabongo tayari wamesha-apply political asylum wakitumia haya mauaji ya albino, watu hawachelewi kukwambia kuwa wana wazazi ambao ni albino kwa hiyo na wao wana genes ambazo zinaweza kuzaa mtoto ambaye atakuwa albino kwa hiyo kurudi kwao Tanzania kunaweza hatarisha maisha ya vizazi vyao vijavyo, mtu anatafuta lawyer mzuri halafu ana-file. Nakwambia wewe subiri tu.
 
Kuna mtu anaweza kufafanua Political Asylum inakuwaje? Na ina mahusiano vipi na Albino!!
Naomba kueleweshwa tu...
Natanguliza shukrani.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu wangu unayafanya haya kwa nia nzuri sana lakini sidhani kama utaratibu wa Asylum unakwenda hivyo, pamoja na kwamba barua yako ni nzito kichizi.....

Kwanza si wanatakiwa watoke nje, na wafike huko waendako wachukue hiyo asylum au unataka kunambia serikali ya Tanzania italazimishwa kuwapa visa na ticket hao Albino waondoke nchini baada ya kuwa granted asylum wakiwa ndani!.. Sijawahi kusikia wala kuona utaratibu kama huu!

si lazima kuwa hivyo. Endapo serikali ya mojawapo ikatambua kuwa kundi fulani ndani ya nchi fulani liko katika hali ya wasiwasi basi wanaweza kuwapa nafasi hiyo. HIlo limetokea kwa Wasomalia na Wasudan ambao ndani ya nchi zaoo walikuwa wanaangamizwa.

Kinachotakiwa ni hilo kundi kuwa designated kama ni "threatened group" au kitu kama hicho. Marekani ilihamisha mamia ya Wasudan na Wasomalia kutoka nchini mwao (kupitia Kenya) baada ya kuwatambua, kuwapa taarifa zote sahihi.

Hata hivyo, mimi nadhani msaada mkubwa utapatikana ndani nchini yaani sisi wenyewe na vyombo hivyo vya kimataifa NGOs wanaweza kuwasaidia hawa jamaa zetu na suluhu ya maswala ya Albino yapo ndani chumbani mwetu..

Hilo ni kweli, lakini katika historia ya maisha ya wanadamu mahali popote ambapo maisha hayo yanatishiwa basi watu na jamii inayohaki ya kuwalinda watu hao. Hii ndiyo sababu kuna watu ambao kuanzia wakati wa mapinduzi ya Bolshevik, vita ya pili ya dunia, n.k Nchi mbalimbali zilitengeneza utaratibu wa kutambua na kuwapokea watu ambao maisha yao yanakuwa hatarini.

Zaidi ya hivyo naamini sisi hatuna uwezo wa kuzuia mauaji ya albino kwa kadiri ya kwamba serikali iliyopo ndiyo inatakiwa kusimamia sheria hizo. Inapofikia serikali ya fedha nyingi, vyombo vingi vya ulinzi inafikia mahali kuagiza UVCCM na Sungusungu kufanya kazi za kipolisi na kiusalama kana kwamba vyombo hivyo vimeapishwa kufanya mambo hayo ina maana moja tu. Tumeshindwa.

Hawa sii kizazi kinachokwisha kesho kiasi kwamba tufikirie kuwatenga na sisi wananchi kukubali kuwa Tanzania sii mahala pao isipokuwa huko nje.


Hii siyo tafsiri sahihi. Tunachofanya ni kusema kuwa "sisi tumeshindwa kuwalinda, na hivyo tunaomba wengine watusaidie kufanya hivyo". Kukiri upungufu huo siyo kukosa uzalendo au kutokuwa mtaifa bali ni kupima kipi kilicho juu kati ya kutaka waendelee kukaa Tanzania wakati mchana na usiku wanawindwa kama paa au kuwapatatia nafasi na mahali ambapo ujinga wa imani za kishirikina hauna nguvu hiyo? Ni uzalendo kuwalinda maalbino na vikongwe mahali popote pale.


Hawa ni raia, solution ni LAZIMA itoke ndani ikiwa sisi sote tunaamini kuwa serikali imeshindwa kuwalinda..

