Sheria ya PPF Pensions Fund inaruhusu mafao ya kujitoa

Mu-Israeli

JF-Expert Member
Mar 21, 2012
2,454
975
Wana JF,
Nimefuatilia mijadala mimngi hapa JF inayohusu swala la mafao ya kujitoa.
Nimeona kuwa watu wengi hawajui kuwa mafao ya kujitoa PPF yapo kisheria na kudhani kuwa mafao hayo yanatolewa na PPF kama hisani tu.
Kwa sababu hiyo, SSRA, serikali na watu wengine wametumia mwanya huo kupotosha ukweli kuhusu mafao hayo, na kusema kuwa mafao hayo hayapo kisheria.

PPF Act No. 25 ya mwaka 2001, kifungu cha 44 kinasema yafuatayo:-

“Withdraw Befefits"

44.-(1) Where a member ceases to be employed in circumstances in which he is not eligible for any pension, gratuity or any other benefit under the provisions of this Act, he shall be refunded the amount of his own contributions and that of his employer to the Fund.
(2) Where a member has been employed for a period of not less than five years and the
cessation of such employment is not due to dismissal for misconduct the amount of his own
contribution and that of his employer together with a simple interest at that rate to be determined
by the Board of Trustees shall be paid to him.


Kwa kifupi kabisa, mafao ya kujitoa PPF yapo kisheria kabisa, na wala sio hisani, na wala sio kinyume cha sheria.
 
tusaidie basi na sheria ya mwaka 2012 ambayo inarekebisha hizo sheria zilizopita inasemaje?
 
Usichanganyikiwe mkuu,mafao ya kujitoa yalikuwepo whether kulikua na sheria au hakuna,nssf/ppf walikua wanatoa so hakuna haja ya kutafuta kwamba kulikua na sheria au hakuna sie tumejiandikisha kwa kua tuliambiwa na maofisa wa nssf kwa ukiacha kazi unachukua mafao yako!
 
tusaidie basi na sheria ya mwaka 2012 ambayo inarekebisha hizo sheria zilizopita inasemaje?

Hiyo sheria inayopiga marufuku mafao ya kijitoa nisheria ya SSRA (mamlaka ya udhibiti wa mifuko ya pensheni tanzania).
Sheria hii imepitishwa ili kuzuia mifuko ya penseni kutoa mafao ya kujitoa.
Hapa kuna mkanganyiko wa sheria, maana sheria za mifuko ya pensheni za PPF na LAPF zinaruhusu mafao ya kujitoa, wakati sheria ya SSRA inakataza mafao hayo.
Hii ina maana kuwa upitishaji wa sheria ya SSRA ulifanywa kwa kukurupuka sana bila kuangalia sheria za mifuko ya pensheni zinasemaje.
 
Watupe pesa zetu! Waache Kutafuta hela za kupatia kura 2015! Ccm ni uozo!
 
tunataka mafao yetu, suala la kusubir mpk retirement age 55-60 ni jambo sio muafaka kwa watz wa sasa ukizingatia our Tanzanian's life expectancy ni miaka 51 kwa wanaume na 54 kwa wanawake( source indexmundi-CIA) wanasiasa zingatieni hili
 
Usichanganyikiwe mkuu,mafao ya kujitoa yalikuwepo whether kulikua na sheria au hakuna,nssf/ppf walikua wanatoa so hakuna haja ya kutafuta kwamba kulikua na sheria au hakuna sie tumejiandikisha kwa kua tuliambiwa na maofisa wa nssf kwa ukiacha kazi unachukua mafao yako!

Mwanzoni kabisa wakati swala hili lilipojitokeza hadarani, SSRA walisema kuwa mifuko yote ya pensheni haina mafao ya kijitoa. Wakasema kuwa mafao ya kujitoa yalikua yanatolewa kimakosa, hivyo sheria mpya ililetwa ili kuhakikisha kuwa mifuko ya pensheni haiendelei kutoa mafao hayo ya kujitoa. Hapo ndipo upotoshaji ulipoanza, kwa kuwahadaa wananchi kuwa sheria zote za mifuko ya pensheni haziruhusu mafao ya kujitoa.
SSRA na serikali waliwahadaa wananchi kwa kudhani kuwa watu wengi hawajui sheria.
 
Mbona huyo dada Irene hakuja kwa kipindi cha channel ten Juzi kujibu hoja za kuhusu hizo office zao za SSRA juu ya sakata hilo la malipo ya pension mpaka ufikishe miaka 55. Na kama kweli wana hoja ya msingi si wajitokeze kwa umati wa watanzania waone kama wataweza simamia hoja zao.

