Shoga ambaye alivuma katika skendo la ngono lililomkumba mchezaji nyota wa Brazili Ronaldo de Lima amefariki kutokana na ugonjwa wa ukimwi.
Andre Albertini, shoga mwenye umri wa miaka 22 ambaye alikuwa akijiita "Andreia", alizikwa ijumaa baada ya kufariki siku ya alhamisi hospitalini katika kitongoji cha Maua jijini Sao Paulo.
Chanzo cha kifo chake ni ugonjwa wa neurotoxoplasmosis, ugonjwa ambao husababishwa na maambukizi kwenye ubongo unaosababishwa na ukosefu wa kinga mwilini, cheti chake cha kufariki kiliandikwa hivyo.
Andreia alikuwa miongoni mwa mashoga watatu ambao Ronaldo de Lima aliwaalika kwenye chumba chake cha hotelini mwezi wa nne mwaka jana.
Andreia alilalamika kuwa Ronaldo aligoma kuwalipa kiasi cha pesa walichokubaliana naye awali kwaajili ya ngono.
Ronaldo alikanusha madai hayo na kusema aliwachanganya mashoga hao na wanawake na alikataa kulipa kwa huduma zao baada ya kugundua walikuwa ni wanaume.
Ronaldo alidai mashoga hao walitishia kumchafulia jina asipowalipa.
Mama yake na Andreia alisema kuwa mwanae alipata ukimwi mwaka 2006 jijini Rio de Janeiro. Aliongeza kuwa siku ya jumanne alizidiwa na ilimbidi amwahishe hospitali na ndipo siku ya alhamisi alifariki.
Ronaldo ambaye wakati wa skendo hilo alikuwa akiichezea AC Milan ya Italia hivi sasa anakiputa kwenye ligi ya Brazili akiichezea timu ya Corinthians baada ya kukaa nje ya uwanja kwa mwaka mzima kutokana na kuwa majeruhi.
Source: Nifahamishe.com