Na nikirudi ktk usemi huu wa serikali kushindwa kuwalinda, inaonyesha pia sisi wananchi tumeshindwa kuwalinda hivyo unapopingana na usemi wa waziri mkuu ni bora uje na suggestion ya kitu gani wananchi wanatakiwa kukifanya tofauti na waziri mkuu..

Nimeshatoa suggestion yangu kuhusu hilo. Kuna thread nimeanzisha mbili na moja wameanza kufanyia kazi lakini kiuvivu. Hawana dhamira ya wazi na ya makusudi ya kukomesha mauaji haya zaidi ya amri za kukurupuka na maagizo ya kihalifu.


Laa sivyo itaonyesha sisi sote tumejiunga kuwabagua hivyo wanapochukua asylum nje tutajumuishwa sote na serikali yetu kuwa tumewatenga...
Huo ndio ushauri wangu!..

Hapana atakayefikiri tumewatenga sidhani kama tunaweza kumzuia. Kama serikali imeshindwa imeshindwa. Kwa mtu albino haitaji kuambiwa kuwa anatengwa au la, anahitaji kujua kuwa yuko salama. Tukiendelea kuacha mambo yaendelee hivi hivi tukiamini kuwa ati kuna wana usalama wenye uwezo wa kuzuia mauaji haya tunajidanganya.

Tunachofanya ni kuishika ile tunu iliyotuunda sisi kama taifa kuwa "binadamu wote ni sawa" na ya kuwa "kila mtu ana haki ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake". Katika hayo yote hatujasema "kila raia" ni sawa au "kila raia ana haki..."

Tumesema binadamu na mtu. Kwa maneno mengi haki zetu kama binadamu ni za juu zaidi kuliko haki zetu kama raia. Unaweza ukapunguza au kuzuia baadhi ya haki za raia, lakini kuzia haki za binadamu ni karibu haiwezekani. Na haki ya kwanza ya msingi na kubwa kabisa ambayo ni haki ya binadamu ni haki ya kuwa hai.

Jamii inaposhindwa kuilinda haki hiyo au kuhakikisha uwepo wake basi jamii hiyo haiwezi kuwa kikwazo kwa yule ambaye uhai wake unatiishiwa kuamua kutafuta njia nyingine ya kulinda maisha yake.

Naamini kuwafungulia mlango katika nchi za magharibi ni jaribio la kufanya hivyo.
 
Good idea, lakini nakubaliana na Mkandara.
Ila na matatizo ya economy haya, wataenda nchi gani? Watu wana usongo na immigrants, unaweza kuwaongezea matatizo mengine.
The fact tunashindwa kutatua hili tatizo, says a lot more about us....which is not much. Noma, noma.
 
Good idea, lakini nakubaliana na Mkandara.
Ila na matatizo ya economy haya, wataenda nchi gani? Watu wana usongo na immigrants, unaweza kuwaongezea matatizo mengine.
The fact tunashindwa kutatua hili tatizo, says a lot more about us....which is not much. Noma, noma.

Oh yeah...hivi sisi tunaweza nini?
 
Mzee Mwanakijiji,
si lazima kuwa hivyo. Endapo serikali ya mojawapo ikatambua kuwa kundi fulani ndani ya nchi fulani liko katika hali ya wasiwasi basi wanaweza kuwapa nafasi hiyo. HIlo limetokea kwa Wasomalia na Wasudan ambao ndani ya nchi zaoo walikuwa wanaangamizwa.
Kinachotakiwa ni hilo kundi kuwa designated kama ni "threatened group" au kitu kama hicho. Marekani ilihamisha mamia ya Wasudan na Wasomalia kutoka nchini mwao (kupitia Kenya) baada ya kuwatambua, kuwapa taarifa zote sahihi.

Mkuu labda nifafanue zaidi pengine hukunielewa mahala...
Mtu yeyote anayetaka Asylum ni lazima awe nje au akimbilie Ubalozi wa nchi fulani kutokana na Politcal issue iliyomweka maisha yake hatarini, kisha toka hapo ndipo anaweza kuvutwa nje..Process yake ni tofauti kabisa na refugee..
Asylum haitolewi kwa huruma kwa kundi la watu fulani waliokuwa threatened, laa sivyo tungeona Asylum kibao zikitoka hasa kwa nchi kama Burma, Palestina na kadhalika licha ya kwamba asylum hutolewa zaidi kwa Political figures ambao wanapingana na utawala..Na watu wengi sana hufanya makosa wanapokimbilia immigration za nje na kuomba asylum wakati wao sio wanasiasa...Mfano wako wa Wasomali na Wasudan hawa ni wakimbizi tu wanapewa refugee status na sio asylum..

