Shibuda out

Tatizo hapa ni Zitto na Lema au ni Shibuda? Na waliomteua Shibuda kukaimu nafasi hiyo hawakujua sheria kuhusu taratibu na kanuni za Chama?
 
CDM mwaongoza kwa siasa za majitaka, nyie ni shari tu! mara mnataka kupigana. Hiki chama hakina future.

CCM mwaongoza kwa ulafi wa mali za watanzania, chadema ina maisha marefu zaidi kuliko ccm, ndio kwanza inazaliwa. ccm jiandaeni kuzikwa tu bado siku ngapi muwavulie uvivu mapacha watatu?
 
mkuu ni kweli kabisa aliyenena hapo juu yupo sahihi, leo nusura lema na zitto zipigwe pale lema alipo mwambia zitto ukweli kuwa aache kutumiwa na hata kaa afanikiwe kwenye mipango yake hiyo na kuwaacha wajumbe wote midomo wazi kila mmoja akishangaa kijana lema asivyo mumunya maneno na kuamua kumtolea uvivu zitto

unapokataa jina lako kwe Jf unataka 2kuelewe vipi wewe dogo?
 
chadema hawakubali mawazo yanayopingana na mwenye chama mtei na mkwewe mbowe.

zitto kadandia basi asilolijua. kama kabouru siku itafika atadondoka.

shibuda mambo yake yalikuwa yanavumuliwa ccm tu chadema watamwita msaliti. hawataki kusikia mbowe anapingwa.

hakuna demokrasi hapo ni kamchezo ka kuigiza.
 
Akiondoka zitto ana sababu,na hizo sababu lazima aziseme.....na akizisema moto utawaka.....najua wapo washabiki wasio jua ninalosema watataka kunirushia matusi ila zito anakubalika ndani ya chama na wapo humo ndani wanaomchafua nje ya chama ili wamharibu kisaikolojia....na wameshindwaa...nitawataja tu siku yaja.......hadharani sio humu namaanisha magazetini na tv.....pumbavu zao kabisaaaaaaa wanaharibu chama.....
 
nani atamuua? sema sasa usikike ww quinine....tena usitake kuwaamushia watu hisia mbaya....yaani wewe hufai kusimama mbele ya watu na kutoa hotuba kaka/dada....looo neno kama hilo sio la kuropoka kwa chadema ambayo imehusishwa na matukio hayo...au ww ni wale wajanja wa ccm mnaanza kuwajengea cdm vihoja hivyo na wao wakikurupuka kama heche wataanza kugombana,nyie mnakula maiani....pitia mbali ww
 
huyo ni kimeo mkuu, uwezi kushindana kwa hoja na mtu anayewinda kukutoa macho
huyo yuko kazini
Mkuu ungetoa hoja na si kumtukana mwenzio Mkuki Moyoni!! Hujaonyesha ukomavu wa kupingana kwa hoja. Tukiendelea hivi kuna siku tutataka milango ifungwe ili tupigane humu ndani ya jamvi!!
 
TAARIFA HII SIO YAKWELI, IPO KICHONGANISHI, haya mambo sio rasmi, tuweni makini. Jf itakuwa sasa kibanda cha kahawa!

Umesema vyema mkuu hebu tupatie yakwako iliyo sahihi.(Binafsi naamini hujakurupuka) Tafadhari tumwagie hapa .
 
