Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Ni lazima watu wanaovunja ndoa wawe na sababu ya msingi? Kwenye State kama Michigan (US) wana kitu kinaitwa "no fault divorce" yaani haiitajiki kuwepo kosa kwenye ndoa kumfanya mtu atake divorce. Basically mtu anaweza kuwa divorce for any reason or for no reason at all. Je katika Tanzania kama hiyo inahitajika, itasaidia, au itachochea talaka?
Hadi hivi sasa ili mtu aweze kupata talaka kuna masharti magumu na ambayo yote yanataka sababu ya kuhalalisha talaka na hata ikiwepo sababu ni lazima mfuate utaratibu wa usuluhishi n.k n.k
Katika Tanzania hivi sasa talaka haiwezi kutolewa mpaka mahakama iridhike kuwa ndoa haiwezi kutengamaa tena na kwamba ndoa imevunjika pasipo shaka ili kuthibitisha hili sharti muhimu la kisheria, mdai talaka anapaswa kuonyesha mahakamani mambo kadhaa yanayoweza kuvunja ndoa. Si lazima aoneshe yote bali hata mojawapo likiwa na uzito ambao utaridhisha mahakama. Lakini kimsingi ni lazima kuwe na sababu ya kutosha.
1. Talaka ya Kiislam
2. Desertion including constructive deserttion
3. Cruelty...hapan ni mambo mengi yanayotafsiriwakuwa ni ukatili
4. Kubadili dini
5.Kifungo cha muda mrefu
6. nadhani hata ugonjwa kama kichaa
Sasa inakuwaje pale mtu ambapo anajua kua ndoa yake kweli imefikia magogoni? Afanye nini? aendelee kusumbuka miaka nenda rudi kutafuta talaka yake?
Maana hata kama mtu anataka kuoa au kuolewa tena anajikuta anashindwa kwa sababu hata potential wachumba wanaachia mbele ya safari kwani talaka haiji na muda unapita. Lakini ikiwekwa sheria ya kusema kuwa yeyote kati yenu anaweza kuinitiate divorce proceeding na ya kuwa at the end divorce itatolewa hata kama mwingine hataki itasaidia watu kuwa waangalifu kwani watajua hawawezi kuchezea ndoa kwani inaweza ikavunjwa wakati wowote?
Open floor.
Hadi hivi sasa ili mtu aweze kupata talaka kuna masharti magumu na ambayo yote yanataka sababu ya kuhalalisha talaka na hata ikiwepo sababu ni lazima mfuate utaratibu wa usuluhishi n.k n.k
Katika Tanzania hivi sasa talaka haiwezi kutolewa mpaka mahakama iridhike kuwa ndoa haiwezi kutengamaa tena na kwamba ndoa imevunjika pasipo shaka ili kuthibitisha hili sharti muhimu la kisheria, mdai talaka anapaswa kuonyesha mahakamani mambo kadhaa yanayoweza kuvunja ndoa. Si lazima aoneshe yote bali hata mojawapo likiwa na uzito ambao utaridhisha mahakama. Lakini kimsingi ni lazima kuwe na sababu ya kutosha.
1. Talaka ya Kiislam
2. Desertion including constructive deserttion
3. Cruelty...hapan ni mambo mengi yanayotafsiriwakuwa ni ukatili
4. Kubadili dini
5.Kifungo cha muda mrefu
6. nadhani hata ugonjwa kama kichaa
Sasa inakuwaje pale mtu ambapo anajua kua ndoa yake kweli imefikia magogoni? Afanye nini? aendelee kusumbuka miaka nenda rudi kutafuta talaka yake?
Maana hata kama mtu anataka kuoa au kuolewa tena anajikuta anashindwa kwa sababu hata potential wachumba wanaachia mbele ya safari kwani talaka haiji na muda unapita. Lakini ikiwekwa sheria ya kusema kuwa yeyote kati yenu anaweza kuinitiate divorce proceeding na ya kuwa at the end divorce itatolewa hata kama mwingine hataki itasaidia watu kuwa waangalifu kwani watajua hawawezi kuchezea ndoa kwani inaweza ikavunjwa wakati wowote?
Open floor.