Shibuda ashangiliwa na wabunge wa CCM

JAMANI NI VYEMA TUKAELEWA KUWA CHADEMA SASA NI CHAMA KIKUBWA, SI SAWA NA TLP, NRD, UDP, JAHAZI ASILI, NLD nk. Mnapokuwa ktk chama kikubwa ni lazima mtofautiane ktk mambo mengi mengine ni madogomadogo na mengine ni ya msingi. Mfano CCM ni chama kikubwa na sasa wanatofautiana sana ktk njia ya kutumia kuwashughulikia MAFISADI maana ktk watoa maamuzi MAFISADI pia wamo. Si vyema kusema SHIBUDA Afukuzwe, apewe ONYO au ATENGWE na CHAMA. CDM watakuwa hawajengi bali wanabomoa maana haitapata kutokea DUNIANI wote tukaamini na kuongea lugha moja ktk HOJA itakayokuwa mbele yetu. Hivyo kuvumiliana na kuchukuliana ni jambo la msingi ktk kujenga CHAMA CHA KIDEMOKRASIA kama ilivyo CDM.

Tukumbuke kosa lilishafanywa na VIONGOZI wa CDM kwa kuwapokea wakina PROF. KAHIGI, SHIBUDA, WENJE, NYIMBO na wengine wengi Bila kuwafanyia VETTING kama kweli hawa watu wanaamini ktk Demokrasia na Ideology za CDM au wanajiunga ili wapate nafasi ya Kugombea UBUNGE, najua muda ulikuwa hautoshi kwa VETTING kufanyika hivyo viongozi walikuwa na uamuzi wa aina tatu, moja wawapokee na kuwapitisha kugombea au wawapokee na wasiwapitishe kugombea ubunge au wasiwapokee kabisa. SASA viongozi wa CDM waliona ni BUSARA kuwapokea na kuwapitisha kugombea UBUNGE wapo walioshinda ndio hao wakina KAHIGI,WENJE na SHIBUDA na wapo walioshindwa kama mzee NYIMBO. SASA si sahihi kutumia hasira ktk kushughulikia matatizo yanayosababushwa na wageni hawa ndani ya CDM. Maana Viongozi wa CDM wakati wanafanya uamuzi wa kuwapokea na kuwapitisha wawe wagombea ubunge kupitia CDM iliwapasa watambue kuwa mbeleni kuna matatizo kama haya yanaweza kujitokeza, sasa yamejitokeza dawa si kutimuana dawa ni kuyakabili na kuyatatua kwa busara na mbinu za kisasa za usuluhishi wa mogogoro.

Tukumbuke SHIBUDA na wenzake walisha zoea ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI WA CCM, na siku zote walisha zoea kuwaogopa na kuwatii viongozi wenye nguvu ya kiserikali(dola) na kichama. Viongozi wa CDM hawana nguvu za DOLA hivyo kwa SHIBUDA kuwahofia ni ngimu. Pia tukumbuke SHIBUDA anaungomvi na Mbunge mwenzie wa CDM mh. WENJE na aliwapelekea viongozi wa CDM mgogoro huo wautatue lakini wameupotezea sasa SHIBUDA anaamini yeye anachukuliwa kama mtoto wa kambo CDM. Hivyo kauli nyingine zinatokana na Hasira alizonazo.

PIA wana CDM kumbukeni kauli za SITTA na MWAKYEMBE pia zinawaudhi viongozi wa CCM lakini wanazipotezea na kuandaa mkakati wa kichama kuwashughulikia, (naomba nieleweke sio kwamba nawaunga mkono, bali muelewe kwa wana siasa MASLAHI ( wachumia tumbo) kwao chama kwanza nchi na wananchi baadae) sasa CDM isiingie ktk mtego huo ktk kushughulikia suala la SHIBUDA ni lazima MASLAHI ya TAIFA yawekwe mbele na ya CHAMA yafuate baadae.

Kumbukeni SHIBUDA kwa zaidi ya miaka 40 yeye anaimba wimbo wa CCM hivyo inawezekana hajajijua kuwa sasa yupo CDM na wimbo wa CDM ni peoples power bila kujali nguvu za DOLA za kiongozi. AMINI nawaambia SHIBUDA itafika mahala atabaini CCM si nyumbani tena hivyo hatokuwa na jinsi bali kutii uongozi na chama cha CDM


Asante kwa maelezo yako mazuri na yenye umakini. Hata hivyo nini maelezo yako kuhusu tuhuma hizi za cdm kutokuwa makini? Kuna viongozi wengine wa cdm ambao waliwahi kuwa ccm, kama Slaa, mbona wao hawana tabia za kuogopa vyombo dola kama wakina shibuda na wenzake tofauti yao nini hasa?
 
