Shibuda kufukuzwa CHADEMA

Bwana Joseph Kulangwa, watanzania mamia kwa mamia wanakufa kila siku kwa ajili ya uzembe na mizaha ya wanasiasa kama hii. Kina Shibuda, John Cheyo n.k hawa ni sawa na mashetani kwani kila jambo kwao ni mzaha na utani wakati watu wanakufa. Hutawasikia hata siku moja wakiukemea uovu unaoangamiza wananchi kikweli kweli bali kwao kila jambo ni mzaha na utani. Demokrasia sio uhuru wa kufanya mizaha na utani. Hatuwezi kuwa na nchi ambayo kila kukicha watu wanakimbilia kutangaza tamaa zao za kuwa marais huku wananchi wanakufa kwa vifo vinavyoweza kuzuilika. Halafu huo uongo wako unaotaka kuwalisha watu ''eti watu wakijitokeza mapema kutangaza nia ya kugombea uongozi ndio tunapata nafasi ya kuwapima vizuri'' mimi naukataa. Kwani wakitangaza nia kipindi cha uchaguzi watu watashindwa kurudisha kumbukumbu nyuma na kupima waliyokwisha fanya?
 
Tume ya nini jamani huyu mtu tumechoka naye. kazi yake kuvuruga chama. avuliwe magwanda aende kwa hao magamba nadhani ndo stahili yake.
 
chama cha demokrasia na maendeleo (chadema) kimesema kuwa kitaunda kamati maalum ya kushughulikia tuhuma dhidi ya mbunge wa maswa mashariki, john shibuda (chadema), ambapo akipatikana na hatia atakabiliwa na adhabu nzito ikiwemo kuvuliwa uanachama.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya chama hicho na kuthibitishwa na mmoja wa maafisa wake waandamizi, zimesema kuwa kamati hiyo inayotarajiwa kukutana wakati wowote kuanzia sasa inaongozwa na mjumbe wa kamati kuu, prof. Abadallah safari.
Imedaiwa kuwa kamati hiyo maalumu itamhoji shibuda kabla ya kutoa mapendekezo yake katika kikao cha baraza kuu ambapo kuna habari kuwa litachukua uamuzi mzito na mgumu dhidi ya mbunge huyo, ingawa imedaiwa kuwa naye atakuwa na haki ya kukata rufaa.
Hii itakuwa mara ya pili kwa kamati hiyo kumjadili shibuda kutokana na kupingana mara kadhaa na msimamo wa chadema katika masuala ya msingi ya sera na itikadi, likiwemo suala la nidhamu.
Hivi karibuni, akiwa mjini dodoma, shibuda alikiuka utaratibu wa chama chake na kukidhalilisha hadharani mbele ya wajumbe wa halmashauri kuu ya ccm waliokuwa katika semina, akidai kuwa hajaona chama kinachoweza kuongoza nchi zaidi ya chama tawala.
Akizungumza na tanzania daima, mwenyekiti wa chadema mkoa wa arusha na mjumbe wa baraza kuu, samson mwigamba, alisema kuwa kitendo alichokifanya shibuda hakikubaliki kwa mujibu wa katiba yao, ingawa anaweza kudai ni haki yake ya kikatiba.
Mwigamba alisema katiba inamtaka kila mwanachama wao kukipigania, kukitetea na kukieneza chama chao kwa lengo la kushika dola.
Hivyo kitendo cha shibuda kudai kwamba mpaka sasa hajaona chama kinachoweza kushika dola, ni kukiuka katiba jambo ambalo linaweza kumfukuzisha moja kwa moja uanachama.

