Shibuda apania kugombea dhidi ya JK CCM, ajitoa ghafla

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Msekwa: Shibuda hamuwezi Kikwete

Na Yusuph Katimba
Majira
17 October 2009

MIZENGWE ya kurudisha nyuma juhudi za Mbunge wa Maswa, John Shibuda kutaka kukamilisha nia yake ya kumng'oa Rais Kikwete katika uchaguzi wa kiti cha urais mwakani inazidi kutokota baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Pius Msekwa kusema kuwa hana ubavu wa kumpiku Rais Kikwete.

Alisema kuwa licha ya katiba ya CCM kuruhusu kila mwanachama aliye na sifa kugombea, lakini bado mbunge huyo hawezi kumtetemesha Rais Kikwete katika nafasi hivyo.


Bw. Msekwa alitoa kauli hiyo alipozungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza la BBC jana. Bw. Msemkwa pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisema kuwa kila mwanachama anayo sifa, na kuongeza kuwa baada ya mwanachama kuchukua fomu na kurejesha, mchakato hupita na kuwa yule aliye na sifa ndio hushika hatamu huku akimtaja Rais Kikwete kuwa ndiye aliye na sifa kwa sasa.

Bw. Shibuda amekuwa akikumbwa na misukosuko mbalimbali ndani ya chama chake. Julai mwaka jana, alijikuta akitimuliwa nje ya kikao cha Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya ya Maswa.

Ilidaiwa kuwa hakuwa mjumbe halali wa kamati ya siasa. Alitimuliwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo, Bw. Peter Bunyongoli na Katibu Mwenezi na Itikadi, Bw. Jeremiah Makondeko.

Baada ya kutangaza nia yake ya kumng'oa Rais Kikwete kwa kugombea nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu mwakani, alipingwa huku akisema ana uwezo wa kumung'oa na kuongoza nchi.

Pia alionesha kushangazwa na uamuzi wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) kuondoa jina lake katika kinyang’anyiro cha nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa.

Kipindi hicho, alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Potelea mbali, liwalo na liwe, nimechoka kuwa mfungwa wa kisiasa ndani ya CCM wakati nina uwezo wa kuwaongoza Watanzania.”

Akizunguimzia suala la rushwa jinsi inavyohusishwa katika uchaguzi, Bw. Msekwa alisema suala la fedha kuhusishwa katika uchaguzi ni suala la kawaida kwa kuwa hakuna uchaguzi unaofanyika bila kutumia fedha. Aliongeza kuwa rushwa na matumizi ya fedha lazima vitenganishwe.
 
17 October 2009
Na Yusuph Katimba


MIZENGWE ya kurudisha nyuma juhudi za Mbunge wa Maswa, John Shibuda kutaka kukamilisha nia yake ya kumng'oa Rais Kikwete katika uchaguzi wa kiti cha urais mwakani inazidi kutokota baada ya Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Pius Msekwa kusema kuwa hana ubavu wa kumpiku Rais Kikwete.

Alisema kuwa licha ya katiba ya CCM kuruhusu kila mwanachama aliye na sifa kugombea, lakini bado mbunge huyo hawezi kumtetemesha Rais Kikwete katika nafasi hivyo.

Bw. Msekwa alitoa kauli hiyo alipozungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza la BBC jana. Bw. Msemkwa pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alisema kuwa kila mwanachama anayo sifa, na kuongeza kuwa baada ya mwanachama kuchukua fomu na kurejesha, mchakato hupita na kuwa yule aliye na sifa ndio hushika hatamu huku akimtaja Rais Kikwete kuwa ndiye aliye na sifa kwa sasa.

Bw. Shibuda amekuwa akikumbwa na misukosuko mbalimbali ndani ya chama chake. Julai mwaka jana, alijikuta akitimuliwa nje ya kikao cha Kamati ya Siasa ya CCM ya Wilaya ya Maswa.

Ilidaiwa kuwa hakuwa mjumbe halali wa kamati ya siasa. Alitimuliwa na Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya hiyo, Bw. Peter Bunyongoli na Katibu Mwenezi na Itikadi, Bw. Jeremiah Makondeko.