Huyu ni pandikizi la CCM kule CHADEMA, CHADEMA kama hawakuwa makini anaweza kabisa kukivuruga chama halafu akatangaza kurudi kwenye chama cha mafisadi.

BAK Inawezekana kabisa kuwa Shibuda 2010 alipohama CCM na kuhamia CDM alifanya hivyo kwa utashi wake wa kutaka kuendelea kuwa mbunge. Mambo ambayo yanayonifanya nisiamini kuwa alikuwa pandikizi then ni kitendo cha kuwekwa ndani na katika mauji wakati wa kampeni na Makamba kuanza kumhukumu kwenye majukwaa. Kitu ambacho ninaweza kuamini kimefanyika ni kumuweka chini kwa sasa baada ya CCM kuona CDM inakuja juu na kutafuta mbinu ya kukifunga Spidi gavana.

Mambo yafuatayo yatakuwa yamefanyika.

1. CCM na TISS watakuwa wamekaa na kutafakari ni nani ndani ya CDM anayeweza kuwafanyia kazi zao za kikuvuruga chama kwa ufasaha na kuona kuwa wakimfuata kada wao wa siku nyingi na kumueleza hali halisi na pia kumuomba radhi kwa kumuengua katika kugombea ubunge kwa ticketi ya chama hicho na kumuahidi kuwa watamlinda na hata CDM wakimfukuza wao watamsimamisha kugombea na atashinda kwa vyovyote ni SHIBUDA.

2. CCM watakuwa wamegundua kuwa wanaokidhoofisha Chama chao baada ya kuwatosa ni wana-CCM na hivyo kuweka mkakati wa kuwatumia hawa jamaa waliowahi kuwa ndani ya CCM kama wavurugaji na si vijana ambao wengi hawajawahi kuwa hata na kadi za umoja wa vijana kwa hiyari yao katika maisha ambao wanataka mabadiliko.

3. CDM wanatakiwa kutumia busara sana katika kumhandle mtu kama Shibuda kwani huenda moja ya mbinu za CCM ni kupunguza ruzuku ya CDM ili kukidhoofisha chama na kama watapoteza hata mmbunge mmoja wa kuchaguliwa basi watapigwa panga ruzuku na kupunguza nguvu za kuimarisha chama kuelekea 2015. CDM wamchukulie Shibuda kama alivyo, wasimwite na kutaka kumpatia adhabu yoyote ile kwani wameishajua kuwa si mtu mzuri kwa ustawi wa CDM lakini pia wanahitaji kiti hicho cha ubunge wa Shibuda. Nina hakika kabisa huenda Shibuda alishinda na wakataka kuchakachua kumtosa mwisho ikaja amri ya kumwacha atawasaidia kwani kama alishinda kwa kura 75 ni dhahiri CCM na Tume yao ya uchaguzi walikuwa na uwezo wa kuchakachua na kumfanya ashindwe(Rejea uchaguzi wa Ukonga) maana kama wameweza kubadili tofauti yao wao kushindwa kwa kura elfu ishirini mpaka kushinda kwa kura elfu tano ni dhahiri hizi 75 zilikuwa ni cha mtoto.

4. CDM wanatakiwa kujua kuwa kwa sasa wao ni ua zuri lenye kunukia hivyo lazima litavutia wadudu wa kila aina kulidhuru. CCM walitaka kutumia hoja ya udini kama walivyotumia kuimaliza CUF na kukifanya wakristo kukiogopa ila kwa upande wa CDM ime - backfire hivyo ni lazima wasilale watafute kila linalowezekana kuhakikisha kuwa 2015 CDM is no more a threat.

5. Ninashauri kuwa CDM watafute kichwa hasa katika kuwapitisha kwenye mitego ya panya yote watakayowekewa na CCM na vyombo vyake vya usalama (Wawe na msemaji mkuu na siyo kumwachia Mbowe ambaye kwa mtazamo wangu naona kama ni rahisi kuingizwa King kwenye diplomasia), Chadema wameisha tegua mitego ya ukabila, udini na sasa mtego mmoja wapo ni huu wa kumu-handle Shibuda. They should unleash him rather than try to control him, by doing that they would be able to reach 2015 with Shibuda on Board bila ya kumpa nafasi ya kuchomoa pini akiwa ndani ya CDM.
 
Back
Top Bottom