Vigogo wameua mashirika ya Bima ya kiserikali sasa wamekosa fund wanakuja kwa haya mashirika mengine ati wanakuwa Police wa kuchunga fund zetu
 
Hii ishu hawa jamaa waiweke wazi ili kila mtu aelewe vizuri, haya mambo ya kucheza na pesa za watu hayafai hata kidogo.
 
Mbona huyo dada Irene hakuja kwa kipindi cha channel ten Juzi kujibu hoja za kuhusu hizo office zao za SSRA juu ya sakata hilo la malipo ya pension mpaka ufikishe miaka 55. Na kama kweli wana hoja ya msingi si wajitokeze kwa umati wa watanzania waone kama wataweza simamia hoja zao.

Vigogo wameua mashirika ya Bima ya kiserikali sasa wamekosa fund wanakuja kwa haya mashirika mengine ati wanakuwa Police wa kuchunga fund zetu

Mashirika mengi yalikufa kwa sababu serikali imechota pesa bila ya kurudisha. Mashirika mengine kama Tanesco yana hali mbaya ya kifedha kwa sababu yanaidai serikali pesa nyingi sana.
Hii inanikumbusha ile ripoti ya CAF iliyosema kuwa NSSF ipo hatarini kufilisika.
Baada tu ya ripoti ya CAG. ndio ikapitishwa 'sheria' hii ya SSRA kuzuia mafao ya kujitoa.
 
Mwanzoni kabisa wakati swala hili lilipojitokeza hadarani, SSRA walisema kuwa mifuko yote ya penseni haina mafao ya kijitoa. Wakasema kuwa mafao ya kujitoa yalikua yanatolewa kimakosa, hivyo sheria mpya ililetwa ili kuhakikisha kuwa mifuko ya penseni haiendelei kutoa mafao hayo ya kujitoa. Hapo ndipo upotoshaji ulipoanza, kwa kuwahadaa wananchi kuwa sheria zote za mifuko ya penseni haziruhusu mafao ya kujitoa.
SSRA na serikali waliwahadaa wananchi kwa kudhani kuwa watu wengi hawajui sheria.

Irene, Urio na wengine wote are all embedded; mere pipers blowing their trumpets of to serve the ineterest of their master "He who pays the piper calls the tune" kuna ajenda ya siri na ya kishetani nyuma ya mkakati huu, lakini bottom line ni kwamba "tunataka pesa zetu" period
 
Kwa kweli me naona hii sheria imekaa kifisadi zaidi,watupe hela zetu haraka kabla hatujaandamana.

Mkurugenzi mtendaji wa SSRA, Irene Isaka alijaribu kuwatisha wafanyakazi kwa kusema:-

"... hata hivyo mifuko yote ya hifadhi iliyoko nchini haitoi fao la kujitoa na kwamba waliokuwa wakitoa fao hilo walikuwa hawafuatia sheria ya mafao saba yanayotajwa kisheria..."

Hapa alitaka kuwatisha wafanyakazi kuwa mafao ya kujitoa hayapo kisheria.
Hakujua kuwa watanzania wa sasa wanasoma sheria na kuzijua vizuri. Mifuko ya PPF, LAPF na PSPF inatoa mafao ya kujitoa kisheria kabisa.
 
Irene, Urio na wengine wote are all embedded; mere pipers blowing their trumpets of to serve the ineterest of their master "He who pays the piper calls the tune" kuna ajenda ya siri na ya kishetani nyuma ya mkakati huu, lakini bottom line ni kwamba "tunataka pesa zetu" period

Mkuu na sasa sio ajenda ya siri tena wamekula pesa zetu na wameshindwa rudisha na sasa wanatafuta mbinu hapo ya kufanya either kutuambia NSSF,PPF wako bankrupt sasa wananchi si wamestuka au twasema NGASTUKA MACHALE KUNDESA.

Mkuu ukiona SERIKALI fulani inashindwa kukusanaya KODI na kuna viuzembe uzembe mwingi hivi ukiukaji wa HAKI na SHERIA kupindishwa pindishwa hivi na RUSHWA kujaaaaa maofisini mwao hiyo Nchi inatatizo kubwa sana ndio sisi sasa Serikali haiwezi kujenga Hoja haiwezi kusimamia resource zingine kama madini mbuga gas, Serikali inakimbilia pesa za walipa kodi kweli kweli does this make any sense?