Baada ya kutangaza nia yake ya kumng'oa Rais Kikwete kwa kugombea nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu mwakani, alipingwa huku akisema ana uwezo wa kumung'oa na kuongoza nchi.

Pia alionesha kushangazwa na uamuzi wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) kuondoa jina lake katika kinyang’anyiro cha nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa.

Kipindi hicho, alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Potelea mbali, liwalo na liwe, nimechoka kuwa mfungwa wa kisiasa ndani ya CCM wakati nina uwezo wa kuwaongoza Watanzania.”

Akizunguimzia suala la rushwa jinsi inavyohusishwa katika uchaguzi, Bw. Msekwa alisema suala la fedha kuhusishwa katika uchaguzi ni suala la kawaida kwa kuwa hakuna uchaguzi unaofanyika bila kutumia fedha. Aliongeza kuwa rushwa na matumizi ya fedha lazima vitenganishwe.


WAZO LANGU!

Kilichonifurahisha sana ni suala la Msekwa kudai fedha kuhusishwa na uchaguzi ni suala la kawaida.
CCM ni typical bandits.Yaani hawa watu ikifika Uchaguzi,wanaanza kutafutia rushwa majina mengine na kuita Takrima hata kui-justify!
Watanzania hebu tuone mbele na tuache kuwa makondoo tuuuuuu!
 
Shibuda amvaa Msekwa

Na Gladness Mboma
Majira
20 October 2009

MBUNGE wa Maswa, Bw. John Shibuda amesema kauli ya Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Bw. Pius Msekwa, kuwa hana ubavu wa kumvaa na kumpiku Rais Jakaya Kikwete, katika kinyang'anyiro cha urais ni sawa na kumpa kadi nyekundu hata kabla ya kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo.

Bw. Shibuda ambaye tayari ametangaza nia yake ya kuwania kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka 2010 kwa tiketi ya CCM, aliliambia gazeti hili jana kuwa kauli ya Bw. Msekwa ni maoni yake binafsi kwani uamuzi wenyewe utatolewa na vikao vya chama.

Akihojiwa na Shirika la Utangaza la Uingereza (BBC) mwishoni mwa wiki, Bw. Msekwa alisema Bw. Shibuda hana ubavu wa kumpiku Rais Kikwete katika nafasi ya urais.

"Ninampongeza Bw. Msekwa kwa kutoa maoni ambayo ni yake binafsi, vikao ndivyo vitakavyotoa dira ya nani atakuwa mbadala wa JK (Rais Kikwete), kwani uwezo, sifa na vigezo vyote ninavyo, nia na dhamana ya urais siyo ya kukurupuka na ndio maana sasa tupo wawili tunaogombea," alisema.

Alisema kuwa Mwalimu Nyerere enzi za uhai wake alisema mtu yoyote anayetaka kugombea urais anapaswa kujitangaza mapema na ndio maana aliamua kufanya hivyo mapema. Alisema kwa sasa watu ambao wametangaza kuwania kiti hicho ni yeye na Rais Kikwete.

"Nasisitiza kama kuna mtu mwenye uwezo na shabaha ajitokeze na ajitangaza na siyo mtu aje kuotea kwenye mpira wa kuvizia, watuache mimi na JK ndio tulio na uwezo wa kujipima ubavu," alisema Bw. Shibuda na kuongeza.

"Bw. Msekwa ni refarii, anaanza kunipa Red Card mapema kabla sijaucheza mpira wenyewe... kauli yake inanipa shaka kuwa anaweza asinitendee haki katika vikao vya kupendekeza wagombea kwa sababu yeye ndiye msimamizi mkuu,"alisema.

Bw. Shibuda alisema anamshangaa ni kwa Bw. Msekwa ameanza kumtetemekea mapema na kwamba inawezekana ana wasiwasi nafasi yake ya Makamu Mwenyekiti wa CCM itaipoteza pindi akichaguliwa kuwa Rais.