Kifupi mkuu wangu panga pangua haiwezekani! huwezi kuwapa asylum kundi la watu isipokuwa taasisi za haki duniani zinaweza kushinikiza kimataifa watu hawa wawekwe ktk kundi la kusaidiwa hivyo ni mpaka huyo Albino au kundi lao wafike ktk kambi au vituo vinavyopokea refugees na wajisalimishe hapo.. Hakuna sheria wala utaratibu wa kupokea refugee within the same country inayowakadamiza, labda iwe ni shelter ya muda kwa refugee kama ilivyo Kongo..
Mbali na hayo, case ya albino ni complicated zaidi kwa sababu wanatafutwa na kundi dogo sana la watu wenye imani za Uchawi na sio serikali yenyewe..It's not a Political case.
 
Last edited:
Gosh, hivi tunafikiria mambo kwa kutumia akili au ubongo?

Kwanini watu wanakuwawalegevu wa kufikiri au bado tuna dhana ya matatizo yetu yatatuliwa na 'mjomba'?

Nakiri kuwa waafrika ndivyo tulivyo na viongozi ni reflection ya sisi wananchi tulivyo.

Simlaumu mtu yeyote.
 
...waende wakapige camp tuu American Embassy hakuna atakayewafukuza hata kama hawaletwa States lakini nina uhakika kuna kitu kizuri kitafanyika juu yao,na ni kweli wanauwawa hata hizo balozi wako aware na hii kitu na serikali imeshindwa kuwasaidia,naamini asylum ni njia mojawapo ya kuwasaidia ...wajaribu tuu,sisi tunaongea tuu sometimes bila kujua lakini seriously hawa wenzetu wako in fear of imminent death!
 
Koba,
Mkuu hakuna mtu anayekataa maoni ya Mwanakijiji lakini tujaribu kufahamu sheria zinakwenda vipi.. Hawawezi kupewa asylum ikiwa serikali yetu sio adui yao isipokuwa kundi la watu wasiofahamika sana sana watai pressure serikali yetu, jambo ambalo nadhani barua ya Mwanakijiji inaweza kusaidia, nje ya hapo tunavuta siku tu..

Wakienda Ubalozi wa Marekani na kuomba asylum, mkuu wangu labda unasahau kwamba hata kama kuna vita nchini Marekani watafunga gate lao na hakuna mtu anaruhusiwa kupewa shelter unless ni Mmarekani, European au unayo hata green card. Usiwaone hawa jamaa kuwa ni watu wanasema sana lakini bila kuwepo interest zao mara nyingi hutega mgongo...tena tukio kama hili wao huweza kuuza news zao na watasema sana!...Umeona ya Zimbabwe walishindwa/ wanashindwa nini kuwapa hifadhi wananchi MDC hadi wanakimbilia South..
 
Gosh, hivi tunafikiria mambo kwa kutumia akili au ubongo?

Kwanini watu wanakuwawalegevu wa kufikiri au bado tuna dhana ya matatizo yetu yatatuliwa na 'mjomba'?

Nakiri kuwa waafrika ndivyo tulivyo na viongozi ni reflection ya sisi wananchi tulivyo.

Simlaumu mtu yeyote.

toa pendekezo lililobora badala ya cheap shots. Wewe unatumia ubongo na akili wengine tunatumia meno.
 
A very interesting suggestion indeed.But even those countries you are suggesting shoud take our Albinos do not have any human rights at all.I wish you knew what is happening in their own countries and what they are doing to the world.They do not have respect for human life at all.If they had they wouldn't turn a deaf ear to the slaughter which which happens in many parts of the world,and only recently the slaughter in Palestine.Shamelessly they stood by while innocent people were being slaughtered by the Iraelis!The long term solution to this problem and many others is is for us to make our leaders more accountable to us.We can do it,only that we haven't been serious enough.
 
Mkandara,

You are right on point, well said, couldn't have said better myself!

