Ahsante Mkuu kwa kuongezea!Amesema pia Ukimpeleka mwanamke chongo kwa Membe kwa jinsi alivyo na maneno matamu na ya uongo atakwambia huyo mwali sio chongo! Souce: Shibuda.
Hajataja CHADEMA popote, nimemsikiliza!
Amesema pia Ukimpeleka mwanamke chongo kwa Membe kwa jinsi alivyo na maneno matamu na ya uongo atakwambia huyo mwali sio chongo! Souce: Shibuda.
Kama hajakitaja CHADEMA kila mtu anaweza kutafsiri awezavyo! Kwa mfano naweza kutafsiri kwamba kwa kuwa CCM walipambana naye Maswa hawamwezi tena kwa kuwa anapendwa na Wana-Maswa!Unless kama uliingia kichwani kwa Shibuda huwezi kubishana na mimi!Humuelewi Shibuda ww, Shibuda anawapiga madongo CHADEMA kwa mafumbo, na watu kama nyie hamuwezi kumuelewa hata siku moja
issue siyo siri za chama kumfukuza ubunge siyo rahisi kama unavyo dhani kumbuka CUF walishindwa kumfukuza ubunge mbunge wa Viti maalum toka TANGA alipo sema ataendelea kumtambua rais wa Zenji kwa Sababu yeye yupo bara hivyo siasa za Z'BAR hazimuhusuKichama Shibuda hana nguvu, anaweza kuwekewa mkakati, akafukuzwa uanachama na kupoteza hata ubunge.
Kinachwapa watu maswali hapa ni, Shibuda anathubutu vipi kuwa na kiburi hiki? Je, kashajichukulia siri nzito za CHADEMA kiasi cha kuweza kubwabwaja bila kuogopa huku akijua kwamba inawawia vigumu CHADEMA kumfukuza kwa kuwa wanajua ana siri za uongozi wa juu wa chama?
Aondoshwe tu!!! Kwani walipokuwa wabunge 11 mbona mambo yalienda.!!!Akifananisha chama hicho na utelezi wa mlenda.
Aonya kamati kuu iliyojadili haina ubavu kumtimua.
Atamba wakithubutu hilo wataona cha mtema kuni.
Adai kukataa posho ni sera za chama kilichoshinda.
Adaiwa kukutana na madiwani,Arusha wapanga siri.
Source gazeti la taifa letu:ijumaa julai 22- julai 28
www.ippmedia.com
Unataka Wabunge wa "ndio mzee?" Wanazidi kupungua siku hadi siku!shibuda shibuda
Chadema wanamuogopa Shibuda kwa kuwa wanahofia nyadhifa zao katika chama zilizokaa kikabila na kikanda. Shibuda ni zaidi yao wote kwa siasa, hawamuwezi.
Chadema wanamuogopa Shibuda kwa kuwa wanahofia nyadhifa zao katika chama zilizokaa kikabila na kikanda. Shibuda ni zaidi yao wote kwa siasa, hawamuwezi.
Akifananisha chama hicho na utelezi wa mlenda.
Aonya kamati kuu iliyojadili haina ubavu kumtimua.
Atamba wakithubutu hilo wataona cha mtema kuni.
Adai kukataa posho ni sera za chama kilichoshinda.
Adaiwa kukutana na madiwani,Arusha wapanga siri.
Source gazeti la taifa letu:ijumaa julai 22- julai 28
www.ippmedia.com
Yote2 yawezekana jibu sahihi anaro shibudaKama hajakitaja CHADEMA kila mtu anaweza kutafsiri awezavyo! Kwa mfano naweza kutafsiri kwamba kwa kuwa CCM walipambana naye Maswa hawamwezi tena kwa kuwa anapendwa na Wana-Maswa!Unless kama uliingia kichwani kwa Shibuda huwezi kubishana na mimi!
Kusema ukweli hizi kauli za Shibuda zimekosa adabu. Kwa mpenda maendeleo na anaethamini watu waliomchagua na chama alichotumia kufika Dodoma huwezi kuwakejeli maneno ya dhihaka namna hiyo. Huyu ana agenda ya siri na CCM ya kukibomoa CDM. Lakini madamu tumesha mjua ya kuwa ni mbayumbayu hakuna haja ya kuhangaika nae ila CDM mtafute mbinu ya kumchomoa aondoke. Chadema kinapendwa hatakikiamua kuchukua maamuzi maguni hakita yumba, tena ndio kitajiimarisha zaidi na watu wataendelea kukiamini. Watanzania wana kiu ya maendeleo sio propaganda za hawa walevi wa madaraka wanatusumbua na kodi zetu tunazolipa.huyu jamaa si ni yule aliyetaka kugombea urais against kikwete kupitia ccm kinyume na makubaliano ya chama. Unategemea nini zaidi kama alidiriki kupingana na maamuzi ya chama ndani ya ccm. Atawaharibia kokote atakakoenda