"Napenda kumuondolea wasiwasi kuwa nitakapochaguliwa nitatenda haki nikiwa kama Rais na Mwenyekiti wa CCM, hivyo ninaomba aondoe wasiwasi, ila kwa wale waliojaza nafasi zisizo na wajibu wa dhamana nitawaondoa sitawaonea huruma,"alisema.

Alisisitiza kuwa Bw. Msekwa asianze kumuonesha kadi nyekundu kwani yeye ni mcheza mpira asubiri dakika 90 za mchezo na siyo kuanza kumuonesha red card.

Alibainisha kuwa hadi sasa wagombea wanaofahamika ni wawili na kutaka wengine wanaotaka kuwania kiti hicho wajitangaze na siyo kuzungumza kichinichini.

Bw. Shibuda alisema anashukuru CCM haijamfanyia lolote baya tangu atangaze nia yake ya kugombea, ila anamshangaa refarii Mkuu (Bw. Msekwa) kuanza kutangaza matokeo ya mchezo kabla ya mpira kuwekwa uwanjani.

"Nampongeza Katibu Mkuu wa CCM, (Yusuf Makamba) kanyamaza kimya na wengine wanatakiwa kumuiga, kwani alinipongeza kwa uamuzi wangu wa kutangaza kuwania kiti hicho," alisema Bw. Shibuda na kuongeza;

"Ninachoomba ni jina langu lifikishwe katika vikao husika na wanijadili na kunipitisha kwani mimi ni pambazuko jipya na nuru ya matamanio kwa wanyonge ambayo ndiyo sera ya CCM."

Aliishukuru CCM kwa kumuandaa vyema kushika madaraka ya urais na kuwataka wanachama wa chama hicho kuwa makini ili wasichanganywe na kauli ambazo zimeanza kutolewa.

Kuhusu baraza la mawaziri atakalo unda pindi akichaguliwa kushika wadhifa huo, Bw. Shibuda alisema hiyo ni siri yake.

Alisema kama Mungu ameamua kwamba yeye ndiye atakayekuwa Rais, basi itakuwa hivyo na kama amempangia JK kuwa Rais basi akishinda ataunga mkono uteuzi huo.

Alitoa mwito kwa wabunge wasizuie watu kwenda kugombea katika majimbo wanayoyashikilia, kwa kuwa ni haki ya kila mtu mwenye uwezo kupeleka posa.

"Wabunge ni lazima wajitwishe ukomavu wa demokrasia ndani ya CCM," alisema. Mwaka 2005 Bw. Shibuda alichukua fomu za kuomba kuwania nafasi hiyo kwa tiketi ya CCM lakini jina lake liliondolewa kwenye vikao vya vyanzo vya CCM.

Hivi karibuni alitangaza nia yake ya kuwania kiti hicho ndani ya CCM. Katika mahojiano hayo, Bw. Msekwa alisisitiza kuwa Rais Kikwete, ndiye mwenye sifa za kuendelea kuwa rais.

 
Msekwa haifai Tanzania. Hana mawazo mapya kwa TAnzania na kwa watanzania. ni mtu ambaye anatakiwa kupumzika, anaweza kuplay role kama Sumaye na Mzee Msuya waliokaa pembeni na kusema wanayaona, lakininsio kuanza kutuchagulia wagombea au kuanza kuwanyamazisha anaodhani wanatoa changamaoto.
 
Shibuda amtisha Rais Kikwete, asisitiza kumvaa 2010

Ramadhan Semtawa na Sadick Mtulya

MBUNGE wa Maswa John Shibuda amezidi kupandisha joto la uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, baada ya kutangaza kujiandaa kurusha makombora dhidi ya Rais Jakaya Kikwete ambayo aliahidi kuwa, yataduwaza watu wakati akichukua fomu.

Shibuda ni mwana CCM wa kwanza na pekee hadi sasa ambaye alitangaza kumvaa Rais Kikwete, katika mbio za urais ndani ya chama hicho na kuvunja utamaduni wa kumwachia mgombea ngwe ya pili bila kupingwa.