Source:tanzania daima
mimi naona cdm wampuuze; maanake amefanya makusudi; ni kosa la wazi kabisa; tuokoe fedha za walala hoi kwa kutofanya uchaguzi mwingine. Kuvumiliana ndio ukomavu wa kisiasa
 
Bwana Joseph Kulangwa, watanzania mamia kwa mamia wanakufa kila siku kwa ajili ya uzembe na mizaha ya wanasiasa kama hii. Kina Shibuda, John Cheyo n.k hawa ni sawa na mashetani kwani kila jambo kwao ni mzaha na utani wakati watu wanakufa. Hutawasikia hata siku moja wakiukemea uovu unaoangamiza wananchi kikweli kweli bali kwao kila jambo ni mzaha na utani. Demokrasia sio uhuru wa kufanya mizaha na utani. Hatuwezi kuwa na nchi ambayo kila kukicha watu wanakimbilia kutangaza tamaa zao za kuwa marais huku wananchi wanakufa kwa vifo vinavyoweza kuzuilika. Halafu huo uongo wako unaotaka kuwalisha watu ''eti watu wakijitokeza mapema kutangaza nia ya kugombea uongozi ndio tunapata nafasi ya kuwapima vizuri'' mimi naukataa. Kwani wakitangaza nia kipindi cha uchaguzi watu watashindwa kurudisha kumbukumbu nyuma na kupima waliyokwisha fanya?
Naye ni gamba.
 
Tatizo amedhihilisha anaamini CCM na alikuja Chadema ili kupata ubunge tu lkn hana imani na CDM,
Hili ni kosa lake kubwa.

Ni mnafiki na mbinafsi sana huyu mzee!

Hafai kabisa
 
Huyo akija kuwa kiongozi wa ngazi ya juu kama rais, hatakuwa na tofauti na viongozi waliopo sasa madarakani. Hatutakuwa na mabadiriko yoyote, zaidi ya kujiongezea mali zake tu.
 
Maoni yangu ni kwamba msimfukuze kwani mkimfukuza ataenda mahakamani matakeo yake majaji wa magamba watamlinda mpaka 2015 kwani wanamtumia huyu mshe ..nzi nyie mpotezeeni aanze choko choko nyie pigeni kazi. Anataka kuwapotezea muda ili muache mambo maana mufuate upuuzi wake.
 
Wadau,
Hili andiko la bwana joseph limeenda skuli sana hebu tulipitie bila jazba.


MBUNGE wa Maswa Mashariki na mwanachama asiye wa siku nyingi wa Chadema, John Shibuda, amejikuta katika mtafaruku na ‘wenye chama chao', kwa linaloitwa kosa la kutangaza kuwania urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho mwaka 2015.

Kinachowauma Chadema kupitia Baraza lake la Vijana (Bavicha) chini ya Mwenyekiti John Heche, ni kwanza kujitangaza kwa Shibuda mapema, pili kujinasibu kwamba atamwomba
Rais Jakaya Kikwete awe Meneja wake wa kampeni, lakini tatu mahali alikotangazia.

Bavicha wanalalamika Shibuda kutangaza azma yake hiyo katika semina ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Dodoma, lakini wanaloliona baya zaidi ni aliposema kwamba hakuna chama cha upinzani chenye uwezo wa kuongoza Dola kama CCM.

Hapo ndipo wanapotamka wazi, kuwa kama anaona hakuna chama cha upinzani chenye uwezo wa kuongoza Dola huku kila chama kikiwania kushika Dola, basi na aende katika chama anachoona kina uwezo huo, ambacho kwa mujibu wa Shibuda ni CCM.

Chadema wana haki ya kujibu pigo hilo la Shibuda, hasa pale ilipoona kama inabezwa kuwa si
miongoni mwa vyama vyenye uwezo wa kushika Dola, huku kikijinasibu kuwa ndicho kinachoelewa matatizo ya wananchi na kimbilio lao, lakini pia mpaka kikaonya dhidi ya
wanaotaka kukizuia kushika Dola mwaka 2015.

Pande hizi mbili za mgogoro huu zina haki ya kimsingi, kwamba Shibuda ana haki zote za kutangaza azma yake kama Mtanzania huru lakini mwanachama wa chama kinachojinasibu kujenga demokrasia na maendeleo kwa mujibu wa jina lake.

Lakini Chadema nayo ina haki ya msingi ya kujitetea, ili isidharauliwe wala kutibuliwa mipango yake ya kutwaa madaraka na kumsimamisha mgombea inayemtaka, ingawa hata
alichokifanya Shibuda kinaweza kuirahisishia kupata mgombea wake.

Ila kilichofanywa na Bavicha kumshambulia Shibuda, kinaonesha wazi kuwa demokrasia ndani ya Chadema ni ya hatihati, na huenda kuna wateule wachache ndani ya chama hicho wanaojua nani atagombea muda ukifika – ni kinyume cha Demokrasia.

Tumeshuhudia Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ambaye ni mwanachama wa siku nyingi, Kabwe
Zitto, akisakamwa ndani ya Chadema pale alipotangaza kwamba urais anautaka na muda mwafaka ukifika atagombea.

Tulipata kushuhudia alivyosakamwa Zitto alipotaka kugombea uenyekiti wa Chadema dhidi
ya Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe; lakini ilikuwa vivyo hivyo kwa marehemu Chacha Wangwe, alipoonesha nia ya kugombea pia nafasi hiyo huko nyuma.

Chadema inataka kutwambia nini sisi ambao tulidhani kweli inajenga demokrasia sawa na jina lake? Inataka kutueleza kuwa ni ya wateule wachache na ndiyo wenye haki ya kugombea uongozi wa juu wa Taifa hili? Kwa nini iwe nongwa kwa wengine kujitangaza?

Mimi nadhani Shibuda hajakosea kiasi hicho kama ambavyo Bavicha inataka kuufahamisha umma, yeye alionesha nia na kuitangaza, ambalo si kosa katika Katiba ya chama chochote
achilia mbali ya nchi.

Kutangazia mbele ya wajumbe wa NEC ya CCM nalo si tatizo, kwa sababu Shibuda hakwenda pale kama mwanachama wa CCM, bali mjumbe wa Mpango wa Kujitathmini Kiutawala Bora Afrika (APRM) ambao ndio ulikuwa umeandaa semina ile kwa wajumbe wa NEC.

Shibuda kumwomba Rais Kikwete awe Meneja wake wa Uchaguzi nayo ni hiari yake kwa sababu kwanza ni mtani wake, lakini pia wakati huo Kikwete atakuwa amemaliza muda wake wa uongozi na kubaki kuwa Rais mstaafu, ambaye yawezekana kabisa hatakuwa na kikwazo.

Badala ya Chadema kumlalamikia Shibuda kwa uamuzi wake huo alioutangaza uwe mzaha, utani au uliodhamiriwa kwa dhati ya moyo wake, ungemtumia kujitangaza na kujenga uhusiano chanya na vyama vingine vya siasa vinavyoamini katika ujenzi wa demokrasia nchini.

Lakini pia kinapaswa kuwapa uhuru wanachama wao kutangaza azma zao mapema na hivyo kupata fursa ya kuona ni nani pumba na nani mchele, badala ya kubana fikra za wanachama katika kutoa hisia zao.

Chadema mlimpokea Shibuda kwa nderemo, vifijo na vigelegele alipohama CCM mkamsaidia mpaka akapata ubunge, iweje anapotaka urais mnaanza kumletea mikingamo na mizengwe na kuamini kuwa si afaaye?


SOSI: HabariLeo | Lipi kosa la Shibuda katika medani hii?

Msaidieni badala ya kumkatisha tamaa.

excellent...huu ndio ukweli

imefikia muda mtoto wa shule ya msingi akisema anataka awe rais kwa tiketi ya chadema, bavicha watakuja juu!!
 
Wadau,
Hili andiko la bwana joseph limeenda skuli sana hebu tulipitie bila jazba.


MBUNGE wa Maswa Mashariki na mwanachama asiye wa siku nyingi wa Chadema, John Shibuda, amejikuta katika mtafaruku na ‘wenye chama chao’, kwa linaloitwa kosa la kutangaza kuwania urais wa Tanzania kwa tiketi ya chama hicho mwaka 2015.

Kinachowauma Chadema kupitia Baraza lake la Vijana (Bavicha) chini ya Mwenyekiti John Heche, ni kwanza kujitangaza kwa Shibuda mapema, pili kujinasibu kwamba atamwomba
Rais Jakaya Kikwete awe Meneja wake wa kampeni, lakini tatu mahali alikotangazia.

