Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Shibuda achafua hali ya hewa mkutano wa pamba
MBUNGE wa Maswa Mashariki (Chadema), John Shibuda, jana alichafua hali ya hewa katika mkutano wa wadau wa pamba baada ya kuwashambulia wakuu wa wilaya ya wakurugenzi wa halmashauri za wilaya kuwa, wanakwamisha mafanikio ya kilimo cha zao hilo, huku nao kuja juu kumshambulia.
Shibuda alisema tangu mkutano huo uanze na majadiliano, watu wamekuwa wakiwatupia lawama wanasiasa kuwa ndiyo tatizo kwa mafanikio ya kilimo cha pamba kwa mkataba, lakini wanaoshutumu wajue kuwa wanamshutumu Rais Jakaya Kikwete na Waziri mkuu wake, Mizengo Pinda, kwa vile nao ni wanasiasa.
Nasikitishwa kwa kauli ya kuwa wanasiasa ni tatizo, basi mjue mnamsema rais na waziri mkuu na mawaziri wote kuwa ndiyo tatizo, hata wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa nao ni tatizo wapo kila siku kwenye vikao lakini hawafikishi taarifa kwa wananchi wao alisema Shibuda na kukatishwa na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Abihudi Saidea, ambaye alipaza sauti kuwa hata wabunge wamo katika vikao.
Kutokana na kukatishwa huko, Shibuda alimgeukia mkuu huyo wa wilaya na kusema, "tuanzie Meatu ambako wananchi wanalia na kulalamika hawajapelekewa mbegu, baadhi ya mizani zimekuwa zinalalamikiwa pia na kumtaka mkuu huyo wa wilaya kutoogopa kujadiliwa, hali ambayo ilizua tafrani na kurushiana maneno ya hapa na pele."
Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Pamba, Raphael Mlolwa, aliwatuliza washiriki na kumuomba Shibuda kumalizia kwa vile alikuwa mchangiaji wa mwisho ili wajumbe watoke kuelekea katika chakula cha mchana kisha kurejea.
Shibuda alihitimisha kwa kueleza kuwa, kilimo cha mkataba kina wapinzani wengi ambao ni changamoto kwa wanaosimamia, lakini aliwaomba kutowachukua watu wanaopinga kwa vile wanataka kuelimishwa.
MBUNGE wa Maswa Mashariki (Chadema), John Shibuda, jana alichafua hali ya hewa katika mkutano wa wadau wa pamba baada ya kuwashambulia wakuu wa wilaya ya wakurugenzi wa halmashauri za wilaya kuwa, wanakwamisha mafanikio ya kilimo cha zao hilo, huku nao kuja juu kumshambulia.
Shibuda alisema tangu mkutano huo uanze na majadiliano, watu wamekuwa wakiwatupia lawama wanasiasa kuwa ndiyo tatizo kwa mafanikio ya kilimo cha pamba kwa mkataba, lakini wanaoshutumu wajue kuwa wanamshutumu Rais Jakaya Kikwete na Waziri mkuu wake, Mizengo Pinda, kwa vile nao ni wanasiasa.
Nasikitishwa kwa kauli ya kuwa wanasiasa ni tatizo, basi mjue mnamsema rais na waziri mkuu na mawaziri wote kuwa ndiyo tatizo, hata wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa nao ni tatizo wapo kila siku kwenye vikao lakini hawafikishi taarifa kwa wananchi wao alisema Shibuda na kukatishwa na Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Abihudi Saidea, ambaye alipaza sauti kuwa hata wabunge wamo katika vikao.
Kutokana na kukatishwa huko, Shibuda alimgeukia mkuu huyo wa wilaya na kusema, "tuanzie Meatu ambako wananchi wanalia na kulalamika hawajapelekewa mbegu, baadhi ya mizani zimekuwa zinalalamikiwa pia na kumtaka mkuu huyo wa wilaya kutoogopa kujadiliwa, hali ambayo ilizua tafrani na kurushiana maneno ya hapa na pele."
Kutokana na hali hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Pamba, Raphael Mlolwa, aliwatuliza washiriki na kumuomba Shibuda kumalizia kwa vile alikuwa mchangiaji wa mwisho ili wajumbe watoke kuelekea katika chakula cha mchana kisha kurejea.
Shibuda alihitimisha kwa kueleza kuwa, kilimo cha mkataba kina wapinzani wengi ambao ni changamoto kwa wanaosimamia, lakini aliwaomba kutowachukua watu wanaopinga kwa vile wanataka kuelimishwa.