Wakati mwanasiasa mkongwe na Waziri Mkuu mstaafu John Malecela akitaka Rais Kikwete aachiwe tena mwaka huu kama sehemu ya utamaduni huo wa chama, Shibuda amebeza hatua hiyo na kumfananisha Malecela sawa na utwana.

Juzi usiku akizungumza katika kipindi cha Kurunzi kinachorushwa na kituo cha Luninga cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Mlimani TV), Shibuda alipandisha joto hilo baada ya kusema utaratibu wa kumuachia mgombea vipindi viwili, si utaratibu rasmi.

"Kumwacha Rais Kikwete agombee peke yake ni utwana, tuanze kubadilika tusiruhusu mazoea hakuna kukubali mazoea yatutawale kwani mazoea ni mabaya,"alifafanua Shibuda.

Shibuda mbunge mwenye kupenda kuzungumza kwa methali, misemo na lafudhi ya Pwani, alisema wakati ukifika ambao ni baada ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho, kutangaza watu kuchukua fomu, ndipo atakaporusha makombora hayo.

"Nikisema sasa hivi nimejiandaaje nitakuwa napiga kampeni wakati muda wa kampeni bado ndugu yangu, nasubiri siku ya NEC ikitangaza kuchukua fomu nitasema kwanini nataka kumrithi Rais Kikwete, nitazungumza mambo mazito ambayo yataduwaza wengi," alitamba Shibuda.

Shibuda alisema hawezi kuzungumzia sababu za kuingia katika kinyanganyiro hicho, kwa kuwa anaogopa kufanyiwa mchezo mchafu, na kwamba atazitoa baada ya kuchukua fomu ya kuomba ateuliwe kugombea nafasi hiyo, kabla ya Mei, mwaka huu.

"Kila kitu kina wakati wake na mahala pake. Nasubiri Halmashauri Kuu(NEC) itangaze rasmi siku ya kuchukua fomu ambayo itakuwa kabla ya Mei, lakini ninasema Watanzania watashtushwa na sababu nitakazozitoa za kwa nini ninataka kuomba ridhaa ya wanaCCM wanitechague kugombea urais katika uchaguzi ujao," alisema Shibuda.

Alisema ana kila sababu ya kuchukua nafasi hiyo huku akibeza utabiri wa Shekhe Yahaya Hussein kwamba, kwa kutamba kwamba haamini katika mizimu, mashetani na maruhani.

"Sheikh Yahaya anasema eti hanioni ni kweli hawezi kuniona katika utabiri wake kwasababu mimi nalindwa na Malaika mkuu Gabriel, kwa taarifa ni kwamba Sheikh Yahaya hanipati ng'o," alizidi kutamba mbunge huyo anayejiita pambazuko jipya la uongozi nchini.

Kuhusu mpasuko ndani ya CCM, Shibuda alisema chama hicho hakina mpasuko bali ni, "harakati hai za fikra huyu anasema kile huyu lile siyo mpasuko huo."
 
Shibuda anajifurahisha tuu. Wacha aendelee kwani hakuna kitu kizuri kama day dreaming. Hivi rais wa nchi hii awe Shibuda Tehe tehe tehe
 
Nina wasiwasi na Dhamira halisi ya Shibuda, isije akwa anafanya mzaha wa kupunguza Mass * Velocity za watu
 
hehehe!
kuna status fulani ya watu SHIBUDA ANAWEZA KUWAHADAA...!lakini sio JF!
POLE SHIBUDA.(hata hivyo gazeti limeuzwa,na watu wameingiza siku)
 
Vyovyote vile. Shibuda analeta jambo jipya na muhimu ktk historia ya siasa za CCM na nchi kwa ujumla. Whatever, I support Shibuda.

Hivi Mwiba yuko wapi?
 