Mwanakijiji,

Sidhani kama kuwatafutia albino asylum ni solution maana albinos wataendelea kuwepo tu watakuwa wanaendelea kuzaliwa sasa sijui utashauri wakizaliwa tu tuwawahishe US au EU??? How practical is that?
Hivi kweli tunashindwa kukomesha huu unyama wanaofanyiwa kweli? Ama kweli...
 
CAVEAT: Iam not a immigration expert, but it doesnt require one..to appreciate the plight of Albino in TANZANIA.

Kimsingi Mwanakijiji mawazo yako yanatekelezeka na wala si ya kufikirika as some of us might think.

Katika kuomba asylum kila nchi ina sheria zake. Lakini cheafly tuna sheria mbili ambazo hapa ziko relevant. Geneva Convention for the Protection of Refugees ya 1951 na Protocal ya OAU Convention ya mwaka 1969. Ila hii haizuii kila nchi kuwa na sheria zake.

Mkandara yupo right kwamba one cane make his case for asylum well if is already outside his country. Now can albino claim asylum? in another country? Yes they can: Kwa sababu they fear for PERSECUTION and evidence are ample that they have been persecuted enmasse-simply because they are Albino!. The government and the internationa community know this. Can they avail themselves the protection of their country? Not really, because, as Mwanakijiji said, serikali imeshindwa kuwalinda na kwa hili wana case kwamba hawana protection ya aina yoyote na wengi wanaishi maisha ya woga kwamba hawajui watakufa lini.

How do they get this asylum? Either mtu anaweza kwenda straight (kama wengi wanavyojilipua). Ukishafika huko hawawezi kukurudisha as long as wanajua kwamba your life is in danger. And for this Albino can make a serious case! Infact this is how many women from West Africa especially Mauritania and Mali get their asylum in US. In US FGM (ukeketaji wa wanawake) ni ground ya asylum. But ukienda in other countries FGM is not a ground for asylum. So for Albino vitu vikubwa hapa ni viwili (fear of persecution and failure to avail themselves protection of their country).

Alternatively wanaweza kwenda US embassy wakaomba visa (ofcourse hii itakuwa ngumu (mfano anybody from Somalia akishaingia Ulaya au US hawezi kurudishwa kwao maana hakuna serikali/protection, lakini huyo huyo msomali hawezi kwenda US au UK embassy kuomba asylum ya kwenda nje-hawatampa). So kikubwa ni jinsi utakavyofika kwenye hizo nchi. By the way option ya kuombea visa nchini kwako it is almost impossible maana itaonyesha kwamba serikali imeshindwa kuwalinda watu wake-ambayo ni fedheha machoni mwa jamaii ya kimataifa). Hata kama kweli imeshindwa as Pinda has said.

By the way hata ile kauli ya Pinda kwamba anayeuwa Albino auawe, inaweza kuwa ground nzuri ya kuomba asylum, maana inadhihirisha kwamba hata serikali IMESHINDWA kusimamia sheria zake yenyewe, na imeamua ipromote "street justice" So hapa somebody can use this statement against the government.

Just know, US have what they call "third country rule" which means ukipandia ndege Dar kwenda US..ukapitia Canada..ukiingia US hata kama una ground credible hawawezi kukupa asylum..watakwambia urudi Canada ukaombee huko (sofar as I know this rule is valid between US and Canada).

Lakini ukweli ni kwamba Albino wanaweza kuomba asylum popote pale..maana case yao imeshapigiwa kelele na watu mbali mbali including UN, EU and others...Ofcourse Albino wanazaliwa kila siku..lakini huwezi ukaweka maisha ya mtu rehani kisa..watazaliwa wengine..kila mtu yupo kivyake...Its complex, but if you meet immigration lawyer anayeijua kazi yake..basi wewe utaungana na akina Mwanakijiji kula kuku huko unyamwezini!
 
Inaweza kuwa ni feasible solution wakati huu tunapooneka kushindwa kutatua tatizo la mauaji haya. Practicalities zinaweza kuwa sorted out e.g. kupitia UNHCR.

Hili la Albinos linafanana fanana na la Somali Bantus ambao huko nyuma walikuwa resettled in the United States, Mozambique na Tanzania.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom