Shibuda kufukuzwa CHADEMA

Huyu ni VUVUZELA tu asitupe shida maana taifa zima linajua kuwa huyu ni gamba tu kama magamba mengine.

Tusipoteze fedha za chama kumjadili shibuda hana chochote ndani ya jamii yetu achana nae
 
MBOWE, SLAA, ZITTO, Chonde chonde jamani, tuhurumieni wanachama wenza wenu, tafadhalini sana! Tunawaomba nyie na uongozi mzima wa CDM tuondoleeni hicho KIRUSI KIITWACHO JOHN SHIBUDA. Kama ni jimbo potezeeni, anatutia kichefu chefu sana pimbi huyu.
 
Mimi pia naona Shibuda ni wa kumzarau tu, yeye bado anafikiri watz wote bado wapo gizani na yeye yupo kwenye kundi la wajanja, kumbe amepitwa na wakati, Viongozi wa chama wasirumbane na mtu kama huyu kuna mambo ya muhimu zaidi ya kufanya kuliko kujibishana na Shibuda. na kama itabidi wasisite kumvua uanachama sisi wenye nchi tutauelewa uongozi hata kama Vuvuzela zikipulizwa to pande za magamba au hata yeye mwenyewe.
 
Sioni sababu ya CDM kulumbana na huyu jamaa because he is politically dead. Hana influence yeyote kwenye jamii hata katika jimbo lake la Maswa. Wamwache tu abwabwaje, baadae wanaMaswa watamwonyesha njia ya kutokea 2015. Endapo CDM wakianzisha malumbano yeyote na Shibuda kwa sasa, sanasana watampaisha katika vyombo vya habari, na anaweza kujenga influence. Wamwache tu maana hata CCM wanajua yule kwa ni insane...

Sema yote kuhusu Shibuda lakini usimnyang'anye haki yake ya kuwa na influence hko kwao. CDM imebebwa na Shibuda huko Shinyanga na wasipo tumia busara safari ya kuelekea kwa NCCR ya kina Mrema na Marando.
 
huyu jamaa ni mroho wa madaraka mi naona hivyo sababu aliondoka ccm baada ya kukosa kura za kutosha
hana mapenzi ya dhati na cdm ni njaa tu inampa ukichaa huo
maji na mafuta huwa haviivi kwa pamoja ataondoka tuu arudi huko alikozoea nyambaf zake
Mi naona shibda ni kichaa flani hivi,dawa yake ni kumvua gwanda na kumvalisha gamba alilokuwa nalo na kumrudisha kwenye chama cha mafisadi a.k.a magamba
 
CHADEMA CHAMA CHANGU!CHONDECHONDE NA SHIUDA.Huu ni mkakati mahususi wa ccm kupitia kwake,epukeni malumbano na huyu kichaa mwingi wa tamaa za fedha,hana madhara huyo kwa sasa ila mkimgusa watu wengi waliopo kwenye huo mtandao(wanasiasa, wanazuoni, wanasheria,viongozi wastaafu, viongozi wa dini na wanaharakati) watajitokeza kumtetea na kukitukana chama kwa manufaa ya magamba.Nashauri mwacheni atabaki tu kama vuvuzela bila negative impact kubwa kwa chama.
 
CDM kinasonga na Shibuda akiwa ndani ya Nyumba, ondoeni wasiwasi wajameni huyo mtu hana pakushika ndio maana ana tapatapa.
 
Mfukuzeni muone! anamaono ya mbali sana. Hawezi kufungwa na minyororo ya ukabila. Nyinyi watu (hasa vijana) wa Mwanza, Shinyanga, Tabora, Mara na Rukwa, hebu jaribuni kuwa neutral (mawazo huru) mchambue hivi kweli cdm ni chama cha wanyonge wa nchi hii au mnatumiwa na hao wanaotaka kujitenga na kutangaza jamhuri yao. Ole wao wavivu wa kufikiri, watapiginia hata kitakachowaangamiza.

Kristo Yesu alikufa kwa ajili ya yako so ni vyema uumpe leo maisha yako ili akuondolee ukilaza wako wote.
 
Wewe bwana mdogo Negate_r punguza pumba kichwani mwako ili uishi maisha mzuri bila cameroon anakunyemelea.yaan wewe shibuda unamuona anakili sawa?nakushanga sana tena yawezekana wewe ndio ukawa fyatu kuliko hata shibuda
 
Last edited by a moderator:
KATUNI%28701%29.jpg

Shibuda

mamaaaaaaaaaaaaa huyu mzee kapotea njia! kumbe lengo lake kwenda ikuuuuulu!
 
