Chadema wawe makini kwani kwa sasa ni mbadala wa CCM, uwezekano wa kuongoza TZ unajionyesha kwa CCM sasa kutekeleza sera zake kwa kuziigiza. Hivyo wawe makini na viongozi mapandikizi au wenye tamaa ya madaraka. Tunawaombea Chadema mje mshinde uchaguzi ili muikomboe TZ.Jana Baraza kuu la CHADEMA Mkoa wa Shinyanga limemtangaza John Magale Shibuda kuwa Kaimu Mwenyekiti wa mkoa wa Shinyanga (Soma majira la leo).Habari hizi zilinishtua kidogo nikawa na maswali machache:
Kweli Shibuda ametubu na kuutii uongozi wa Taifa chini ya Mh Mbowe.??
Je,Shibuda ataacha kutofautiana na viongozi wenzake hasa wabunge??
Si ni Shibuda huyuhuyu aliyekashifu wabunge wa Chadema bungeni??
Si ni Shibuda huyuhuyu aliyesema Mh Wenje hana adabu??
Si ni Shibuda huyu huyu aliyesema Chadema ni mkusanyiko wa wanaharakati wasio wanasiasa??
Je,Shibuda si alileta vurugu kwenye vikao vya wabunge wa Chadema huko Bagamoyo??
Ikumbukwe Shibuda ni mbunge pekee wa jimbo ambaye hakupewa wizara kivuli bungeni.
Nimeeleza yote haya si kwa chuki na Shibuda bali changamoto kwake kwamba alikuwa amepoteza imani na wanachama wengi kwa matendo yake yasiyotabirika na anapaswa kurejesha heshima yake kwa kutii viongozi wa chama na wabunge wa chama chake...