Sheria kandamizi ya magazeti;Katiba mpya haiwezi kuwa suluhu ya tatizo hili?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Miongoni mwa watu ambao wamesikitishwa na kuathirika na uamuzi wa kimabavu wa serikali wa kulifungia gazeti la mwanahalisi mimi ni mmoja wao.Mimi ni msomaji na mpenzi wa gazeti hili ambalo kwakweli limekuwa mstali wa mbele kufichua maovu ya serikali na viongozi wake.Ushahidi kuwa gazeti hili hutoa tuhuma za kweli ni pale tunaposhuhudia serikali kushindwa kulifikisha mahakani pale linapoibua tuhuma nzito kwa mfano hii iliyohusu usalama wa taifa na utekaji wa Dr.Ulimboka.Kama tuhuma hizi zilikuwa ni za uongo na uzushi kama serikali inavyodai mbona hawakulifikisha gazeti hili mahakamani?

Tangu gazeti hili lifungiwe ni wazi tunakosa kujua mambo mengi sana na kwa kweli tunakosa haki ya kupata habari.Bila shaka kwa watawala hali hii ni afueni na furaha kwao kwani baadhi ya madhambi yao umma utakosa kuyajua.

Bunge ndio chombo pekee ambacho tulitarajia kingeweza kuibadili kama sio kuifuta kabisa sheria hii.Bahati mbaya sana bunge letu limejaa watu wasio na uzalendo na wasiojua wajibu wao.Nasema hawajui wajibu wao kwasababu wengi wao wanadhani wajibu wao ni kuilinda na kuitetea serikali na chama chao na sio kumtetea mwananchi.Hata ikitoka hoja ya kufuta sheria hii naamini itapingwa kwa nguvu zote.Kibaya zaidi hata kiongozi wa bunge ndio kinara wa kulinda serikali.

Sasa wadau mimi nafikri kama kubadilisha sheria hii kupitia katiba mpya ni jambo linalowezekana basi ni wakati muafaka wa kufanya hivyo.Wadau wanaohusika waelimishe umma juu ya ubovu wa sheria hii, ili kupita katiba mpya kama inawezekana, umma wa watanzania uifutilie mbali sheria hii.

Sheria hii ni janga la kitaifa kama ulivyo ufisadi.
 
Miongoni mwa watu ambao wamesikitishwa na kuathirika na uamuzi wa kimabavu wa serikali wa kulifungia gazeti la mwanahalisi mimi ni mmoja wao.Mimi ni msomaji na mpenzi wa gazeti hili ambalo kwakweli limekuwa mstali wa mbele kufichua maovu ya serikali na viongozi wake.Ushahidi kuwa gazeti hili hutoa tuhuma za kweli ni pale tunaposhuhudia serikali kushindwa kulifikisha mahakani pale linapoibua tuhuma nzito kwa mfano hii iliyohusu usalama wa taifa na utekaji wa Dr.Ulimboka.Kama tuhuma hizi zilikuwa ni za uongo na uzushi kama serikali inavyodai mbona hawakulifikisha gazeti hili mahakamani?

Tangu gazeti hili lifungiwe ni wazi tunakosa kujua mambo mengi sana na kwa kweli tunakosa haki ya kupata habari.Bila shaka kwa watawala hali hii ni afueni na furaha kwao kwani baadhi ya madhambi yao umma utakosa kuyajua.

Bunge ndio chombo pekee ambacho tulitarajia kingeweza kuibadili kama sio kuifuta kabisa sheria hii.Bahati mbaya sana bunge letu limejaa watu wasio na uzalendo na wasiojua wajibu wao.Nasema hawajui wajibu wao kwasababu wengi wao wanadhani wajibu wao ni kuilinda na kuitetea serikali na chama chao na sio kumtetea mwananchi.Hata ikitoka hoja ya kufuta sheria hii naamini itapingwa kwa nguvu zote.Kibaya zaidi hata kiongozi wa bunge ndio kinara wa kulinda serikali.

Sasa wadau mimi nafikri kama kubadilisha sheria hii kupitia katiba mpya ni jambo linalowezekana basi ni wakati muafaka wa kufanya hivyo.Wadau wanaohusika waelimishe umma juu ya ubovu wa sheria hii, ili kupita katiba mpya kama inawezekana, umma wa watanzania uifutilie mbali sheria hii.

Sheria hii ni janga la kitaifa kama ulivyo ufisadi.

Mkuu una hoja ya msingi.Kinachotakiwa ni wahusika kuchukua hatua.
 
Haihitaji katiba mpya kwani hata katiba ya sasa inatoa suluhu kwa jambo hili. Ibara ya 18(1) inasema hivi:

{Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati}

Hakuna chombo cha habari kilichowahi kupeleka kesi mahakamani kwa mujibu wa kifungu hivi bali vinabaki vinalalama tu kama mtumwa anayeonewa.
 
hivi magazeti ta tanzania yanataka uhuru gani tena . kikwete amewaachia huru muandike chochote mtakacho au mnataka nini zaidi
 
Back
Top Bottom