Bavicha wanalalamika Shibuda kutangaza azma yake hiyo katika semina ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Dodoma, lakini wanaloliona baya zaidi ni aliposema kwamba hakuna chama cha upinzani chenye uwezo wa kuongoza Dola kama CCM.

Hapo ndipo wanapotamka wazi, kuwa kama anaona hakuna chama cha upinzani chenye uwezo wa kuongoza Dola huku kila chama kikiwania kushika Dola, basi na aende katika chama anachoona kina uwezo huo, ambacho kwa mujibu wa Shibuda ni CCM.

Chadema wana haki ya kujibu pigo hilo la Shibuda, hasa pale ilipoona kama inabezwa kuwa si
miongoni mwa vyama vyenye uwezo wa kushika Dola, huku kikijinasibu kuwa ndicho kinachoelewa matatizo ya wananchi na kimbilio lao, lakini pia mpaka kikaonya dhidi ya
wanaotaka kukizuia kushika Dola mwaka 2015.

Pande hizi mbili za mgogoro huu zina haki ya kimsingi, kwamba Shibuda ana haki zote za kutangaza azma yake kama Mtanzania huru lakini mwanachama wa chama kinachojinasibu kujenga demokrasia na maendeleo kwa mujibu wa jina lake.

Lakini Chadema nayo ina haki ya msingi ya kujitetea, ili isidharauliwe wala kutibuliwa mipango yake ya kutwaa madaraka na kumsimamisha mgombea inayemtaka, ingawa hata
alichokifanya Shibuda kinaweza kuirahisishia kupata mgombea wake.

Ila kilichofanywa na Bavicha kumshambulia Shibuda, kinaonesha wazi kuwa demokrasia ndani ya Chadema ni ya hatihati, na huenda kuna wateule wachache ndani ya chama hicho wanaojua nani atagombea muda ukifika – ni kinyume cha Demokrasia.

Tumeshuhudia Mbunge wa Kigoma Kaskazini, ambaye ni mwanachama wa siku nyingi, Kabwe
Zitto, akisakamwa ndani ya Chadema pale alipotangaza kwamba urais anautaka na muda mwafaka ukifika atagombea.

Tulipata kushuhudia alivyosakamwa Zitto alipotaka kugombea uenyekiti wa Chadema dhidi
ya Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe; lakini ilikuwa vivyo hivyo kwa marehemu Chacha Wangwe, alipoonesha nia ya kugombea pia nafasi hiyo huko nyuma.

Chadema inataka kutwambia nini sisi ambao tulidhani kweli inajenga demokrasia sawa na jina lake? Inataka kutueleza kuwa ni ya wateule wachache na ndiyo wenye haki ya kugombea uongozi wa juu wa Taifa hili? Kwa nini iwe nongwa kwa wengine kujitangaza?

Mimi nadhani Shibuda hajakosea kiasi hicho kama ambavyo Bavicha inataka kuufahamisha umma, yeye alionesha nia na kuitangaza, ambalo si kosa katika Katiba ya chama chochote
achilia mbali ya nchi.

Kutangazia mbele ya wajumbe wa NEC ya CCM nalo si tatizo, kwa sababu Shibuda hakwenda pale kama mwanachama wa CCM, bali mjumbe wa Mpango wa Kujitathmini Kiutawala Bora Afrika (APRM) ambao ndio ulikuwa umeandaa semina ile kwa wajumbe wa NEC.

Shibuda kumwomba Rais Kikwete awe Meneja wake wa Uchaguzi nayo ni hiari yake kwa sababu kwanza ni mtani wake, lakini pia wakati huo Kikwete atakuwa amemaliza muda wake wa uongozi na kubaki kuwa Rais mstaafu, ambaye yawezekana kabisa hatakuwa na kikwazo.

Badala ya Chadema kumlalamikia Shibuda kwa uamuzi wake huo alioutangaza uwe mzaha, utani au uliodhamiriwa kwa dhati ya moyo wake, ungemtumia kujitangaza na kujenga uhusiano chanya na vyama vingine vya siasa vinavyoamini katika ujenzi wa demokrasia nchini.