 
Chakushangaza eti hawa SSRA ni watetezi wa wanachama kama ilivyo watetezi walaji, uwura na nk. sasa wamegeuka kuwa watetezi wa serikali na mifuko.
 
Serikali Nyie vipi?
•Mmekwapua fedha za EPA,Kagoda mmetumia kwenye kampeni
•Mmekwapua Fedha za Rada
•Mmeua viwanda vyote(99%) na kubwia fedha
•Mmekwapua fedha za DART 2008
•Mmeuza ardhi yetu kwa wazungu
•Mmekula mirungula ya madini wakati wananchi hawafaidiki
•Mnakata Paye 30% kila mwezi
•Mmeuza twiga,vitalu,faru bado haziwatoshi
•Mmetuuzia Nguzo za South Afrika(Iringa) bado tu?
•Mmekula na Richmond,mmekula na Puma energy,mmetuuzia mabox ya misumali,matairi mabovu,bado tu hazijawatosha?
•Mazao ya misitu na bahari haziwatoshi?
•Mmekula bil6 kila mwezi kifisadi kwa miaka miwili,hazijawatosha?
•Fedha za wazee wa EAC hamjawalipa mnataka na zetu? Hapa ndio mmeingia choo cha kike.

Serikali yetu ni currupt,dhaifu,legelege,kama mmeshindwa kuongoza nchi wapeni watu wenye uwezo waendeshe
•Mmekabidhiwa resources zote lkn still tunatembeza bakuli,sector ya madini,misitu na bahari+Usafirishaji zinaweza kupata fedha za kuendesha nchi vizuri tu pasipo kuwatumia walevi(bia na sigara)! Kodi za TRA ni nyingi mno gari nanunua japan 3000$ huku nakuja kulipia 4000$ ushuru khaa yani mnakamua wananchi mpaka basi!! Tumechoka tupeni break jaman
•Mmeifilisi mifuko ya hifadhi sasa mnataka kutuingilia hadi kuchukua hela mifukoni mwetu? Hapa ndio mmechemka,hapa ndio tutapowaondoa madarakani,na hata mking'ang'ania tutaanzisha movement tusipeleke fedha zetu huko mpaka hoja ya msingi ijadiliwe na tufikie muafaka!

Irene na Jeikei+Some of wapiga madesk mmechemka!!!
 
Wana JF,
Nimefuatilia mijadala mimngi hapa JF inayohusu swala la mafao ya kujitoa.
Nimeona kuwa watu wengi hawajui kuwa mafao ya kujitoa PPF yapo kisheria na kudhani kuwa mafao hayo yanatolewa na PPF kama hisani tu.
Kwa sababu hiyo, SSRA, serikali na watu wengine wametumia mwanya huo kupotosha ukweli kuhusu mafao hayo, na kusema kuwa mafao hayo hayapo kisheria.

PPF Act No. 25 ya mwaka 2001, kifungu cha 44 kinasema yafuatayo:-

“Withdraw Befefits"

44.-(1) Where a member ceases to be employed in circumstances in which he is not eligible for any pension, gratuity or any other benefit under the provisions of this Act, he shall be refunded the amount of his own contributions and that of his employer to the Fund.
(2) Where a member has been employed for a period of not less than five years and the
cessation of such employment is not due to dismissal for misconduct the amount of his own
contribution and that of his employer together with a simple interest at that rate to be determined
by the Board of Trustees shall be paid to him.


Kwa kifupi kabisa, mafao ya kujitoa PPF yapo kisheria kabisa, na wala sio hisani, na wala sio kinyume cha sheria.
Sote tunajua kwamba yalikuwepo, lakini sheria mpya ya kuanzisha mamlaka ya kusimamia mifuko ya jamii maarufu SSRA imefuta mafao ya namna hiyo na hicho ndicho kinacholalamikiwa. Kwa ufupi ni kwamba hiyo sheria unayonukuu leo imeishapitwa na wakati na haina nguvu tena kisheria
 
:: PPF Pensions Fund ::-

WITHDRAWAL BENEFIT
Qualifying condition
Where a member ceases employment through summary dismissal or termination.
Mode of granting withdrawal benefit
i) Granted as Lump sum immediately on ceasing employment.

Documents required
� Benefit Claim duly filled by the employer; (See Page 25)
� Confirmation from the employer that the member has been dismissed or terminated from employment;
� Two passport-size photographs of the member.
 
Back
Top Bottom