Sheria ya Talaka TZ ilegezwe au isilegezwe?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Ni lazima watu wanaovunja ndoa wawe na sababu ya msingi? Kwenye State kama Michigan (US) wana kitu kinaitwa "no fault divorce" yaani haiitajiki kuwepo kosa kwenye ndoa kumfanya mtu atake divorce. Basically mtu anaweza kuwa divorce for any reason or for no reason at all. Je katika Tanzania kama hiyo inahitajika, itasaidia, au itachochea talaka?

Hadi hivi sasa ili mtu aweze kupata talaka kuna masharti magumu na ambayo yote yanataka sababu ya kuhalalisha talaka na hata ikiwepo sababu ni lazima mfuate utaratibu wa usuluhishi n.k n.k

Katika Tanzania hivi sasa talaka haiwezi kutolewa mpaka mahakama iridhike kuwa ndoa haiwezi kutengamaa tena na kwamba ndoa imevunjika pasipo shaka ili kuthibitisha hili sharti muhimu la kisheria, mdai talaka anapaswa kuonyesha mahakamani mambo kadhaa yanayoweza kuvunja ndoa. Si lazima aoneshe yote bali hata mojawapo likiwa na uzito ambao utaridhisha mahakama. Lakini kimsingi ni lazima kuwe na sababu ya kutosha.

1. Talaka ya Kiislam
2. Desertion including constructive deserttion
3. Cruelty...hapan ni mambo mengi yanayotafsiriwakuwa ni ukatili
4. Kubadili dini
5.Kifungo cha muda mrefu
6. nadhani hata ugonjwa kama kichaa

Sasa inakuwaje pale mtu ambapo anajua kua ndoa yake kweli imefikia magogoni? Afanye nini? aendelee kusumbuka miaka nenda rudi kutafuta talaka yake?

Maana hata kama mtu anataka kuoa au kuolewa tena anajikuta anashindwa kwa sababu hata potential wachumba wanaachia mbele ya safari kwani talaka haiji na muda unapita. Lakini ikiwekwa sheria ya kusema kuwa yeyote kati yenu anaweza kuinitiate divorce proceeding na ya kuwa at the end divorce itatolewa hata kama mwingine hataki itasaidia watu kuwa waangalifu kwani watajua hawawezi kuchezea ndoa kwani inaweza ikavunjwa wakati wowote?

Open floor.
 
mnh kama mmoja hajiamini,hatakuwa na amani,muda wote atakuwa na wasiwasi ataachwa wakati wowote,hii inaweza leta pressure,msongo wa mawazo lol
 
Katika taasisi za kale ndoa ni mojawapo. Jamii zote duniani zilijitahidi kuhakikisha ndoa inakuwepo kwa kujua kuwa hakuna ndoa iliyo kamili kwa asilimia mia. Ni kweli kulegeza sheria kama unavyosema kutasaidia watu kuwa waangalifu, lakini kizazi cha sasa hiyo itachochea sana uvunjikaji wa ndoa. Endapo ndoa imefika'magogoni' kuna sababu zilizoifikisha hapo na kama sababu hizo hazikubaliki basi ipo nafasi kwa wakati huo kutengeneza sababu zitakazokubalika, na hii itasaidia wanaowahi potential wachumba kufikia malengo.

Nadhani ni muhimu watu wakaelewa kwanini wanaoa na wanamuoa nani na kwa dhati gani. Itasaidia kuwa na ndoa stable,lakini watu kama wataoana kwa mtindo wa 'hollywood' mwisho utakuwa huo huo.

Hili la kulegeza sheria, Marekani na Ulaya linawaletea matatizo sana na kila mara wamekuwa wanatunga vijisheria indirect ili kuhakikisha wanaoamua kuvunja ndoa basi iwe ni lazima na si 'ndoa for covinience'. Kuna nchi zinasema kuvunja ndoa ni mwaka mmoja baada ya ku 'separate', zingine zinaweka masharti ya ulezi n.k. ikiwa ni njia ya kuhakikisha kuwa kuvunjika kuna msingi wa maana.

Kwa jamii yetu ambayo ndoa haiwezi kuvunjika kwa sababu mume hakuleta maua siku ya birth day, nadhani tuendelee na taratibu zetu na ikiwa ni lazima kuvunja basi na iwe hivyo. Nisingependa tuige mambo ya nje kwasababu mazingira yetu ni tofauti kabisa na nina amini sisi bado tunabeba thamani ya ndoa kuliko jamii nyingi za ulaya na marekani.
Ama sheria za ndoa ziachwe kama zilivyo, kama yupo aliyechoka tu basi atafute sababu ambazo zipo nyingi.
 
hii nafikiri kwa tanzania itakuwa si sahihi, itapelekea watu wengi kuweka dhana kuwa ndoa ni jambo jepesi, naweza kuoa leo na kuacha kesho,suala zima la uvumilivu na kusameheana ktk maisha ya ndoa litakuwa matatani, watu wanaweza kuwapa talaka wenzi wao ili kukwepa majukumu yao ya kifamilia .....
 