Lakini pia kinapaswa kuwapa uhuru wanachama wao kutangaza azma zao mapema na hivyo kupata fursa ya kuona ni nani pumba na nani mchele, badala ya kubana fikra za wanachama katika kutoa hisia zao.

Chadema mlimpokea Shibuda kwa nderemo, vifijo na vigelegele alipohama CCM mkamsaidia mpaka akapata ubunge, iweje anapotaka urais mnaanza kumletea mikingamo na mizengwe na kuamini kuwa si afaaye?


SOSI: HabariLeo | Lipi kosa la Shibuda katika medani hii?

Msaidieni badala ya kumkatisha tamaa.

Alichokifanya Shibuda ni mzaha usioweza kuvumilika, alienda NEC ya CCM kufanya nini, na kwa nini alipewa audience na kusema yale aliyosema, kumbuka tunataka kujenga upinzani usio na mzaha, kitendo cha kuidhalilisha CDM kama hiki hakiwezi kuvumiliwa na wapenda mageuzi.Kumkemea Shibuda si kukosa demokrasia ila hata hiyo demokrasia inahitaji utaratibu. ingekuwaje kama kusingekuwa na tume ya uchaguzi na taratibu za kujaza fomu za kugombea halafu uitishwe uchaguzi hiyo haitakuwa demokrasia ila fujo.
 
Ni heri afukuzwe sasa hivi ili uchaguzi ufanyike mapema hatimae Jimbo akabidhiwe mtu anaeheshimu Chama. Tukifanya hivi itasaidia kumkomoa yeye mwenyewe kwani hatakuwa na pa kwenda. CCM hawawezi kumpokea kwani alishanyea kambi. UDP kule ilishakufa imebaki kwa Cheyo tu.

Tukisubiri hadi 2015 tunaweza kumfaidisha maana ataibuka kama Mgombea Mbinafsi (Kama Katiba Mpya itaruhusu) na hivyo itakuwa ngumu kumshinda. This is best time.

TUMBIRI wa JF.
 
Ni heri afukuzwe sasa hivi ili uchaguzi ufanyike mapema hatimae Jimbo akabidhiwe mtu anaeheshimu Chama. Tukifanya hivi itasaidia kumkomoa yeye mwenyewe kwani hatakuwa na pa kwenda. CCM hawawezi kumpokea kwani alishanyea kambi. UDP kule ilishakufa imebaki kwa Cheyo tu.

Tukisubiri hadi 2015 tunaweza kumfaidisha maana ataibuka kama Mgombea Mbinafsi (Kama Katiba Mpya itaruhusu) na hivyo itakuwa ngumu kumshinda. This is best time.

TUMBIRI wa JF.

Mkuu TUMBILI, yaani kumbe uoga wako ni jamaa kugombea kama mgombea binafsi? Rumbili unaogopa kimvuli eeh?
 
Huyu mchambuzi wa habari lazima anaumwa, anaumwa ugonjwa wa uccm vinginevyo asingeweza kuandika vitu shallow kiasi hiki halafu auite uchambuzi. Ni wazi kuwa Shubuda haamini kuwa chama anachokiwalisha kina uwezo wa kushika dola na hapa ndo kuna tatizo na kwngine koote kule. Hivi katika akili ya kawaida unaweza kuwa kwenye chama kisichokuwa na uwezo wa uongozi?? kwa maneno mengine Shibuda hana uwezo wa uongozi kwa sababu yeye ni sehemu ya wapinzani wasio na uwezo wa kuongoza dola.
 
Shibuda ni kansa ndani ya CDM tusipompopoa mapema atatusumbua... bora tumtoe mapema na hii nusu shari aliyoileta kuliko kusubiri mpaka alete shari kamili. ashaonyesha mapema kuwa anazeeka vibaya bora tumpumzishe mapema kwa amani.
 
