MARIJANI
Member
- Mar 31, 2010
- 20
- 0
Tanzania imepoteza rasilimali ya madini nyingi na mapato mengi huku umasikini wa wananchi ukiongezeka. Sasa sheria Mpya ya madini inakuja Bungeni tarehe 19 na 20 April 2010 kwa hati ya dharura ambayo wabunge wanatakiwa kujadili na kupitisha siku hiyo hiyo! Tunauliza, kwanini hati ya Dharura bila ushirikishaji na majadiliano ya kutosha?
Ewe Mbunge, Hatima ya Nchi hii sasa ipo mikononi mwako, kataa kuburuzwa kwa masilahi ya wengine, Jadili kwa umakini, pinga usiri, sheria kandamizi na nyonyanji ya nchi. Tanzania tajiri na yenye ustawi inawezekana!
Tangazo Hili linaletwa kwenu na:
Agenda Participation 2000 kwa ushirikiano na
Revenue Watch Institute (RWI)
Ghorofa ya Tano
Ubungo Plaza
Simu: +255 22 2460036/39
Sms + 255 782 550379/ 0758318914
SOURCE MICHUZI