Usije ukafikia wakati wa Kuchukua fomu akasema "Baada ya kutafakari kwa kina na kutathmini mafanikio ya Serikali ya awamu ya nne nimeona nimuunge mkono Mh Rais katika ngwe ya Pili". Yangu masikio and mark my word, Nina wasi wasi na dhamira halisi ya Shibuda
 
Kama akina Dr. Salim, Prof. Mwandosya, Dr. Magufuli, Idd Simba, Hans Kitine na wote waliogombea 2005 wamenywea it is time for 'Rajolina' to rise. Nani aliwahi kufikiria kuwa DJ Rajo angekuja kuwa Rais? tena akiwa na umri mdogo kuliko unaoruhusiwa na katiba ya nchi yao. Go Shibuda. Ni afadhali Rais akawa Shibuda kuliko huyu Muungwana.
 
Kama akina Dr. Salim, Prof. Mwandosya, Dr. Magufuli, Idd Simba, Hans Kitine na wote waliogombea 2005 wamenywea it is time for 'Rajolina' to rise. Nani aliwahi kufikiria kuwa DJ Rajo angekuja kuwa Rais? tena akiwa na umri mdogo kuliko unaoruhusiwa na katiba ya nchi yao. Go Shibuda. Ni afadhali Rais akawa Shibuda kuliko huyu Muungwana.

I Like that and I wish him all the best
 
Shibuda hata kama hatateuliwa lakini atakuwa ametusaidia kuonesha kwamba haya mazoea ya kusema Rais lazima apewe terms mbili kwasababu ni utamaduni wa CCM hauna maana yeyote kwa jamii inayotaka maendeleo. Rais achaguliwe kuanza au kuendele na uongozi on the basis ya performance na track record yake; huu utamaduni wa kumpa kiongozi muhula mwingine hata pale asipostahili unaweza siku moja tukapata Rais asiye na akili timamu wakati wapo watu wenye akili timamu ambao wangeweza kuongoza!! Go SHIBUDA GO!!!
 
hivi mnajua shibuda alikuwa anafanya kazi gani na mpaka sasa hivi bado anaifanya? wako wengi kama yeye.....
 
Kama akina Dr. Salim, Prof. Mwandosya, Dr. Magufuli, Idd Simba, Hans Kitine na wote waliogombea 2005 wamenywea it is time for 'Rajolina' to rise. Nani aliwahi kufikiria kuwa DJ Rajo angekuja kuwa Rais? tena akiwa na umri mdogo kuliko unaoruhusiwa na katiba ya nchi yao. Go Shibuda. Ni afadhali Rais akawa Shibuda kuliko huyu Muungwana.

Endelea kuishi katika ndoto.
 
Shibuda amtisha Rais Kikwete, asisitiza kumvaa 2010

Ramadhan Semtawa na Sadick Mtulya

MBUNGE wa Maswa John Shibuda amezidi kupandisha joto la uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, baada ya kutangaza kujiandaa kurusha makombora dhidi ya Rais Jakaya Kikwete ambayo aliahidi kuwa, yataduwaza watu wakati akichukua fomu.

Shibuda ni mwana CCM wa kwanza na pekee hadi sasa ambaye alitangaza kumvaa Rais Kikwete, katika mbio za urais ndani ya chama hicho na kuvunja utamaduni wa kumwachia mgombea ngwe ya pili bila kupingwa.

Wakati mwanasiasa mkongwe na Waziri Mkuu mstaafu John Malecela akitaka Rais Kikwete aachiwe tena mwaka huu kama sehemu ya utamaduni huo wa chama, Shibuda amebeza hatua hiyo na kumfananisha Malecela sawa na utwana.

Juzi usiku akizungumza katika kipindi cha Kurunzi kinachorushwa na kituo cha Luninga cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Mlimani TV), Shibuda alipandisha joto hilo baada ya kusema utaratibu wa kumuachia mgombea vipindi viwili, si utaratibu rasmi.

"Kumwacha Rais Kikwete agombee peke yake ni utwana, tuanze kubadilika tusiruhusu mazoea hakuna kukubali mazoea yatutawale kwani mazoea ni mabaya,"alifafanua Shibuda.