CHADEMA mnatakiwa muheshimu demokrasia. CCM ambacho mnakilaumu kina demokrasia pana kulikoni nyny

sabodo kada wake mkuu anasaidia CHAMA CHENU NA PIA ANASEMA ANATAKA MABADILIKO NA CCM HAKIJAMFUKUZA. sasa iweje nyny mnajidai mnaheshimu demokrasia mnakuwa wa mwanzo kuikunja demokrasia .

hivi ingekuwa sabodo ni Chadema na anawasaidia CCM ingekuwaje ?
 
jamani siku nzote mimi hujivunia wabunge wa CDM, kwa kweli wako makini kama Chama chenyewe, lakini nashindwa kujua hivi huyu ZUZU shibuda MLIMLOKOTA wapi? naomba mumrudishe katika HILO JALALA mlilomtoa, huyu yupo kuturudisha nyuma tu, hapendi speed tunayoenda nayo, yaani nashindwa nimfananishe na kitu gani mtu mzima ovyo tu, kwa hili CHADEMA tumetoa uchafu JALALANI tukamweka mahali pasafi, sasa harufu ya uchafu imeanza kutunukia ndani, harufu nzito ya mzoga, dawa si kuongea kwamba huu ni uchafu,ila tunachotakiwa kufanya ni kuutupa uchafu. hatufai hata kidogo ZEZETA huyo.
 
HALI ya mambo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), si shwari, baada ya Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda (pichani), kuwatolea uvivu viongozi wa juu wa chama hicho, akisema hatishiki na vitisho vinavyofanywa na viongozi hao.Alisema kutokana na hali hiyo, yuko tayari kufukuzwa katika chama kwa kosa la kusema ukweli siku zote.-Hivi karibuni, Shibuda amedaiwa kwenda kinyume cha msimamo wa chama chake, kuhusiana na suala la posho za wabunge, kitendo ambacho kimemfanya aonekane muasi ndani ya chama na hivyo kuundiwa tume ya kumchunguza.-
Akizungumza na MTANZANIA Jumapili mjini Dodoma jana, Shibuda alibeza shutuma hizo zilizoelekezwa kwake na kuwataka viongozi wa juu wa chama hicho kumwomba radhi kutokana na kumchafua.-Shibuda aliwataja viongozi hao ambao alidai wanamchafua kupitia vyombo vya habari kuwa ni Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto.-Hata hivyo Shibuda alisema mbali ya kuombwa radhi, pia atalazimika kuandaa mikutano ya hadhara yenye lengo la kuwaeleza wananchi tabia za viongozi hao.-“Natarajia kusafiri kwenda nje ya nchi kwa shughuli za kibunge, nitakaporudi, nitaitisha mikutano ya hadhara katika maeneo mbalimbali nchini kuwaeleza wananchi juu ya Zitto na Mbowe, ambao tayari wameshanishutumu kupitia vyombo vya habari.-“Mikutano hiyo nitaianzia jimboni kwangu mwishoni mwa mwezi huu, nitaweka wazi kila kitu kwa sababu wananchi ndio wenye chama na wana haki ya kujua nani anasema ukweli na nani anasema uongo.-“Hata hivyo, kabla mimi sijaenda kwa wananchi nawaruhusu wao waende kwa wananchi wakanishitaki, wakaeleze ubaya wangu ili mimi nitakapowaeleza wananchi basi wao ndio wapime wenyewe.-“Mimi nayajua mengi sana ya CHADEMA, kwa muda mfupi niliokaa katika chama hicho nimejionea mengi sana na nalazimika kusema kuwa alichokuwa akikisema Chacha Wangwe (marehemu) ni sawa kabisa na hakukosea kitu.-“Nakwambia sura ya CHADEMA ukiwa nje ya chama ni tofauti na sura ya CHADEMA ya ndani, ni tofauti kabisa kwa sababu yanayofanyika humo ni mambo ya ajabu sana.-“Mbowe anaendesha chama kibabe na anaungwa mkono na Zitto ambaye anaonekana kuwa na tabia ya ukuwadi na unafiki.
 
Leo hii Shibuda huyu huyu anakwenda kwenye chama cha zitto, ACT. Kuna chama hapo...au kuna Usanii?
 
Back
Top Bottom