Mbu
JF-Expert Member
- Jan 11, 2007
- 12,753
- 7,844
Marhaba! Hujambo ww?
...ee, mi' sijambo.
Na je kama mke ndiyo kamzidi umri bado amwamkie mumewe?
Nadhani "shikamoo" kama salamu ina maana ya kumnyeyekea mtu... kuonyesha kuna ambaye yuko juu ya mwingine - kiumri, kicheo, n.k. Sasa kwenye ndoa kuna hiyo hierachy? au kwa vile imani nyingine zinasema mume ni kichwa?
Inapendeza heshima iwe ya hiari na siyo ya kulazimisha.. na kwa wanandoa salamu yenye kuonyesha mapenzi ni bora zaidi kuliko ile yenye kuonyesha matabaka.
...umegundua siku hizi unaweza kupewa shikamoo na kufuatiwa na kuombwa shilingi mia ya daladala?
...au kina dada wanatumia "shikamoo" kuwafungisha breki wanaume wakware?