Jamani nashindwa kuelewa,jamaa kama kasema ukweli ndio ulivyo,je, kwa nn unampangia maneno ya kuonge,eti asiongee ya ndani yaliyotokea.na mbona hilo la shibuda out umelipokea...je sio la ndani? halafu huyu dogo huyu Lema anamwambia zitto katumwa...hahaaa ni shida kweli kweli na huyu asipokaa sawa mwisho wa siasa zake za upepo uko karibu sana, au na yeye anatumwa na Mbowe? huu ni ulimbukeni tu unamsumbua lema .....na kama watu hawana nidhamu wataambiwa tu,kisa cha zito kumtetea shibda ni haki yake ya upenzi na uwezo wake wa kuona mbali,je mbowe anahofia shibudaa kumng'oa cheo na kukirudisha chama kanda ya ziwa?tusubiri tutaona mengi...mmejaribu kumchafua shibuda magazetini na jf lakini jueni shibua anaheshimika na kukubarika kuliko huyo slaa na mbowe..kwanza hawawezi kuwa marais wa nchi hii,mfanyabiashara na mwizi wa wake za watu....lema umechemka dogo...bado unasafari ndeeefu sanaaa.
Najaribu kujiuliza pale mwana CCM anapomtetea Shibuda sipati jibu, lakini for your information unaowaandikia hapa JF wanaweza kuwa na IQ kubwa pengine kuzidi yako.
 
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.
Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.

Boma umekosea ka si mahaba yako kwa Zitto kwani c kweli kuwa Zitto ana vision kuliko Slaa na Mbowe vinginevo tupe ushahidi wako katika hili! Uelewa wa Slaa hauwez kulinganishwa na wa Zitto hata kidogo labda umlinganishe Zitto na Shibuda.
 
Kilichotokea SI KITU CHA AIBU WALA AJABU.... zitto na lema wote wana mapenzi mema na chama na wako passionate na wanachofanya, hizo ndio growing pains zenyewe

NAPONGEZA SANA KUENGULIWA KWA SHIBUDA KWANI YULE BWANA PAMOJA NA KWAMBA ANAFANYA KAZI NZURI SANA, HE IS NOT A TEAM PLAYER

NAKUMBUKA KUNA WAKATI WANACCM WALIOKUA WANASAFIRI KWA TRENI WALIMPA KISAGO NA KUMSHUSHA KWENYE TRENI

SHIBUDA IS SELF CENTRED PERSON
 
TAARIFA HII SIO YAKWELI, IPO KICHONGANISHI, haya mambo sio rasmi, tuweni makini. Jf itakuwa sasa kibanda cha kahawa!

OK sasa tuambie nini kilijiri haiwezekani jamaaa kaanza tu na waliochangia wengi katika hii thread inaonekana wanaafiki kwamba kuna kitu kilitokea. Sasa wewe inaonekana unao ukweli. WEKA MAMBO HADHARANI la sivyo sipendi unafiki na ndo maana siasa na mie kama maji na mafuta.
 
ni kweli tunaweza kusema huu ni ukweli na lazima tujulishwe, na watu mnachukulia kwa upande huo ya kwamba hii ni habari muhimu na ya ukweli,

ila mimi nimechimba mbali zaidi ya ukweli wa hii habari, ya kwamba kama hii habri ni ya kweli , then kazi bado ni ngumu
maana mtoa habari anasema kulikua na kutaka kushikana mashati na hiyo ndilo tatizo na wala hiyo sio democrasia kama tunavyotaka kuipachika hapo,
huo ni utoto na kutokoma kima hekima kama ili tatizo lipo ni bora likatafutiwa suruhisho kuliko kuzuga wakati kuna siku hawa watu wanaweza kuwa mawazari au viongozi kitaifa na kushikana mashati,

si hivyo tu umma wa watanzania siodhani kama wako tayari kutuona tukikunjana mashati wenyewe kisha wao kutupigia kura. sio kwamba natoa hukumu, muda ni sasa wa kutafuta suhuhisho na kuwafunza viongozi wetu jinsi ya kutoa hoja, nasio kutumia maneno ya maudhi kwa kisingizio cha kutomung'unya au kusema ukweli, kuna njia bora za kusema ukweli mgumu na watu wakaelewa, bila kuvuruga wengine, HESHIMA NI KITU MUHIMU SANA hata kwa

