Sheria ya mswaada binafsi ifutwe

Jaxx

Senior Member
Mar 22, 2011
129
28
Kwa kumbukumbu zangu ni Muswaada Binafsi uliwahi kupita ni mmoja tu wa Bro Lau Masha wa kutumia picha ya Karume kwenye Pesa ya Tanzania; Pamoja na Miswaada Lukuki inayopelekwa na Wabunge kutupiliwa mbali kwenye kapu la takataka (Dustbin) la Mh Speaker,Kwa maana hii naona hakuna haja tangu miaka 50 ya Uhuru in maana hakuna Muswaada ulioletwa kwa speaker wenye maslahi ya taifa letu?, Au wabunge wetu hawana ufahamu wa kuandaa miswaada?, Au Serikali haina uwezo wa kuchambua miswaada mipya maana imezoea copy & paste kama ile ya katiba kutoka Kenya?, Au wataalamu wa mambo ya Sheria Serikalini wako shallow?, Au ni uoga wa Serikali kuonekana kuwa haitimizi wajibu wake wa kupeleka misawaada Bungeni?,
Kimsingi cpati jibu lolote hapo na nikiamua hayo yote yawe majibu basi naona hatuhitaji Sheria hiyo?
Ahsanteni, ngoja nipiganie daladala nirudi kwetu nikanywe Ghahawa na Kashata 2 nilale!!!
 
Isifutwe bunge liache unafiki hapo kitaeleweka, sasa kama bunge limejaa mijitu vilaza, mambumbumbu wa sheria hopefully litaendelea kuwa rubber stamp as usual. Kazi ya Bunge ni kutunga sheria na sio kupitisha sheria, na katika katiba mpya tuhakikishe bunge lishiriki ipasavyo hata kuandaa bajeti na iletwe bungeni ktk ministerial statement two month kabla ya kusomwa, siyo 2ngoje zee lenye upara lije na mikaratasi kama Britanica encyclopidia na vilaza waanze kusema naunga mkono mia kwa mia, kimsingi katiba mpya itizame bunge na mihimili yote ktk sura mpya.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom