Shosti zima simu: Utasema mtandao wa TIGO ulikuwa unasumbua! (wanaume someni hapa)

Hehehe, mtenda akitendwa huhisi kaonewa! Kuna mwanaume anapigiwa simu anakuta missed call 10 afu anasema simu haikuita kabisa! Khabari yake banaa!
 
Hehehe, mtenda akitendwa huhisi kaonewa! Kuna mwanaume anapigiwa simu anakuta missed call 10 afu anasema simu haikuita kabisa! Khabari yake banaa!
He he he....tena anaapa kwa jina la mungu na la mizimu yote ya kwao...lol
 
All above tukubali bila ya kuyatia maneno yetu kunako Bleander ! Kua simu zina advantage na dis. Kama simu zingekua hazina tatizo kwa 100% . Basi kuanzia Primary, Secondary Schools student wangeruhusiwa kuanazo mashuleni. Hata prisoners wangeruhusiwa.
 
Kama unawasiwasi na dem wako kwamba nasingizia mtandao wewe nunua cm ya line mbili ya samsung mwekee lini za voda na Airtel, pamoja na tigo yake anakuwa na line 3, kwisha habari yake.
 
Hivi Balck Berry nazo zinapoteza network?

BB kama BB ni simu ya kawaida tu, ukijiunga na mtandao wowote ndo utapata hizo huduma za BBM na Emails kwa hio ukichagua Tigo kupoteza network ni kama kawa, mi hapa natumia mtandao wa Tigo kwenye BB basi Emails zinaweza kaa hewani hata wiki ndo upate notification!
 
Mkuki kwa nguruwe kwa binadam mchungu, mnavyowatendea wadada mnafikiri ni vizuri au wao hawaumii? mnawapanga kama wako kwenye foleni za Dar, ukipigiwa uko kwa huyu unajifanya nimfanyakazi mwenzio anakusumbua hupokei, ukienda kwake mwingine akapiga ni hivyo hivyo. Huyu dada alikuwa sahihi kwani hata yeye kwa Fred hayuko peke yake, kwanini yeye Fred awe peke yake
 
Mkuki kwa nguruwe kwa binadam mchungu, mnavyowatendea wadada mnafikiri ni vizuri au wao hawaumii? mnawapanga kama wako kwenye foleni za Dar, ukipigiwa uko kwa huyu unajifanya nimfanyakazi mwenzio anakusumbua hupokei, ukienda kwake mwingine akapiga ni hivyo hivyo. Huyu dada alikuwa sahihi kwani hata yeye kwa Fred hayuko peke yake, kwanini yeye Fred awe peke yake

shusha munkari madam, changia taratibu hasira za nini sasa!
 
Haya maneno nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe toka kwa dada mmoja aliyekuwa akienda kwa buzi lake ili hali jamaa yake akiwa anamfuatilia kwa simu. Rafiki yake alipoona shostito wake hana mbinu za kumuepuka huyo mpenzi wake 'halali', akamshauri aizime simu yake ya TIGO ili awe free na huko alikokuwa akiupeleka 'mzigo' kwa njemba mwingine. Atakufanya ukose kuonana na John wakati ulimuahidi siku nyingi leo tungeenda kwake. Aaah! Huyu Fred naye yaani anavyokung'ang'ania, halafu ndoa yenyewe kila siku anakupiga kalenda. Nenda tu kwa John mwaya, pengine anaweza kuwa wa maana kuliko Fred. Na kweli rafiki yule akazima simu huku akikenua mdomo. Mie nikabaki hoi, huku nikiwa nimepata funzo, kwamba huu ubabaishaji wa mtandao wa simu wa TIGO kumbe unachangia pia watu 'kuibiwa mali' zao kiulainiiii. Jamani wanaume, sio kila unapomkosa mpenzio kwa mtandao wa TIGO ukadhani eti ni kwa sababu ya ubabaishaji wa huo mtandao. Inawezekana wakati mwingine mtandao uko ok, ila simu imezimwa makusudi kuepuka 'usumbufu' wako. Unaibiwaaaaaa kwa kisingizio cha TIGO, ebbo!
Hii ishu sio kwa wadada tu,
Hata wanaume wanaiaplai sn tu,
Tena wao some time hata ikipatikana km kawekwa mtu kati wala hapokei,
Km vp wenye presha hizi wanunuliene watu wenu line zaidi ya moja,
Japo itakuwa ni kujifariji tu ila haiizuii mtu kuchiti.
 
Back
Top Bottom