Shibuda mbunge mwenye kupenda kuzungumza kwa methali, misemo na lafudhi ya Pwani, alisema wakati ukifika ambao ni baada ya Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho, kutangaza watu kuchukua fomu, ndipo atakaporusha makombora hayo.

"Nikisema sasa hivi nimejiandaaje nitakuwa napiga kampeni wakati muda wa kampeni bado ndugu yangu, nasubiri siku ya NEC ikitangaza kuchukua fomu nitasema kwanini nataka kumrithi Rais Kikwete, nitazungumza mambo mazito ambayo yataduwaza wengi," alitamba Shibuda.

Shibuda alisema hawezi kuzungumzia sababu za kuingia katika kinyanganyiro hicho, kwa kuwa anaogopa kufanyiwa mchezo mchafu, na kwamba atazitoa baada ya kuchukua fomu ya kuomba ateuliwe kugombea nafasi hiyo, kabla ya Mei, mwaka huu.

"Kila kitu kina wakati wake na mahala pake. Nasubiri Halmashauri Kuu(NEC) itangaze rasmi siku ya kuchukua fomu ambayo itakuwa kabla ya Mei, lakini ninasema Watanzania watashtushwa na sababu nitakazozitoa za kwa nini ninataka kuomba ridhaa ya wanaCCM wanitechague kugombea urais katika uchaguzi ujao," alisema Shibuda.

Alisema ana kila sababu ya kuchukua nafasi hiyo huku akibeza utabiri wa Shekhe Yahaya Hussein kwamba, kwa kutamba kwamba haamini katika mizimu, mashetani na maruhani.

"Sheikh Yahaya anasema eti hanioni ni kweli hawezi kuniona katika utabiri wake kwasababu mimi nalindwa na Malaika mkuu Gabriel, kwa taarifa ni kwamba Sheikh Yahaya hanipati ng'o," alizidi kutamba mbunge huyo anayejiita pambazuko jipya la uongozi nchini.

Kuhusu mpasuko ndani ya CCM, Shibuda alisema chama hicho hakina mpasuko bali ni, "harakati hai za fikra huyu anasema kile huyu lile siyo mpasuko huo."
 
hehehe!
kuna status fulani ya watu SHIBUDA ANAWEZA KUWAHADAA...!lakini sio JF!
POLE SHIBUDA.(hata hivyo gazeti limeuzwa,na watu wameingiza siku)


kama JF ni hii ambayo mimi ni memba- SHIBUDA is supported at least by me. Unamaana gani kusema sio JF kila siku JF inalaani Ufisadi, inalaani kigugumizi cha maamuzi mazito, ina tambulika kama social think tank inayoguswa na hali mbaya ya jamii kutokana na uongozi mbovu! hafu G unaleta kauli gani? au hata huku tunazugwa tu si wanamadiliko halisi?

It is so disappointing to hear this from a great thinker!

to me, anything in state house but kikwete will open opportunities for development at least the culture to challenge and hence promoting accountability at individual level.

re: mode, iache ipite please)
 
Jamani hadi leo hamuielewi CCM na mbinu zake inawezekana ni mbinu ili ionekane kuna demokrasia ndani yake, kwani hamjui utitiri wa vyama umetokana na nini ni yale yale tu ndugu zangu. CUF wakigomea uchaguzi Zanzibar vyama kama kumi vitashiriki, Chadema, CUF wakigomea uchaguzi bara ishirini vingine vitashiriki itaonekana ambavyo havikushiriki ndivyo vinasaliti wananchi lakini ukweli ni kinyume chake.

Mimi binafsi nam-support Shibuda kujitokeza kwa kuwa anatimiza haki yake ya msingi kikatiba lakini sioni kama yuko serious.
 
I hope now is a time for change regardless that who is going to lead that changes, because some traditions are making us delay on our real issues, let the man take the track and voters will decide which is correct direction are we taking.

Once for number of years we failed to get a right canditate from oppositions then let us encourage within this huge party to exercise real democracy. Although the main question will remain is it going to be realy?
 
Back
Top Bottom