Lakini kwanini ionekane kana kwamba sheria inalazimisha watu wasiopatana kuendelea kuwa pamoja katika ndoa zilizoshindwa?
 
Lakini kwanini ionekane kana kwamba sheria inalazimisha watu wasiopatana kuendelea kuwa pamoja katika ndoa zilizoshindwa?
Mzee mwanakijiji,
Ndoa is an institution which was founded by God himself and since then African community has been culturally maintaining this institution very strong. Labda kabla hujaleta mjadala wa sheria za ndoa na talaka ni vizuri tena umwage hapa jamvini procedure wanazofuata hao watu kabla ya kufunga ndoa na kuona kama zina-relate na za kwetu. Hapa kwetu najua ndoa inajumisha zaidi ya wazazi wa pande zote mbili na linakuwa jambo la koo mbili kuungana na kwa hiyo watu woote hawa wanajisikia kuwa na wajibu wa kulinda ndoa tarajwa! I think for Michigan may be wako sawa since kijana na binti wanaweza kufungia ndoa popote na sidhani kama details za milolongo kama hii yetu zinahusishwa.
Na nido maana vijana wa ndoa za makaratasi huwa wanazimudu bila madhara makubwa kwa muda kitambo kisha wanaendelea na mambo yao hapo ughaibuni wakisha pata papers
 
hii nafikiri kwa tanzania itakuwa si sahihi, itapelekea watu wengi kuweka dhana kuwa ndoa ni jambo jepesi, naweza kuoa leo na kuacha kesho,suala zima la uvumilivu na kusameheana ktk maisha ya ndoa litakuwa matatani, watu wanaweza kuwapa talaka wenzi wao ili kukwepa majukumu yao ya kifamilia .....
Hapo kwenye red mkuu
Wengi wa hapo wamarekani hulichukulia hivyo! huu ni mtazamo wangu!
 
I am a big proponent of no-fault divorce and I think the law(s) should be eased. It is long overdue!

Here is my rationale. After being together for so long people (couples) do grow apart and their love for each other, bond, and romance starts petering out. This is a fact though I don't mean to imply that every couple is like that. But at least the majority of them have that experience at some point in their matrimonial life together .

That weakening of their love may push one or both husband and wife to commit adultery which is illicit in many people's eyes. So if this is the case why then cling on to a marriage that you are not wholeheartedly committed to? I see no point whatsoever.

If you are tired with your husband or wife for whatever reason or no reason then I think you should be able to free yourself from that marriage by legal recourse. You shouldn't be required to show any evidence of breach of the marital contract by your spouse. Irreconcilable difference(s) should suffice.
 
Nikikuchoka tu
nakutumia sms tatu tu kwenye simu

ni ttalaka tosha....

Hiyo ndo ilivyo nchi za kiarabu...

Na bongo iwe hivyo...
 
I am a big proponent of no-fault divorce and I think the law(s) should be eased. It is long overdue!

Here is my rationale. After being together for so long people (couples) do grow apart and their love for each other, bond, and romance starts petering out. This is a fact though I don’t mean to imply that every couple is like that. But at least the majority of them have that experience at some point in their matrimonial life together .

That weakening of their love may push one or both husband and wife to commit adultery which is illicit in many people’s eyes. So if this is the case why then cling on to a marriage that you are not wholeheartedly committed to? I see no point whatsoever.

If you are tired with your husband or wife for whatever reason or no reason then I think you should be able to free yourself from that marriage by legal recourse. You shouldn’t be required to show any evidence of breach of the marital contract by your spouse. Irreconcilable difference(s) should suffice.

This is too dangerous,
why did you marry in the first if you knew you could end up in love-less marriage after sometime??

African countries should not accept these kind of laws, we are still poor. At least in USA, one can afford to live as a single parent and survive well, not so in Tanzania particularly, where there is still so much dependence among 'married' families. Putting these easy-to-break laws will jeopardise our generation in the years ahead.
 
Sheria ibaki hivyo hivyo. Ingekuwa ku divorce ni rahisi nadhani sasa hivi ningekuwa single. Na labda ningekuwa najutia hasira zangu. Niliwahi kugombana vibaya sana na hubby nikaenda kuomba ushauri kwa lawyer (friend of mine) kuhusu utaratibu wa kufuata nipate talaka yangu. Procedure alizonambia zilinifanya nigairi. Na leo hii tunaishi vizuri na tumeshasahau yaliyotokea.

Nimejifunza kwenye marriage life talaka si kitu cha kukimbilia. Ugomvi ni wa mpito na ukiisha mahusiano yanachipua upyaaa!
 