waliokosea, na nchi zote zinafanya hivyo, hatuko vitani hapa LEMA ashushi MUKALI kidogo na tuhache ushabiki tutaua chama, kama ZITTO ni tatizo basi zitafutwe njia za kumsaidia, tena unaweza kukuta kafanya kosa la kibinadamu tu na hayo ni mambo ya kawaida katika uongozi, kama CHADEMA tutaanza kutafunana kwa visingizo vyovyote basi hii inatia walakini tukizingatia sasa watanzania ni waelewa na wanapima kwa makini je, kuna ubora wote wote wa kuiondoa CCM madarakani au ni bora wao hawa CHADEMA wana jaziba,

jamani tunatakiwa kuishi kwenye ulimwengu halisi na sio hapa JF tu moja ya mashaka watanzania waliyonaju juu ya chadema ni udini, ukabila, vurugu/ ghasia has huyo LEMA
mbona dr slaa au mbowe. mnyika au wengine hatujasikia wakitaka kushikana na ZITTO mashati hata kama anaoneka ni tatizo? mnyonge mnyongeni haki yake mpen
i


wanaJF

kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) iliyokutana tarehe 30/4/2011 imeamua kumtoa shibuda kwenye nafasi ya kukaimu nafasi ya uenyekiti wa mkoa wa shinyanga, lakini kwnye kikao hicho nusura zichapwe kati ya lema na zitto baada ya lema, kumjia juu zitto ya kuwa mambo yote hayo ya shibuda kayasababisha yeye pale shinyanga kwa kuwaambia baraza la uongozi la mkoa kumteua shibuda kuwa kaimu mwenyekiti wakati katiba ya chama inasema kaimu mwenyekiti anapaswa kutokana na baraza la uongozi la mkoa,

huku shibuda akiwa si mjumbe wa baraza hilo, ndipo aliposimama zitto na kupinga kauli hizo ndipo wabunge na wajumbe wa kamati kuu walipo kuja juu na kumkumbusha zitto juu ya shibuda ya kuwa aliwatukana wabunge na akaambiwa aombe radhi akakataa na mpaka sasa hajaomba kwanini zitto unamtetea huyu jamaa, aliuza mjumbe huyo ambaye ni swahiba wa zitto bwana Msafiri mtemelwa

ili balaa gani kati ya zito na lema,
duh mbona mapema au mkuu umechakachua hii kitu,
kuna haja ya kuwa makini na kutumia busara, kama haya yanatokea
chama kiko hatarini na hekima ya wazee inatakiwa kukinusuru chama,
na kanuni za chama zinatakiwa kufuatwa, ili zinapokosewa kuna haja ya kuongea kwa kuheshimiana
ila hii habari yako ninaifanyia uchunguzi kama ina ukweli,

HEKO WAHESHIMIWA ZITTO NA LEMA KWA UKOMAVU WENU KIDEMOKRASIA:
HATA SIKU MOJA WALA MSIOGOPE KUKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA KATIKA HOJA BILA CHUKI WALA MIZENGWE


Waheshimiwa Zitto, Lema na kamati kuu zima, napenda niwapongeze tena saaana kwa jinsi mnavyohakikisha kwamba NEMBO YETU YA 'DEMOKRASIA' kweli inafanya kazi kiukweli ndani ya chama katika vyombo vyetu vyote vya maamuzi.

Huo ndio ukomavu wa kidemokrasia, uwazi wa kuendesha mambo kuonyesha utayari wa CDM kuongoza taifa bila kwepo TABAKA LA WATEULE ndani ya chama ambao kauli zao hazipingwi. Nawapongeza pia kukataa kubariki maamuzi ya barabarani katika kuteuana ukaimu mwenyekiti huko Shinyanga. Mhe Shibuda sasa ajindae tu kuingia kwenye kinyang'anyiro katika kukijenga chama huku kwa ushirikiano zaidi.

Ndio demokrasia ndani ya vyama inapokomaa na baada ya hapo wote wawili kuendelea kusalimiana na kuendeleza harakati za kufanya kazi kwa pamoja zaidi kutetea maslahi ya umma wa Tanzania.