Tusubiri hiyo kamati imuhoji naye apewe nafasi ya kujitetea.Ila kuendelea kubebe mzigo usio na faida/tija ni gharama kuliko kukausha bahari.
 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kuwa kitaunda kamati maalum ya kushughulikia tuhuma dhidi ya Mbunge wa Maswa Mashariki, John Shibuda (CHADEMA), ambapo akipatikana na hatia atakabiliwa na adhabu nzito ikiwemo kuvuliwa uanachama.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya chama hicho na kuthibitishwa na mmoja wa maafisa wake waandamizi, zimesema kuwa kamati hiyo inayotarajiwa kukutana wakati wowote kuanzia sasa inaongozwa na mjumbe wa Kamati Kuu, Prof. Abadallah Safari.
Imedaiwa kuwa kamati hiyo maalumu itamhoji Shibuda kabla ya kutoa mapendekezo yake katika kikao cha baraza kuu ambapo kuna habari kuwa litachukua uamuzi mzito na mgumu dhidi ya mbunge huyo, ingawa imedaiwa kuwa naye atakuwa na haki ya kukata rufaa.
Hii itakuwa mara ya pili kwa kamati hiyo kumjadili Shibuda kutokana na kupingana mara kadhaa na msimamo wa CHADEMA katika masuala ya msingi ya sera na itikadi, likiwemo suala la nidhamu.
Hivi karibuni, akiwa mjini Dodoma, Shibuda alikiuka utaratibu wa chama chake na kukidhalilisha hadharani mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM waliokuwa katika semina, akidai kuwa hajaona chama kinachoweza kuongoza nchi zaidi ya chama tawala.
Akizungumza na Tanzania Daima, mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Arusha na Mjumbe wa Baraza Kuu, Samson Mwigamba, alisema kuwa kitendo alichokifanya Shibuda hakikubaliki kwa mujibu wa katiba yao, ingawa anaweza kudai ni haki yake ya Kikatiba.
Mwigamba alisema katiba inamtaka kila mwanachama wao kukipigania, kukitetea na kukieneza chama chao kwa lengo la kushika dola.
Hivyo kitendo cha Shibuda kudai kwamba mpaka sasa hajaona chama kinachoweza kushika dola, ni kukiuka katiba jambo ambalo linaweza kumfukuzisha moja kwa moja uanachama.

Source:Tanzania Daima

Imekuwaje kazungumza hayo kwenye kikao cha CCM wakati ni mwanachama wa CDM? sielewi, naomba ufafanuzi.
 
Shibuda ni tatizo sana,tena ni hatri kuliko watu wanavyodhani,wakati anatoka CCM ilikuwa ni sababu ya madaraka na akili yake fyongo,na ndio maana hata wakati wa uchaguzi CCM walikaza uzi ili asirudi,walimweka mgombea kijana na rafiki wa Riz 1,ambae kwenye sakata la kampeni ndie aliempiga OCD pale kituo kikuu cha wilaya ya Maswa,kufuatia Shibuda kuachiwa na polisi baada ya kukamatwa kufuatia mauaji ya wapambe wa CCM katika mkutano wa Malampaka.Makamba alikwenda maswa kukazia ile so na hata Riz 1 alikwenda maswa kujaribu kufaikisha ushindi wa Robert Simon Kisena ambae ndio walieshirikiana na Riz kuinunua UDA,hapa najaribu kuwaonyesha kuwa Shibuda hakuondoka CCM kuja kufanya uzandiki CDM ila ni akili yake ya kutoeleweka na kutaka madaraka.
Ila kadri siku zimekuwa zikisonga mbele amegeuka kuwa lulu kwa CCM huku wakimtumia kuvujisha mambo na kuivuruga CDM,na tayari kuna habari kuwa anatumika ipasavyo kuivuruga CDM,na hii inatokana na akili yake pia ya kujipendekeza kwa baba RIZ,na ndio maana anropoka mambo kibao kwa ahadi alopewa kuwa atapokelewa na atapewa support akiwa upande wa magamba for the next elextion.
Ushauri wangu:Shibuda hafai kuendelea kuwa CDM,nigependa atimuliwe fasta,hapa tunalea sumu,tunalea hatari,na hata hivyo hana anachokisaidia CDM,hata kama kuna ruzuku inayopatikana kwenye chama kutokana na yeye kuwa mbunge ni bora kuikosa ruzuku na kulikosa jimbo kuliko kuwa na shibuda,huyo ni sawa na popo,hafai kuwa kwenye siasa za ukombozi wa nchi.LET HIM GO NOW
 
