Ustaadh
JF-Expert Member
- Oct 25, 2009
- 413
- 19
PROFESA Issa Shivji amepinga msimamo wa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa kutaka nchi za Afrika Mashariki kuweka malengo ya kupata chochote kutoka Marekani kutokana na kuongozwa na Rais Barack Obama .
Amesema itakuwa fedheha kama nchi za Afrika Mashariuki zitabweteka na kusubiri fadhila kutoka Marekani na kwamba kwa vyovyote vile hakuna kitakachotolewa Marekani bure.
Juzi, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Diodorus Kamala akizungumza kwenye kongamano la jinsi ya kunufaika na utawala wa Rais Obama alisema Afrika Mashariki ni lazima inufaike na uongozi wa rais huyokwa kuwa ni mwwenye asili ya Afrika Mashariki.
Kamala alisema Afrika Mashariki ingalie ni vitu gani ambavyo vitaiwezesha Marekani kuisaidia ikiwa ni pamoja na kuboresha miundo mbinu kudumisha amani na demokrasia ya kweli.
Lakini Shivji alisisitiza kwamba ni bora Afrika Mashariki ikajitegemea ili kuepuka kutawaliwa kiuchumi na Marekani.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Profesa Shivji alisema Afrika Mashariki isitegemee kunufaika na uongozi wa Barack Obama kutokana na ukweli kwamba hakuna sera iliyobadilika nchini Marekani na kwamba Obama anaendeleza Sera za Bush.
"Suala hili tutapoteza uhuru wetu, kwanini tutegemee Marekani kutuamlia mambo yetu, Marekani ni nani ?, sanasana Marekani watatusaidi silaha za kijeshi, je tunataka kujenga bara letu kijeshi? "alihoji Shivji ambaye ni Mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
"Mbona kipindi cha chama cha TANU hakikuwa chini ya taifa lolote na tuliendelea mpaka tukapata CCM sasa hapo
"Kwa kifupi mimi nataka Marekani iwe mbali na Afrika Mashariki, Afrika isitegemee mjomba , ikitaka kupata maendeleo ipigane yenyewe kama ni kudumisha amani tudumishe kwa manufaa yetu wenyewe sio Marekani ije"alisema.
Hata hivyo, alisema wasomi wa Afrika Mashariki wanapaswa kulaumiwa na kujilaumu wenyewe kwa kutowaelimisha watu juu ya ubaya wa kutegemea wafadhili kwa kuwa bara letu kihistoria ndefu.
Source:http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=17852
Amesema itakuwa fedheha kama nchi za Afrika Mashariuki zitabweteka na kusubiri fadhila kutoka Marekani na kwamba kwa vyovyote vile hakuna kitakachotolewa Marekani bure.
Juzi, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Diodorus Kamala akizungumza kwenye kongamano la jinsi ya kunufaika na utawala wa Rais Obama alisema Afrika Mashariki ni lazima inufaike na uongozi wa rais huyokwa kuwa ni mwwenye asili ya Afrika Mashariki.
Kamala alisema Afrika Mashariki ingalie ni vitu gani ambavyo vitaiwezesha Marekani kuisaidia ikiwa ni pamoja na kuboresha miundo mbinu kudumisha amani na demokrasia ya kweli.
Lakini Shivji alisisitiza kwamba ni bora Afrika Mashariki ikajitegemea ili kuepuka kutawaliwa kiuchumi na Marekani.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Profesa Shivji alisema Afrika Mashariki isitegemee kunufaika na uongozi wa Barack Obama kutokana na ukweli kwamba hakuna sera iliyobadilika nchini Marekani na kwamba Obama anaendeleza Sera za Bush.
"Suala hili tutapoteza uhuru wetu, kwanini tutegemee Marekani kutuamlia mambo yetu, Marekani ni nani ?, sanasana Marekani watatusaidi silaha za kijeshi, je tunataka kujenga bara letu kijeshi? "alihoji Shivji ambaye ni Mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
"Mbona kipindi cha chama cha TANU hakikuwa chini ya taifa lolote na tuliendelea mpaka tukapata CCM sasa hapo
"Kwa kifupi mimi nataka Marekani iwe mbali na Afrika Mashariki, Afrika isitegemee mjomba , ikitaka kupata maendeleo ipigane yenyewe kama ni kudumisha amani tudumishe kwa manufaa yetu wenyewe sio Marekani ije"alisema.
Hata hivyo, alisema wasomi wa Afrika Mashariki wanapaswa kulaumiwa na kujilaumu wenyewe kwa kutowaelimisha watu juu ya ubaya wa kutegemea wafadhili kwa kuwa bara letu kihistoria ndefu.
Source:http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=17852