  • Thanks
Reactions: EMT
And that will increase population hence poverty. Maana mtu anapoacha mke au kuachika maanake anaenda kuanza upya familia. Kwa hiyo anaanza kuzaa upya. Wakati angekaa na mke mume mmoja angejizalia watoto wawili. Sasa with new wife anaongeza wengine wawili. Na wife with new husband anaongeza wengine watatu.


This is too dangerous,
why did you marry in the first if you knew you could end up in love-less marriage after sometime??

African countries should not accept these kind of laws, we are still poor. At least in USA, one can afford to live as a single parent and survive well, not so in Tanzania particularly, where there is still so much dependence among 'married' families. Putting these easy-to-break laws will jeopardise our generation in the years ahead.
 
Lakini kwanini ionekane kana kwamba sheria inalazimisha watu wasiopatana kuendelea kuwa pamoja katika ndoa zilizoshindwa?

Kwa sababu watu waliopendana ni ngumu kuchukiana. Sheria inawapa nafasi ya kujifikiria. Unless ndoa hiyo iwe ilikuwa ya mkeka. But if there was love, sheria imeona possibility of reconcilling ipo. Na tuna ushaidi wa watu ambao wameweza kuyashinda majaribu ya ndoa na sasa ndoa zao ni mifano ya kuigwa.
 
This is too dangerous,
why did you marry in the first if you knew you could end up in love-less marriage after sometime??
This is the basic question.
Matrimony as an institution is governed by the laws, regulations and ethics. Millions have benefited as opposed to minority who want to make use of institution as a legal organ to justify their interest.
For those who are skeptical they should not marry in first place, instead they have to take another path which is legally recognized i.e. live as common law. The common law is the simple way of living together if the couple is uncertain.
The couple can marry or walk away without infringement or any legal string attached.
 
I am a big proponent of no-fault divorce and I think the law(s) should be eased. It is long overdue!

Here is my rationale. After being together for so long people (couples) do grow apart and their love for each other, bond, and romance starts petering out. This is a fact though I don't mean to imply that every couple is like that. But at least the majority of them have that experience at some point in their matrimonial life together .

That weakening of their love may push one or both husband and wife to commit adultery which is illicit in many people's eyes. So if this is the case why then cling on to a marriage that you are not wholeheartedly committed to? I see no point whatsoever.

If you are tired with your husband or wife for whatever reason or no reason then I think you should be able to free yourself from that marriage by legal recourse. You shouldn't be required to show any evidence of breach of the marital contract by your spouse. Irreconcilable difference(s) should suffice.


Kwenye issue ya kugawana mali itakuwaje? Tutafuata the same old law or will have to create a new law as well?
 
This is too dangerous,
why did you marry in the first if you knew you could end up in love-less marriage after sometime??

Things do happen and no one can predict the future. Do you know how many people are unhappily married? It's a lot! If all of those unhappily married people would have known beforehand that their marriage would at some point sour, I doubt if many of them would have gotten married. But most people don't live their lives like that. Most people live their lives optimistically. But when things turn out to be not as they were expected people have to adapt.

African countries should not accept these kind of laws, we are still poor. At least in USA, one can afford to live as a single parent and survive well, not so in Tanzania particularly, where there is still so much dependence among 'married' families. Putting these easy-to-break laws will jeopardise our generation in the years ahead.

Very weak argument! So basically what you are saying is that someone should hold on to an unhappy marriage just because our society is poor? That just doesn't make sense. Most people I think would trade an unhappy marriage life for a hard but happy single-life in a heartbeat. Just think about it, who wants to live in misery?
 
Kwenye issue ya kugawana mali itakuwaje? Tutafuata the same old law or will have to create a new law as well?

Hakuna ubaya kuzifanyia marekebisho sheria zinazohusu ugawanaji wa mali ili mradi ugawanaji huo ni wa haki. Kama sheria zilizopo ni za haki basi hakuna ulazima wowote wa kuzibadilisha. Kwa hiyo kwa ujumla kitu cha msingi hapa ni haki tu.
 
Sheria ibaki hivyo hivyo. Ingekuwa ku divorce ni rahisi nadhani sasa hivi ningekuwa single. Na labda ningekuwa najutia hasira zangu. Niliwahi kugombana vibaya sana na hubby nikaenda kuomba ushauri kwa lawyer (friend of mine) kuhusu utaratibu wa kufuata nipate talaka yangu. Procedure alizonambia zilinifanya nigairi. Na leo hii tunaishi vizuri na tumeshasahau yaliyotokea.

Nimejifunza kwenye marriage life talaka si kitu cha kukimbilia. Ugomvi ni wa mpito na ukiisha mahusiano yanachipua upyaaa!

Huyo ni wewe. Wengine wana mtazamo tofauti na wana matakwa tofauti. Ili mradi inahusu maisha yao binafsi basi sioni kwa nini sheria isiwasitiri na wao.
 
Back
Top Bottom