Shibuda Shibuda Shibuda, we shibuda,
Ni nani? Ni mtu wa aina gani? Kwa nini sasa ndiyo aone ni wakati wa kuvuruga CDM?
Kujibu maswali haya, inahitaji kugundua ujanja wa kisiasa, Shibuda ninayemjua mimi ni yule aliyeomba kugombwa urais mwaka fulani huko nyuma, shibuda huyo huyo ni yule aliyepingana na sera za wenzake CCM (MAGAMBA) na akatoq ada ya shs 1,000,000 za fomu?!!!!!!!
Shibuda huyu ni yule, uliyelazimisha kutaka kugombea urais mwaka 2010 hata kama chama chake kilitaka agombee Kikwete bila kupingwa?!!!!,
Shibuda huyu ni yule aliyejibu kwa kejeli alipoambiwa protocal za MAGAMBA hazirusu kugombea na Rais aliye madarakani?
Kilichofuata Huyu jamaa akatoswa kwenye hizo vurugu zake akabaki analalamika.
Akakimbilia kwenye ubunge, kura za maoni zikambwaga kule Maswa.
Kwa hisani za CDM kumuona labda huyu jamaa ni potential CDM wakamumkubalia agombee ubunge kule maswa kweli akashinda ubunge kupitia CDM, Shibuda ni buda kweli, akadhani kuwa ameshinda ubunge kwa sababu ya umaarufu wake, kumbe moto wa CHADEMA kanda ya ziwa ulikuwa juu mno, kwamba yoyote angeweza kushinda hata kama si Shibuda.
Kwa ufupi huyo ndiyo Shibuda, ni msumbufu sana kisiasa, hilo si jambo baya lakini kutafuta umaarufu wa kisiasa kwa njia hiyo kwa kweli si sahihi kabisa.
Mimi kama Mwana CDM nasema kwamba haikubaliki na ni usaliti wa msafiri aliye ndani ya boat ya kasi anayejaribu kuitoboa boat hiyo ili izame akijidanganya kwamba yeye yupo salama kwa vile anawasiliana na muongoza meli aliye nchi kavu. (Nincompoops) INATIA HASIRA NA KUKERA. Ni bora atoswe yeye haraka ili hayo waliomtuma waone kama huo utakuwa mgogoro ndani ya CHADEMA.
Shibuda ni mtu mdogo sana ndani ya CHADEMA, ningejisikia vibaya kama hata angekuwa mtu mwenye mchango mkubwa kwa nchi ama CDM, lakini huyo ni mchumia tumbo tuu,
Inaelekea alidandia boat asiyoijua inakoelekea, si vibaya kumwambia yuko wrong direction hivyo ashuke atafute uelekeo sahihi kwake.
Shibuda ameingia chama ambacho si saizi yake, ni kama maji na mafuta kamwe hayachanganyiki kabisa hata kama ukiyafukia udongoni yatajitenga.
Shibuda si mwana CDM, ila ni mwanaCCM anayetafutia maisha CDM, sasa naona ameshiba kwa hiyo ameamua kunyea kambi. LAANA ya wanamageuzi itamtafuna yeye na vizazi vyake leo, kesho, na hata milele.
Shibuda anatumiwa na CCM, angalia ameanza uppuzi huu baada ya kikao chao cha NEC.NEC ya CCM imeweka strategy zao za mwisho baada ya kuiona hatari inayowakabili, hivyo, wanadhani makuwadi wao waliomio ndani ya CDM watawasaidia.
Wimbi la wanaCCM kuhama is a real threat to CCM, kwa kuwa wananchi wanaikubali sana CDM.
CDM kwa taarifa yako Shibuda si chama laini kinachoweza kudhoofishwa na wewe, ni chama kinachoweka misingi bora sana ya upinzani wa sera na ubora wa utawala.
CDM inao uongozi bora, wananchi tunaelewa hivyo, CDM ina strategy makini na nzuri sana ambazo haziharibiwi hata kidogo na uppuzi wa SHibuda ama kuwadi mwingine yoyote. CDM inao wanachama wanaoelewa kwa nini wao ni wanaCDM ni si kwa kufuata mkumbo ama kulazimishwa kama ilivyo kwa CCM.
Viongozi wangu wa CDM muinangalie kwa mtazamo huo, kwamba hiyo ni dhana ambayo CCM wameipima na kuona labda itapunguza kasi ya uhamaji wa wanachama wao.
Iaminike wazi kwamba wimbi hili la mageuzi ni kama kimbunga ambacho kinakumba miti, viti, mbao, nyumba nakadhalika hakizuwi na shuka la kitandani.
Kwa heri Shibuda kwenye ulingo wa siasa, huwezi kukubalika CDM na hakika hata CCM hutakubalika unatumika kama punda ili mzigo ufike. CHADEMA tulikupenda lakini CCM wamekupenda zaidi, kalale pema JAHANAMU.
 
Back
Top Bottom