Nasema ni ndani ya CHADEMA tu ndimo kulimo kiwango hicho cha juu cha demokrasia na misingi ya maadili ya vipi kushika uongozi KWA KUZINGATIA ITIKADI YETU YA 'NGUVU NA MAMLAKA YA UMMA' katika kila tulitendalo na maamuzi tunayoingia.

Mwisho, chama bila mikiki mikiki ya ndani lakini kwa misingi ya disciplined democratic space exercising tayari ni marehemu mtarajiwa kama kilivyo CCM ambako tofauti tu ya maoni kesho yake mtu anakolimbwa kwa kile anachokiamini.
 
Zitto naye kazidi undumilakuwili. Inabidi ifike mahali zitto ajulikane kama yuko kushoto au kulia kwani kwa sasa tunamwona kotekote yaani ccm na chadema
 
Haya mambo yanayo ongelewa yawe ya ukweli au uongo ukweli utabaki palepale kwamba"ZITTO ANAIIMBA CHADEMA LAKINI MOYO WAKE UPO MBALI NA CHADEMA".nasema hivyo kwa sababu hakuna mgogoro wowote ninaoukumbuka ambao ulitokea cdm zitto asihusishwe.kila baya chadema zitto yupo.na hii hali itaendelea hivi hadi atakapojiengua mwenyewe CDM.zitto hana msaada wowote chadema zaidi ya kuleta migogoro.kadili siku zinavyoenda umaalufu wa cdm unapungua kigoma.je ni kwanini?
Si kwamba Zitto moyo wake hauko CDM hapana ila ana asili ya kujiona yeye na mawazo yake ni bora zaidi kuliko ya wengine, naelewa si vibaya kutofautiana kimawazo lakini kama wewe ni kiongozi wa chama cha watu consensus ikifikiwa (majority) ni busara kukubaliana na kuheshimu maamuzi ya wengi, yeye hilo hana atalazimisha wazo lake hata kwa ku-lobby watu wengine alimradi afanikishe anachokitaka hata kama anaona wazi litaharibu image ya chama au mahusiano yake na wengine kwa kisingizio cha free opinion. Matokeo yake anaonekana mbinafsi na asiyejali matokeo yeyote kwa chama.
 
Zitto anatakiwa amshukuru lema kwa kumweleza wazi tena kwenye kikao halali cha chama. Kuna watu kadhaa kwenye hiyo kamati wanamchukia zitto lakini wanamchekea kisha wanamshambulia kupitia JF kwa majina bandia.

Better an enemy who attacks you than a friend who flatters you. Kumbukeni alivyotoswa Bagamoyo na rafiki zake hadi akalazwa agha khan.

Lakini zitto amekua sasa, aache siasa za kuchakachua kanuni ili kupitisha maswahiba kwa ajili ya kujiimarisha ndani ya taasisi. Aache mambo aliyoyafanya DARUSO, amekua sasa.
 
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.

Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.

Kwa hapa nafikiri umepotoka tena sana sina budi kuoji uelewa wako kuhusu VISION. For your information kiongozi wa kweli lazima awe na VISION lakini vision pekee haitoshi isipokuwa inatakiwa iwe SHARED VISION ni kimaanisha kwamba ni jukumu la kiongozi kuwa eleza wafuasi wake juu ya hiyo vision na kuhakikisha ana wamobilize wakubaliane na hiyo vision yake. In fact shared vision utoka kwa watu wenyewe na ndipo uwa passion ya kuitetea na hatimaye siku moja wafike kule wanakotaka kwenda. Sasa huyo zitto ana vision gani?

Zaidi ya kutaka kuwa raisi wa Tanzania 2030? Basi aweke wazi na sio kutupandikizia mamluki na kuwa agent wa CCM!!! LEMA fanya kazi baba sie hatuangaliii huyu jamaa amekaa muda gani na amekifanyia nini chama kama amepotoka lazima aelezwe ukweli. Chadema tunataka iendelee kuwepo na si kwa kumtegemea mtu fulani.

We need to have a very good system ambayo ndo itakuwa muongozo wetu kufika kule tunapo taka kwenda!!!!
 
Back
Top Bottom