ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
mwiba,
ni kweli kuna matatizo ya uvaaji kwa wanawake na wanaume pia; nguo za kubana au vimini kwa wanawake, suruali za milegezo kwa wanaume na mambo kama hayo. Lakini haya ni mambo ya kimaadili zaidi kuliko mambo ya kushughulikiwa na sheria. Makanisa mbali mbali huwa wanazo taratibu zao za kushughulika na mambo haya na hizo taratibu hutofautiana kutoka kanisa moja hadi jingine. Haya mambo ya uvaaji hayahusiani moja kwa moja na imani bali ni mambo ambayo yanaonekana kuathiriwa na mila na desturi mbali mbali.
Ni kweli kabisa kuna maeneo kuingia kanisani na mini-skirt si issue kubwa na kutokana na mila na desturi za maeneo yale kama hakuna mtu anayekuwa "offended" wanawake huwa huru kujimwaga vile wapendavyo! Hata wanaume vile vile. Kwa ninavyojua, mafundisho mengi ya ukristo huangalia mambo ya ndani zaidi kuliko mambo ya nje kama mavazi anayovaa mtu au chakula anachokula; ambayo mara nyingi hubadirika kutokana na mila, desturi na mazingira ya mahali husika. Haya si mambo ya kushughulikiwa kisheria sana. Hata jamii zinazokaa uchi kabisa wanaweza kuwa wakristo na wakaendelea kusali bila matatizo ikiwa kukaa uchi kwenye jamii husika si tatizo!! Ukristo husisitiza zaidi mambo ya upendo na ukiangalia katika amri kumi za mungu ambazo wakristo huzifuata hadi leo, uvaaji halimo katika amri hizo kumi! Hata wakatoliki ambao wanazo amri sita za kanisa bado katika zile amri sita uvaaji si mojawapo ya amri hizo!
Mambo ya kuhukumu mwizi katika ukristo si masuala ya kiimani hivyo hukumu juu ya wizi (au mambo yote ya kijinai) huchukuliwa kuwa ni mambo ya kushughulikiwa na serikali; wezi hata wakiiba sadaka au mali ya kanisa hushitakiwa katika vyombo vya sheria vya kiserikali.
imesisitizwa tuvae kwa kujistiri. Sasa kujistiri kwa masai, siyo sawa na kujistiri kwa mchaga, mpare na kadhalika. Nakubaliana na wewe kuwa huathiriwa na tamaduni zetu, kama yalivyo majina, kristo alituachia jina moja tu, yaani wakristo. Sasa kuitwa iman, ramadhan, juma, adamu, ntamaholo nk, havina uhisiano wowote na ukristo. Jina ni jina tu